chilamjanye
Senior Member
- Oct 5, 2007
- 110
- 3
Kinana anasema Dr Slaa akipunguza mishahara ya wabunge haitotosheleza matumizi anasahau kwamba kuna Methali ya Aba na Aba Hujaza Kibaba nakumbuka vizuri Dr Slaa amehahidi hata kupunguza baraza la Mawaziri ikiwa na maana posho na vikao na misafara ya kitalii itapungua na hivyo fedha hizo kwenda kwenye Maendeleo. Lakini Slaa ametwambia akiwa Mbunge kuwa Bajeti ilikuwa na mabilioni kwa ajili tu ya Vitafunwa na chai wakati CCM wakwahadaa wananchi eti Kasungura Kadogo ndo maana fedha za Maendeleo ni kiduchu mbona haya mabilioni kinana hataki kusema kwamba yanaweza kujenga mahabara kwenye shule?
Kinana anatwambia DR Slaa akikata wabunge asilimia 15 kila Mbunge atakatwa laki saba na Nusu 750,000/= lakini hajaweka bayana ni asilimia 15 ya shilingi ngapi kama Dr Slaa alivyosema kuwa wabungu wanalipwa yapata milioni saba na Kitu. Tumtake Kinana atueleze ni asilimia 15 ya shilingi ngapi lakini hatukuambiwa walirudisha fedha za EPA ni kina nani tuna hamu ya kuwajua ili tuamini kweli Viongozi wa CCM ni wakweli kwa watanzania. Mimi naona Elimu bure yaja na Afya Bure na nilikuwa sijaanza kulipa Mkopo wa Bodi nasubiri uchaguzi upite ili Dr Slaa akipita nina Imani hata tuliokopeswa atatwambia Tusilipe Kitu. CCM na KINANA ndo naona wanaGhiliba
Kinana anatwambia DR Slaa akikata wabunge asilimia 15 kila Mbunge atakatwa laki saba na Nusu 750,000/= lakini hajaweka bayana ni asilimia 15 ya shilingi ngapi kama Dr Slaa alivyosema kuwa wabungu wanalipwa yapata milioni saba na Kitu. Tumtake Kinana atueleze ni asilimia 15 ya shilingi ngapi lakini hatukuambiwa walirudisha fedha za EPA ni kina nani tuna hamu ya kuwajua ili tuamini kweli Viongozi wa CCM ni wakweli kwa watanzania. Mimi naona Elimu bure yaja na Afya Bure na nilikuwa sijaanza kulipa Mkopo wa Bodi nasubiri uchaguzi upite ili Dr Slaa akipita nina Imani hata tuliokopeswa atatwambia Tusilipe Kitu. CCM na KINANA ndo naona wanaGhiliba