Kimbembe cha mahabusu

Mserengeti

Member
Mar 1, 2007
18
0
Kimbembe:Mahabusu Dar wazua zali upyaa!

2007-10-02 17:05:12
Na Mwandishi Wetu, Jijini


Baada ya kutuliza boli kwa muda, mahabusu Jijini Dar es Salaam wameanzisha zali upyaa kwa kutia ngumu kushuka kutoka kwenye karandinda na kwenda kortini.

Kimbembe hicho kimeanza leo asubuhii ambapo mahabusu kutoka gereza la Keko waling`ang`ania kwenye makarandinga yao huku wakifoka kwa kusema, `safari hii hakitaeleweka hadi tupewe haki zetu `.

Licha ya mapolisi kuwalilia wakiwataka washuke na kwenda kortini, waliendelea kukomaa huku wakiwarushia makombora ya tuhuma kibao.

Mahabusu hao ambao huanza kushushwa katika Mahakama ya Mwanzo na ya Wilaya ya Temeke kabla ya kusambazwa kwenye mahakama nyinginezo Jijini, waliwaliza polisi kwa kukataa amri yao ya kuwataka washuke kwenye karandinga ili waende kortini.

Badala yake, mahabusu hao waliokuwa wamejazana tele wakawa wakizomea na kupiga kelele za kila aina.

Kisha kwa umoja wao wakawa wakiimba nyimbo za kukumbushia madai yao ya kutaka watendewe haki kwa kesi zao kusikilizwa na hatimaye waweze kupata dhamana badala ya kuendelea kusota rumande.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo lililozua zogo la aina yake pale Temeke, ni kwamba mahabusu hao toka Keko walikuwa wakiimba nyimbo za kuilalamikia Serikali juu ya kuahirishwa kwa kesi zao kila kukicha na wakati huohuo, wakawa wakisisitiza kuwa wanataka kuonana na Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema.

`Tumechoshwa, tunataaaka?.haki yeetu!` mahabusu hao wakasikika wakiimba kwa jazba huku wengine wakipunga makaratasi yenye ujumbe unaofafanana na huo.

Katika madai yao, mahabusu hao wamekumbushia sababu zilezile zilizowafanya wawahi kugoma mwanzoni mwa mwaka huu, ambazo ni pamoja na kutaka haki ya kusikilizwa fasta-fasta kwa kesi zao ambazo wamedai zimekuwa zikiahirishwa kila mara kwa maelezo kuwa `upelelezi bado haujakamilika`.

`Tunakabiliwa na matatizo kibao huko mahabusu, haki hakuna kabisaaa tunamtaka Waziri Mkuu (Lowassa), Waziri Nagu na IGP Mwema ili tuwaeleze kuwa hakuna kilichofanyika kati ya wale waliyowahi kuahidi,`akasema mmoja wa mahabusu hao aliyekuwa akizungumza kupitia kwenye nondo za karandinga.

Walipoamriwa na polisi kushuka kwenye karandinga, mahabusu hao toka Keko waliendelea na msimamo wao na kudai kuwa hata wakirejeshwa lupango, pia hawatashuka na watang`ang`ania kukaa ndani ya karandinga hadi waonane na viongozi wanaowataka.

Hata hivyo, wakati mahabusu wa Keko wakigoma kutinga kortini leo, wenzao wa magereza ya Ukonga na Segerea walishuka kama kawaida na shughuli za mahakama ziliendelea kama zilivyopangwa.

Wakati wa mgomo kama huo mwanzoni mwa mwaka huu, mahabusu walitoa madai kadhaa, kubwa likiwa ni kusikilizwa haraka kwa kesi zao.

Walichukua hatua hiyo ikiwa ni siku chache tu baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Kapteni Mstaafu Ditopile Mzuzuri kuweza kuachiwa kwa dhamana katika kesi yake ya kutuhumiwa kumuua dereva wa daladala.

SOURCE: Alasiri



mwamko sasa umehamia hadi magerezani,i wish wakati wanaimba wangemtajakaramagi na buzwagi
 
haki ni kwa viongozi na sio kwa walalahoi,nafikiri viongozi wetu wakae mkao wa kula maana sasa ni zamu yao kuingia huko si kutesa kwa zamu.hivi hakuna uwezekano wa kuwarundika wabunge wote wa ccm pamoja na mawaziri wao japo kwa wiki tu ili wakitoka huko wawa wamebadilika na kusimamia sheria kisawa sawa
 
...inaonekana jinsi serikali hii isivyowajibika na hakuna kazi wanayofanya zaidi ya kula rushwa tuu na uzembe na sio hapo tuu pameoza nendeni kwenye mafao ya wastaafu wanavyosota kwa sababu kama vile file lako halionekani kumbe ni rushwa tuu...kuna haja ya kusafisha kila kitu na ushahidi hakuna haki ni jinsi wafungwa wenye makosa sawa ni ditopile wako rumande kwa miaka zaidi ya mitano bil kesi kusikilizwa kwa uzembe tuu....na huyu Waziri wa sheria sijui mahakama inabidi ajiuzulu kwa kushindwa kazi,yaani ni uozo baada ya uozo na ni hawa viongozi ndio wanaosababisha yote haya
 
huu moto wa safari hii natamani uwe mkali zaidi,
mahabusu wooote Tanzania waungane na wagome kama walivyofanya wenzao wa keko na wasikubali suluhu hewa safari hii,
wananchi wakazane kuzomea viongozi wabovu popote watakapoenda kwenye mikutano na hasa watakapokuwa wanasema uongo,
wafanyakazi wasikubali hadi kieleweke kuhusu maslahi yao,
Maovu mengi ya serikali yazidi kuanikwa ili wakose mlango wa kutokea.
 
JK hizo pesa za safari na yale mashangingi ya wabunge karibu mia tano si bora wangetrain mahakimu wengi zaidi ili kesi zisikilizwe watu wapate haki zao...hii kitu ya kukaa jela is very destructing,niliwahi kuwekwa ndani jela Marekani just for some hrs lakini moto niliuona huko kichwani...sasa ukiniambia yrs bila kesi kusikilizwa kwa kweli i feel these bro's
 
JK hizo pesa za safari na yale mashangingi ya wabunge karibu mia tano si bora wangetrain mahakimu wengi zaidi ili kesi zisikilizwe watu wapate haki zao...hii kitu ya kukaa jela is very destructing,niliwahi kuwekwa ndani jela Marekani just for some hrs lakini moto niliuona huko kichwani...sasa ukiniambia yrs bila kesi kusikilizwa kwa kweli i feel these bro's

pole sana,koba.ama kweli humu JF tupo mchanganyiko tosha
 
Mbona kesi ya Dito ilisikilizwa haraka na yeye yupo nnje anakula maisha na kuuza asali? Kwani mahakimu hao walitoka wapi? Huu ni unyanyasaji tuu na hao jamaa waendelee kugoma hadi kieeleweke. Kwanza idara ya mahakama imejaa sana rushwa hapo Tanzania. Japo mahakimu ni wachache lakini wakifanya kazi kwa uaadilifu mahabusu wasingeteseka bila sababu.

Lakini kamashara ka TSH 1500 (USD 130) kwa mwezi unafikiri haya yatawezekana?
 
Kipindi kama hiki kilikuwa kinafaa sana iwapo wafanyakazi nao wangeibua tena madai yao na kuandamana tena, ungekuwa mseto mtamu sana; Maana unachukua List of shame, unaongeza Buzwagi, mgomo wa mahabusu na kisha mgomo wa wafanyakazi!! patamu hapo!!!

Ila mimi bado nina wasiwasi na suala la msimamo na uimara wa wafanyakazi katika kutetea maslahi yao, hasa msimamo wa huyu Katibu Mkuu wa TUCTA, anaonekana kama hajiamini vile na kana kwamba ni Yuda Eskarioti. Au ninyi mnamwonaje?
 
Mbona kesi ya Dito ilisikilizwa haraka na yeye yupo nnje anakula maisha na kuuza asali? Kwani mahakimu hao walitoka wapi? Huu ni unyanyasaji tuu na hao jamaa waendelee kugoma hadi kieeleweke. Kwanza idara ya mahakama imejaa sana rushwa hapo Tanzania. Japo mahakimu ni wachache lakini wakifanya kazi kwa uaadilifu mahabusu wasingeteseka bila sababu.

Lakini kamashara ka TSH 1500 (USD 130) kwa mwezi unafikiri haya yatawezekana?

Mtoto wa Mkulima uliondoka lini huku Tanzania? Sasa hivi dola moja hapa Tanzania inaelelea kwenye Tsh 1500, na sio Tsh 1500 ni dola 130. Lakini hata hivyo unachosema kina ukweli ndani yake, mahakimu wengi wanapokea mshara mdogo sana na kushawishika kupokea rushwa na kupindisha sheria.
Ya Ditto ni Simple and clear, yeye mtu Mkubwa hawezi kukaa mahabusu, ilibidi mahakimu wapatikane na mengine yote yashughulikiwe ili issue iishe. Hao mahabusu watapiga kelel sana na wataishia tu huko huko na hakuna litakalofanikiwa, sana sana wasubiri FFU wakawatie mkong'oto. This is Tanzania Bwana.
 
Mtoto wa Mkulima uliondoka lini huku Tanzania? Sasa hivi dola moja hapa Tanzania inaelelea kwenye Tsh 1500, na sio Tsh 1500 ni dola 130. Lakini hata hivyo unachosema kina ukweli ndani yake, mahakimu wengi wanapokea mshara mdogo sana na kushawishika kupokea rushwa na kupindisha sheria.
Ya Ditto ni Simple and clear, yeye mtu Mkubwa hawezi kukaa mahabusu, ilibidi mahakimu wapatikane na mengine yote yashughulikiwe ili issue iishe. Hao mahabusu watapiga kelel sana na wataishia tu huko huko na hakuna litakalofanikiwa, sana sana wasubiri FFU wakawatie mkong'oto. This is Tanzania Bwana.

Bongo lander sorry nilimaanisha TSH 150,000 (laki moja na hamsini)= USD 130 (mia moja thelathin.

mkuuu nakubaliana na wewe waache wagome tuu hata kama ni vizungu wapigwe lakini siku moja kilio chao kitasikika kama sio na serikali basi hata jumuiya ya kimataifa.
 
Back
Top Bottom