Kilio cha Mlalahoi: Kupanda kwa bei ya umeme wanasiasa mko wapi?

Stabilaiza

JF-Expert Member
Jul 11, 2012
1,843
1,143
Nimeshangazwa sana na ukimwa wa wanasiasa kuhusu kupanda kwa bei ya umeme.

Ifike mahali wanasiasa wawajibike kwa wananchi dhidi ya ugumu wa maisha kila kukicha. Kupanda kwa bei ya umeme kutasababisha ugumu wa maisha na mfumko wa bei hivyo kuimarisha umaskini kwa wanachi. Au ni maandalizi ya uchaguzi mwaka 2015 ili kuwahonga kirahisi watu chumvi, kanga na sukari kwa sababu ya ugumu wa maisha?
 
Tangu lini aliyeshiba akamjua mwenye njaa!? Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe, bila Watanzania kuja juu na kuukataa huu mfumo dhalimu wa MACCM hali ya maisha kwa Watanzania walio wengi itazidi kudidimia. Wamethubutu, wameweza na sasa wanasonga mbele.
 
Tangu lini aliyeshiba akamjua mwenye njaa!? Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe, bila Watanzania kuja juu na kuukataa huu mfumo dhalimu wa MACCM hali ya maisha kwa Watanzania walio wengi itazidi kudidimia. Wamethubutu, wameweza na sasa wanasonga mbele.
Sasa tuanzie wapi, maana suala hili linagusa wengi. Swali ni nani ataratibu kupinga kupanda kwa bei ya umeme?. Sisi tunawalipa mishahara wanasiasa kupitia kodi tunazotoa. Kuna ruzuku kwa vyama vya siasa, wasifikiri wanalipwa bure. Sasa wawajibike ili kwa pamoja tupinge kupanda kwa bei ya umeme
 
Nimeshangazwa sana na ukimwa wa wanasiasa kuhusu kupanda kwa bei ya umeme. Ifike mahali wanasiasa wawajibike kwa wananchi dhidi ya ugumu wa maisha kila kukicha. Kupanda kwa eni ya umeme kutasababisha ugumu wa maisha na mfumko wa bei hivyo kuimarisha umaskini kwa wanachi. Au ni maandalizi ya uchaguzi mwaka 2015 ili kuwahonga kirahisi watu chumvi, kanga na sukari kwa sababu ya ugumu wa maisha?

Wanasiasa pekee wanaoweza kusema juu ya bill ya umeme ni Chadema sasa nyie kila mnawatukana mara Babu , mara hawana shule , mara Saccos sasa you face it .Maana wao wana pesa they can afford wako kimya tuumie wote .Wanaungana na wabunge wa CCM kukaa kimya .Si ni Saccos ? Tafuteni isiyo saccos iwasemee .
 
Wanasiasa pekee wanaoweza kusema juu ya bill ya umeme ni Chadema sasa nyie kila mnawatukana mara Babu , mara hawana shule , mara Saccos sasa you face it .Maana wao wana pesa they can afford wako kimya tuumie wote .Wanaungana na wabunge wa CCM kukaa kimya .Si ni Saccos ? Tafuteni isiyo saccos iwasemee .
Wanaotukana ni wale wanaokula kuku kwa mrija, siyo wananchi wa kawaida.
 
hata wanaharakati wanalo la kutusemea katika hili.................huenda tunahitaji Big Bhang
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Watanzania nasi tumekuwa mno wapole, huvi kwa umoja wetu tukikubaliana wstumiaji wa umeme tukubali kutotumia hiyo nishati kwa wiki moja tu watapata wapi income hao tanesco??? Viwanda wazime umeme wstumie generators na sisi hohehahe tutumie vinatari tuone
 
magamba in action wanafanya usanii,wanapandishe bei ya umeme wenyewe kisha watakuja MAJUKWAANI na mashairi na vibwagizo serikali yenu sikivu inawajali ,INAWATAKIA MEMA NA MSHIKAMANO na kupunguza kama walivyopitisha kodi ya line ya simu kwa kishindo mara wameondoa ili waonekane wana huruma kwa wananchi tusahau ujangiri,wageni waliokamatwa na maliasili zetu ,mikataba mibovu ya gesi,mafuta,pesa za Uswiz na uranium subiri utaona!!!!!
 
hili swala halihitaji wanasiasa ni letu sote mimi na wewe. lakini naona kama hizi gharama zimepita na kukubarika na jamii.
Hili ndio tatizo letu Watanzania kuona yanyotuhusu kuwa si yetu na kuwakabidhi na kuwategemea wana siasa kama akina Zitto watuongoze na kupinga upuuzi unaofanywa na watawala wetu wakati wana Siasa wenyewe wanajishibishaa matumbo yao
 
  • Thanks
Reactions: BAK
wametegea watu wako busy na sikukuu, magamba wakapiga hapo hapo, mijamaa mijizi sana
 
Tatizo letu ni hilo la kutegemea wanasiasa watutatulie kero zetu,
hao hawana shida sisi ndio wenye shida kwa nini tusi react kwa nguvu zetu zote?
 
Tangu lini aliyeshiba akamjua mwenye njaa!? Kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe, bila Watanzania kuja juu na kuukataa huu mfumo dhalimu wa MACCM hali ya maisha kwa Watanzania walio wengi itazidi kudidimia. Wamethubutu, wameweza na sasa wanasonga mbele.

Ask not what your Country can do for you ask what you can do for your Country. - John F. Kennedy
 
Alafu si nasikia kuna bil 400 imepatikana kwenye hisa...!
Walipe madeni yao sie tupunguziwe bei.

Wanasiasa sio wenzetu, wapo kwa msimu na msimu wao 2014 zaidi 2015
 
Ask not what your Country can do for you ask what you can do for your Country. - John F. Kennedy

Hiyo ni kwa America sio Bongo kaka..Kwa bongo it's vice versa kwa ushahidi zaidi muone uncle Lukuvi
 
  • Thanks
Reactions: BAK

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom