king'amuzi

CharmingLady

JF-Expert Member
Apr 16, 2012
18,250
12,868
Habar ya mchana wadau....
Mwenzenu mie miaka yote nilikuwa natumua Chadema kuangalizia TV station. Sasa ndo washatangaza kuwa from 31st December,2012 hatutoeza kupata station yeyote. So nataka kununua king'amuzi je ninunue kipi kati ya vifuatavyo:-

- Ting

- Startime

- Zuku na vinginevyo

NB. unaponishauri unanimbia faida na hasara zake!!!!
 
1.Startimes
Bei rahisi na kina local stations nyingi, mawimbi yake hupatikana kwa urahisi. Sina uhakika sana na waliopo nje ya Dar kutokana na aina ya teknolojia itumikayo kurusha matangazo.

2.Zuku
Hii ni tofauti kidogo na ving'amuzi vingine kwani aina ya urushaji matangazo hutumia satelaiti. Wana packages nzuri ila gharama yao kidogo ipo juu kwa Mtanzania wa maisha ya kawaida.

3. EasyTV
Bei zao hazipishani sana na Startimes. Wana packages zilizopangiliwa vizuri kwani wana karibia kila station ya nyumbani. Kama ni mpenzi wa filamu walau hawa wandugu wanajitahidi.

4. Ting
King'amuzi chao ni gharama sana(bei ni zaidi ya mara mbili) ukilinganisha na Startimes, mpaka sasa bado idadi ya local stations ni chache. Kama ni mpenzi wa mpira hawa wandugu wanajitahidi ukilinganisha na ving'amuzi vingine.

NB; Hadi sasa serikali kupitia TCRA wameingia mkataba na makampuni 3 tu na ndio yenye vibali kama wabia. Nayo ni Agape(Ting), Starmedia(Startimes) na Sahara Media(ITV & StarTv).Hii ya mwisho sina uhakika sana maana habari zao bado hazijawa wazi.
 
Daughter, if you have cash, go for Zuku ingawa hutaweza kuona local channels
 
Bora na mie nipate ufaham kabla sijatupa kiantena changu cha M4C, na haka ka TV kangu ka jicho moja cjui itakuwaje.
 
mbona sielewi,ina maana kuanzia january ukinunua ka tv kako hutoweza kuona tbc,itv etc mpaka ujiunge na kina zuku?mbona mambo ya ajabu haya? Terrestial tv zipo kote duniani hazihitaji king'amuzi jamani,kunani,au ni dili za watu?
 
Hahahah geto kwenyewe narudi kulala 2 sa ninunue king'amuz cha nn?

hahaha ikiwa warudi muda huo mbona unaweza kuangalia Series why not TV programs?
am telling you utahitaji tu dear...
 
mbona sielewi,ina maana kuanzia january ukinunua ka tv kako hutoweza kuona tbc,itv etc mpaka ujiunge na kina zuku?mbona mambo ya ajabu haya? Terrestial tv zipo kote duniani hazihitaji king'amuzi jamani,kunani,au ni dili za watu?

ITU regulation, by 2015 all countries should shift to Digital broadcasting tech...
Hakuna usanii kaka...
 
Hizo tv programz za kibongo nyingi hazina mvuto, bunge ntaangalia kwenye viti virefu hahahahah
hahaha ikiwa warudi muda huo mbona unaweza kuangalia Series why not TV programs?
am telling you utahitaji tu dear...
 
Hizo tv programz za kibongo nyingi hazina mvuto, bunge ntaangalia kwenye viti virefu hahahahah

ni kweli kabisa vipindi vingi hatuna ubunifu, kinachofanyika ni kuelekeza tu camera mahali na kuchukua tukio linaloendelea...though bado kuna vipindi maridhawa kama Mechi za soka, Kambi Popote(Clouds TV), Nirvana(EATV), na StarTV huwa wana makala zao flani hivi za WWF, UNDP n.k na Dira ya Dunia ya BBC
 
ITU regulation, by 2015 all countries should shift to Digital broadcasting tech...
Hakuna usanii kaka...
sijakupata vizuri mkuu,una maana ili utumie digital ni lazima utumie king'amuzi,kwani TV za kisasa hazina in built system mahsusi kukamata terrestial signal kama Itv/channel ten etc? Samahani kwa usumbufu nataka tu kujua.
 
1.Startimes
Bei rahisi na kina local stations nyingi, mawimbi yake hupatikana kwa urahisi. Sina uhakika sana na waliopo nje ya Dar kutokana na aina ya teknolojia itumikayo kurusha matangazo.

2.Zuku
Hii ni tofauti kidogo na ving'amuzi vingine kwani aina ya urushaji matangazo hutumia satelaiti. Wana packages nzuri ila gharama yao kidogo ipo juu kwa Mtanzania wa maisha ya kawaida.

3. EasyTV
Bei zao hazipishani sana na Startimes. Wana packages zilizopangiliwa vizuri kwani wana karibia kila station ya nyumbani. Kama ni mpenzi wa filamu walau hawa wandugu wanajitahidi.

4. Ting
King'amuzi chao ni gharama sana(bei ni zaidi ya mara mbili) ukilinganisha na Startimes, mpaka sasa bado idadi ya local stations ni chache. Kama ni mpenzi wa mpira hawa wandugu wanajitahidi ukilinganisha na ving'amuzi vingine.

NB; Hadi sasa serikali kupitia TCRA wameingia mkataba na makampuni 3 tu na ndio yenye vibali kama wabia. Nayo ni Agape(Ting), Starmedia(Startimes) na Sahara Media(ITV & StarTv).Hii ya mwisho sina uhakika sana maana habari zao bado hazijawa wazi.

Startimes wanaboa sana siku hizi.
Mie kila siku nahangaika kusearch mpaka natamani kukipigiza hata hicho king'amuzi chenyewe!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom