MwanaDiwani
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 5,536
- 2,264
Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Nkungi, wilayani Mkalama wakati wa mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusukuma ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya CCM, kukagua maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Kinana akisoma majina ya vijiji lukuki vitakavyopata umeme katika Wilaya mpya ya Mkalama, Kata ya Nduguti,Jimbo la Iramba Mashariki, mkoani Singida.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Nkungi, wilayani Mkalama
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Nkungi, Mkalama.
Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Singida, Martha Mlata pia alipata wasaa wa kuwahutubia wananchi.
Katibu Mkuu akihutubia kikao cha wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM ya Wilaya ya Mkalama.
Kinana akipata chai nyumbani kwa Balozi Fatuma Kasimu katika Kata ya Gumanga alipoenda kumtembelea na kuongea na wanachama wake wa shina namba 5.Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone na Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Kone (kulia), wakitoka kukagua ujenzi wa Daraja la Mto Simiti linalounganisha wilaya za Meatu mkoani Simiyu na Mkalama, Singida