Kinachojiri katika sherehe za mapinduzi ya Zanzibar kutoka uwanja wa Amani

Don san tan

JF-Expert Member
May 23, 2015
562
433

Mapinduzi ya Zanzibar yalitokea mwaka 1964 ili kumuondoa madarakani Sultani wa Zanzibar na serikali yake, iliyoundwa hasa na Waarabu , na hatimaye kuweka uongozi mikononi mwa Waafrika , ambao ndio wengi visiwani humo (230,000 hivi).

Tarehe 12 Januari 1964 asubuhi na mapema, mwanachama wa ASP John
Okello ( 1937 - 1971 ?) kutoka Uganda aliongoza wanamapinduzi 600–800 wa kisiwa kikuu cha Unguja kushinda polisi wa nchi na kuteka silaha zao. Halafu walielekea Zanzibar Town walipompindua Sultani Jamshid bin Abdullah na serikali yake.

Kiongozi wa ASP Abeid Karume ,asiyekuwa na msimamo mkali akawa rais wa kwanza wa nchi.
Karume alifanikisha majadiliano ya kuunganisha Zanzibar na Tanganyika ili kuunda hatimaye muungano wa Tanzania.

Mapinduzi yalikomesha miaka 200 ya utawala wa Waarabu Zanzibar, na yanaadhimishwa kila mwaka kama sikukuu ya taifa zima la Tanzania.

Karibuni kuweka Updates za kuhusu kinachojiri kisiwani humo, leo ikiwa ni Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sherehe ambazo mgeni rasmi atakuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Rais Dr. Ally Mohamed Shein.

Nawatakia kumbukumbu njema katika Sherehe hizo za mapinduzi ikiwa leo ni tar 12/1/2017.
 
Ndugu zangu,JK bado yupo mioyoni mwa watu wengi.

Leo alipowasili hapa Zanzibar kwenye sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar, watu waliona kama Mungu ameshuka. Furaha, bashasha, nderemo, hamu, na joto la watu lilipanda ghafla.

Hata kwangu mm, moyo wangu leo umesuuzika vyema.Nina amani ya moyo japo sina pesa.Sina biashara na huyu Mh Rais Mtaafu, sijawahi kuteuliwa nae, sijawahi fanya nae kazi.Yaani basi tu.

Asante JK
 
Huyo ndiye alisimamia uporaji wa kura huku bara na huko zanzibar, wanaomshangilia ni jecha na familia ya jecha
 
Hizi sherehe zinanishangaza kweli jamani hizi ni sherehe za CCM ama.
Maana haya mapinduzi hayana maana tena
Ni nchi gani inayosherehekea umwagaji wa damu na mapinduzi yasiyo na maana?
Eti mapinduzi matukufu kweli? Kuna kitu behind the scene
 
Hizi sherehe zinanishangaza kweli jamani hizi ni sherehe za ccm ama.
Maana haya mapinduzi hayana maana tena
Ni nchi gani inayosherehekea umwagaji wa damu na mapinduzi yasiyo maana?
Eti mapinduzi matukufu kweli? Kuna kitu behind the scene
CCM kila kitu chao hata siku ya Uhuru ni CCM siku ya ukimwi ni CCM
 
Jamani kumbee hii siku ni ya CCM nlkuwa sijajua na kuishi kwangu kotee kwa maana hiyo watu hawaendi makazini kwa ajili ya sikukuu ya kichama na siyo kitaifa? Maana naona sare ya hapa ni kijani tuuu
 
Wanajamvi:

Kama mmekuwa mkifuatilia hizi sherehe mbali mbali za kitaifa na pia mmekuwa mkifuatilia wakati wa tukio la salamu za kijeshi kwa viongozi ama salamu za maafisa wetu wa kijeshi kwa viongozi wa kitaifa. Mtakubaliana na mimi huwa wanatoa heshima hizo kizembe sana ama kiulegevu sana. Hasa wale wenzetu wa kule........

Leo hii kama kuna mtaalamu ajaribu kurejesha kuweka salute aliyopiga mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Tanzania General Davis Adolf Mwamunyange, utagundua ni kweli yeye ni mtu sahihi kuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama. Mara aliposhuka katika gari yake special car alipoanza kupokea heshima ya salute kwa junior officer wake waliojipanga kumpokea.

Kila salute aliyoitoa kama ishara yakupokea salute za subordinate wake ilikuwa speed & accuracy, mkono ulipanda na kushuka kwa speed na kwa usahihi wa hali ya juu, mkono wake ulilinganga na miishilio ya miimo ya kofia yake bila kukosea na bila kuangalia, mwili wake ukiwa umetulia kimya bila kuyumba, wala ku-ben popote. alinyooka kama namba moja. mkono peke yake ndiyo uliokuwa ukipanda na kushuka na kuonyesha ukakamavu na weledi wa hali ya juu.

Na amekuwa akirudia salute hiyo kwa usahihi uleule kwa kila afisa na kiongozi wa kitaifa aliyekutana naye. Huku mkono wake wa kushoto ukiwa umekunjwa vizuri ile nusu ngumi ya ukakamavu kama fumba lenye kiashirio cha kuficha kitu ndani ya mkono. Huku kidole chake gumba kikiwa kimelala sawasawa na mguu wake wa kushoto akiwa mguu sawa.

Maafisa wengine wa majeshi yetu jifunzeni salute aliyopiga mkuu wa majeshi leo siku ya tar.12, January,2017. kwenye sherehe za muungano. Mnatia aibu hapo kuna mabalozi wa nchi za nje na viongozi wengine foreigners delegates wanaona weakness zetu. Senior officers wa vyombo vyetu vya usalama wanapiga salute mwili wote unayumba, wana-ben muelekeo wa salute wanapopiga na pia ule mkono wanapanda nao na kushuka yaani wanaufuata.

Kwa askari wa dogo hatuna shaka nao kabisa tena majeshi yote wako fit, lakini hawa senior officers wakuhesabu nini kinachowaangusha au ni vyeo na madaraka?. Basi mkuu akiona inafaa awatume vijana wake akawa-train. TUNAOMBA CDF AONGEZEWE TENA MUDA
 
Habari jf
Mwenye uwelewa wa mambo ya kijeshi atusaidie,
Kwata ya kimya kimya kivita ina mchango gani!!
Au hutumika kwenye kutoa burudani tu!!
 
Back
Top Bottom