Kilio cha kukosa huduma ya TANESCO kwa wananchi kitaisha lini?

Ndokeji

JF-Expert Member
Jun 9, 2011
698
475
Kila Mahali wananchi wanaendelea kulia bila Msaada wa viongozi kuhusu kukoswa huduma ya Tanesco kama.

1) kukoswa huduma ya surveyor

2) zaidi ya wananchi 210000 walio lipia huduma ya kuunganishiwa umeme , Hawajaunganishiwa kwa sababu ya upungufu wa meter,nyaya na watu wakuunganisha umeme.

3) Matatizo ya Luku.

4) Umeme Kukatika.

Hali Hii inakua kwa kasi sana Huku viongozi wa nchi wako kimya.

Je, hili tatizo litaisha lini?
 
Yote nakubaliana nayo.Ila ndugu zangu ninyi hilo neno "kukoswa" huwa mnakosea.Muwe mnaongea "kukosa" siyo "kukoswa"!Mnakuwa kama mpo Pida.😝😝😝😝
 
Narudia kusema tena, kuna haja ya kulivunja shirika na kuform mashirika mawili; shirika moja litadeal na masuala ya uzalishaji umeme na kuipeleka kwenye gridi ya taifa na kuwauzia shirika la pili ambao watadeal na usambazaji umeme na mauzo kwa wateja.

Pamoja na hayo waruhusiwe makampuni mengine kusambaza umeme kwa wateja kwa maana wawe na uwezo wa kununua kwa wazalishaji na kuuzia wateja independently kama ilivyo kwa ving'amuzi ili kuweza kuweka ushindani kwa haya mashirika bila hivyo hii Monopoly waliyonayo Tanesco itaendelea kututesa endlessly.
 
Narudia kusema tena, kuna haja ya kulivunja shirika na kuform mashirika mawili; shirika moja litadeal na masuala ya uzalishaji umeme...
Shida sio Shirika, wanasiasa ndio tatizo hata ukiligawa wafanyakazi watakuwa watanzania walewale wanaongozwa na CCM.

Angalia miradi na manunuzi aliyoyafanya JPM, ndio utajua wanasiasa wakiamua kukomaa na jambo fulani wanaweza na wakiamua kutelekeza na kupuuizia jambo wanaweza.
 
Kwa kweli tanesco ni shida kila mahali hata hapa Morogoro mjini kuna maeneo kama kiegea, mkundi watu hawana umeme, nyumba zaidi ya 100 hazina Huduma ya umeme Mitaa ya kiegea na Nguvu kazi, ukifuatilia, wanakuambia wasubiri mradi.

Mradi ulipokuja wakachagua baadhi ya nyumba za wenye pesa wakawekewa umeme, waliobaki wakaambiwa nguzo hazitoshi au nguzo 3 mtu Alipie 1.5m hapo nyaya bado, mi nashauri hili shirika libinafsishwe ili serikali ukusanye tu mapato kutoka kwa hao investors
 
Kila Mahali wananchi wanaendelea kulia bila Msaada wa viongozi kuhusu kukoswa huduma ya Tanesco kama.

1) kukoswa huduma ya surveyor

2) zaidi ya wananchi 210,000/=walio lipia huduma ya kuunganishiwa umeme , Hawajaunganishiwa kwa sababu ya upungufu wa meter,nyaya na watu wakuunganisha umeme.

3) Matatizo ya Luku.

4) Umeme Kukatika.

Hali Hii inakua kwa kasi sana Huku viongozi wa nchi wako kimya.

Je, hili tatizo litaisha lini?
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
Asantee Mkuu!! Sisi wananchi wa mkundi CCT Morogoro, tunaomba mtuwekeee umeme jamanii!! Na sisi tunatamani kuangalia TV na kunywa maji ya baridi. Mwaka jana mliweka kisehemu kidogo mkasema kabla ya mwezi wa 9 mwaka jana hiyo hiyo mngemalizia kote, lakini hadi leo tuko gizaniii Tuhurumieni watanzania wenzenu

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Asantee Mkuu!! Sisi wananchi wa mkundi CCT Morogoro, tunaomba mtuwekeee umeme jamanii!! Na sisi tunatamani kuangalia TV na kunywa maji ya baridi. Mwaka jana mliweka kisehemu kidogo mkasema kabla ya mwezi wa 9 mwaka jana hiyo hiyo mngemalizia kote, lakini hadi leo tuko gizaniii Tuhurumieni watanzania wenzenu

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Tafadhali tuonesha ni Wilaya gani? Namba ya simu tafadhali
 
TANESCO mnasumbua sana tangu mwezi wa sita mpaka leo sijapatiwi control number ya kulipia kuunganishiwa huduma.
Mara form ime expire mara sibiri mnakera sana.
 
Shirika hili binafsi natamani libinafsishwe iwe kama ilivyo kwa makampuni ya simu...yaani nimehangaika yapata miaka minne ili niweze kupata umeme kwenye eneo langu lakini mpaka sasa sijapata... TANESCO TANESCO TANESCO..Sina hamu kabisa...
 
Shirika hili binafsi natamani libinafsishwe iwe kama ilivyo kwa makampuni ya simu...yaani nimehangaika yapata miaka minne ili niweze kupata umeme kwenye eneo langu lakini mpaka sasa sijapata... TANESCO TANESCO TANESCO..Sina hamu kabisa...
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.


Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
 
Shirika hili binafsi natamani libinafsishwe iwe kama ilivyo kwa makampuni ya simu...yaani nimehangaika yapata miaka minne ili niweze kupata umeme kwenye eneo langu lakini mpaka sasa sijapata... TANESCO TANESCO TANESCO..Sina hamu kabisa...
Tafadhali weka taarifa kamili tufatilie tatizo lako na kama linawezekana litatuliwe leo hii
 
Bora hata Tanesco kuna hawa watu idara ya maji wao muda wote wamelala na nyumba zinazidi kuongezeka na hawaoneshi dalili zozote za kupanua huduma yao hasa hawa wa Mwanza ( mwawasa)
 
Back
Top Bottom