Kimbisa nani kakutuma kwenda kujipendekeza kwa Kenyatta?

K-Boko

JF-Expert Member
Aug 3, 2013
697
218
Jana Adam Kimbisa kwa kutumia kofia yake ya mbunge wa Afrika Mashariki alikuwa akijiapiza kwa mbwembwe mbele ya Rais Kenyatta kuwa katika suala la ICC "(Watanzania) tulikuwa na wewe, tumekuwa na wewe na tutaendelea kuwa na wewe"! Hivi ni nani aliyemtuma Kimbisa kufanya ujinga ule?
 
Wewe unashangaa ya Kimbisa? Hushangai ya Rais wake Kimbisa na serikali yake?.

Naamanisha jinsi JK na serikali yake anavyoicheza hiyo ngoma ya ICC kwa kujaribu kumjengea wigo mpana kupinga mkono wa ICC (sheria) dhidi ya hao hao akina UhuRuto?

In fact JK amefanya 'shuttle diplomacy' nchi mbalimbali na ku advocate kesi ya akina UhuRuto kwenye majukwaa mbalimbali ya kimataifa mpaka kutuma Attorney General wake awaandikie ICC. Wanachi wanabakia wanajiuliza yote haya kwa pesa za WaTanzania ili iweje? Badala kujikita kwenye kutatua kero za Wananchi wake.

Halafu cha ajabu zaidi na kushangaza hapo hapo anakuja kulia faulu bungeni kuwa nchi yake inatengwa (sidelined) na genge hilo hilo la akina UhuRuto & Co.

WaTanzania makini wanajiuliza Rais huyu anajielewa na kujitambua kweli? Ndio maana pamoja na kuwa taifa kubwa katika ukanda wa EAC lakini hata vinchi vidogo vinatuiona kuwa sisi ni taifa 'Kubwa Jinga" flani hivi kwa kukosa staili na kutokujua kusema hatutaki kutumiwa. Tuna dhana ya kutaka ku furahisha watu kwa misifa ya kijinga wakati mwingine. Na sasa hata majirani hawa wamejenga dhana ya madharau kuwa akili za Wabongo wote ni kama viongozi wao tu.
 
Wewe unashangaa ya Kimbisa? Hushangai ya Rais wake Kimbisa na serikali yake?.

Naamanisha jinsi JK na serikali yake anavyoicheza hiyo ngoma ya ICC kwa kujaribu kumjengea wigo mpana kupinga mkono wa ICC (sheria) dhidi ya hao hao akina UhuRuto?

In fact JK amefanya 'shuttle diplomats' nchi mbali mbali na kuliongelea suala hilo kwenye majukwaa ya kimataifa na mpaka kutoma Attorney General wake awaandikie ICC. Unabakia unajiuliza yote haya kwa pesa za WaTanzania ili iweje?

Halafu cha ajabu zaidi na kushangaza hapo hapo anakuja kulia faulu bungeni kuwa nchi yake inakuwa 'sidelined' na genge hilo hilo la akina UhuRuto.

WaTanzania makini wanajiuliza Rais huyu anajielewa na kujitambua kweli?

Inakera sana sana! Ni sawa na ile ya kupenda usipopendwa!! Hawa jamaa, in fact, wanatushangaa sana maana tunaicheza ngoma tusoipiga!!
 
Back
Top Bottom