FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,793
- 5,372
Ndugu zangu:
· Mtoto anayeitwa Leonard Kipapi alizaliwa tarehe 05.11.2000 tukakabidhiwa tuishi naye akiwa na umri wa siku mbili (2) kufuatia kifo cha mama yake mzazi hapo tarehe 08.11.2000
· Mwezi January 2010 alipelekwa kwa baba yake mzazi huko Njombe kuendelea na shule akiwa darasa la pili
· Juzi tarehe 07.09.2010 nililetewa taarifa kwamba mtoto Leonard amelazwa katika hospitali ya Kibena (Njombe) hoi taabani baada ya kupokea kipigo toka kwa mama yake wa kambo
· Jana asubuhi (tarehe 08.09.2010) mishale ya saa moja (07:20 hours) na dakika ishirini mtoto Leonard alifariki dunia.
· Mazishi yake yanafanyika leo hii tarehe 09.09.2010 huko Njombe.
Nimewashirikisha taarifa hii ili kuonyesha hudhuni iliyonipata baada ya kupigania maisha ya kichanga Leonard hadi kufikia mwaka huu 2010 akiwa na umri wa miaka 10.
Halafu ametokea mtu Mkatili asiye na moyo wa upendo wala huruma akamponda mtoto bila sababu ya msingi hadi kufa.
Huyu ni mama wa Kambo.
Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mtoto wetu mpendwa mahala pema peponi
NB: wapendwa sio mie ..ila yamewatokea ndugu jamaa na rafiki.
· Mtoto anayeitwa Leonard Kipapi alizaliwa tarehe 05.11.2000 tukakabidhiwa tuishi naye akiwa na umri wa siku mbili (2) kufuatia kifo cha mama yake mzazi hapo tarehe 08.11.2000
· Mwezi January 2010 alipelekwa kwa baba yake mzazi huko Njombe kuendelea na shule akiwa darasa la pili
· Juzi tarehe 07.09.2010 nililetewa taarifa kwamba mtoto Leonard amelazwa katika hospitali ya Kibena (Njombe) hoi taabani baada ya kupokea kipigo toka kwa mama yake wa kambo
· Jana asubuhi (tarehe 08.09.2010) mishale ya saa moja (07:20 hours) na dakika ishirini mtoto Leonard alifariki dunia.
· Mazishi yake yanafanyika leo hii tarehe 09.09.2010 huko Njombe.
Nimewashirikisha taarifa hii ili kuonyesha hudhuni iliyonipata baada ya kupigania maisha ya kichanga Leonard hadi kufikia mwaka huu 2010 akiwa na umri wa miaka 10.
Halafu ametokea mtu Mkatili asiye na moyo wa upendo wala huruma akamponda mtoto bila sababu ya msingi hadi kufa.
Huyu ni mama wa Kambo.
Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mtoto wetu mpendwa mahala pema peponi
NB: wapendwa sio mie ..ila yamewatokea ndugu jamaa na rafiki.