Mbunge wa ilula
JF-Expert Member
- Jun 3, 2012
- 211
- 18
Ni katika kuendeleza ubabe wake na ulevi wa madaraka DC wa kilolo bw.Gerald John Guninita amemweka rock up ya mbigili police station mwenyekiti wa kijiji cha udekwa bila sababu ya msingi.
DC huyu alifika kijijini hapo kwaajili ya kuendesha mkutano wa kumng'oa mwenyekiti huyo wa kijiji (CHADEMA) ambapo fununu zilishavuja siku chache kuwa ujio wake utakuwa maalumu kwaajili ya kuja kumng'oa mwenyekiti huyu ambaye hana hatia yoyote zaidi ya kuwa mwanachama wa CHADEMA.
Lakini gafla alibadilisha mkutano na kuwa kikao cha ndani hali iliyowashangaza wengi na wakiwa ndani ya kikao alimuuliza mwenyekiti huyo kwanini anarekodi kikao kwa njia ya simu,ambapo mwenyekiti alijibu kuwa anarekodi kwa kumbukumbu hivyo DC akaamuru polisi walioongozana nao wamkamate mwenyekiti huyo ili akamtie adabu.
Hata hivyo mmoja ya askari waliomkamata amekiambia chanzo changu kuwa DC amewaamuru wamweke ndani kwa siku mbili na baadaye wamwachie kwa masharti ya kuripoti kituoni kila siku assubuhi kwa muda wa wiki moja
Ikumbukwe kuwa hoja ya DC kutaka kumng'oa mwenyekiti huyu ni baada ya wananchi wake kumzomea mbunge wa kilolo miezi kadhaa iliyopita pale alipoenda kijijini hapo kama mbunge huku akiambatana na makada wa ccm kwa lengo la kukinadi chama hali iliyomfanya m/kiti ahoji kama ziara ile ilikuwa kwa shughuli za chama au kibunge,Hata hivyo diwani wa viti maalumu kata ya mahenge aliendeleza uchama baada ya kuendeleza salamu chama huku akijua kwamba kijiji hicho kinaongozwa na mwenyekiti kutoka CHADEMA hali hii ilimfanya mwenyekiti wa kijiji kuondoka eneo la mkutano ili awaachie Mbunge na makada wake waendelee kufanya shughuli za chama chao ccm.Baada ya mwenyekiti kuondoka Mbunge alikutana na zomeazomea ya peoples power hali iliyomfanya aahirishe mkutano wake.
Hivyo baada ya tukio hilo wajumbe wa halmashauri ya kijiji ambao wote wanatokea ccm walianza kumshinikiza mwenyekiti huyu Obadia Lubugo (Chadema) kwamba aombe msamaha kwa kuondoka kwenye mkutano wa Mbunge lakini Mwenyekiti aligoma kuomba msamaha kwa madai ya kutotambua kosa lake,Lakini baadaye alifikishwa katani kwa hatua zaidi ambapo Diwani(ccm) na mtendaji kata waliendelea kumshinikiza mwenyekiti huyu aandike barua ya kuomba msamaha kwa kuondoka kwenye mkutano lakini mwenyekiti aliwajibu kwamba hataomba msamaha kwani hakuwa na kosa la kuondoka kwenye mkutano uliokuwa unafanya shughuli za chama cha ccm ili hali yeye anatokea chama kingine cha CHADEMA.Ikumbukwe kuwa mkutano huo ulikuwa na lengo la kugawa bendera za ccm na kadi za ccm zilizokuwa zimewekwa mezani kwa mbunge hali hii ilimtibua kabisa ndugu Lubugo ambaye mara kadhaa alijaribu kumshauri Mbunge kwamba kama wanataka kufanya kampeni wangeandaa mkutano mwingine wa chama lakini mkutano ule wangefuata utaratibu wa kawaida wa serikali badala ya chama.
Hivyo kutokana na hilo Diwani wa kata aliamua kumwita Mkuu wa wilaya ndugu G.Guninita ili aje amng'oe mwenyekiti huyu jambo ambalo liliishia kwa DC huyu kumweka ndani katika kituo cha polisi mbigili, mwenyekiti huyu bila sababu ya msingi na kwa muda usiojulikana.
DC huyu alifika kijijini hapo kwaajili ya kuendesha mkutano wa kumng'oa mwenyekiti huyo wa kijiji (CHADEMA) ambapo fununu zilishavuja siku chache kuwa ujio wake utakuwa maalumu kwaajili ya kuja kumng'oa mwenyekiti huyu ambaye hana hatia yoyote zaidi ya kuwa mwanachama wa CHADEMA.
Lakini gafla alibadilisha mkutano na kuwa kikao cha ndani hali iliyowashangaza wengi na wakiwa ndani ya kikao alimuuliza mwenyekiti huyo kwanini anarekodi kikao kwa njia ya simu,ambapo mwenyekiti alijibu kuwa anarekodi kwa kumbukumbu hivyo DC akaamuru polisi walioongozana nao wamkamate mwenyekiti huyo ili akamtie adabu.
Hata hivyo mmoja ya askari waliomkamata amekiambia chanzo changu kuwa DC amewaamuru wamweke ndani kwa siku mbili na baadaye wamwachie kwa masharti ya kuripoti kituoni kila siku assubuhi kwa muda wa wiki moja
Ikumbukwe kuwa hoja ya DC kutaka kumng'oa mwenyekiti huyu ni baada ya wananchi wake kumzomea mbunge wa kilolo miezi kadhaa iliyopita pale alipoenda kijijini hapo kama mbunge huku akiambatana na makada wa ccm kwa lengo la kukinadi chama hali iliyomfanya m/kiti ahoji kama ziara ile ilikuwa kwa shughuli za chama au kibunge,Hata hivyo diwani wa viti maalumu kata ya mahenge aliendeleza uchama baada ya kuendeleza salamu chama huku akijua kwamba kijiji hicho kinaongozwa na mwenyekiti kutoka CHADEMA hali hii ilimfanya mwenyekiti wa kijiji kuondoka eneo la mkutano ili awaachie Mbunge na makada wake waendelee kufanya shughuli za chama chao ccm.Baada ya mwenyekiti kuondoka Mbunge alikutana na zomeazomea ya peoples power hali iliyomfanya aahirishe mkutano wake.
Hivyo baada ya tukio hilo wajumbe wa halmashauri ya kijiji ambao wote wanatokea ccm walianza kumshinikiza mwenyekiti huyu Obadia Lubugo (Chadema) kwamba aombe msamaha kwa kuondoka kwenye mkutano wa Mbunge lakini Mwenyekiti aligoma kuomba msamaha kwa madai ya kutotambua kosa lake,Lakini baadaye alifikishwa katani kwa hatua zaidi ambapo Diwani(ccm) na mtendaji kata waliendelea kumshinikiza mwenyekiti huyu aandike barua ya kuomba msamaha kwa kuondoka kwenye mkutano lakini mwenyekiti aliwajibu kwamba hataomba msamaha kwani hakuwa na kosa la kuondoka kwenye mkutano uliokuwa unafanya shughuli za chama cha ccm ili hali yeye anatokea chama kingine cha CHADEMA.Ikumbukwe kuwa mkutano huo ulikuwa na lengo la kugawa bendera za ccm na kadi za ccm zilizokuwa zimewekwa mezani kwa mbunge hali hii ilimtibua kabisa ndugu Lubugo ambaye mara kadhaa alijaribu kumshauri Mbunge kwamba kama wanataka kufanya kampeni wangeandaa mkutano mwingine wa chama lakini mkutano ule wangefuata utaratibu wa kawaida wa serikali badala ya chama.
Hivyo kutokana na hilo Diwani wa kata aliamua kumwita Mkuu wa wilaya ndugu G.Guninita ili aje amng'oe mwenyekiti huyu jambo ambalo liliishia kwa DC huyu kumweka ndani katika kituo cha polisi mbigili, mwenyekiti huyu bila sababu ya msingi na kwa muda usiojulikana.