Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
September 29, 2009
Shirika la ujasusi la Marekani limeanzisha uchunguzi kuwatafuta watu waliozindua kura za maoni kwenye mtandao wa Facebook wakijadili kuuliwa kwa rais wa Marekani, Barack Obama.
Mtandao wa Facebook jana jumatatu ulizifunga kura za maoni zilizozinduliwa kwenye mtandao huo na watu wasiojulikana wakijadili kuuliwa kwa Obama.
Kura hizo za maoni zilikuwa na kichwa cha habari kinachosema "Je Obama Auliwe?" na kulikuwa na majibu manne yaliyopendekezwa ambayo yalikuwa ni "Ndio, Hapana, Labda na 'Kama akikata bima zangu za afya'".
"Wakati tulipogundua kura hizo za maoni, tuliwasiliana na Facebook kutaka ziondolewe" alisema msemaji wa shirika la ujasusi la Marekani, Malcolm Wiley alipokuwa akiongea na shirika la habari la AFP.
"Tunendelea na uchunguzi kama ambavyo huwa tunafanya kwa kesi zingine za vitisho vya maisha yake".
Zaidi ya watumiaji 750 wa Facebook walishiriki kwenye kura hizo za maoni hadi wakati programu ya kura hizo za maoni ilipoondolewa kwenye Facebook.
"Hii inasikitisha sana", aliandika mtumiaji mmoja wa Facebook anayejiita Cocoa Fly wakati kura hizo za maoni zilipoanza kujipatia umaarufu wa ghafla kwenye Facebook kabla ya kuondolewa.
"Harakati zote hizi za kumpinga Obama zimejaa ubaguzi tu" aliandika Cocoa Fly.
Programu ya kura hizo za maoni iliandaliwa mwishoni mwa wiki na kisha kuwekwa kwenye Facebook kupitia programu nyingine ambayo huwapa nafasi watumiaji wa Facebook kuandaa kura zao za maoni kuhusiana na kitu chochote kile.
Facebook iliamua kuifunga programu nzima ya kutoa maoni ili kuepukana na kura za maoni za Obama na ilisema kwamba programu hiyo itaendelea kufungiwa mpaka wamiliki wake watakapoihakikishia Facebook kwamba imeziondoa kura za maoni zenye kuleta mfarakano na itarekebisha miundombinu yake kuepuka watu wengine kuingiza programu zao za kura za maoni yenye utata kupitia programu hiyo.
Source: AFP
Shirika la ujasusi la Marekani limeanzisha uchunguzi kuwatafuta watu waliozindua kura za maoni kwenye mtandao wa Facebook wakijadili kuuliwa kwa rais wa Marekani, Barack Obama.
Mtandao wa Facebook jana jumatatu ulizifunga kura za maoni zilizozinduliwa kwenye mtandao huo na watu wasiojulikana wakijadili kuuliwa kwa Obama.
Kura hizo za maoni zilikuwa na kichwa cha habari kinachosema "Je Obama Auliwe?" na kulikuwa na majibu manne yaliyopendekezwa ambayo yalikuwa ni "Ndio, Hapana, Labda na 'Kama akikata bima zangu za afya'".
"Wakati tulipogundua kura hizo za maoni, tuliwasiliana na Facebook kutaka ziondolewe" alisema msemaji wa shirika la ujasusi la Marekani, Malcolm Wiley alipokuwa akiongea na shirika la habari la AFP.
"Tunendelea na uchunguzi kama ambavyo huwa tunafanya kwa kesi zingine za vitisho vya maisha yake".
Zaidi ya watumiaji 750 wa Facebook walishiriki kwenye kura hizo za maoni hadi wakati programu ya kura hizo za maoni ilipoondolewa kwenye Facebook.
"Hii inasikitisha sana", aliandika mtumiaji mmoja wa Facebook anayejiita Cocoa Fly wakati kura hizo za maoni zilipoanza kujipatia umaarufu wa ghafla kwenye Facebook kabla ya kuondolewa.
"Harakati zote hizi za kumpinga Obama zimejaa ubaguzi tu" aliandika Cocoa Fly.
Programu ya kura hizo za maoni iliandaliwa mwishoni mwa wiki na kisha kuwekwa kwenye Facebook kupitia programu nyingine ambayo huwapa nafasi watumiaji wa Facebook kuandaa kura zao za maoni kuhusiana na kitu chochote kile.
Facebook iliamua kuifunga programu nzima ya kutoa maoni ili kuepukana na kura za maoni za Obama na ilisema kwamba programu hiyo itaendelea kufungiwa mpaka wamiliki wake watakapoihakikishia Facebook kwamba imeziondoa kura za maoni zenye kuleta mfarakano na itarekebisha miundombinu yake kuepuka watu wengine kuingiza programu zao za kura za maoni yenye utata kupitia programu hiyo.
Source: AFP