Kilio changu kwa DSTV Tanzania

Huu ujinga wanaoufanya hawa jamaa kwa kujiona wameshaliteka soko litakuja liwaponze muda si mrefu!

King'amuzi hakina channel za taarifa za habari za ndani kwa lugha ya kiswahili ukitoa TBC pekee!

Ni watanzania wangapi wanajua kiingereza hadi wakaangalie aljazeera or sky news?!

Kumpata mteja ni rahisi ila ukimpoteza kuja kumrudisha tena ndio shida!

Ni suala la muda tu waache waendelee kuzani hizo channel hazina impact kwao watakuja wastuke kumeshakucha!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo unajiona umeandika mwenyewe.
Ushaambiwa DSTV sio ya watu wa kimasikini kama wewe.
Startimes na TING ndio size yako.
 
Hadi leo mnaangalia local chanels. Nunua waya wako wa kuunga cm na TV, ukitaka kuangalia kitu unanunua GB zako kadhaa unajiunga then unatazama kipindi kikiisha unawarudishia katuni au unachomeka external kwenye tv watoto wajisomee kupitia TV.
Mkuu ufafanuzi kidogo hapo
 
Mimi nina DSTV ila leo nataka nifanye maamuzi ya kununua kingamuzi kingine kati ya Azam na Startimes kipi Bora? Nisaidieni tafadhali ili ninunue leo leo.
 
Hadi leo mnaangalia local chanels. Nunua waya wako wa kuunga cm na TV, ukitaka kuangalia kitu unanunua GB zako kadhaa unajiunga then unatazama kipindi kikiisha unawarudishia katuni au unachomeka external kwenye tv watoto wajisomee kupitia TV.
Mkuu saidia zaidi hapa maujanja
 
Tangu nimehamia dstv miaka 8 iliyopita sijawahi juta.
Local chanel zenyewe ni kuimba na kusifu tu hata pasipo na haja.

Habari za ndani nakunaza nazo hapa jf inatosha. Tena ni habari zisizopikwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ujinga wanaoufanya hawa jamaa kwa kujiona wameshaliteka soko litakuja liwaponze muda si mrefu!

King'amuzi hakina channel za taarifa za habari za ndani kwa lugha ya kiswahili ukitoa TBC pekee!

Ni watanzania wangapi wanajua kiingereza hadi wakaangalie aljazeera or sky news?!

Kumpata mteja ni rahisi ila ukimpoteza kuja kumrudisha tena ndio shida!

Ni suala la muda tu waache waendelee kuzani hizo channel hazina impact kwao watakuja wastuke kumeshakucha!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii suala la channels zingine, ni suala la kimaslahi nasikia .. unaweza kucheck thread ipo humu kitambo, ilifafanua hilo.
 
Naunga mkono hoja TBC haina hadhi ya kuwepo Dstv, iondolewe tu.
TBC ipo pale kisheria na hawawezi kuiondoa, ndio maana hata bando lako la mwezi likikata yenyewe ipo hewani tu. Huna sababu ya kutaka iondolewe as zipo channels nyingi ndani ya kisimbusi chako, angalia vile vinavyokupa elimu, habari na kukiburudisha.

Hata mimi sipendi kuangalia TBC na sikumbuki lini ndani kwangu watu wali-tune TBC, ilà sioni sababu za kutaka kiondolewe, wapo wanaoangalia hicho usichokipenda.
 
Local channels zinazoripoti "Nyoka anamuokoa Samaki asizame kwenye maji"!! Bora tu zisiwepo, hakuna habari ya kuvutia sasa hv nchi hii! Mkuu kama huwezi kulipa hamia Azam!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TBC ipo pale kisheria na hawawezi kuiondoa, ndio maana hata bando lako la mwezi likikata yenyewe ipo hewani tu. Huna sababu ya kutaka iondolewe as zipo channels nyingi ndani ya kisimbusi chako, angalia vile vinavyokupa elimu, habari na kukiburudisha.

Hata mimi sipendi kuangalia TBC na sikumbuki lini ndani kwangu watu wali-tune TBC, ilà sioni sababu za kutaka kiondolewe, wapo wanaoangalia hicho usichokipenda.
Sawa Mkuu nimekuelewa.
 
Back
Top Bottom