Kinana, Dkt. Migiro na Nape wachanja mbuga za kisiasa Njombe

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Mar 22, 2013
5,536
2,264
[h=2][/h]
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanafuzni wa vyuo vikuu mkoani Njombe wakati alipowasili katika Chuo cha maendeleo ya jamii Njombe ambapo amekutana na wanafunzi mbalimbali wa elimu ya juu mkoani humo na kusikiliza kero zao mbalimbali Kinana amefanya ziara maalum ya kikazo katika koa wa Njombe baada ya kumaliza ziara yake ndefu ya mikoa ya Ruvuma kamati na Mbeya Alhamisi iliyopita akiongozana na wajumbe wa kamati kuu ya CCM Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi, kinana pia alishiriki katika uzinduzi wa albam ya kikundi cha sanaa cha Vicheko Sanaa Group cha Njombe uliofanyika mjini Njombe Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa akisalimiana na Mhadhili wa Chuo cha Amani Njombe wakati alipowasili katika mkutano na wanafunzi wa elimu ya juu mjini Njombe. Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika mkutano huo. Baadhi ya wanafunzi wa elimu ya juu wakiskiliza kwa makini wakati karibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza nao chuoni hapo. Mmoja wa wanafunzi kutoka chuo cha uuguzi Njombe Omary Sadiki akitoa kero mbalimbali zinazokabili chuo hicho wakati wa mkutano huo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wanafunzi hao katika mkutano uliofanyika kwenye chuo cha maendeleo ya jamii Njombe. Mkuu wa wilaya ya Njombe Sara Dumba akifafanua mambo mabalimbali yanayokwamisha maendeleo katika chuo cha uuguzi cha Njombe wakati akijibu maswali ya wanafuzi wa chuo hicho. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika uzinduzi wa albam ya kikundi cha Vicheko Sanaa Group Njombe iitwayo Amani Tanzania uliofanyika mjini humo leo. Kikundi cha Vicheko Sanaa Group cha mjini Njombe kikitumbuizakatika uzinduzi huo uliofanyika mjini Njombe Hiki ni miongozni mwa vikundi vya sanaa vilivyoshiriki katika uzinduzi huo. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi huo. Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi akizungumza katika uzinduzi huo Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika uzinduzi huo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza wakati akizindua albam hiyo ya Amani Tanzania Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi akishiriki kupiga ngoma katika uzinduzi huo wa albam ya Amani Tanzania o Kikundi cha ngoma za asili ya mkoa wa Njombe kikitumbuiza katika uzinduzi huo. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha albam ya Amani Tanzania iliyorekodiwa na kikundi cha Vicheko Sanaa Group cha mkoani Njombe leo katika uzinduzi uliofanyika mjini humo kushoto ni mwenyekiti wa umoja wa vijana mkoa wa Njombe Amani Fute.
Baadhi ya wanachama wapya wa Chama cha Mapinduzi CCM wakila kiapo huku wakiwa wamenyanyua kadi zao juu mara baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 
Uongozi ni thawabu na jukumu la kuongozwa liko mikononi mwa wananchi na linakabidhiwa na wananchi kupitia sanduku la kura.

They can delay political and economic development but they can't stop them.

CCM ni vikao, CCM ni maamuzi na CCM ni utendaji.

CCM ilithubutu, ikaweza na sasa inatenda.

Like it or not, this is the true reality. CCM inaongoza na itaendelea kuongoza huku vyama vingine vikishambuliana kwa sababu ya pesa za ruzuku na posho mbali mbali.
 
bora mmefanyia ndani manake jana mliaibika
hao mliowasomba kwa malori mmeshawalipa stahihiki yao na kuwarudisha?
ahadi mlizoahidi 2010 mmeshawatimizia?
 
bora mmefanyia ndani manake jana mliaibika
hao mliowasomba kwa malori mmeshawalipa stahihiki yao na kuwarudisha?
ahadi mlizoahidi 2010 mmeshawatimizia?

Nimeona vi-comment vyako vingi ambavyo vinasukumwa na blind mentality.

Wewe niwa kusamehewa tu kwa sababu huna ufahamu zaidi ya kujihusisha na siasa za kwenye mitandao na keyboard.

Hujapata makaratasi ya kukufanya usafiri kutoka kwenye nchi za watu ili tukupe mwariko uje ujionee kwa macho yako kazi inayofanyika kwenye ground zero.

CCM hatupigi makelele bali tunatenda.

Fanya research ndogo kufahamu historia ya Njombe na CCM ili uelewe maana ya andiko langu.

Get out of BAVICHA mentality. Dude!
 
Ni jambo jema kuwa na vikundi kama hiki mana vinaunganisha vijana na kuwawezesha kuwa na sauti kwenye mambo yanayowahusu na hasa changamoto za kiuchumi. Lakin ni vizuri vikund hivi vikawa huru yani visiwe na mtizamo wa kisiasa kama huu ili na sisi ambao hatuna egemeo ktk siasa tuweze kujiunga. Vinginevyo vikundi hivi vyaezatumika kwa maslahi ya wanasiasa wachache na kuharibu malengo ya vikund hivyo
 
mtoa mada hebu thibitisha hiko chuo cha maendeleo ya jamii nicha elimu ya juu..hiko ni chuo kama VETA,tafadhali usipotoshe ukweli...njombe hakuna chuo kikuu
 
Sisi hatutumi ngoma wala wana muziki
maccm lazima mkubali kuiaga ikulu hapata kalika tz 2015
 
kinana kaanza uhuni wa kufanya siasa vyuoni, na huu ndio ushahidi wa yale yakataa. lakini yote ya yote huu ndio wakati wao wa kuteketea wao pamoja na chama chao hata wakifanya mikutano ya chumbani.
 
Sisi hatutumi ngoma wala wana muziki
maccm lazima mkubali kuiaga ikulu hapata kalika tz 2015
Hufahamu kilichotokea huko Kigoma jioni hii?.

Badala ya CHADEMA kupambana na changamoto za matatizo ya wananchi kwa sasa wanapambana na ubinafsi wao kwa wao.

Wanataka kutoana macho kwa sababu ya ruzuku na posho mbali mbali za kibunge mpaka kwa sasa wanaangaliana kwa sura za ukabila, ukanda na udini.

Hivi vyama vya siasa vya upinzani ni hasara kubwa na mzigo mkubwa kwa wananchi masikini walipa kodi.

1478988_613771452015965_517396885_n.jpg


1462988_1495113184048044_19835484_n.jpg

1450192_1495155387377157_1063479637_n.jpg

1476459_1495113377381358_40530360_n.jpg
 
Hufahamu kilichotokea huko Kigoma jioni hii?.

Badala ya CHADEMA kupambana na changamoto za matatizo ya wananchi kwa sasa wanapambana na ubinafsi wao kwa wao.

Wanataka kutoana macho kwa sababu ya ruzuku na posho mbali mbali za kibunge mpaka kwa sasa wanaangaliana kwa sura za ukabila, ukanda na udini.

Hivi vyama vya siasa vya upinzani ni hasara kubwa na mzigo mkubwa kwa wananchi masikini walipa kodi.

1478988_613771452015965_517396885_n.jpg


1462988_1495113184048044_19835484_n.jpg

1450192_1495155387377157_1063479637_n.jpg

1476459_1495113377381358_40530360_n.jpg

Yaan hata sura zao zinasema!! Ukimwambia asome alichoandika ni kasheshe,,,, bangi tupu,,,, art iliyotumika ni ya mtu mmoja,,,,,, hata hamtudanganyii tunaipenda CHADEMA kutoka moyoni
 
Back
Top Bottom