Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 36,570
- 44,227
January, Nape, Muhongo na wengine wa aina yenu fahamuni kwamba legacy ya Magufuli ndani ya chama imewafunika sana na hamtaweza kuizidi. Hamtaweza kuwashawishi wenzenu walio wengi kwamba Legacy ya Magufuli sio "special" tofauti na legacies za wenzake waliomtangulia.
Juzi na jana mmeongea kwa kuzunguka, uchungu na tahadahari sana katika mkutano wa bunge unaoendelea. Watoto wa mjini kama wanasema mmetanguliza mpira mkutane nao kwa mbele "long game" mkitaka kuwaaminisha wabunge wengine kwamba hizi ni zama za kitabu kipya na hakuna haja ya kung'ang'ana na yaliyopita. Haikuchukua muda mrefu mliyapata majibu yenu kutoka kwa Gwajima leo.
Ukiachana na Muhongo hahiitaji wachambuzi wa wabobevu mahiri wa siasa kufahamu nyinyi wengine ambao wakati fulani mlidukuliwa mkimsengenya mwendazake mnafanya hivyo kwa sababu mna malengo makubwa zaidi ya ubunge katika uongozi wa nchi siku za mbeleni.
Zaidi sana mlikuwa hamkubalini kwa kiasi kikubwa na sera za serikali iliyopita lakini mnafahamu jinsi gani serikali hiyo ilivyojizolea kundi kubwa la wananchi waliyoimani kupitiliza kiwango cha kuweza kuitwa 'cult'. Hivyo mnajaribu kuchanga karata zenu vizuri kwenda na makundi yote ndani ya chama.
Tanzania ya leo sio ile ya mwaka 2015 kurudi nyuma.Wakati fulani iliitwa ni Tanzania ya Magufuli, huenda sasa sio Tanzania ya Magufuli tena kwa sababu hayupo lakini hii ni Tanzania mpya na Magufuli 'footprints' au alama zake alizoacha ziko kila mahali.
Haitakuwa rahisi kwenu kufikia madaraka makubwa zaidi ya uwaziri kama mtafanikiwa kuendelea kuwa wabunge baada ya 2025, tena ikiwa ni kwa chama chenu.
Muda utazungumza.
Juzi na jana mmeongea kwa kuzunguka, uchungu na tahadahari sana katika mkutano wa bunge unaoendelea. Watoto wa mjini kama wanasema mmetanguliza mpira mkutane nao kwa mbele "long game" mkitaka kuwaaminisha wabunge wengine kwamba hizi ni zama za kitabu kipya na hakuna haja ya kung'ang'ana na yaliyopita. Haikuchukua muda mrefu mliyapata majibu yenu kutoka kwa Gwajima leo.
Ukiachana na Muhongo hahiitaji wachambuzi wa wabobevu mahiri wa siasa kufahamu nyinyi wengine ambao wakati fulani mlidukuliwa mkimsengenya mwendazake mnafanya hivyo kwa sababu mna malengo makubwa zaidi ya ubunge katika uongozi wa nchi siku za mbeleni.
Zaidi sana mlikuwa hamkubalini kwa kiasi kikubwa na sera za serikali iliyopita lakini mnafahamu jinsi gani serikali hiyo ilivyojizolea kundi kubwa la wananchi waliyoimani kupitiliza kiwango cha kuweza kuitwa 'cult'. Hivyo mnajaribu kuchanga karata zenu vizuri kwenda na makundi yote ndani ya chama.
Tanzania ya leo sio ile ya mwaka 2015 kurudi nyuma.Wakati fulani iliitwa ni Tanzania ya Magufuli, huenda sasa sio Tanzania ya Magufuli tena kwa sababu hayupo lakini hii ni Tanzania mpya na Magufuli 'footprints' au alama zake alizoacha ziko kila mahali.
Haitakuwa rahisi kwenu kufikia madaraka makubwa zaidi ya uwaziri kama mtafanikiwa kuendelea kuwa wabunge baada ya 2025, tena ikiwa ni kwa chama chenu.
Muda utazungumza.