Kwa muda sasa nimekuwa nikitafakari sana kwamba huenda kama binadam asingekuwa na shughuli nyingi sana zinazohitaji ubongo wake kufikiri kwa kina sana ili kupata majibu au matokeo ya kile anachokifanya, basi angedumu kwa muda/miaka mingi sana bila kuzeeka. Nina mifano michache hapa:
Nina rafiki mmoja ambae kabla ya kuajiriwa miaka mitatu nyuma alikuwa kijana kabisa wala huwezi kumfikiria kuwa na umri mkubwa kwa namna yoyote ile. Baada ya kupewa majukumu mazito ambayo mara nyingi yanahitaji matumizi makubwa ya akili, ameanza kuota mvi kwa haraka sana ndani ya mwaka mmoja tu na sura yake sasa inaonesha ni mtu wa makamo ilihali ni kijana mdogo tu.
Mfano wa pili, narejelea, muonekano wa Barack Obama kabla ya kuwa rais na baada ya kuwa rais(kama picha zilizowekwa mtandaoni ni sahihi). Mfano wa mwisho, nimewahi kuangalia pia picha za Kikwete kabla ya urais na muda mfupi baada ya kuwa rais.
Ndugu wanajamvi, kuna uwezekano jambo hili likawa na uhalisia? Kwa wakristo, rejea kwa manabii, mitume na wafalme wa zamani katika biblia miaka walioishi. Huenda kudumu kwa muda mrefu kulichangiwa na namna walivyoishi, yaani hawakuhitaki kuumiza kichwa sana kufikiria kuishi maisha yenye uhitaji wa mikiki mikiki ya akili.
Nina rafiki mmoja ambae kabla ya kuajiriwa miaka mitatu nyuma alikuwa kijana kabisa wala huwezi kumfikiria kuwa na umri mkubwa kwa namna yoyote ile. Baada ya kupewa majukumu mazito ambayo mara nyingi yanahitaji matumizi makubwa ya akili, ameanza kuota mvi kwa haraka sana ndani ya mwaka mmoja tu na sura yake sasa inaonesha ni mtu wa makamo ilihali ni kijana mdogo tu.
Mfano wa pili, narejelea, muonekano wa Barack Obama kabla ya kuwa rais na baada ya kuwa rais(kama picha zilizowekwa mtandaoni ni sahihi). Mfano wa mwisho, nimewahi kuangalia pia picha za Kikwete kabla ya urais na muda mfupi baada ya kuwa rais.
Ndugu wanajamvi, kuna uwezekano jambo hili likawa na uhalisia? Kwa wakristo, rejea kwa manabii, mitume na wafalme wa zamani katika biblia miaka walioishi. Huenda kudumu kwa muda mrefu kulichangiwa na namna walivyoishi, yaani hawakuhitaki kuumiza kichwa sana kufikiria kuishi maisha yenye uhitaji wa mikiki mikiki ya akili.