Kinana awataka Madiwani na Wabunge wa CCM kutopitisha na kutunga Sheria kandamizi kwa Wananchi

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Na Mwandishi wetu,
Korogwe, Tanga

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana amewataka madiwani na wabunge kukataa kupitisha miswada ya Sheria yenye kukandamiza haki na kuminya fursa ya wananchi wanyonge kujiendeleza kiuchumi.

Pia, amesema Sasa ni wakati muafaka kulitazama vyema kundi la wajasiriamali wadogo wakiwemo Machinga, mamalishe, waendesha bajaji na bodaboda ili wawekewe mazingira mazuri ya kunufaika na juhudi zao za kujitafutia kipato kujikwamua na umaskini.

Kinana ameyasema hayo leo mjini Korogwe, wakati akizungumza na wana CCM katika ukumbi wa Lembeni, akiwa katika ziara ya kukagua uhai wa Chama na kujitambulisha kwa wanachama.

"Madiwani ninyi ndio mnaosimamia sheria ndogo ndogo za Halmashauri, mkiona sheria hizo hazina uhusiano na wananchi kataeni. Mkiletewa sheria pelekeni kwanza kwa wananchi muwashirikishe kupata maoni yao, rahisisheni maisha ya watu, wasaidieni wakue."

"Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na ninyi sheria ikija bungeni waambieni (serikali) kwa sasa hatuipitishi mpaka tukashauriane na wananchi waliotutuma," alisema.

#CCMImara
#KaziIendelee

IMG-20220425-WA0106.jpg

IMG-20220425-WA0101.jpg

IMG-20220425-WA0091.jpg
IMG-20220425-WA0071.jpg
IMG-20220425-WA0088.jpg
IMG-20220425-WA0066.jpg
IMG-20220425-WA0063.jpg
IMG-20220425-WA0073.jpg
 
Naona makada wananongonezana kweli legacy mpya imeingia maana awamu ya 5 ya CCM, lugha hii ya neno HAKI kwa wote ilikuwa ni "matusi" kwa kufuatana na kamusi maalum ya lugha ya CCM ya wakati huo wa kuanzia 2015 -2021.

1650886889401.png



Newspeak is the fictional language of Oceania, a totalitarian superstate that is the setting of the 1949 dystopian novel Nineteen Eighty-Four, by George Orwell. In the novel, the Party created Newspeak to meet the ideological requirements of Ingsoc (English Socialism) in Oceania.
 
Kinana anataka wabunge na madiwani wakatae sheria kandamizi mpaka wajadiliane na wananchi, kwani wananchi ndio wamewachagua? Hao wote wapo kwenye hizo nafasi kwa maagizo ya serikali, hiyo nguvu ya kupinga sheria kandamizi wanaitoa wapi? Rasimu ya Warioba ilikuwa ya maoni ya wananchi ambao Kinana anataka leo waulizwe, mbona wabunge wa ccm walikataa mapendekezo mengi ya wananchi yasiyo na maslahi kwao, leo hii Kinana anategemea muujiza gani? Au ndio anacheza hadaa ya kisiasa?
 
Chama kiangalie namna ya kutukomboa wanyonge maana makabaila yanatukandamiza hatupumui kabisa.

Gharama za maisha zipo juu mno.
 
"Madiwani ninyi ndio mnaosimamia sheria ndogo ndogo za Halmashauri, mkiona sheria hizo hazina uhusiano na wananchi kataeni. Mkiletewa sheria pelekeni kwanza kwa wananchi muwashirikishe kupata maoni yao, rahisisheni maisha ya watu, wasaidieni wakue."

"Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na ninyi sheria ikija bungeni waambieni (serikali) kwa sasa hatuipitishi mpaka tukashauriane na wananchi waliotutuma," alisema.

Naye mwenyekiti wa CCM aliye katika ziara ndefu ya kikazi Marekani, ambaye pia ana kofia ya urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania naye anasisitiza Tanzania mpya , katiba mpya na mwenendo mpya wa kuwashirikisha waTanzania wote maana Mh. Rais Samia Hassan awasisitiza wana diaspora wa kiTanzania kuwa nchi ni yetu sote na haiwezi kuwa ya mtu mmoja :



23 April 2022

Washington DC
Marekani


Hotuba nzima ya Mh. Rais Samia Hassan na diaspora ya waTanzania nchini Marekani


  1. Uchumi
  2. Afya
  3. Siasa tunaendelea na mazungumzo ya mabadiliko
  4. Nawaelewa kwanini CHADEMA wanasitasita, lakini tunaendelea na mazungumzo nao
  5. R4 : Reconciliation, Resilience, Reforms and Rebuilding the Nation
  6. International relation inasukwa upya iwe kama ya wakati wa Mwalimu Nyerere
  7. Hadhi maalum kwa diaspora, urithi wao nyumbani, fast line airport za Tanzania kwa diaspora n.k
  8. Kodi
  9. N.k

Source : Ikulu Mawasiliano
 
Kinana anategemea muujiza gani? Au ndio anacheza hadaa ya kisiasa?

Swali zito hili kwa wana-mtaa-wa Lumumba maana siku zote hiki chama dola kongwe kinawakumbusha wanaCCM juu ya mila na desturi zao ambazo hazipo ktk maandishi.

Sasa hii desturi na mila gandamizi kweli wataweza kuiacha ? Muda utatuambia kama kweli wameamua kutupilia mbali desturi na mila hizo potovu.
 
Naona makada wananongonezana kweli legacy mpya imeingia maana awamu ya 5 ya CCM, lugha hii ya neno HAKI kwa wote ilikuwa ni "matusi" kwa kufuatana na kamusi maalum ya lugha ya CCM ya wakati huo wa kuanzia 2015 -2021.

View attachment 2200038


Newspeak is the fictional language of Oceania, a totalitarian superstate that is the setting of the 1949 dystopian novel Nineteen Eighty-Four, by George Orwell. In the novel, the Party created Newspeak to meet the ideological requirements of Ingsoc (English Socialism) in Oceania.
Hayo ni maneno ya hadharani, mbaya ni Yale anayoyafanya nyuma ya pazia.
Na anajua watanzania ni mbumbumbu ukiwaambia maneno matamu wanakupenda.

Kinana huyuhuyu wa ile kampuni ya TALL, unasema anazungumzia haki? Tushakubali kuwa wajinga taifa zima wacha tupelekwe tu na uzuri Hawa watu Wana pesa za kununua watu kuwasafisha
 
Hiyo huruma Ccm wameitoa wapi? Na wata juaje ni sheria kandamizi wakati elimu yao ni darasa la saba B?? aka Lusinde#Sukuma
 
Tunataka maendeleo ya kweli. Tunataka wale wote wanaofanya wizi na ubadhilifu wa mali ya umma wawajibishwe. Tunataka nidhamu kwa watumishi wa umma.
Tumeshapiga hadithi imetosha. Tuonyeshe kwa vitendo sasa tunataka maendeleo ya kweli kwa nchi yetu
 
Lugha na kamusi ya maneno ya CCM inayotumiwa na makada wake ambayo wao CCM wanadai ni Kiswahili lakini si kiswahili ambacho sisi wananchi tunachokielewa cha TUKI - Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili UDSM kinachotumika ktk Mawasiliano ya kila siku katika jamii yetu , lugha hiyo maalum ya CCM ambayo hatuielewi inafafanuliwa na mwanafilosofa Alexander Dugin toka Russia


 
Back
Top Bottom