Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

mkuu kwa uchumi tulionao, wabunge wa sasa hawata mtetea mtu, km mtu fisadi atakatwa tu, tena magufuli anahasira nao sanaa[

ni vigumu kwa mwnasiasa yeyote kukubari kutenguliwa kwa sheria kama hiyo, hasa kwa nchi kama tz inayotamaniwa kalibu dunia nzima, maana hakuna rais atakaeongoza, amalize mudawake na akose kashfa. ingekua hivyo hata nyerere angeshtakiwa.
 
Wakuu habari....

Kwa jinsi serikali ya awamu ya nne ilivyovurunda hasa kwenye matumizi mabovu ya fedha na rasilimali za wananchi, natamani Rais kama mkuu wa nchi, kiongozi mkuu wa serikali ashitakiwe mahakamani.

Lakini nimesoma katiba yetu ibara ya 46 kifungu cha kwanza hadi cha tatu vinasema nimarufuku kumshitaki rais akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu kutokana na makosa aliyotenda akiwa madarakani.

vifungu vyenyewe ni kama kama vifuatavyo...

46.-(1) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, itakuwa ni marufuku kumshitaki au kuendesha mashataka ya aina yoyote juu yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

(2) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia wa kawaida ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au ametumiwa kwamba taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.

(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A(10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.


Sasa nauliza je bunge linaweza muondolea Rais mstaafu kinga ya kutokushtakiwa mahakamani??

Naomba ufafanuzi wa kisheria tafadhali....

Kwa huyo nadhani ni kumpa msamaha tu kama wale waliotajwa kwenye vitabu vya ibada
 
Watanzania kila siku na kila kukicha tunalalamika juu ya wizi,rushwa na ufisadi wa viongozi.Malalamiko haya kwa hivi sasa ndio yameteka media na ndio imekuwa ni agenda ya kitaifa.

Hata hivyo,utashangaa hakuna media yoyote, Taasisi yoyote,wanaharakati wowote wale wala mitandao ya kijamii inayojaribu kuendesha harakati za kupinga na kutaka kuondolewa kwa kipengele cha katiba kinachotoa kinga ya raisi kutoshitakiwa mahakamani kwa makosa aliyoyafanya awapo madarakani na hata baada ya kustaafu.

Kama sikisei,hata katiba ya Warioba na katiba inayopendekezwa badao imebeba kipengele hiki!!

Maswali ninayojiuliza.

Hivi kweli tunajitambua?

Hivi kweli tuko serious?

Tunataka mpaka nini kitokee ndio tujue hii kinga inatugharimu?

Kama tumeridhika na uwepo wa kinga hii,tuna haki gani au tuna uhalali gani wa kulalamika?

Watanzania wenzangu, ni nani kalutuloga?

Kama ni "limbwata",litakuwa ni limbwata la aina gani hili?
 
Sasa hili neno kwamba no one is above the law inatakiwa lirekebishwe liseme no one is above the law except the ones with hiyo kinga.
 
kipengele hicho kikiondolewa Raisi kazi yake itakuwa kushinda mahakamani badala ya kufanya kazi za kiraisi,Wahuni utasikia leo wamemfungulia kesi mahakama ya kisutu,kesho anatakiwa mahakama kuu kanda ya mwanza keshokutwa anatakiwa mahakani songea nk.Kufuta hiyo sheria ni ujinga mtupu.Kuiweka ni kumwezesha afanye shughuli zake asikae anakesha mahakamani.Ukiruhusu kwa viinchi vyetu hivi kila siku watu watakuwa wanamburuza raisi hata kwa vitu vya kijinga tu mara kanichukulia mke wangu au mume wangu n.k

Raisi sio sawa namwanachama Chapombe wa UKAWA ambaye kutwa anatakiwa mahakamani kwa kesi za kunywa viroba bila kulipa
 
Sisi ni watu wa kulalamika kila kukicha kuhusu ufisadi na wakati mwingine tunawalalamikia sana waliopata kuwa maraisi wa nchi hii.

Kwanini malofa:Nani kati yetu humu JF,vyombo vya habari,wapinzani,Tume ya Warioba na hata Bunge la katiba wameonyesha umuhimu wa kujadili na kupinga kinga hii ya raisi?

Ni lini tumewahi kuwa na mjadala wa kitaifa juu ya hii kinga ya raisi na madhara yake?

Ni lini umewahi kuwasika ITV,Channel 10,Star tv,TBC1,Azam tv n.k,wakiwa na mada kuhusu kinga ya raisi ya kutoshitakiwa mahakani?

Kwenye Bunge la Katiba hii ilikuwa ni hoja ya msingi?

Katiba ya Warioba iliondoa kinga ya raisi?

Mara ya mwisho kusoma makala au habari katika gazeti lolote inayohusu kinga ya raisi ni lini?

Mkapa alituita baadhi yetu malofa ila naona alipaswa kuwa more general kwa kuwahusisha na watu wa chama chake pia.
 
Back
Top Bottom