Kina Kaka: Kati ya hivi viwili....

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,930
Kati ya Hivi viwili, wewe ungekula kipi?

Swali hili nalipanga, lawahusu kina kaka,
Nalipanga kwa kutunga, kwa beti za uhakika,
Ni miye gwiji malenga, wa kijiji nimefika,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Ni kisa kimenikuta, miye nikatatizika,
Siku chache zilopita, Jenifa kanialika,
Kwa haraka kama ndata, gia nikazichomeka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

“Karibu mtu wa shamba”, bibiye akatamka,
Mkono kama kwa kamba, kizingiti nikaruka,
Sebule yenye kutamba, kapanga ikapangika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Kaaga kwenda jikoni, na nyuma akageuka,
Nkajikuta taabani, dada kweli kaumbika,
Nikanguruma tumboni, na njaa ikanishika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Moyo ukaenda mbio, akili zikaniruka,
Nikatafuta pambio, kuituliza mizuka,
Nikasema leo ndiyo, ujanja umenitoka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Karudi kajiandaa, kanga moja kafunika,
Nikabaki kushangaa, ni nini anachopika,
Nikatamani chang’aa, mifukoni nikashika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Twende chemba wa kijiji, vitafunwa nimeweka,
Si vya chai wala uji, nikazidi weweseka,
Na ushamba wa kijiji, ute ukanidondoka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Chagua chako kimoja, ukile mpaka kuchoka,
Dada akatoa hoja, meza akaiandika,
Nikila hicho kimoja, kingine kitaondoka,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Vitumbua ni viwili, sambusa moja kaweka,
Vyote havina shubili, ni vitamu vya hakika,
Hanipi vyote viwili, kimoja ametamka,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Kwa ufundi wa maneno, hoja nikazitamka,
Napenda vyote vinono, kwani miye navitaka,
Kanijibu kwa mguno, kimoja akakishika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Hamu yote ikatoka, ya njaa iliyoshika,
Viwili vyote nataka, msimamo kaushika,
Nikasema naondoka, naenda kwake Jessika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Siku chache zimepita, bado nimeghadhibika,
Alileta ya kuleta, na masharti ya kushika,
Kama njaa inaita, vyakula vyote nataka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
 
kijiji nami nakuja, nnaingia uwanjani
nakuja na kiunguja, na lahaja za kipwani
tamaliza yako haja, inokupa mtihani


ikiwa mpenda chumvi, sambusa itakufaa
huchapuzwa tangawizi, nyama kusaga murua
pia pili pili mbuzi, na ndimu ilokolea

amini takula sana, binti tamwita tena
ule huku ukipuma, na kutaja lake jina
ukae ukisimama, kwa raha utazoona

ikiwa mtu wa sukari, kitumbua ni chaguo
utakula kwa fahari, tena bila gugumio
chukua na tahadhari, usije toka umio

kijiji leo yatosha, haya niliokujuvya
usikae ukikesha, domo mate kulirovya
chukua kilichokukosha, si vyema kudovya dovya
 
Kati ya Hivi viwili, wewe ungekula kipi?

Karudi kajiandaa, kanga moja kafunika,
Nikabaki kushangaa, ni nini anachopika,
Nikatamani chang’aa, mifukoni nikashika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Vitumbua ni viwili, sambusa moja kaweka,
Vyote havina shubili, ni vitamu vya hakika,
Hanipi vyote viwili, kimoja ametamka,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Kwa ufundi wa maneno, hoja nikazitamka,
Napenda vyote vinono, kwani miye navitaka,
Kanijibu kwa mguno, kimoja akakishika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Hamu yote ikatoka, ya njaa iliyoshika,
Viwili vyote nataka, msimamo kaushika,
Nikasema naondoka, naenda kwake Jessika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Siku chache zimepita, bado nimeghadhibika,
Alileta ya kuleta, na masharti ya kushika,
Kama njaa inaita, vyakula vyote nataka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)

Mzee Mwanakijiji, mie ningesusa kama wewe maana vyote ninavitaka.
 
Kati ya Hivi viwili, wewe ungekula kipi?

Swali hili nalipanga, lawahusu kina kaka,
Nalipanga kwa kutunga, kwa beti za uhakika,
Ni miye gwiji malenga, wa kijiji nimefika,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Ni kisa kimenikuta, miye nikatatizika,
Siku chache zilopita, Jenifa kanialika,
Kwa haraka kama ndata, gia nikazichomeka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

“Karibu mtu wa shamba”, bibiye akatamka,
Mkono kama kwa kamba, kizingiti nikaruka,
Sebule yenye kutamba, kapanga ikapangika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Kaaga kwenda jikoni, na nyuma akageuka,
Nkajikuta taabani, dada kweli kaumbika,
Nikanguruma tumboni, na njaa ikanishika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Moyo ukaenda mbio, akili zikaniruka,
Nikatafuta pambio, kuituliza mizuka,
Nikasema leo ndiyo, ujanja umenitoka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Karudi kajiandaa, kanga moja kafunika,
Nikabaki kushangaa, ni nini anachopika,
Nikatamani chang’aa, mifukoni nikashika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Twende chemba wa kijiji, vitafunwa nimeweka,
Si vya chai wala uji, nikazidi weweseka,
Na ushamba wa kijiji, ute ukanidondoka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Chagua chako kimoja, ukile mpaka kuchoka,
Dada akatoa hoja, meza akaiandika,
Nikila hicho kimoja, kingine kitaondoka,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Vitumbua ni viwili, sambusa moja kaweka,
Vyote havina shubili, ni vitamu vya hakika,
Hanipi vyote viwili, kimoja ametamka,
Vitumbua na sambusa, wewe ungekula kipi?

Kwa ufundi wa maneno, hoja nikazitamka,
Napenda vyote vinono, kwani miye navitaka,
Kanijibu kwa mguno, kimoja akakishika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Hamu yote ikatoka, ya njaa iliyoshika,
Viwili vyote nataka, msimamo kaushika,
Nikasema naondoka, naenda kwake Jessika,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

Siku chache zimepita, bado nimeghadhibika,
Alileta ya kuleta, na masharti ya kushika,
Kama njaa inaita, vyakula vyote nataka,
Vitumbua na Sambusa, wewe ungekula kipi?

M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)

Mkuu Mzee Mwanakijiji, Hii Sambusa ni ile ya Nyama au ya Viazi?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom