BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
KILIO CHA WAALIMU NCHINI TANZANIA!
Nimepokea waraka kutoka kwa mmoja wa waalimu akiwawakilisha waalimu wenzake. Kwa sababu za unyeti wa maudhui ya waraka huo, kiapo changu cha Uaskofu kinaniruhusu kutokutaja jina la mtu aliyeniletea! Nimeamua kuuchapa waraka huo katika ukurasa wangu ili kusaidia kilio cha waalimu kuwafikia wahusika na jamii kwa ujumla!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
"Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Heri ya Mwaka Mpya 2021. Nataka nikueleze kuhusu kilio cha walimu wa Tanzania kwa sasa.
Kilio kikubwa cha walimu ni madaraja. Kama unavyofahamu, mishahara katika Utumishi wa Umma haijaongezwa kwa miaka 5 iliyopita, hivyo tegemeo kubwa la walimu ni kupanda madaraja lakini nako ni kugumu.
Mathalani, wako walimu wa ajira mpya wa mwaka 2014, hawa ilikuwa wapande madaraja mwaka 2019 (mwaka 1 probabation +miaka 4 ya kutumikia cheo). Wapo walimu waliopanda madaraja 2015, hawa walipaswa kupanda 2019 baada ya kutumikia cheo kipya kwa miaka 4 lakini hawajapanda na hakuna dalili za kuwapandisha.
Chama cha Walimu (CWT) kipo kimya, hakuna wa kuwasemea Walimu wa Tanzania. Walimu nao wapo kimya, wanaogopa. Utumishi wa Umma umekuwa mzigo mzito ndani ya awamu hii ya uongozi. Naomba Baba Askofu, lizungumzie hili jambo pengine wenye mamlaka watasikia na kutendea kazi!
Ni mimi Mwalimu."
Nimepokea waraka kutoka kwa mmoja wa waalimu akiwawakilisha waalimu wenzake. Kwa sababu za unyeti wa maudhui ya waraka huo, kiapo changu cha Uaskofu kinaniruhusu kutokutaja jina la mtu aliyeniletea! Nimeamua kuuchapa waraka huo katika ukurasa wangu ili kusaidia kilio cha waalimu kuwafikia wahusika na jamii kwa ujumla!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
"Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Heri ya Mwaka Mpya 2021. Nataka nikueleze kuhusu kilio cha walimu wa Tanzania kwa sasa.
Kilio kikubwa cha walimu ni madaraja. Kama unavyofahamu, mishahara katika Utumishi wa Umma haijaongezwa kwa miaka 5 iliyopita, hivyo tegemeo kubwa la walimu ni kupanda madaraja lakini nako ni kugumu.
Mathalani, wako walimu wa ajira mpya wa mwaka 2014, hawa ilikuwa wapande madaraja mwaka 2019 (mwaka 1 probabation +miaka 4 ya kutumikia cheo). Wapo walimu waliopanda madaraja 2015, hawa walipaswa kupanda 2019 baada ya kutumikia cheo kipya kwa miaka 4 lakini hawajapanda na hakuna dalili za kuwapandisha.
Chama cha Walimu (CWT) kipo kimya, hakuna wa kuwasemea Walimu wa Tanzania. Walimu nao wapo kimya, wanaogopa. Utumishi wa Umma umekuwa mzigo mzito ndani ya awamu hii ya uongozi. Naomba Baba Askofu, lizungumzie hili jambo pengine wenye mamlaka watasikia na kutendea kazi!
Ni mimi Mwalimu."