KIMENUKA: Diva atakiwa kumlipa Michael Lukindo Milioni 50 kwa kumdhalilisha

Zakamwamoba

Senior Member
Jul 28, 2016
177
609
DIVA-640x640.jpeg


Msanii wa Bongo fleva na mtangazaji wa Cloud Fm ,Diva Gissele Malinzi maarufu kama "Diva the bawse" ametakiwa kuomba radhi pamoja na kulipa faini ya Tsh.Milioni 50 kwa kosa la kumdhalilisha msanii mwenzake ambaye alikuwa mtangazaji mwenza wa Cloud Fm ,Michael Lukindo.

Diva amepewa agizo hilo na taasisi ya wanasheria ya "East Woods Attorney" ambako Michael Lukindo aliwasilisha madai yake ya kudhalilishwa.

Picha liko hivi
Siku chache zilizopita Michael Lukindo alifanya mahojiano na XXL ya Clouds Fm na alikuwa anatambulisha nyimbo yake mpya ya " Basi Iwe" lakini Kwenye mahojiano hayo alifunguka amewahi kuwa Kwenye Mahusiano na Diva.

Baada ya kusikia taarifa hizo Diva alitumia ukurasa wake wa Instagram na kumwaga povu zito na kukataa kata kata kama yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na Michael Lukindo.

Baada ya Tetesi hizo kusambaa Soudy Brown alimsaka Michael ambaye alikiri kuwa alikuwepo Kwenye Mahusiano na Diva lakini walifanya siri na mpaka sasa Diva hayupo tayari kuzungumzia hayo mahusiano.

Baada ya kusikia maneno hayo Diva ambaye kwa muda huo alikuwa studio alimtolea matusi mazito Michael Lukindo:


“Wewe mata** unikome shika adabu yako umeshawahi kuwa na Mahusiano na mimi lini na wapi?na nilikwambia kabisa kwamba nimekushtaki I have defamation letter for you utajifunza kufunga huo mdomo wako sitaki mambo ya kise*** k*** la mama ako umeenda umemzungumzia Jokate on the same same thing haukutosheka ukamuandika Miriam Odemba kuwa una Mahusiano naye sasahivi unataka kwangu mimi kunitafutia kiki sasa mimi ntakukomesha nimeshakushtaki”.

"East Woods Attorney" wamemwamndikia barua Diva ambapo wamemtaka amwombe msamaha mteja wao Michael Lukindo pia amlipe Tsh .Milioni 50 . Diva ametakiwa kufanya hayo ndani ya siku 14 kuanzia tarehe 19 April ,2018.Akishindwa kufanya hayo hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa

Hii hapa barua aliyoadnikiwa Diva na wanasheri wa Michael Lukindo.



 
Halafu wanawake wengine huwa hawajielewi kabisaa hata kama leo umemuona wa kazi gani sio kumtusi mwanaume alioona uchi wako namna hyo. Ndo maana hamuolewi kwa tabia zenu mbaya kama hizi. Kama alikukula alikukula tuu hata kama leo unakataa kwa matusi. Hata kama umepata bwana mwingine mpya usimkashfu wa zamani.
 
Bravo Wa ea radio, informer Wa clouds,,,jamaa haeleweki kabisa unabishana na mpuuzi kama huyo, umeniangusha sana
 
Huyu dada kwanza sipendagi lipua lake, pili anatafutiwa sababu akaungane na baba yake Malinzi, maana za chini ya kapeti wooote waliokuwa karibu na Malinzi wanaunganishwa kwenye kesi kimya kimya.....binti anpotea huyu ohooo. kama unamdai mautamu malizana nae kabisa, isije kuwa kama kwa Lulu. kaenda jelakaacha watu wanamdai papuchi maana waliweka booking 3 months before.
 
Back
Top Bottom