Nimekuta ugomvi mkubwa kati ya mtu na wifi yake. Ni kwamba kabla hajaoa, huyo kaka mtu alizaa na mwanamke flani hivi, kisha hazikuiva kwa hiyo hakumuoa. Sasa ana mke wa ndoa na wana watoto. Mkewe kamkuta dada wa mumewe akizungumza kwa bashasha na mzazi mwenza huyo huku neno 'wifi' likitumika kama ndio uhusiano baina yao; huyu akiongea anasema 'wifi hivi na vile' mwenzie hali kadhalika. Mke wa ndoa ameumizwa sana na hali hiyo, akalianzisha na wifi yake kuwa "iweje huyu naye wamwita wifi ilhali si mke wa kakako? Au tuambizane kabisa, kakako ana wake wawili?" Dada nae kaja juu "unataka nimwiteje?" Basi ugomvi mtindo mmoja almanusura watoane macho.
Sasa nawauliza akina dada, mtu kama huyo anastahili kuitwa wifi au la? Na kwa hiyo aitweje basi? Uzoefu wenu kinadada ambao kaka zenu wana watu wa namna hiyo, huwa mnawaitaje hao kinamama?
Sasa nawauliza akina dada, mtu kama huyo anastahili kuitwa wifi au la? Na kwa hiyo aitweje basi? Uzoefu wenu kinadada ambao kaka zenu wana watu wa namna hiyo, huwa mnawaitaje hao kinamama?