MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,264
Kinana akilakiwa na ngoma ya asili alipowasili kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mukiungu, katika Jimbo la Singida Mashariki la Tundu Lissu wa Chadema.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara ulofanyika katika Kijiji cha Makiungu, wilayani Ikingu, Jimbo la Singida Mashariki la Mbunge Tundu Lissu wa Chadema. Kinana alimponda Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kwa kitendo chake cha kuwakataza wananchi kuchangia fedha za miradi maendeleo na kusababisha jimbo hilo kudorora kimaendeleo tofauti ma majimbo mengine nchini. Alisema badala ya kuwasaidia wananchi badala yake anaendekeza masuala UKAWA
Nape akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mukiungu wilayani Ikungi.
Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Ikungi, Jimbo la Singida Mashariki na kuwataka wananchi wamhoji kama kuna miradi aliyoitekeleza katika ahadi zake wakati wa awamu yake hii ya ubunge wa jimbo hilo.
Nape akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Ikungi.
Wananchi wakila kiapo ili kuwa wanachama wapya wa CCM katika mkutano hou.
Mwenyekiti wa CCM, Mkoa, Msindai akimpatia tofari Kinana walipokuwa wakisaidia ujenzi wa Shule ya Msingi Unyaghumpi, katika Jimbo la Singida Mashariki la Mbunge Tundu Lissu. Mbunge huyo aliwakataza wananchi kuchangia fedha za kujengea vyumba vya madarasa katika shule hiyo. Lakini baada ya kuona watoto wao wanateseka kwa kukosa elimu wananchi wameamua kupuuza katazo hilo na kuanza kujitolea kujenga vyumba hivyo vya madarasa.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Katibu wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Singida, Sija Lukwale wakisaidia kuvuna mtama na uwele kwenye shamba bibi mjane asiye na mtoto, Mayasa Mkhandi katika Kata ya Unyaghumpi, Jimbo la Singida Mashariki, mkoani Singida.
Kinana akikagua shamba la maharage akiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Singida Agriculture, Ally Mohamed katika Kijiji cha Mkiwa, wilayani Ikungi. maharage hayo huuzwa nje ya nchi.
Wafanyakazi wa shamba hilo, wakichuma maharage katika shamba hilo.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nanuye akitumia treka kulima shamba la kampuni hiyo
Nape akisaidia kuchambua maharage ili kuyaandaa kusafirishwa.
Kinana akiangalia makasha yenye maharage yaliyohifadhiwa kwenye kontena lenye jokofu linalotumika kusafirishia nje
Picha juu ni Jengo la Zahanati ya Kimbwi, Kata ya Mungaa, ambayo ilikamilika wakati Kata hiyo ikiongozwa na Diwani wa CCM, lakini hadi sasa haitumiki baada ya Diwani wa sasa wa Chedema na Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu kuwakataza wananchi kuchangia fedha za ujenzi wa nyumba ya madaktari. Kinana (kulia) na Nape pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Msambya wakiondoka baada ya kukagua zahanati hiyo isiyotumika
Wananchi wakijitolea kukwatua nje ya vyumba vya madarasa ya Shule ya Msingi Unyaghumpi ambayo ujenzi wake ulikwamishwa na Tundu Lissu.
Wananchi wakiwa wamejipanga kusomba matori ya kujengea vyumba vya madarasa vya shule ya Unyaghumpi, wakati wa ziara ya Kinana wailayani Ikungi.