mfarisayo
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 5,160
- 2,001
Inasikitisha sana kuona Secretariat ya CCM kuendelea kutumia fedha za walala hoi kuzunguka nchi nzima kutangaza propaganda/mikakati na mipango ya chama isiyotekelezwa miaka nenda rudi. Kwa sasa watanzania hawahitaji kuambiwa nini kitafanywa, Watanzania wanahitaji kuona nini kimefanywa hivyo haina haja ya wao kuzunguka kwa kutumia fedha za walalahoi na kueneza porojo zao, wanapaswa kutenda wanayoyahubiri na watanzania tuna macho na masikio ya kuona na kusikia.
Ikumbukwe wakati wa Kina Mukama walifanya hayohayo ya kuzunguka na kujinadi kuwa watafanya makubwa lakini hadi sasa hakuna jipya na zaidi wanakuja tena na porojo.
Ikumbukwe wakati wa Kina Mukama walifanya hayohayo ya kuzunguka na kujinadi kuwa watafanya makubwa lakini hadi sasa hakuna jipya na zaidi wanakuja tena na porojo.