Kinachosababisha Foleni jiji la Dar es Salaam nyakati za asubuhi na jioni tofauti na ufinyu wa barabara

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,825
9,528
Moja ya sababu kubwa inayochangia foleni majira ya asubuhi na jioni kwenye barabara nyingi za Dar es salaam ni ufinyu wa VITUO VYA DALADALA.

Kusema kweli VITUO VYA DALADALA jijini Dar es salaam ni vifinyu sana kiasi kwamba havitoshelezi DALADALA angalau 5 kuegesha kwa pamoja ili kushusha abiria.

Mbali na ufinyu huo pia, ipo tabia ya baadhi ya madereva wa daladala kupenda kupakilia abiria nje ya vituo hasa MWANZO na MWISHO wa kituo sehemu ambayo ni nje ya kituo suala hili husababisha msongamano mkubwa wa magari mengine kwa kuwa daladala hilo kufunga upande mmoja wa barabara kama ni double lane.

Changamoto nyingine ni Madereva wa DALADALA kupakia abiria maeneo ambayo siyo vituo. Kusema ukweli wenzetu wa Polisi kwenye eneo hili la kuwadhibiti madereva wanaopakia abiria maeneo yasiyo vituo wamelifumbia macho.

Hapa nawaza kwamba kama Traffic Police wakifanya kazi yao vema foleni itapungua pakubwa... Madereva wa daladala wadhibitiwe kufuata sheria na wawazoeze abiria kupanda gari kwenye vituo ili kupunguza foleni.
 
Aisee sababu nyingine ni huu mradi wa DART sijui kama mkataba wao ulikataza kujenga sehem za vituo vya daladala pemben ya barabara. daladala zinakosa sehem za kusimama wanalazimika kusimama kwenye driving lane, hiyo inasababisha foleni maeneo mengi hili suala limekua kero sehem zote na hakuna njia ya dart yenye kituo cha daladala nje ya lane. This is practically not good kwa maisha yetu.
 
Moja ya sababu kubwa inayochangia foleni majira ya asubuhi na jioni kwenye barabara nyingi za Dar es salaam ni ufinyu wa VITUO VYA DALADALA.

Kusema kweli VITUO VYA DALADALA jijini Dar es salaam ni vifinyu sana kiasi kwamba havitoshelezi DALADALA angalau 5 kuegesha kwa pamoja ili kushusha abiria.

Mbali na ufinyu huo pia, ipo tabia ya baadhi ya madereva wa daladala kupenda kupakilia abiria nje ya vituo hasa MWANZO na MWISHO wa kituo sehemu ambayo ni nje ya kituo suala hili husababisha msongamano mkubwa wa magari mengine kwa kuwa daladala hilo kufunga upande mmoja wa barabara kama ni double lane.

Changamoto nyingine ni Madereva wa DALADALA kupakia abiria maeneo ambayo siyo vituo. Kusema ukweli wenzetu wa Polisi kwenye eneo hili la kuwadhibiti madereva wanaopakia abiria maeneo yasiyo vituo wamelifumbia macho.

Hapa nawaza kwamba kama Traffic Police wakifanya kazi yao vema foleni itapungua pakubwa... Madereva wa daladala wadhibitiwe kufuata sheria na wawazoeze abiria kupanda gari kwenye vituo ili kupunguza foleni.
Salasala hata uwawekee stendi kubwa kiasi gani lazima atakaa barabarani ili atege abiria wenye haraka anakuwa anaact Kama gari ndio linaondoka .

Yani daladalawana mambo yao na hawatabadilika hata wewe tukikupa uendeshe utakuwa Kama wao tu maana ukikaa kotuoni hauchekechi gari au kuziba barabara ili uchukue vichwa juu kwa juu hautapata abiria fasta.

Kuna wakati nilipomaliza form six nilikuwa naendesha coaster ya home nilijikuta nakuwa dereva mhuni tu maana hakuna namna na konda ndio anakula maelekezo usimame wapi maana yeye ndio anakusanya hela anajua hesabu ipoje.

Noma sana hiyo kazi ni sawa na ukianza kuendesha bodaboda utajikuta unakuwa mwehu tu.
 
Salasala hata uwawekee stendi kubwa kiasi gani lazima atakaa barabarani ili atege abiria wenye haraka anakuwa anaact Kama gari ndio linaondoka .

Yani daladalawana mambo yao na hawatabadilika hata wewe tukikupa uendeshe utakuwa Kama wao tu maana ukikaa kotuoni hauchekechi gari au kuziba barabara ili uchukue vichwa juu kwa juu hautapata abiria fasta.

Kuna wakati nilipomaliza form six nilikuwa naendesha coaster ya home nilijikuta nakuwa dereva mhuni tu maana hakuna namna na konda ndio anakula maelekezo usimame wapi maana yeye ndio anakusanya hela anajua hesabu ipoje.

Noma sana hiyo kazi ni sawa na ukianza kuendesha bodaboda utajikuta unakuwa mwehu tu.
Kwa hiyo hapa tuwatetee waendeleze uhuni?!
 
Kwa hiyo hapa tuwatetee waendeleze uhuni?!
Nimetoa hali halisi ya wao wanavyooperate, nimeona Kama solution iliyosemwa haiwezi kuwa na msaada wa kupunguza foleni.
Mie nadhani ili wasipaki vibaya lazima turudishe Ile kampuni walikuwa wanakamata daladala zikipaki vibaya wanapiga fine.

Ile ilisaidia sana kuwanyoosha
 
Na watanuaji wanaojifanya wana haraka sana kuliko wenzao walioko kwenye foleni ndiyo zaidi. Hasa zile barabara zenye service roads.
 
Moja ya sababu kubwa inayochangia foleni majira ya asubuhi na jioni kwenye barabara nyingi za Dar es salaam ni ufinyu wa VITUO VYA DALADALA.

Kusema kweli VITUO VYA DALADALA jijini Dar es salaam ni vifinyu sana kiasi kwamba havitoshelezi DALADALA angalau 5 kuegesha kwa pamoja ili kushusha abiria.

Mbali na ufinyu huo pia, ipo tabia ya baadhi ya madereva wa daladala kupenda kupakilia abiria nje ya vituo hasa MWANZO na MWISHO wa kituo sehemu ambayo ni nje ya kituo suala hili husababisha msongamano mkubwa wa magari mengine kwa kuwa daladala hilo kufunga upande mmoja wa barabara kama ni double lane.

Changamoto nyingine ni Madereva wa DALADALA kupakia abiria maeneo ambayo siyo vituo. Kusema ukweli wenzetu wa Polisi kwenye eneo hili la kuwadhibiti madereva wanaopakia abiria maeneo yasiyo vituo wamelifumbia macho.

Hapa nawaza kwamba kama Traffic Police wakifanya kazi yao vema foleni itapungua pakubwa... Madereva wa daladala wadhibitiwe kufuata sheria na wawazoeze abiria kupanda gari kwenye vituo ili kupunguza foleni.
Umesahau watu wa bolt ,pia madereva wengine nao wazembe asubuhi ni rushing hours wao wanaendesha ka ndo wanarudi home
 
Umesahau watu wa bolt ,pia madereva wengine nao wazembe asubuhi ni rushing hours wao wanaendesha ka ndo wanarudi home
Kabisa madereva wa bolt wanaendesha taratibu wanabana bajeti ya mafuta nadhani wanaleta kero sana barabarani
 
Back
Top Bottom