Kinana ukiingia Tanga mtafute Bhoke Nyarobi, Afisa Elimu aliyenyanyaswa akaacha kazi

Tuacheni Unafiki Tanzania nzima aliyenyanyasika sana ni huyu Bhoke wako tu? Kinana apiganie Haki na Usawa kwa Watanzania wote na siyo hawa Wachache.
Hawezi kupigania haki za watanzania bali harakati zake za chama.Ameingia kwa mkakati maalum kuelekea2025.Sisi tuendelee kupalua
 
Ameacha kwasababu ya kunyanyaswa. Neno kunyanyaswa ni pana sana mkuu. Wewe shangaa afisa aliyeamua kuacha kazi kwa kunyanyaswa kisa tu amechokonoa maslahi ya chombo ya wakubwa.
Nadhani hapo umeshanielewa mkuu
Mkuu, ni kweli neno kunyanyaswa ni pana, lakini kumbuka kuwa Sheria huwa haitendi haki wakati wote, maana kuna wakati utatakiwa utoe ushahidi wa jambo hilo halafu ukawa huna ingawa ni kweli umetendewa, hapo sheria itakutupa nje.
 
Mkuu, ni kweli neno kunyanyaswa ni pana, lakini kumbuka kuwa Sheria huwa haitendi haki wakati wote, maana kuna wakati utatakiwa utoe ushahidi wa jambo hilo halafu ukawa huna ingawa ni kweli umetendewa, hapo sheria itakutupa nje.
Hata sheria inaangalia mazingira mkuu
 
Katika mapokezi ya makamu mwenyekiti wa CCM bara ndugu Abrahaman Omari Kinana jana, amesema amepewa maelekezo na mwenyekiti wake aanze kupitia baadhi ya mikoa ikiwemo mkoa wa Tanga.

Kinana utakapo karibia Tanga fanya liwezekanalo hata kwa dakika chache uonane na aliyekua afisa elimu taaluma upande wa sekondari anayeitwa Bhoke ili upate picha ya ukatili uliopo jiji la Tanga

Baada ya mama huyo kuibua wizi wa mamilioni ya fedha za ujenzi zilizoliwa na mkuu wa shule moja jijini hapo na mabosi wake,manyanyaso yalianza ofisini kutoka kwa afisa elimu sekondari na aliyekua mkurugenzi wa jiji ambae kwa sasa hayupo. Kutokana na manyanyaso hayo mama huyo akaamua kuacha kazi. Je nimanyanyaso ya namna gani? Kinana mtafute mama huyo utapata picha kamili ya uozo uliopo Tanga jiji.

Baada ya wizi huo mkuu wa shule alisimamishwa kazi na TAKUKURU wakaingia kazini. Kumbe waliokua wanachunguza nao waliingia bei wakaanza kunyanyasa waliotoa ushahidi na kumuacha akijitamba mtaani mwizi huyo.

Tena kwa kuthibitisha na kuonesha udhaifu mkubwa wa kila aina ya rushwa mkuu huyo wa shule ambae ni mwanamke ati akapewa nafasi akaenda kukalia kiti cha afisa elimu taaluma. Kutoka tuhuma ya wizi hadi kukaa kwenye kiti cha afisa elimu. Hii rushwa iangaliwe vizuri. Ikumbukwe afisa elimu naye ametajwa katika wizi huo mkubwa.

Baadae walikuja watu wa TAMISEMI wakatoa amri mwanamke huyo atoke haraka sana ndani ya ofisi ya afisa elimu sekondari.

Ili kuonesha Tanga imeoza mtu ambaye ana tuhuma ya wizi na anachunguzwa na TAKUKURU eti anapewa uafisa elimu kata.

Tanga ni rushwa na rushwa ni Tanga. Mifumo imekua ya rushwa.

Ofisi ya afisa elimu ichunguzwe vizuri dhidi ya mwanamke huyo. TAKUKURU nao watoe muelekeo wa fedha zilizoibiwa.

Pia TAKUKURU na afisa elimu sekondari wachunguzwe kwamba je wana maslahi gani katika mamilioni yaliyoibiwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Comrade Kinana usifanye makosa
Nakuja
 
Sasa Kinana nae unamshtakia kuhusu rushwa, maajabu haya. Kinana nae ana kashfa kibao za kampuni yake ya clearing
Nmeshangaa ..... Haka kajamaa ni katoto hata hakajui kalisemalo. Kabisa unaenda kushtaki kwa kinana? Anyway labda kwa kuwa hana maslah huko. But kinana ni nani mpaka aambiwe haya? So alikuwa anamsubiria kinana muda wote huo?
 
Katika mapokezi ya makamu mwenyekiti wa CCM bara ndugu Abrahaman Omari Kinana jana, amesema amepewa maelekezo na mwenyekiti wake aanze kupitia baadhi ya mikoa ikiwemo mkoa wa Tanga.

Kinana utakapo karibia Tanga fanya liwezekanalo hata kwa dakika chache uonane na aliyekua afisa elimu taaluma upande wa sekondari anayeitwa Bhoke ili upate picha ya ukatili uliopo jiji la Tanga

Baada ya mama huyo kuibua wizi wa mamilioni ya fedha za ujenzi zilizoliwa na mkuu wa shule moja jijini hapo na mabosi wake,manyanyaso yalianza ofisini kutoka kwa afisa elimu sekondari na aliyekua mkurugenzi wa jiji ambae kwa sasa hayupo. Kutokana na manyanyaso hayo mama huyo akaamua kuacha kazi. Je nimanyanyaso ya namna gani? Kinana mtafute mama huyo utapata picha kamili ya uozo uliopo Tanga jiji.

Baada ya wizi huo mkuu wa shule alisimamishwa kazi na TAKUKURU wakaingia kazini. Kumbe waliokua wanachunguza nao waliingia bei wakaanza kunyanyasa waliotoa ushahidi na kumuacha akijitamba mtaani mwizi huyo.

Tena kwa kuthibitisha na kuonesha udhaifu mkubwa wa kila aina ya rushwa mkuu huyo wa shule ambae ni mwanamke ati akapewa nafasi akaenda kukalia kiti cha afisa elimu taaluma. Kutoka tuhuma ya wizi hadi kukaa kwenye kiti cha afisa elimu. Hii rushwa iangaliwe vizuri. Ikumbukwe afisa elimu naye ametajwa katika wizi huo mkubwa.

Baadae walikuja watu wa TAMISEMI wakatoa amri mwanamke huyo atoke haraka sana ndani ya ofisi ya afisa elimu sekondari.

Ili kuonesha Tanga imeoza mtu ambaye ana tuhuma ya wizi na anachunguzwa na TAKUKURU eti anapewa uafisa elimu kata.

Tanga ni rushwa na rushwa ni Tanga. Mifumo imekua ya rushwa.

Ofisi ya afisa elimu ichunguzwe vizuri dhidi ya mwanamke huyo. TAKUKURU nao watoe muelekeo wa fedha zilizoibiwa.

Pia TAKUKURU na afisa elimu sekondari wachunguzwe kwamba je wana maslahi gani katika mamilioni yaliyoibiwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Comrade Kinana usifanye makosa
Majungu Work!!
 
Back
Top Bottom