Kinana na Nape Tumechoka Porojo Zenu Kwa Sasa Tunahitaji Utekelezaji

mfarisayo

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
5,160
2,001
Inasikitisha sana kuona Secretariat ya CCM kuendelea kutumia fedha za walala hoi kuzunguka nchi nzima kutangaza propaganda/mikakati na mipango ya chama isiyotekelezwa miaka nenda rudi. Kwa sasa watanzania hawahitaji kuambiwa nini kitafanywa, Watanzania wanahitaji kuona nini kimefanywa hivyo haina haja ya wao kuzunguka kwa kutumia fedha za walalahoi na kueneza porojo zao, wanapaswa kutenda wanayoyahubiri na watanzania tuna macho na masikio ya kuona na kusikia.

Ikumbukwe wakati wa Kina Mukama walifanya hayohayo ya kuzunguka na kujinadi kuwa watafanya makubwa lakini hadi sasa hakuna jipya na zaidi wanakuja tena na porojo.
 
Inasikitisha sana kuona Secretariat ya CCM kuendelea kutumia fedha za walala hoi kuzunguka nchi nzima kutangaza propaganda/mikakati na mipango ya chama isiyotekelezwa miaka nenda rudi. Kwa sasa watanzania hawahitaji kuambiwa nini kitafanywa, Watanzania wanahitaji kuona nini kimefanywa hivyo haina haja ya wao kuzunguka kwa kutumia fedha za walalahoi na kueneza porojo zao, wanapaswa kutenda wanayoyahubiri na watanzania tuna macho na masikio ya kuona na kusikia.

Ikumbukwe wakati wa Kina Mukama walifanya hayohayo ya kuzunguka na kujinadi kuwa watafanya makubwa lakini hadi sasa hakuna jipya na zaidi wanakuja tena na porojo.
Sisi CCM hatulalamiki, ndio tumelipitisha na kuyaazimia hiyo. Wewe inakuuma nini? Au kwasababu tumewamaliza nguvu kabisa hao movement for Chagaz???
 
Inatia kichefuchefu kuona viongozi hao hao wameishiwa hoja zinazolenga changamoto za maisha ya mtanzania badala yake wamekalia vijembe.

Nilishangaa kusikia Nape anatumia propaganda rahisi kuwa Slaa bado ana kadi ya CCM. So what? Nape au hajui au anapotosha makusudi, kwa kuwa katiba ya CCM inatamka wazi kuwa mtu anapojiunga tu na chama kingine uanachama wake CCM unakoma kwa mujibu wa katiba.

Wananchi wanapowaona majukwaani, wanawazia mambo yanayowakabili na wana matumaini kuwa ninyi mna habari njema: shughuli zao za kiuchumi, bei za bidhaa zao, ajira, pato, shule za watoto, kodi, gharama za matibabu, usalama wao na mali zao n.k. Badala yake wanaambulia mipasho, porojo, upotoshaji n.k.

Pathetic.
 
Sisi CCM hatulalamiki, ndio tumelipitisha na kuyaazimia hiyo. Wewe inakuuma nini? Au kwasababu tumewamaliza nguvu kabisa hao movement for Chagaz???
hiv kumbe huku kuzunguka nchi nzima ni kushindana na chadema badala ya kuwatekelezea ahadi wananchi wa tz?
mimi binafsi kwanza nawashangaa sana hao jamaa kuna siku moja nilikuwa namsikiliza nape akiwa anaponda chadema na kusema wanaanzisha operation za kipumbavu, sasa nashangaa wanalamba matapishi na kuwaiga chadema kwa kufanya ziara nchi nzima, waliwapandikiza cuf wakaenda arusha wakapiga kambi leo hii cuf wako wapi na ile operation iliyoanzia arusha? wakamteua mbatia awe mbuge ili ili kuidhofisha chadema lakini haijasaidia leo wameamua waanze ziara mikoani......... ila ni mbio za sakafuni
 
Sisi CCM hatulalamiki, ndio tumelipitisha na kuyaazimia hiyo. Wewe inakuuma nini? Au kwasababu tumewamaliza nguvu kabisa hao movement for Chagaz???
Mutalalamika nini wakati viongozi wenu wanachota fedha hazina tangu mwezi wa tisa toka muanze vikao vyenu Dodoma hakuna mishahara,au ikilipwa inalipwa nusu au inalipwa imechelewa mno tena kwa mafungu wafanyakazi wa serikali wamepoteza morale kabisa,sisi tunalalamika kwa sababu hamtumii fedha ya chama chenu wezi nyie munatumia fedha ya umma
 
nyinyi waacheni pesa hazina si itaisha,tutaona vinginevyo waamue na mishahara kutokulipa of which it will fuel deeply.
 
Binafsi siwashangai kwakuwa wameajiriwa kwenye chama kwa kazi hiyo tu, POROJO!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom