Kinachotokea kwenye msafara wa Rais Magufuli kinatoa picha gani?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi kuhusu msafara wa Rais Magufuli.

Kwa watu ambao wana fikra pana na wamebahatika kuwa katika msafara wa Rais Magufuli lazima pia watakuwa wanajiuliza maswali mengi.

Ukiachilia mbali uwingi wa wananchi wanaojitokeza barabarani mpaka wengine wanaamua kwa nguvu kusimama kati kati ya barabara na kufunga barabara ili gari la Rais lisimame lakini ndani yake kuna hoja za msingi ambazo kama taifa tunapaswa kujiuliza.

Wananchi wa Mkoani Tanga baada ya kuiona gari ya Rais Magufuli waliamua kusimama mbele ili kuhakikisha haendelei na safari yake.

NOTA BENE:
Kutokana na kukosa watu wengi wenye fikra pana Sitashangaa kuona wachangiaji wengi watajikita kwenye dhana kuwa wananchi hawawezi au wanaweza kusimamisha msafara wa Rais badala ya kuangalia hoja zangu nje ya dhana hizo kama ninavyojaribu kubainisha katika mada.

VIDEO:


Madhumuni yao makuu ni kutaka Rais Magufuli atatue matatizo yao achilia mbali kuongea nao. Ukisikiliza matatizo yao unagundua mengi yamesababishwa na utendaji wa Serikali za Mitaa na sio Serikali Kuu.

Ieleweke kuwa Serikali za Mitaa ni vyombo vya wananchi ambavyo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huundwa, huendeshwa na huwajibika kwa wananchi.

Dhumuni la kuwapo kwa Serikali za Mitaa ni kupeleka madaraka kwa wananchi. Hii ni kwa kuwa wananchi ndio chimbuko la mamlaka yote katika nchi yeu.

Katiba inaelekeza pia kwamba vyombo vya Serikali za Mitaa vitakuwa na haki na mamlaka ya kushiriki na kuwashirikisha wananchi katika kupanga na kutekeleza shughuli za maendeleo na utoaji wa huduma sehemu zao na chini kote kwa jumla.

Ikumbukwe kuwa, baada ya Wajerumani kuja na kukuta utawala wa serikali za wenyeji uliamua kuweka mawakala wake.

Mwingereza alipokuja, yeye akaamua kuhalalisha utawala wa wenyeji kwa Sheria Na.72 ya mwaka 1926.

Baada ya kupata uhuru, Mwl. Nyerere alifuta tena Serikali za Mitaa mwaka 1972 na kuanzisha mfumo wa Madaraka Mikoani.

Mwaka 1982, Mwl. Nyerere aliamua kurudisha tena serikali za mitaa lakini pamoja na kuendelea kuboreshwa tunashuhudia matatizo mengi yakijitokeza hasa kwa wananchi wanyonge wa vipato.

Kila mwaka taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inaonyesha matumizi mabaya ya fedha, watumishi na mali za halmashauri kwenye serikali za mitaa. Wananchi wanaporwa ardhi za vijiji, huduma duni za kijamii na umangimeza.

Nini kifanyike ZAIDI ili tuboreshe Utawala wa Serikali za Mitaa hasa ikichukuliwa kuwa kuanzia mwaka 1990 kumeanza kufanyika uboreshaji wa Serikali za Mitaa lakini matatizo yanazidi kuongezeka?

Je, ni wakati tena wa kufuta utawala wa serikali za mitaa?

Kama taifa, tunakosea wapi hasa ikichukuliwa tuna viongozi mbali mbali waliopewa majukumu ya kutatua matatizo ya wananchi kutoka kijijini mpaka Taifa?. Tuna viongozi wa Vitongoji, Mitaa, Vijiji, Kata, tarafa, Madiwani, Wabunge, Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa, Mawaziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais wa Tanzania.

Ni vyema ieleweke kuwa Serikali za Mitaa si wakala wa Serikali Kuu bali ni serikali kamili zenye mamlaka chini ya Sheria ndiyo maana zimepewa ‘’bunge’’ lake la kutunga sheria ambalo linaitwa Baraza la Madiwani.
 
Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi kuhusu msafara wa Rais Magufuli.

Kwa watu ambao wana fikra pana na wamebahatika kuwa katika msafara wa Rais Magufuli lazima pia watakuwa wanajiuliza maswali mengi.

Uliachilia mbali uwingi wa wananchi wanaojitokeza barabarani mpaka wengine wanaamua kwa nguvu kusimama kati kati ya barabara na kufunga barabara ili gari la Rais lisimame.

Wananchi wa Mkoani Tanga baada ya kuiona gari ya Rais Magufuli waliamua kusimama mbele ili kuhakikisha haendelei na safari yake.
VIDEO:


Madhumuni yao makuu ni kutaka Rais Magufuli atatue matatizo yao achilia mbali kuongea nao. Ukisikiliza matatizo yao unagundua mengi yamesababishwa na utendaji wa Serikali za Mitaa na sio Serikali Kuu.

Ieleweke kuwa Serikali za Mitaa ni vyombo vya wananchi ambavyo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huundwa, huendeshwa na huwajibika kwa wananchi.

Dhumuni la kuwapo kwa Serikali za Mitaa ni kupeleka madaraka kwa wananchi. Hii ni kwa kuwa wananchi ndio chimbuko la mamlaka yote katika nchi yeu.

Katiba inaelekeza pia kwamba vyombo vya Serikali za Mitaa vitakuwa na haki na mamlaka ya kushiriki na kuwashirikisha wananchi katika kupanga na kutekeleza shughuli za maendeleo na utoaji wa huduma sehemu zao na chini kote kwa jumla.

Ikumbukwe kuwa, baada ya Wajerumani kuja na kukuta utawala wa serikali za wenyeji uliamua kuweka mawakala wake.

Mwingereza alipokuja, yeye akaamua kahalalisha utawala wa wenyeji kwa Sheria Na.72 ya mwaka 1926.

Baada ya kupata uhuru, Mwl. Nyerere alifuta tena serikali za mitaa mwaka 1972 na kuanzisha mfumo wa madaraka mikoani.

Mwaka 1982, Mwl. Nyerere aliamua kurudisha tena serikali za mitaa lakini pamoja na kuendelea kuboreshwa tunashuhudia matatizo mengi yakijitokeza hasa kwa wananchi wanyonge wa vipato.

Kila mwaka taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) inaonyesha matumizi mabaya ya fedha, watumishi na mali za halmashauri kwenye serikali za mitaa. Wananchi wanaporwa ardhi za vijiji, huduma duni za kijamii na umangimeza.


Je, ni wakati tena wa kufuta utawala wa serikali za mitaa?

Kama taifa, tunakosea wapi hasa ikichukuliwa tuna viongozi mbali mbali waliopewa majukumu ya kutatua matatizo ya wananchi kutoka kijijini mpaka Taifa?. Tuna viongozi wa Mitaa, Vijiji, Kata, tarafa, Madiwani, Wabunge, Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa, Mawaziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais wa Tanzania.


Tufute serikali za mitaaaa


Ili kila kitu aongoze Magufuli

Unajua kuna watu kama nyie ni wa kulaaniwa tu

Mmeua Bunge...mahakama mnaiingilia isivyo mfano...mnategemea magufuli atakuwa controlled na nani?

Mnataka kutengeneza nchi ya namna gani????

Magufuli mwenyewe amefanya maamuzi mengi mabovu ambayo hadi sasa yameiingiza serikali hasara...
 
serikali za mitaa zinafanya kazi vizuri sana....huko kusimamisha msafara ni mbinu tu ya kumuongezea Magufuli umaarufu na hao wananchi wanakuwa wameshapangwa muda mrefu tu


yaaani mtu anahangaika tuuu na kutengeneza publicity stunts

Maisha ya watanzania yanazidi kuwa magumu

Kila kitu kimepanda bei

Sekta ya kilimo inayoajiri 85% ya wananchi imetelekezwa

All he does ni kununua ndege na kujenga uwanja wa ndege huko porini....

na bado kuna watanzania wachace wanashangilia
 
yaaani mtu anahangaika tuuu na kutengeneza publicity stunts

Maisha ya watanzania yanazidi kuwa magumu

Kila kitu kimepanda bei

Sekta ya kilimo inayoajiri 85% ya wananchi imetelekezwa

All he does ni kununua ndege na kujenga uwanja wa ndege huko porini....

na bado kuna watanzania wachace wanashangilia
KITU GANI KMEPANDA BEI MKUU?
NYAMA SASA HIVI KILO 4000-5000, MAFUTA YAMESHUKA. KUHUSU KILIMO HAKIJATELEKEZWA TOZO ZAIDI ZA 70 ZIMEONDOLEWA ,TOZO YA KWATO IMEONDOLEWA
 
KITU GANI KMEPANDA BEI MKUU?
NYAMA SASA HIVI KILO 4000-5000, MAFUTA YAMESHUKA. KUHUSU KILIMO HAKIJATELEKEZWA TOZO ZAIDI ZA 70 ZIMEONDOLEWA ,TOZO YA KATO IMEONDOLEWA

Mkuu Vyakula vimeendelea kupanda bei kwa mfululizo tangu mwezi october 2016...

muwe mnaumiza hata akili zenu kusoma takwimu

Angalia data hizi za ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa mwezi july 2017

http://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/cpi/CPI _Juni_2017_Kiswahili.pdf
upload_2017-8-4_17-24-35.png
 
Back
Top Bottom