Kilimanjaro moja
Member
- Nov 30, 2012
- 67
- 33
HARAKATI mpya za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zinazoratibiwa kwa ukaribu na Katibu Mkuu wake Abdulrahaman Kinana, katika kukabiliana na nguvu za Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zimeonekana kuwatibua baadhi ya mawaziri, Tanzania Daima Jumapili limeelezwa.
Kitendo cha hivi karibuni cha Kinana kuandamana na mawaziri mikoani kujibu kero za wananchi, kimewakera wanasiasa hao hasa kutokana na kile walichodai kulazimishwa na wenzao kukutana na kadhia ya kuzomewa.
Kutokana na hilo, baadhi ya mawaziri sasa wanafikiria namna ya kuongozana na katibu mkuu huyo katika mikutano na hafla mbalimbali za kichama.
Baadhi ya mawaziri waliozungumza na gazeti hili wanaona kuwa kitendo cha Kinana kuongozana na baadhi yao na kuwataka wajibu kero za wananchi, ni kuwalazimisha kwenda nje ya utaratibu wao wa kazi.
Kutokana na hilo, baadhi ya mawaziri sasa wamepanga kukwepa kuongozana na Kinana kwa visingizio mbalimbali, ikiwemo kubanwa na kazi nyingi wizarani.
Mbali ya sababu hizo, mawaziri hao waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wanadai kuwa mbinu hiyo ya kuongozana na Kinana kwa upande wao haiwajengi kisiasa zaidi ya kuwaharibia.
Baadhi wanaona kwamba mbinu hiyo haitawasaidia kisiasa, hasa katika majimbo yao, kutokana na kero nyingi zinazowakabili wananchi wao, huku wapinzani wakizitumia kama mtaji wa kisiasa hali ambayo imesababisha kuzomewa mara kwa mara.
"Kwa mfano mimi katika jimbo langu, hata uchaguzi wa 2010 nilinusurika tu, kuna mambo mengi hatujafanya, wananchi wana kero ya maji, dawa, miundombinu, huku wapinzani wanapita wanasema sisi ni mafisadi, sasa leo hii nikipanda jukwaani hata kama niko Mtwara wananchi wangu si lazima watasikia nimezomewa.
"Siku nikirudi jimboni kwangu si nitazomewa mara mbili?…Sasa kipi bora, nikazomewe au nibaki niendelee na kazi zangu wizarani?…Nikishindwa bora niende kwa wananchi wangu mimi kama mimi," alisema mmoja wa mawaziri hao.
Aidha, mmoja wa mawaziri ambao inasemekana kwamba alikwepa kuongozana na Kinana pamoja na viongozi wengine wa chama wakati wa ziara ya hivi karibuni jijini Arusha, alisema yeye hakwenda kwa sababu alibanwa na kazi wizarani.
Waziri huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema wanaosema kwamba alikwepa ni waongo na kusisitiza kuwa atakapotakiwa kufanya hivyo, atafanya kama atakuwa hajabanwa na majukumu kazini kwake.
"Mimi sio kama wengine, mimi jimboni kwangu sina matatizo makubwa…hata 2010 nilipita bila upinzani mkali…sasa leo niogope nini?...Nitakapotakiwa na chama changu nitakwenda, ingawa na mimi nimesikia baadhi yetu wanalalamika…lakini na wananchi nao waelewe kwamba sisi tunafanya kazi, wasibakie kuzomea," alisema waziri huyo.
Mawaziri waliokumbwa na dhahama ya kuzomewa ni Christopher Chiza wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Hawa Ghasia (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - Tamisemi) na naibu wake, Aggrey Mwanri..
Hoja ya mawaziri hao kwamba, mbinu hiyo haiwasaidii kisiasa, hasa katika majimbo wanayotoka ilidhihirika pale Ghasia ambaye pia ni Mbunge wa Mtwara Vijijini alipozomewa wakati wakiwa katika ziara ya mkoani Mtwara.
Kuzomewa kwa Ghasia kulikuja baada ya mwananchi mmoja kumshutumu yeye na Mbunge wa Mtwara Mjini, Asnein Murji kwamba waliruhusu gesi kupelekwa Dar es Salaam wakati wananchi wa mkoa huo hawajafaidika nayo.
Pamoja na hilo, kuna habari kwamba CCM hivi sasa inaangalia namna bora ya kuwatumia mawaziri hao kutokana na kile kinachoonekana kuwa mkakati wa kuwatumia umegonga mwamba hasa kutokana na zomezomea zilizowakumba.
Alipotafutwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, kuzungumzia taarifa hizo, alisema hawezi kuzungumza mpaka awafahamu hao wanaolalamika.
Alipoulizwa kama utaratibu wa kuambatana na mawaziri ni wa chama au ni wa serikali, Nape pia alikataa kujibu swali hilo akisema: "acheni fitna zisizo na msingi."
Hata hivyo Nape baadae alizungumza na gazeti hili akisema kuwa ziara hizo ni utaratibu wa chama kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa ilani.
Katika maelezo yake, alisema kuwa baadhi ya mawaziri waliozomewa Mtwara waliomba wenyewe kuongozana kwenye mikutano ya Kinana kwenda kujibu kero zinazowakabili wananchi.
Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Ghasia na Chiza ambao alisema kuwa waliwakuta huko huko Mtwara.
Nape alisema kuwa walilazimika kumuomba Mwanri kwa ajili ya kwenda kujibu hoja za masuala mbalimbali ya mitaa.
Alisema kwa upande wake anaamini kuwa, watu wanaofikiri hivyo lengo lao ni kuvuruga baada ya kuona mafaniko ya CCM yaliyopatikana kutokana na ziara hizo.
Septemba mwaka huu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa mara ya kwanza naye alikumbana na kadhia hiyo ya kuzomewa kwenye mkutano wa hadhara jijini Mwanza, kisha msafara wake kupopolewa mawe.
Pinda alikaririwa akisema kuwa kitendo hicho kimemtisha na kusema upo uwezekano mkubwa wa viongozi wengine wa kitaifa kuanza kukumbana na hali hiyo, na kusema kuwa lazima kero zinazowasibu wananchi zitatuliwe kwani hali hiyo siyo nzuri kutokea kwa kiongozi wa taifa kama yeye.
Mbali ya Pinda, itakumbukwa kuwa hali hii ya zomea zomea pia iliwahi kuwakumba mawaziri mwaka 2007 wakati walipoamua kupita katika mikoa mbalimbali nchini kutetea bajeti.
Mawaziri hao pamoja kutumia kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kutetea bajeti hiyo ambayo ilikosolewa vikali na wabunge wa upinzani kuwa haimsadii mwananchi wa kawaida, lakini bado walishindwa kuzima munkari wao.
Hivi karibuni, CHADEMA kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa ilisema kuwa mpango wa viongozi wa CCM wakiwamo mawaziri kuanza ziara mikoani, hauwezi kukisaidia chama hicho kujiimarisha kisiasa wala kuathiri kasi yao ya kujipanua nchi nzima.
Chama hicho kilisema CCM hawatafanikiwa kwa kuwa zimejitokeza tuhuma nzito ambazo hazijajibiwa na serikali yake kwa Watanzania, hivyo kuwafanya wananchi kukosa imani nayo.
Kitendo cha hivi karibuni cha Kinana kuandamana na mawaziri mikoani kujibu kero za wananchi, kimewakera wanasiasa hao hasa kutokana na kile walichodai kulazimishwa na wenzao kukutana na kadhia ya kuzomewa.
Kutokana na hilo, baadhi ya mawaziri sasa wanafikiria namna ya kuongozana na katibu mkuu huyo katika mikutano na hafla mbalimbali za kichama.
Baadhi ya mawaziri waliozungumza na gazeti hili wanaona kuwa kitendo cha Kinana kuongozana na baadhi yao na kuwataka wajibu kero za wananchi, ni kuwalazimisha kwenda nje ya utaratibu wao wa kazi.
Kutokana na hilo, baadhi ya mawaziri sasa wamepanga kukwepa kuongozana na Kinana kwa visingizio mbalimbali, ikiwemo kubanwa na kazi nyingi wizarani.
Mbali ya sababu hizo, mawaziri hao waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wanadai kuwa mbinu hiyo ya kuongozana na Kinana kwa upande wao haiwajengi kisiasa zaidi ya kuwaharibia.
Baadhi wanaona kwamba mbinu hiyo haitawasaidia kisiasa, hasa katika majimbo yao, kutokana na kero nyingi zinazowakabili wananchi wao, huku wapinzani wakizitumia kama mtaji wa kisiasa hali ambayo imesababisha kuzomewa mara kwa mara.
"Kwa mfano mimi katika jimbo langu, hata uchaguzi wa 2010 nilinusurika tu, kuna mambo mengi hatujafanya, wananchi wana kero ya maji, dawa, miundombinu, huku wapinzani wanapita wanasema sisi ni mafisadi, sasa leo hii nikipanda jukwaani hata kama niko Mtwara wananchi wangu si lazima watasikia nimezomewa.
"Siku nikirudi jimboni kwangu si nitazomewa mara mbili?…Sasa kipi bora, nikazomewe au nibaki niendelee na kazi zangu wizarani?…Nikishindwa bora niende kwa wananchi wangu mimi kama mimi," alisema mmoja wa mawaziri hao.
Aidha, mmoja wa mawaziri ambao inasemekana kwamba alikwepa kuongozana na Kinana pamoja na viongozi wengine wa chama wakati wa ziara ya hivi karibuni jijini Arusha, alisema yeye hakwenda kwa sababu alibanwa na kazi wizarani.
Waziri huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema wanaosema kwamba alikwepa ni waongo na kusisitiza kuwa atakapotakiwa kufanya hivyo, atafanya kama atakuwa hajabanwa na majukumu kazini kwake.
"Mimi sio kama wengine, mimi jimboni kwangu sina matatizo makubwa…hata 2010 nilipita bila upinzani mkali…sasa leo niogope nini?...Nitakapotakiwa na chama changu nitakwenda, ingawa na mimi nimesikia baadhi yetu wanalalamika…lakini na wananchi nao waelewe kwamba sisi tunafanya kazi, wasibakie kuzomea," alisema waziri huyo.
Mawaziri waliokumbwa na dhahama ya kuzomewa ni Christopher Chiza wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Hawa Ghasia (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - Tamisemi) na naibu wake, Aggrey Mwanri..
Hoja ya mawaziri hao kwamba, mbinu hiyo haiwasaidii kisiasa, hasa katika majimbo wanayotoka ilidhihirika pale Ghasia ambaye pia ni Mbunge wa Mtwara Vijijini alipozomewa wakati wakiwa katika ziara ya mkoani Mtwara.
Kuzomewa kwa Ghasia kulikuja baada ya mwananchi mmoja kumshutumu yeye na Mbunge wa Mtwara Mjini, Asnein Murji kwamba waliruhusu gesi kupelekwa Dar es Salaam wakati wananchi wa mkoa huo hawajafaidika nayo.
Pamoja na hilo, kuna habari kwamba CCM hivi sasa inaangalia namna bora ya kuwatumia mawaziri hao kutokana na kile kinachoonekana kuwa mkakati wa kuwatumia umegonga mwamba hasa kutokana na zomezomea zilizowakumba.
Alipotafutwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, kuzungumzia taarifa hizo, alisema hawezi kuzungumza mpaka awafahamu hao wanaolalamika.
Alipoulizwa kama utaratibu wa kuambatana na mawaziri ni wa chama au ni wa serikali, Nape pia alikataa kujibu swali hilo akisema: "acheni fitna zisizo na msingi."
Hata hivyo Nape baadae alizungumza na gazeti hili akisema kuwa ziara hizo ni utaratibu wa chama kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa ilani.
Katika maelezo yake, alisema kuwa baadhi ya mawaziri waliozomewa Mtwara waliomba wenyewe kuongozana kwenye mikutano ya Kinana kwenda kujibu kero zinazowakabili wananchi.
Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Ghasia na Chiza ambao alisema kuwa waliwakuta huko huko Mtwara.
Nape alisema kuwa walilazimika kumuomba Mwanri kwa ajili ya kwenda kujibu hoja za masuala mbalimbali ya mitaa.
Alisema kwa upande wake anaamini kuwa, watu wanaofikiri hivyo lengo lao ni kuvuruga baada ya kuona mafaniko ya CCM yaliyopatikana kutokana na ziara hizo.
Septemba mwaka huu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa mara ya kwanza naye alikumbana na kadhia hiyo ya kuzomewa kwenye mkutano wa hadhara jijini Mwanza, kisha msafara wake kupopolewa mawe.
Pinda alikaririwa akisema kuwa kitendo hicho kimemtisha na kusema upo uwezekano mkubwa wa viongozi wengine wa kitaifa kuanza kukumbana na hali hiyo, na kusema kuwa lazima kero zinazowasibu wananchi zitatuliwe kwani hali hiyo siyo nzuri kutokea kwa kiongozi wa taifa kama yeye.
Mbali ya Pinda, itakumbukwa kuwa hali hii ya zomea zomea pia iliwahi kuwakumba mawaziri mwaka 2007 wakati walipoamua kupita katika mikoa mbalimbali nchini kutetea bajeti.
Mawaziri hao pamoja kutumia kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kutetea bajeti hiyo ambayo ilikosolewa vikali na wabunge wa upinzani kuwa haimsadii mwananchi wa kawaida, lakini bado walishindwa kuzima munkari wao.
Hivi karibuni, CHADEMA kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa ilisema kuwa mpango wa viongozi wa CCM wakiwamo mawaziri kuanza ziara mikoani, hauwezi kukisaidia chama hicho kujiimarisha kisiasa wala kuathiri kasi yao ya kujipanua nchi nzima.
Chama hicho kilisema CCM hawatafanikiwa kwa kuwa zimejitokeza tuhuma nzito ambazo hazijajibiwa na serikali yake kwa Watanzania, hivyo kuwafanya wananchi kukosa imani nayo.