Kimara imeikosea nini Serikali?

instagram

JF-Expert Member
May 27, 2014
2,091
4,715
Kimara ni eneo ambalo limekua kwa kasi tangu kipindi cha Mwinyi hadi Mkapa, Kikwete na Magufuli kuliko maeneo mengine yote lakini hadi leo hakuna barabara za ndani za lami.

Ukiondoa kipande cha kutoka Baruti kwenda chuo kilichokamilika juzi, kuanzia Ubungo hadi Mbezi hakuna barabara za ndani zenye lami isipokuwa kipande kidogo cha kilomita 2 kinachotokea Kimara Temboni na kuelekea nyumbani kwa bosi wa TANROADS ndugu Mfugale.

Huyu Mfugale ambaye kasifiwa na bosi wake hadi kuzawadiwa jina la flyover ya Buguruni kwa ushujaa wa kuwanyima wana Kimara wenzie barabara na kujipendelea yeye mwenyewe. Huu ubinafsi wa mtu kujipendelea kwake kwanza kama taifa unatupeleka pabaya mtu anapongezwa badala ya kutumbuliwa.

Kimara ilianza kuchangamka kitambo kabla ya Kinyerezi, Lumo, Goba, Segerea, Tegeta lakini wenzetu wameendelea kimiundombinu kuliko Kimara ni ubishini kuliko maeneo hayo
 
Kimara ni eneo ambalo limekua kwa kasi tangu kipindi cha mwinyi hadi mkapa, kikwete na magufuli kuliko maeneo mengine yote lakini hadi leo hakuna barabara za ndani za lami. Ukiondo kipande cha kutoka baruti kwenda chuo kilichokamilika juzi, kuanzia ubungo hadi mbezi hakuna barabara za ndani zenye lami isipokuwa kipande kidogo cha kilomita 2 kichacho tokea kimara temboni na kuelekea nyumbani kwa bosi wa tanroad ndugu mfugale. Huyu mfugale ambaye kasifiwa na bosi wake hadi kuzawadiwa jina la flyover ya buguruni kwa ushujaa wa kuwanyima wana kimara wenzie barabara na kujipendelea yeye mwenyewe.. Huu ubinafsi wa mtu kujipendelea kwake kwanza kama taifa unatupeleka pabaya mtu anapongezwa badala ya kutumbuliwa.
Kimara ilianza kuchangamka kitambo kabla ya kinyerezi, lumo, goba, segerea, tegeta lakini wenzetu wameendelea kimiundo mbinu kuliko kimara ni ubishini kuliko maeneo hayo

Sasa kama kumbe nia yako Kuu ilikuwa ni Kumzungumzia Injinia Mfugale kwani umezunguka sana hadi unatuchosha huku ukijifanya unawahusisha wana Kimara wote utadhani labda wote waishio Kimara huko wana Chuki na huyo Mfugale wako kama ambavyo Wewe bila Kificho unaonekana unamchukia na wala hukupenda jinsi alivyosifiwa na Boss wake.
 
Sasa kama kumbe nia yako Kuu ilikuwa ni Kumzungumzia Injinia Mfugale kwani umezunguka sana hadi unatuchosha huku ukijifanya unawahusisha wana Kimara wote utadhani labda wote waishio Kimara huko wana Chuki na huyo Mfugale wako kama ambavyo Wewe bila Kificho unaonekana unamchukia na wala hukupenda jinsi alivyosifiwa na Boss wake.
Kwaiyo wewe hujakubaliana kwamba kimara kuna tatizo la barabara, sasa ukiongelea barabara muhusika ni nani?
 
Kimara ni eneo ambalo limekua kwa kasi tangu kipindi cha Mwinyi hadi Mkapa, Kikwete na Magufuli kuliko maeneo mengine yote lakini hadi leo hakuna barabara za ndani za lami.

Ukiondoa kipande cha kutoka Baruti kwenda chuo kilichokamilika juzi, kuanzia Ubungo hadi Mbezi hakuna barabara za ndani zenye lami isipokuwa kipande kidogo cha kilomita 2 kinachotokea Kimara Temboni na kuelekea nyumbani kwa bosi wa TANROADS ndugu Mfugale.

Huyu Mfugale ambaye kasifiwa na bosi wake hadi kuzawadiwa jina la flyover ya Buguruni kwa ushujaa wa kuwanyima wana Kimara wenzie barabara na kujipendelea yeye mwenyewe. Huu ubinafsi wa mtu kujipendelea kwake kwanza kama taifa unatupeleka pabaya mtu anapongezwa badala ya kutumbuliwa.

Kimara ilianza kuchangamka kitambo kabla ya Kinyerezi, Lumo, Goba, Segerea, Tegeta lakini wenzetu wameendelea kimiundombinu kuliko Kimara ni ubishini kuliko maeneo hayo

Kumbuka yafuatayo:-
1. Kimara-Mbezi ni squarter ie hakujapimwa na hivyo hakuna barabara iliyokidhi vigezo vya lami sawa na tegeta.
2.miundombinu haikidhi matakwa ya kuwekwa lami, maeneo mengi ni maeneo ya raia.
3.wamejaa wachaga
 
Kumbuka yafuatayo:-
1. Kimara-Mbezi ni squarter ie hakujapimwa na hivyo hakuna barabara iliyokidhi vigezo vya lami sawa na tegeta.
2.miundombinu haikidhi matakwa ya kuwekwa lami, maeneo mengi ni maeneo ya raia.
3.wamejaa wachaga
Hv umepita mwananyamala mbona skwata zaidi na kumewekwa vilami japo vyembambaa
 
Nilishakuandalia points za kukupinga kumbe uko sahihi.
Mimi Kimara hasa napajua Temboni tu ambako kuna hiyo barabara ya rami. Kumbe barabara zingine za ndani full vumbi!!
Mimi nilijua roads zote zina janvi
 
Kumbuka yafuatayo:-
1. Kimara-Mbezi ni squarter ie hakujapimwa na hivyo hakuna barabara iliyokidhi vigezo vya lami sawa na tegeta.
2.miundombinu haikidhi matakwa ya kuwekwa lami, maeneo mengi ni maeneo ya raia.
3.wamejaa wachaga
Kutopimwa ndio sababu kuu,hata Kigamboni maeneo mengi ndio hivyo hivyo hakuna mitaa ya kueleweka sasa utawekaje lami?
 
Hv umepita mwananyamala mbona skwata zaidi na kumewekwa vilami japo vyembambaa

Mwananyamala ni karibu zaidi na mjini, unavyozidi kwenda mbali na city centre ndivyo hali ya barabara inakuwa za tabu, ila kimara mbezi jamani ni plateu hata uwekaji wa lami ni tabuuu
 
Kimara ni eneo ambalo limekua kwa kasi tangu kipindi cha Mwinyi hadi Mkapa, Kikwete na Magufuli kuliko maeneo mengine yote lakini hadi leo hakuna barabara za ndani za lami.

Ukiondoa kipande cha kutoka Baruti kwenda chuo kilichokamilika juzi, kuanzia Ubungo hadi Mbezi hakuna barabara za ndani zenye lami isipokuwa kipande kidogo cha kilomita 2 kinachotokea Kimara Temboni na kuelekea nyumbani kwa bosi wa TANROADS ndugu Mfugale.

Huyu Mfugale ambaye kasifiwa na bosi wake hadi kuzawadiwa jina la flyover ya Buguruni kwa ushujaa wa kuwanyima wana Kimara wenzie barabara na kujipendelea yeye mwenyewe. Huu ubinafsi wa mtu kujipendelea kwake kwanza kama taifa unatupeleka pabaya mtu anapongezwa badala ya kutumbuliwa.

Kimara ilianza kuchangamka kitambo kabla ya Kinyerezi, Lumo, Goba, Segerea, Tegeta lakini wenzetu wameendelea kimiundombinu kuliko Kimara ni ubishini kuliko maeneo hayo
Mnalipa kodi ili zitumike kumjegea barabara mtu mmoja!!!!!
 
we mtoa mada uwe unafanya na kauchunguzi. asilimia kubwa ya udongo wa kimara ni mfinyanzi. ndio maana kioindi cha mvua balaa linaanza. pia mbona wanaanza jenga,ingawa kwa gharama mfano barabara ya korogwe inayotokea maji chumvi na riverside inatengenezwa kwa kutumia zege nadhani unajua barabara ya zege ni imara na ni gharama sana. ila wanatengeneza. wangechapa lami juu kwa juu mvua ikipiga inasafisha. mfinyanzi ni udongo wenye changamoto sana.
 
Kwaiyo wewe hujakubaliana kwamba kimara kuna tatizo la barabara, sasa ukiongelea barabara muhusika ni nani?

Kwani Tanzania nzima eneo linalohitaji Miundombinu ya Barabara ni Kimara tu peke yake? Kuna Watu ni Maduduna hapa Tanzania hadi mnakera na huenda kutokana na huu Ubinafsi wenu ndiyo maana mnaachwa na hampatiwi hayo Maendeleo mnayoyataka kutoka Serikalini. Badilikeni kwani bado hamjachelewa.
 
Back
Top Bottom