Kimeumana: January, Nape na Muhongo; long game yenu haitawasaidia. Legacy ya Magufuli ni kama mbuyu ndani ya chama mlichopo

Ni mtazamo wako mkuu, yaheshimiwe mawazo yako, Ila Kwa mtazamo wa wengine, haya mawazo yako ni ya kipimbi, kijinga na kipumbavu mno

Kwa sababu pia katikati ya dhambi kuna walionufaika na u dhambi huo, na kama tunataka tusiendeleze haya ni Bora kunyamaza
Pslmp sawa ni mawazo yangu ndiyo maana siyo ya kwako. Na nyie ndiyo wanufaika wa mfumo wa Chato.

Sisi tunasimamia ukweli tu kwamba katika historia ya Tanzania mwaka 2015-21 tulipata ajali ya kisiasa kwa kupata Rais kichaa.
 
Kwa wanaojiita wasomi ndo wanasema maneno haya,lakini tujiulize mpo wangapi nchi hii kulinganisha na wasiosoma?
Kukubali mabadiliko ya misimu nayo ni hekima, watanzania wanyonge wamenyongwa miaka 60 sasa,wamechezewa vya kutosha
wakamlilia Mungu akawajibu kwa kuweka mtu aliyeonyesha njia ya kufuata,sasa ni hekima kukubaliana na huu msimu mpya.
Tunapolalamikia katiba mbovu,lazima kuna aliyeitunga,je alikuwa darasa la saba? hapana aliitunga kulinda maslahi yake,Dhidi ya nani?
Dhidi ya mnyonge ambaye asiporidhika akataka kutumia nguvu ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria.
Ni Watanzania wapumbavu tu ndiyo wanakubali kuitwa wanyonge. Na msivyo na akili akiwaita wanyonge mnampigia makofi.

Jiulize ni mnyonge gani amepiga hatua katika miaka 5 ya Mwendazake? Angalia mtaani kwako muuza genge wa 2015 utakuta bado anauza genge. Muangalie shoe shiner bado anapiga kiwi tu! Angalia muosha magari mtaani bado anaosha magari vile vile.

Mwendazake amewatumia kujijenga kisiasa kwa kuwaita wanyonge. Amewapiga vita matajiri, lakini je baada ya tajiri kufilisika ile mali umepata wewe?

Niambie mali ya Yusuf Manji baada ya kufilisiwa nani kapata?

Jikomboeni enyi Watanzania, mumetumika akiwa hai na bado mnatumika akiwa analiwa na funza na minyoo kaburini?
 
Pslmp sawa ni mawazo yangu ndiyo maana siyo ya kwako. Na nyie ndiyo wanufaika wa mfumo wa Chato.

Sisi tunasimamia ukweli tu kwamba katika historia ya Tanzania mwaka 2015-21 tulipata ajali ya kisiasa kwa kupata Rais kichaa.
Mi naona ungesema ajali mbaya sana ya kisiasa
 
Muuza genge, mmachinga, mama ntile na boda boda wameishi raha mustarehe katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Wataendelea kuishi bila kufukuzwa fukuzwa katika awamu hii??
 
Na hapa ndipo napata nguvu kubwa ya kuwashangaa so called wasomi.
Nikupe mfano mdogo tu wa kukufikirisha.
Baharini kuna samaki anaitwa papa,huyu ni mtaalamu wa kukwapua mawindo yakiwemo pomboo wadogo na samaki wengine wakubwa, kumbuka papa anaporalua windo lake kuna minofu midogo inadondoka,na hivyo samaki wadogo ambao wasingeweza kumwangusha pomboo kupata chakula cha kushiba hata wiki nzima na zaidi. Akitokea mvuvi akamvua huyo papa,huwe na uhakika uwezekano wa samaki wadogo kulala njaa ni mkubwa sababu walishaacha kujitafutia chakula kilicho haki yao na kuishi kwa kutegemea makombo ya huyo papa japo ni nje ya mpango wa Mungu. Kwa Mwenye akili hawezi kushangaa akiona samaki mdogo anahaha baada ya papa kuvuliwa.

Back to the point,
Kwa muda mrefu tumeshuhudia wenye nyadhifa serikalini na mashirika ya umma wakikwapua mabilioni,haya waliyatumia kula bata mahotelini(hoteli zilifanya biashara),kujenga majumba(mafundi walilipwa vizuri), kusafiri nje(wasafirishaji walivuna) n.k. sasa walipotumbuliwa,uwe na uhakika na walionufaika lazima wahisi njaa.na huu ndo tunaita msimu mpya

Kwa mjasiliamali halisi aliyekuwa anaishi kwa misingi ya haki,ameshamili sana kipindi hiki cha awamu ya tano.
kwa wale wakwepa kodi na waliobebwa na mfumo uliokuwepo ikiwemo biashara haramu za madawa ya kulevya lazima walalamike.
Kusema vibaya na kutukana hakutasaidia kurudi kwenye mifumo mibaya tuliyokuwa nayo.
Jiongeze,maana wewe ni msomi tafuta"Bribery act'' ya nchi ya uingereza ambao tumewaiga kwa mambo mengi ujionee mwenyewe
mambo yalivyotakiwa kuwa hapa nchini tangu mwanzo lakini tulilala,nchi ikabebwa na wafanyakazi kwa muda mrefu.

Tujifunze kuishi maisha ya kuridhika na kilichohaki yetu na si kujinufaisha kwa haki za wengine tukidhani mifumo hiyo itadumu milele
lazima itatikiswa.
 
January, Nape, Muhongo na wengine wa aina yenu fahamuni kwamba legacy ya Magufuli ndani ya chama imewafunika sana na hamtaweza kuizidi
Wewe naye mduanzi kweli kama yule mbunge, msukuma ,std7
 
Kwahiyo madawa ya kulevya yalizuiwa na Mwendazake? Kweli mnadanganywa Sana.

Drug lords wakubwa Shkuba ma Lwitiko walikamatwa mwaka 2014 kwa surveillance ya FBI/ CIA. Anayeamini kuwa Makonda aliwakamata wafanya biashara wa cocaine/ heroine siyo mwelewa. Makoknda alikamata drug pushers na 'punda'. Wengine aliwadhalilisha ili wampe pesa
 
Eti kujenga daraja, na barabara ambazo hata wakoloni walijenga.

Sikiliza kampeni za watu wanaojua uongozi,, hautasikia barabara na madaraja( ni ulimbukeni sana huo)
 
Tunawasubiri tuwapoteze kwanza kwenye chaguzi za ndani ya CCM mwakani 2022 kabla ya kuwamaliza kabisa 2025! Watabaki kuwa "wanafalsafa za ovyo" kama Prof. Assad!
 
^Hakujali maisha ya watu^!??? Kwa kauli yako hii, naendelea kuthibitisha ukweli wa hoja ya Mbunge wa Mtera iwapo kweli elimu ya Tanzania inawasaidia wengine wa sampuli yako!?

Hivi hiyo miradi ilikuwa kwa ajili ya kuboresha maisha ya miti au watu!??? Umesahau ile mashine iliyokuwa mbovu Muhimbili NH for months, mgonjwa ambaye angefanyiwa check ups & oparesheni amelala miezi sakafuni akiingoja itengenezwe!??? JPM alipotia timu, just in a week mashine ikapona?

Naona unataka viongozi wanaopishana angani kwenda Dubai & Ulaya, siyo!??? Au waleee wasafirisha twiga!??? Nawaambiaga watu kila kukicha: pls heshimuni sana mvi za Mzee Mwinyi.

Kichwa chake ndiyo bayografi ya JPM kwa sasa -- ^Tulishindwa siye kwa miaka 40, yeye kayaweza, tena kwa muda mfupi!^ Niongeze volume, au!???
Ilikuwaje yeye akakimbiziwa Kenya kutibiwa na kuacha hizo hospital unazo zitaja hapa we msukuma?
 
Usijidanganye kirahisi hivyo.Legacy yake uwe unaipenda au unaichukia bado itaendelea kuwa turufu kwenye uwanja wa siasa za Tanzania angalau kwa miaka kumi ijayo.
Jiwe alikua Rais shetani kabisa
 
Tunawaona hao pia wenye mawazo "kinzani". Uzuri wa hao ni kwamba hawawezi kusimama hata bungeni kuongea h
Kuna theory watu wa nje kwa kushirikiana na takataka za ndani zimesababisha kifo chake.
Kwaiyo Yale mabunduki na zile helicopter vilishindwa kumlinda ? What a wastage of national resources
 
Back
Top Bottom