kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 13,945
- 15,732
Tangu ilipotelewa rasimu ya mabadiliko ya katiba iliyoongozwa na jaji warioba na kufikia kuundwa bunge la kuijadili,rasimu hiyo ilionekana kama ndio suluhisho la wengi na kilio kimepatiwa ufumbuzi lakini ghafla bila kuamini mjadala ule ulivurugwa na watu wasio itakia mema nchi hii wakiwemo waliokuwa wabunge wa maarufu ambao hivi sasa wapo upinzani walisimama kidete kuvuruga mchakato ule kwa kudhani 2015 ni lazima wangepitishwa na chama chao na kugombea urais na kuendelea kutumia katiba ile hatarishi
Baada ya uchaguzi wengi wamerudi na kuidai ile rasimu irudi tena ifanyiwe kazi kwa mategemeo itasaidia hata yule aliyekuwa kinara wa kuikandamiza sasa ameanza kuitamani na kuililia kinafiki kwa kuwa tu nae hivi sasa amekuwa kundi la wenye miguu minne na mikia,
Kilio hiki kimekuwa kikubwa lakini naastajabishwa na hawa jamaa walikuwa ni vinara wa kupinga ufisadi hivi sasa halipo baada ya kununua corruption machine na kuihifadhi ndani ,
sasa wamegeuka kupinga kila kitu hata yale waliokuwa wakiyapigia kelele kama uzalendo,
sasa hapa kwenye hii katiba watu hawa kweli bado wanaaminika si wanaweza kuikana na kuipinga kwa sababu kila walichokipigania ndani ya miaka miwili hii wamekipinga na kukubali kulala selo
Tumshauri rais auendeleze ule mchakato lakini nina hakika pia utapingwa kwa nguvu zote,maana jamaa walifanya kosa kubwa sana la kukumbatia dampo mbele ya nyumba hata likijaribiwa kusafishwa haliachi kubaki na alama chache za uchafu
Ni hakika hiyo katiba inayoliliwa pia itapingwa raisi wape nafasi tuone unafiki wao!
Baada ya uchaguzi wengi wamerudi na kuidai ile rasimu irudi tena ifanyiwe kazi kwa mategemeo itasaidia hata yule aliyekuwa kinara wa kuikandamiza sasa ameanza kuitamani na kuililia kinafiki kwa kuwa tu nae hivi sasa amekuwa kundi la wenye miguu minne na mikia,
Kilio hiki kimekuwa kikubwa lakini naastajabishwa na hawa jamaa walikuwa ni vinara wa kupinga ufisadi hivi sasa halipo baada ya kununua corruption machine na kuihifadhi ndani ,
sasa wamegeuka kupinga kila kitu hata yale waliokuwa wakiyapigia kelele kama uzalendo,
sasa hapa kwenye hii katiba watu hawa kweli bado wanaaminika si wanaweza kuikana na kuipinga kwa sababu kila walichokipigania ndani ya miaka miwili hii wamekipinga na kukubali kulala selo
Tumshauri rais auendeleze ule mchakato lakini nina hakika pia utapingwa kwa nguvu zote,maana jamaa walifanya kosa kubwa sana la kukumbatia dampo mbele ya nyumba hata likijaribiwa kusafishwa haliachi kubaki na alama chache za uchafu
Ni hakika hiyo katiba inayoliliwa pia itapingwa raisi wape nafasi tuone unafiki wao!