Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Katika nchi yetu kuna sheria za ajabu sana, mojawapo ni hii ya kumlinda Rais Mstaafu kutokana na makosa aliyoyafanya akiwa Rais. Habari juu ya Ufisadi uliofanyika katika awamu ya tatu ya Uongozi wa nchi yetu ni dira tosha ya kutufanya tufikirie upya juu ya Kinga ya Rais Mstaafu ya kutoshitakiwa.

Kashfa za kufanya biashara akiwa Ikulu, Wizi wa Mgodi wa Kiwira uliokuwa na thamani ya mabilioni ya shilingi kwa Mkapa-Yona kujiuzia kwa shilingi milioni 700 tu, Uundaji wa Kampuni za wizi na utapeli za Meremeta na Tangold, Wizi wa EPA BoT na Ujenzi wa Twin Towers za BoT, Ubinafsishaji wa NBC kwa Bei ya kutupa,Ununuzi wa Rada kwa bei ya kuruka, Ununuzi wa ndege ya Rais kwa gharama ya Watanzania "kula nyasi" na nyinginezo ni sababu za kutosha kabisa za kutufnaya Watanzania kupigania kuondolewa kwa sheria ya kinga inayomlinda Raisi mstaafu kutoshiotakiwa kwa wizi, ubadhirifu na Ufisadi aliofanya Rais Mstaafu wakati akiwa madarakani.

Sheria ya Kinga ni Msingi mkuu wa Ufisadi na Utawala wa hovyohovyo kwa gharama za Watanzania kama kashfa hizo nilizotaja hapo juu zilivyotugharimu Kiuchu na Kimaadili. Kuvuja kwa Habari za juzi kuhusu Utajiri wa Waziri Chenge kumiliki dola milioni moja katika akaunti nje ya nchi ni ushuhuda mwingine juu ya Sheria hii Fisadi ambayo inaweka misingi ya Wizi na Uhujumu wa mali ya Umma kwa hasara ya Wananchi wa Tanzania. Hebu tujiulize; Je, itawezekana kumshitaki Chenge aliyekuwa MWanasheria Mkuu wakati wa Mkapa bila kumgusa Mkapa (ambaye sheria inamkinga dhidi ya kushitakiwa?)

Tunaweza kumshitaki Daniel Yona kwa kujiuzia Kiwira kwa bei ya bure bila kumshitaki Mkapa ambaye ni "Mjasiriamali" na Mbia mwenzake? KAtika haya mawili haiwezekani kutenda haki maana haiyumkiniki na ni vigumu sana kuwatia watu hawa hatiani (Yona na Chenge) na kumwachia huru Mkapa ambaye ama alishirikiana nao au alishindwa kuwajibika kwa Makusudi na kuwaachia "Wajasiriamali" na Mafisadi kama Chenge kujineemesha kupitia mikataba hewa na feki ambayo naamini kuwa Aliisaini kwa ahadi ambazo ndizo leo imemfanya Chenge kutuhumiwa kuwa na USD Milioni 1 kwenye akaunti zake nje ya nchi!

Kuondolewa kwa shria hii Fisadi, pia kutasaidia kupunguza idadi ya Wagombea urais ambayo wakati wa kinyam]ng'ang'anyioro cha kwenda kugombe Urasi huwa kunakuwa na orodha ndefu ya watu wanaotaka kuwa Marais maana wanajua fika kuwa wakipata nafasi hiyo Ufisadi wao hautakumbukwa milele. Hii itatusaidia kuwa na Wagombea safi na wnaojiamini kuwa ni Waadilifu na ni safi.

Wito wangu kwa Viongozi wa Dini, NGOs, Wananchi, Wabunge na Wanaharakati wengine ni kuwa wakati umefika wa Kushinikiza kufutwa kwa sheria FISADI inayomkinga Rais dhidi ya Rais Mstaafu. Tuanze sasa na ikiwezekana hata kutumia Mahakama ili sheria hiyo iondolewe haraka na kabla hatujapata Rais wa Awamu ya Tano.

Tukifanikiwa kuondoa sheria hiyo Fisadi, tuanze na Mkapa ambaye ndiye chimbuko, Founder na Pioneer wa Ufisadi tunaouona sasa na unaotula kama kansa Watanzania.

Pia soma

Jaji Mstaafu Raymond Mwaikasu ataka Rais aondolewe kinga

JAJI mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Raymond Mwaikasu, amewataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuondoa kinga inayomlinda rais wakati anapostaafu ili aweze kufikishwa mahakamani pindi inapobainika amevunja katiba wakati wa utawala wake.

Jaji Mwaikasu alitoa wito huo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na viongozi wa dini walipokutana kujadili mwenendo wa Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.

Alisema kuondolewa kwa kinga hiyo kutasaidia kudhibiti baadhi ya watu wanaotarajia kuingia madarakani kwa ajili ya kujinufaisha binafsi badala ya kulinda katiba.

Chanzo: Tanzania Daima la 27/3/2014


Waheshimiwa wana Bodi!
Naheshimu sana utaratibu wa Jf jinsi walivyopanga majukwaa yao humu. Ila ukweli ni kuwa jukwaa ambalo linatembelewa na watu wengi, wenye peo mbalimbali, hasi na chanya, hoja nzito na pia dhaifu ni Jukwaa la Siasa anayebisha apinge.

Hoja hii najua inastahili kuweka jukwaa la Sheria lakini mimi nimeiweka humu kwa sababu nilizotaja hapa juu. Naomba Moderator wanisamehe kwa hili na wasiiondoe hoja hii kwani ina maana kubwa sana kwa jamii inayoamka ya Watanzania.

HOJA
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (matoleo yote tangu tupate uhuru mpaka sasa ) sinawakingia kifua viongozi wakuu wa nchi (Marais - Waliopo madarakani na wastaafu) kutoshtakiwa mahakamani.

Hapa majuzi Rais wetu mstaafu Benjamini Mkapa kaenda kutoa ushahidi mahakamani kwenye kesi ya Costa Mahalu inayohusu uhujumu uchumi. Nilipatwa na mshtuko kidogo kwani ukizama ndani zaidi unaona kuwa na Rais alieoko madarakani anakuwa shahidi muhimu kwenye hii kadhia kwani yote yalifanyika akiwa waziri wa mambo ya nje.

Sasa najiuliza na wale mnaojua sheria naomba michango yenu ili baade iwe rejea kwenye kutoa maoni ya katiba mpya na katiba ilitolee ufafanuzi jambo hili.

Endapo mahakama itagundua kuwa Mkapa kasema uongo vipo vifungu vya kumtia hatiani mtu anayeongea uongo mahakamani Je kwa Mkapa au Kikwete itakuwaje ?

Je, Mtu mwenye kinga ya kushtakiwa ana sifa za kumtetea mtu mahakamani

Je, Mtu anaweza kuhukumiwa kutokana na ushahidi wa mtu asiye kuwa na sifa ya kushatakiwa

Naomba kuwasilisha

Hakuna Rais Mstaafu anayeogopa kushtakiwa na serikali

Rais Mstaafu Kikwete hata asipoambiwa na Magufuli anakila sababu ya kuondoa hofu.

Kwa mujibu wa ibara ya 46 ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inasema kwamba Rais akiwa madarakani hawezi kushitakiwa kwa makosa ya jinai wala madai kuhusiana na jambo lolote ambalo Rais alilifanya ama kabla ya kushika kiti cha urais au baada.

Na kama Kesi ilikuwa mahakamani ikimhusu Rais toka mwanzo mara tu mtu huyu anapokuwa Rais kesi hiyo inatakiwa isimame.

Makosa ya jinai ni kama mauaji, wizi, ubakaji nk. wakati makosa ya madai ni kama kutolipa deni, kuvunja mkataba, ugoni nk.

Lakini katiba inatoa mwanya wa kumshitaki Rais kwa makosa ya madai mfano Rais hajalipa deni lako na unataka kumshtaki unatakiwa umtumie notisi mwezi mmoja kabla ya kufungua kesi ukijitambulisha jina lako na anuani yako na ueleze unataka kumshtaki kwa kosa gani.

Hii ni ili kama anaweza akayamaliza ayamalize kabla ya kwenda mahakamani.

Kuhusu Rais Mstaafu ibara hiyo hiyo ya 46(3) inasema kama Rais alimaliza muda wake wa Urais kwa njia ya kawaida (hakuondolewa madarakani na bunge) basi hakuna mashitaka yoyote yatakayofunguliwa mahakamani dhidi ya mtu aliyekuwa Rais kwa jambo lolote alilolifanya akiwa madarakani kama Rais.

Na hata kama sheria na katiba ikibadilishwa kuondoa kinga ya kushtakiwa kwa Marais wastaafu sheria hiyo mpya haiwezi kumgusa Rais mstaafu wa awamu ya nne na waliomtangulia maana sheria hufanya kazi kwenda mbele ikianzia pale ilipotungwa hairudi nyuma. ( The law does not operate retrospectively).

Hivyo Marais wastaafu wanatakiwa wawe na amani tu hata wasipoambiwa na Rais Magufuli.

Bashe ataka kinga ya Rais iondolewe kwenye katiba

Mbunge wa Nzega kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hussein Bashe amefunguka na kutaka katiba ya nchi kubadilika ili ikiwezekana kinga ya Rais iondolewe kwenye katiba kwa kuwa kinga hizi zinawafanya viongozi hao kufumbia macho baadhi ya vitu.

Bashe amesema hayo jana mjini Dodoma baada ya kamati za bunge kutoa ripoti juu ya biashara za madini ya Tanzanite na Almasi ambapo katika ripoti hizo baadhi ya mawaziri wa serikali mbalimbali wametajwa kuhusika katika kufanya maamuzi ambayo yamelitia hasara taifa kwa maslahi yao binafsi.

"Umeona maamuzi yaliyofanywa na mawaziri waliotajwa kwenye hizo ripoti unatakiwa kujiuliza swali la msingi hivi maamuzi yote yale ya kuvunja sheria yaliyofanywa na mawaziri hivi Marais waliokuwa madarakani walikuwa hawajui?

"Leo Rais Magufuli asingekuwa tu amesukumwa na moyo wake kufanya haya anayofanya kwenye uwekezaji wa madini tungeyajua haya? Umefika wakati kama nchi wa kuangalia uwezekano kufanya mabadiliko ya katiba, tuangalie mabadiliko ya sheria tuangalie tunapowapa marais hawa kinga haya mambo ndiyo hutokea" alisema Bashe

Bashe anaamini kuwa maamuzi ambayo hufanywa na mawaziri hao ili kufanya mabadiliko makubwa katika baadhi ya mikataba ambayo imeigharimu serikali na nchi kiujumla kuwa ni lazima viongozi wao wa juu ambao ni Marais walikuwa wakitambua mambo hayo.

Mpekuzi


Spika Ndugai awaonya wapinzani wanaotaka marais wastaafu washtakiwe

Ndugai amesema hayo leo (Jumanne) bungeni baada ya mchango wa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali kusema haiwezekani mawaziri na watendaji wengine wa Serikali wakafanikisha mikataba mibovu ya madini bila ridhaa ya Rais.
----
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa upinzani wanaotaka marais wastaafu washtakiwe kuhusu sakata la mchanga wa madini, wakumbuke wanao mawaziri wakuu wastaafu wawili ambao watahusika pia.

Ndugai amesema hayo leo (Jumanne) bungeni baada ya mchango wa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali kusema haiwezekani mawaziri na watendaji wengine wa Serikali wakafanikisha mikataba mibovu ya madini bila ridhaa ya Rais.

"Haiwezekani mzee wangu (Andrew) Chenge na (Nazir) Karamagi walipitisha mikataba hiyo bila Rais aliyekuwapo kufahamu. Kinga ya Rais kushtakiwa iondolewe ili wahojiwe," amesema Lijualikali.

Baada ya hoja hiyo ya Lijualikali inayofanana na ya Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Ndugai aliwakumbusha juu ya mawaziri wastaafu walionao kwenye chama chao.

"Mabadiliko mnayoyataka yakipitishwa na viongozi mlionao wakikamatwa msije mkalalamika tena," amesemaNdugai.


Chanzo: Mwananchi
 
Hii sheria ikiondolewa ndio mwanzo wa Tanzania kuwa na maraisi kama Mugabe. Hii sheria iko kuzuia maraisi wasing'ang'anie madarakani pindi time yao itakapokwisha. Kama mimi najua nikiachia ngazi brake ya kwanza jela unadhani ntfanya nini?

Hakuna Mtanzania yeyote anayestahili kuwa juu ya sheria pamoja na Rais wa Tanzania. Katiba yetu ina mapungufu mengi sana hata Mzee Warioba ameshatamka kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kuandika katiba mpya. Na kwa maoni yangu hiki kipengele chenye kinga ya Rais kutoshtakiwa kwa yale aliyoyafanya alipikuwa Rais inabidi kiondolewe. Hatuwezi kuwa na Marais mafisadi kama Mkapa wanafanya biashara wakiwa Ikulu wanaiba rasilimali za Watanzania mchana kweupe, halafu wasifunguliwe mashtaka na kufilisiwa kwa ufisadi walioufanya walipokuwa madarakani.

Tunataka viongozi waadilifu ambao wanagombea nafasi za juu za uongozi ili kuwatumikia Watanzania kwa moyo mmoja, na siyo mafisadi ambao wanataka kutumia nyadhifa tulizowakabidhi kujitajirisha wao, familia zao, marafiki na jamaa zao.
 
Hivi ndugu zangu ni kwanini uwezo wetu wa kufikilia unakuwa duni sana kiasi hichi.

Unataka kuniambia hawa wabunge na viongozi wengine wote hawaoni upungufu wa sheria hii kuwa ni mwanzo wa maovu kama haya, angalia mambo ambayo mkapa kayafanya mpaka anaona aibu kuongea na watu, lakini eti sheria inamlinda.

Nadhani sheria hii ilikuwa inastaili enzi hizo za Baba wa Taifa waliokuwa waadilifu na wazalendo kweli ambao mpaka sasa tunatamani wangekuwepo, lakini sio enzi hizi za akina mkapa kikwete, tunaoomba hata wapate matatizo yoyote na watoweke muda wowote kwa jinsi walivyotutesa na wanavyoendela kututesa watanzania,

Na ni kwanini hata wabunge wasishirikiana hata katika hili jamani, hii katiba yetu mbona mbovu namna hii jamani, watu wanaiangalia tu kwa sababu ndo inawapa ulaji tu sio

Poa, ila iko siku itafika tu na mambo yataenda kama tunavyotaka
 
Manung'uniko na mijadala mingi imeonekana ikisema Mheshimiwa Rais Mstaafu angefaa kupelekwa mahakamani, na wengine hudiriki kusema 'angestahili kuozea jela'.

Jambo ambalo najiuliza hata akiondolewa kinga,je katiba inaruhusu rais mstaaf kushtakiwa?

na kama inaruhusu, DPP atamshtaki kwa kosa gani na lililopo katika sheria ipi?, Je ushaidi upo wakutosha?

Adhabu ya makosa au kosa hilo ni ipi?, kifungo au fine?

je na kama kinga yakatiba ikitolewa itakua applied retrospectively?yani namaanisha itamgusa Mpaka Rais mwinyi au ni kwa marais wanaofuatia?

Dhumuni lakuuliza maswali haya ni kwasababu inaonekana kama jamii ya Kitanzania tunashabikia tu kwakusema Mkapa apelekwe mahakamani bila ya kusema kwa kosa lipi na lililokatika sheria ipi, na kujua ugum wa kikatiba unaomlinda. Si maanishi kusema tu Kiwira, la hasha hiyo haitoshi. Si maanishi kufungua kampuni ikulu, tunaweza kusema hayo yote, lakini cha muhimu sheria zetu zinasemaje kuhusu mambo kama hayo? na process yake ikoje ya kikatiba?kama nilivyouliza hapo juu.

Naomba tujadili bila matusi au shutuma.
Asanteni.
 
Kosa pekee ambalo halina kinga kwa Rais Mstaafu Mkapa ni kufanya biashara wakati akiwa IKULU. Hilo litaingia kwenye kutumia madaraka vibaya.
 
Semenya maswali yako mazuri ndugu yangu,

ebu soma kisa hiki;

Kuna kijiji kimoja Malangali kila anayeingia kuchukua uenyekiti wa kijiji anaingia na nyumba ya nyasi, akimaliza muda wake anatoka na nyumba ya bati kali, achilia mbali rasilimali zingine! ishu hii ni ya mjadala wa kitaifa kwa kila mwenye cheo chochote alipo popote pale Tz, Mkapa kaingia na yumo kwenye culture hii ya kitanzania ''wizi''

Solution sio kwa rais, inaanzia chini kabisa , yeye ni matokeo na ni alama tosha ya kuonyesha kuwa mfumo wetu ni mbovu, kumbuka akienda jela leo kwa kisu kile kile wengi sana nao wataenda jela! swali ni nani msafi wa kumpeleka jela,USHAIHIDI WA KUWA HAKUNA WA KUMPELEKA JELA KUNAASHIRIA HATA HAWA WENGINE SIO WASAFI!! kama hakuna sheria kwa nini? rais malaika??

njia pekee ya kubadili mfumo ni kuleta watu wapya serikalini, watakaosafisha uozo uliokuwepo na kuzuia yasitokee tena hapo baadaye.

Hii kulala na kuamka kuandika kuhusu Mkapa mwaka wa tano , serikali ile ile, kuna watu wanajidanganya kuwa JK na MKapa sio marafiki!

System, mahakama, n.k vingi wanaoviongoza mpaka leo hii ni haoa hao akina mkapa, uteuzi wa majji wakuu n.k ni kinga tosha sana

Katiba ibadilishwe, rais kuteua hawa watu azuiliwe.
 
Kibaka anachomwa moto....
Jizi kubwa namna hii linakula a/c...
Nyumbani a/c, kwenye gari a/c, kila aendako a/c
Hiyo ndio tofauti kubwa kati ya vijibaka na jizi mkapa
 
Kama tungeweza kumonitor kwa wiki tu huyu bwana anaishi katika hali gani, tungelijua jinsi majuto alivyo mjukuu. Kitu kimoja hakiwezekani! Kurudisha muda nyuma maana yote yaliyotokea yametokea. Ila imekuwa ngumu sana kwake kukubaliana na hali halisi.

Mi najua kama angekuwa uswazi basi kashachomwa moto maana mwizi wa uswazi watu hutolea uamuzi hapo hapo.

Sasa kwa kuwa ni mtu mkubwa, anayetembea na ving'ora na kupigiwa saluti, hili jambo la hatari ya kufanya kosa la hujuma linakuwa kama ndoto za mchana.

Pekee kilichopotea ni heshima yake ambayo imepotea na itakuwa ngumu sana kuirudisha especially imani kwa watanzania.

Ni kweli nchi yetu wizi umekuwa kama mfumo. wanayeweza kubadili haya bado ni viongozi kwa kuondoa system zinazo hamasisha watu wezi kuingia katika madaraka na kula fedha za umma.

Wakibadilika wao, hata huku chini kutabadilika. Vinginevyo ni kupoteza muda tu kumjadili mtu ambaye is underestimating people who put him in power.
 
Jambo ambalo najiuliza hata akiondolewa kinga,je katiba inaruhusu rais mstaaf kushtakiwa?

Hiyo kinga iko kwenye katiba ya nchi, swali lako hapo limejichanganya kidogo. Kwa hiyo kinga ikitolewa, it will be a fair game kumfikisha mahakamani.

na kama inaruhusu, DPP atamshtaki kwa kosa gani na lililopo katika sheria ipi?, Je ushaidi upo wakutosha?

Kumfikisha mahakamani kutategemea uchunguzi na ushaidi ambao DPP atapelekewa. Kwa hiyo kama kuna ushahidi kwamba alihujumu uchumi, kula rushwa, kutumia ofisi kwa manufaa yake binafsi, n.k. atashitakiwa kama kibaka yeyote yule aliyekamatwa na makosa hayo kama sheria inavyosema. Kifungo kitategemea na sheria inavyosema kwa makosa atakayo kuwa nayo.

je na kama kinga yakatiba ikitolewa itakua applied retrospectively?yani namaanisha itamgusa Mpaka Rais mwinyi au ni kwa marais wanaofuatia?

Sidhani kama watafanya hivyo kumlenga mtu mmoja. Itabidi iwalenge marais wote wastaafu ndio maana inakuwa ngumu hata kwa rais aliye madarakani kuipa green light hiyo sheria.

Just my opinion!
 
Hata nyinyi wote hapa ni wezi wa aina yake kwa kuwa mnatumia muda vibaya badala ya kuchapa kazi mnabwata! Kipimo ni number of posts. Jipime ni mwizi grade gani mwenyewe kisha uone kama mkapa anastahili kufunguliwa mashitaka. Mkapa alifanya yaliyomhusu. Wewe je?
 
Nilishangaa yule askari kigoma amewaua wenzake ktk lindo badala angeua fisadi kama mkapa au RA
 
Manung'uniko na mijadala mingi imeonekana ikisema Mheshimiwa Rais Mstaafu angefaa kupelekwa mahakamani, na wengine hudiriki kusema 'angestahili kuozea jela'.

Jambo ambalo najiuliza hata akiondolewa kinga,je katiba inaruhusu rais mstaaf kushtakiwa?

na kama inaruhusu, DPP atamshtaki kwa kosa gani na lililopo katika sheria ipi?, Je ushaidi upo wakutosha?

Adhabu ya makosa au kosa hilo ni ipi?, kifungo au fine?

je na kama kinga yakatiba ikitolewa itakua applied retrospectively?yani namaanisha itamgusa Mpaka Rais mwinyi au ni kwa marais wanaofuatia?

Dhumuni lakuuliza maswali haya ni kwasababu inaonekana kama jamii ya Kitanzania tunashabikia tu kwakusema Mkapa apelekwe mahakamani bila ya kusema kwa kosa lipi na lililokatika sheria ipi, na kujua ugum wa kikatiba unaomlinda. Si maanishi kusema tu Kiwira, la hasha hiyo haitoshi. Si maanishi kufungua kampuni ikulu, tunaweza kusema hayo yote, lakini cha muhimu sheria zetu zinasemaje kuhusu mambo kama hayo? na process yake ikoje ya kikatiba?kama nilivyouliza hapo juu.

Naomba tujadili bila matusi au shutuma.
Asanteni.
Semenya,
Umeuliza Mkapa ashtakiwe kwa kosa gani. Kosa kubwa alilofanya Mkapa ni kula rushwa akiwa rais wa TZ. Aliuza NBC kwa rushwa. Alileta Net Problems kwa rushwa. Alijiuzia Kiwira kwa kukiuka taratibu za nchi. Hii inaweza kuangukia chini ya sheria za uhujumu uchumi. Na ushahidi upo.
 
Mwacheni Mkapa apumzike zake, amefanya na muda wake umeisha...hakuna fundisho lolote litakalopatikana kwa kumshitaki rais mstaafu zaidi ya kuongeza uwizi, ikulu kwa atakayekuwa rais...kwani atakuwa anahofia..maisha baada ya kustaafu..

Nafikiri tuwe na tabia na utaratibu wa kuanza tulipo na kuendelea mbele..siyo kila siku kurudi kwa mkapa,mwinyi,nyerere..upuuzi huu.
 
Mwacheni Mkapa apumzike zake...amefanya na muda wake umeisha...hakuna fundisho lolote litakalopatikana kwa kumshitaki rais mstaafu zaidi ya kuongeza uwizi, ikulu kwa atakayekuwa rais...kwani atakuwa anahofia..maisha baada ya kustaafu..

Nafikiri tuwe na tabia na utaratibu wa kuanza tulipo na kuendelea mbele..siyo kila siku kurudi kwa mkapa,mwinyi,nyerere..upuuzi huu.
Yes tufike mahala sasa tuchague. Tumepiga kelele imetosha, tuanze kusaka maendeleo yetu
 
Umeuliza Mkapa ashtakiwe kwa kosa gani. Kosa kubwa alilofanya Mkapa ni kula rushwa akiwa rais wa TZ. Aliuza NBC kwa rushwa. Alileta Net Problems kwa rushwa. Alijiuzia Kiwira kwa kukiuka taratibu za nchi. Hii inaweza kuangukia chini ya sheria za uhujumu uchumi. Na ushahidi upo.

You're right hapo mkuu, ila uoni tatizo lingine hapo ki haki itabidi turudi na kwa Ruksa kwani nae anamakosa haya haya, alafu tuna mawaziri nao wanajinai hizi hizi ambao bado wako huru ingawa awatumikii taifa ki-ngazi ya juu.

Kama ni sheria kuchukua mkondo wake hivyo orodha ni ndefu wenye tuhuma hizi. Na walio hai leo hii Tanzania. Kwa upande wangu hayo ni madhambi ambayo yalikua ni-inevitable kutokana na hii hii katiba mbovu. Hivyo solution kung'oa katiba mbovu ili kuweza kuzuia future embezellment na tabia mbaya. Hila tunapo ng'ang'ana na kuwa peleka mahakamani atu likomboi taifa bali tunafanya wajilinde na hizo kinga.

Hivyo ni better ku-forget whith these fools hili tanzania iweze okoa hasara zake leo na kuwa na huhakika wa kumkaba yeyote in the future through the change of katiba yetu leo. Vinginevyo mi naona kama vile tunaruhusu mafisadi wapya watoke through hizi kinga zao na uwoga wa kubadilisha sheria kwa kujuwa wazi watafungwa.

Point ni kwamba katiba mpya ije na promise ya kwamba kesi za zamani azito sikilizwa hili tuweze pata mabadiliko na kuwatoa uwoga hawa wa sasa kama wanadhani wataenda jela chini ya sheria mpya.
 
Kama kushitakiwa hata mwinyi na nyerere nao pia kuna makosa walifanya wakiwa madarakani.

Mwinyi :mnakumbuka loliondo,IPTL, na ile dhahabu iliyokamatwa airpot na mrema.

Nyerere:sababu ya actionalis personalis mortum cum personna in criminal law hawezi kushitakiwa
 
Kitu kinacho zuia rais au rais mstaafu asiweze kushtakiwa ni kinga. Ikisha tolewa kinga rais anaweza kushtakiwa.

Kusema kuwa hakuna sheria za kumshtaki raisi hata akiondolewa kinga ni kukosa logic.

Rais kama mfanyakazi yoyote yule mwingine anaongozwa na katiba ya nchi na pia muongozo wa ofisi yake.

Kwa maana anaweza kushtakiwa kwa kukiuka katiba na pia miiko ya ofisi yake.

Hauwezi kuniambia rais kaiba au kula rushwa halafu ikosekane sheria ya kumshtaki. Ingekua hivyo basi ina maana kusingekua na miiko ya ofisi ya raisi kabisa.
 
Ushaidi upo wakutosha, maana in law its not what u know, but what u can prove before the court of law.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom