Kinachosababisha foleni Kimara Korogwe ni wavuka barabara wanaoshuka mwendokasi

instagram

JF-Expert Member
May 27, 2014
2,091
4,716
Hivi vituo vya mwendokasi ujenzi wake umekosewa tangu mwanzo kutokana na kukosekana ushirikishwaji wa mawazo ya wananchi, wenye akili wachache wamekaa wakaamua kujenga walichojenga mwisho wa siku foleni limekuwa balaa na janga kwa watumiaji wa barabara.

Hivi vituo vya mwendokasi vilitakiwa vijengwe na underground tunnels kwa wavuka kwa miguu ili mtu akiwa ndani ya kituo basi anashuka ngazi na kuingia underground na kuvuka upande anaoenda.

Mainjinia wangeweza kuweka miundombinu hii tena ni cheap kuliko madaraja kama ya Kimara ambayo ni expensive na yanapoteza muda sana kwa wavukaji.

Hizi underground tunnels zingetumia makaravati ya mita tatu ambayo ni gharama nafuu kuliko kujenga madaraja hivyo kuondoa kero ya foleni.

Hata huu ujenzi wa njia nane morogoro road ukikamilika uvukaji wa watembea kwa miguu utasababisha foleni zisizo za msingi kila kwenye mataaa.

Ingekuwa bora kama hawa wabunifu wangeweka underground pedestrian crossing ili wavukaji wasiingiliane na magari kwa sababu njia nane na mwendokasi katikati ni hatari mno kwa wavukaji kwa miguu pia ni kupoteza muda kuweka mataa kwa ajili ya wavuka kwa miguu wakati kungekuwa na underground tunnels za wavuka kwa miguu kusingekuwa na usumbufu wa maingiliano wa magari na wapita njia kwa miguu.

Pia hizi underground tunnels zingeweza kutumika kuingizia kipato cha jiji kwa kuweka mabango kwenye kuta za tunnels kwa matangazo ya biashara kwa kuwa wavukaji ni wengi ambazo pia zingeingiza pesa za kulipia bili za umeme kwa taa za ndani ya tunnels na hata air condition ingewezekana pia vingewekwa hata vibanda vya wafanya biashara pia kulingana na design ya tunnels.
0cdf6a7748cf6ae51dec6042c923958d14337-700x5002.jpg
images%20(15).jpg
 
Pale UDsm naona walionesha mfano...

Sema bongo hao watu wanawaza upigaji tu.. ona kama lile daraja la mwendokasi Ubungo si ni hasara tupu.
 
Kosa lilifanyika kimara korogwe ni kuibana njia tofauti na maeneo mengine ili linachangia foleni kwa kiasi kikubwa hasa mpishano wa watu,bajaji na magari.
 
Pale UDsm naona walionesha mfano...

Sema bongo hao watu wanawaza upigaji tu.. ona kama lile daraja la mwendokasi Ubungo si ni hasara tupu.
Kwanini unasema lile daraja ni hasara tupu. Limeacha kutumika?
 
Ni wazo zuri kuwa wangeweka underground tunnel. Lakini hii foleni ya Kimara Korogwe ni foleni ya kujitakia tu na si vinginevyo. Kwa sababu tujiulize mbona vituo vya mwendokasi vipo kuanzia Kariakoo lakini kote huko hamna foleni kubwa ila Kimara Korogwe mpaka Kimara mwisho tu.

Serikali ikiamua hata leo hii tu pale Kimara Korogwe mpaka Kimara Mwisho kutakuwa hakuna foleni. Pale kinachotakiwa kwanza ni kuondoa vile vibanda vyote vya machinga vilivyojengwa kwenye njia ya wapita kwa miguu. Halafu piga greda jaza kifusi pembeni halafu sogeza vituo vya dala dala pembeni kabisa. Na nafasi ipo ya kutosha pande zote mbili inayowezesha hivyo vituo vya dala dala kusogezwa.

Hii wakifanya wachina tutashangaa na kushangilia kama walivyopunguza foleni pale ubungo kabla daraja halijaisha. Wachina waliongeza tu ukubwa wa mzunguko pale Ubungo wakati wanamalizia daraja foleni ikaisha ikabaki kidogo tu asubuhi na jioni wakati lilikuwa ni tatizo la miaka zaidi ya kumi na hakukuwa na mwenye wazo nini kifanyike.
 
Sijui mkuu.
1. Roof inaweza kuwekwa kwenye kila entrance kuzuia mvua.
2. Uzio wa Kozi mbili wa tofali wakuzunguka kwenye entrance kuzuia maji yasiingie.
3. Drainage channels zinaweza kuwekwa around the entrance kuzuia maji yasitiririke kwenda kwenye entrance.
 
Hata wangeweka wabobgo wasingeitumia hilo daraja la juu kimara tuu watu wanapita kule chini nondo zilikochomoka
 
Back
Top Bottom