Kinana: Rais anasahihisha makosa ya serikali na pia anatekeleza kiapo chake

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Omari Kinana ameyasema hayo wakati akiongea na vyombo vya habari Ikulu baaada ya kupokelewa ripoti ya uchunguzi wa Tume ya pili iliyoundwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuchunguza sekta ya madini.

Kinana amesema kitendo anachokifanya Rais Magufuli cha kuita watu na vyombo vya habari Ikulu na kusoma mapendekezo ya Tume mbali mbali anazoziunda amekipongeza na kimemfurahisha sana kutokana na sababu kuu tatu.

Sababu ya kwanza, watanzania wanajua kuna nini kilichoko kwenye taarifa/ripoti.

Sababu ya pili, Rais mwenyewe anajiwajibisha kwa sababu taarifa inajulikana na kila mtu. Kwa hiyo basi, atasimamia kuhakikisha anatekeleza yote.

Sababu ya tatu, Rais ameunda tume katika dhamira ya kusahihisha makosa ya nyuma lakini amefanya hivyo katika msingi wa kufuata katiba, sheria na taratibu. Tume inaundwa, inaleta mapendekezo halafu anagawa majukumu katika vyombo mbali mbali vya serikali na bunge ili kuhakikisha serikali inasahihisha makosa iliyofanya ili watanzania waweze kupata maslahi wanayostahili.

Kinana amemaliza kwa kusema, hashangazwi na utendani wa kijasiri wa Rais Magufuli kwa sababu anamfahamu vizuri.

Kwa maelezo zaidi ya Kinana angalia video kuanzia dakika ya 1:25.

VIDEO.
 
Kusahihisha iendane na kuwawajibisha wote walioshiriki bila kumuonea haya mtu yeyote na hasa Chenge, Chenge kila dili la mabilioni yupo yaani
 
Hivyo huyu kinana baada ya kutumwa India kwa matibabu ndiyo karudi kapona na kutoa hoja hizi!!. Kama ni hivyo ni bora angetumwa St. Thomas, Uingereza!! Pengune huko kwa sasa wamesha"improve"!!
 
Ni vizuri sana kama umewazoea!

Hata leo JPM anapiga makofi maana kelele zimeisha jana ,wale ACACIA wanaendelea na kazi ya kuliibia TAIFA kama kawaida.

Umeshajiuliza kwanini Kalemani hajadeclare kwamba aliwahi kuwa mwajiriwa wa Douglas Lake Minerals ya Canada?
 
Hivyo huyu kinana baada ya kutumwa India kwa matibabu ndiyo karudi kapona na kutoa hoja hizi!!. Kama ni hivyo ni bora angetumwa St. Thomas, Uingereza!! Pengune huko jwa sasa wamesha"improve"!!
Nadhani hoja za Kinana ziko juu ya uwezo wako wa kiakili na kifikra!
 
Pumbaf kabisa...mmeifilisi nchi alafu mnajisemesha eti mnarekebisha makosa>?????ninyi mnapaswa kunyongwa na sio kupewa nafasi ya hicho mkiitacho kureebisha makosa
 
Muache huyo Tundu Lissu aendelee kuuliza tu huku wengine wakitenda kwa ufasaha.

Hata debe tupu huwa linauliza sana kwa njia ya kupiga kelele!

The man is good on parodying!
Just curious, TL huwa ana-immitate nani, au "parody" imebadilishwa maana?
 
Hata leo JPM anapiga makofi maana kelele zimeisha jana ,wale ACACIA wanaendelea na kazi ya kuliibia TAIFA kama kawaida.

Umeshajiuliza kwanini Kalemani hajadeclare kwamba aliwahi kuwa mwajiriwa wa Douglas Lake Minerals ya Canada?
Waache tu waendelee kuliibia taifa! Kwa nini huendi kuwazuia?

Kuhusu Kalemani, kwani ulitaka akuletee wewe hiyo declaration yake? Nenda kwenye Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
 
Pumbaf kabisa...mmeifilisi nchi alafu mnajisemesha eti mnarekebisha makosa>?????ninyi mnapaswa kunyongwa na sio kupewa nafasi ya hicho mkiitacho kureebisha makosa
Nadhani hujui maana ya neno ''kufilisi''.

Kwa hiyo unataka Lowassa na Sumaye wapewe nchi! Gimme a break!
 
Back
Top Bottom