Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Kelele za wanajamii kutaka katiba mpya, kimeanza kusikika kwa nguvu. Maaskofu na waandishi wa habari ni sehemu tu ya wanaopaza sauti wakitaka nchi iwe na msingi mzuri wa katiba mpya.
Mheshimiwa rais akiongea na waandishi wa habari miezi kadhaa iliyopita, alisema kwa sasa anainyoosha nchi kwanza, kabla ya kutoa kipaumbele kwenye shughuli za michakato ya uandaaji wa katiba mpya.
Uzoefu wa bunge la maalum la katiba mpya nyakati za mheshimiwa Jakaya Kikwete, sio mzuri sana kwa watu makini wenye kutambua maana ya muda ni mali (time is money).
Yaliibuka malumbano mengi ndani ya bunge lile, zikasemwa kauli mbaya na zisizofaa kusikika masikioni mwa watoto wadogo. Watu wazima wakabishana pasipo kuwa na chembe ya kujitambua.
Mwisho watu wakasikia maneno kama interahamwe, na wengine wakasusa na kutoka nje. Mambo ambayo kwa mwenye hekima, hayatoi mwanga mzuri wa mustakabali wa nchi kuwa na katiba bora.
Leo hii ukiandaliwa mkutano mwingine wa katiba, kutaibuka sintofahamu kama zile zile za wakati wa mzee Jakaya Kikwete. Kutakuwa na upotezaji wa muda, kwenye malumbano na matusi mengi, yanayotoka kwenye pande zenye mitazamo tofauti ya kisiasa.
Wapendwa tukumbuke kwamba tunaposema tunataka kujenga reli ya standard gauge wenzetu Kenya na Ethiopia tayari wanayo reli ya ubora huo.
Tunapozungumzia mipango ya kuhakikisha kila kijiji kinafikiwa na umeme, wapo majirani zetu ambao wameshayafanya haya tena miaka kadhaa iliyopita.
Kuna suala la kujipanga ili mamlaka kama ile ya anga iweze kufanikisha uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere unakuwa ni njia panda (hub), hatuwezi kufanikisha mpango huo kama bado tunarudi kule kule kwenye mipasho ya bunge maalum la katiba lililopita!.
Watu wanataka waache kumbukizi kwenye medani za kisiasa lakini Afrika inayotuzunguka haina muda wa kutusubiri eti tuweke kwanza suala la katiba vizuri ndipo tuingie kwenye michakato ya kiuchumi.
Uzoefu wa bunge maalum la katiba lililopita wakati wa JK, sio mzuri. Wajumbe wa bunge lile hawakuangalia gharama za wao kuwa mle ndani ya jengo, na wakaona ni haki yao ya msingi kupoteza muda kwenye malumbano na majibishano yasiyo na faida kwa mwananchi wa kawaida.
Je, tunao ushahidi gani wa mabadiliko ya kihulka na kimtazamo miongoni mwa wadau muhimu watakaokuwemo kwenye mchakato wa kupata katiba tuitakayo?.
Siasa za lawama, kejeli, kunyoosheana vidole, hazijawa na msaada wa kuipeleka mbele Tanzania hata kwa hatua moja ya kimaendeleo. Tunajipanga vipi kuwa sehemu ya Afrika yenye maendeleo na wakati huo huo kilio cha wenye kutaka katiba mpya kikafanyiwa kazi?.
Tukumbuke kuwa uwepo wa katiba mpya na yenye kuridhiwa na wengi ni sehemu tu ya mapambano ya kuuinua uchumi wa nchi. Hapo kwenye balance kati ya siasa na uchumi ndipo mahali muhimu sana kwa sasa.
Mheshimiwa rais akiongea na waandishi wa habari miezi kadhaa iliyopita, alisema kwa sasa anainyoosha nchi kwanza, kabla ya kutoa kipaumbele kwenye shughuli za michakato ya uandaaji wa katiba mpya.
Uzoefu wa bunge la maalum la katiba mpya nyakati za mheshimiwa Jakaya Kikwete, sio mzuri sana kwa watu makini wenye kutambua maana ya muda ni mali (time is money).
Yaliibuka malumbano mengi ndani ya bunge lile, zikasemwa kauli mbaya na zisizofaa kusikika masikioni mwa watoto wadogo. Watu wazima wakabishana pasipo kuwa na chembe ya kujitambua.
Mwisho watu wakasikia maneno kama interahamwe, na wengine wakasusa na kutoka nje. Mambo ambayo kwa mwenye hekima, hayatoi mwanga mzuri wa mustakabali wa nchi kuwa na katiba bora.
Leo hii ukiandaliwa mkutano mwingine wa katiba, kutaibuka sintofahamu kama zile zile za wakati wa mzee Jakaya Kikwete. Kutakuwa na upotezaji wa muda, kwenye malumbano na matusi mengi, yanayotoka kwenye pande zenye mitazamo tofauti ya kisiasa.
Wapendwa tukumbuke kwamba tunaposema tunataka kujenga reli ya standard gauge wenzetu Kenya na Ethiopia tayari wanayo reli ya ubora huo.
Tunapozungumzia mipango ya kuhakikisha kila kijiji kinafikiwa na umeme, wapo majirani zetu ambao wameshayafanya haya tena miaka kadhaa iliyopita.
Kuna suala la kujipanga ili mamlaka kama ile ya anga iweze kufanikisha uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere unakuwa ni njia panda (hub), hatuwezi kufanikisha mpango huo kama bado tunarudi kule kule kwenye mipasho ya bunge maalum la katiba lililopita!.
Watu wanataka waache kumbukizi kwenye medani za kisiasa lakini Afrika inayotuzunguka haina muda wa kutusubiri eti tuweke kwanza suala la katiba vizuri ndipo tuingie kwenye michakato ya kiuchumi.
Uzoefu wa bunge maalum la katiba lililopita wakati wa JK, sio mzuri. Wajumbe wa bunge lile hawakuangalia gharama za wao kuwa mle ndani ya jengo, na wakaona ni haki yao ya msingi kupoteza muda kwenye malumbano na majibishano yasiyo na faida kwa mwananchi wa kawaida.
Je, tunao ushahidi gani wa mabadiliko ya kihulka na kimtazamo miongoni mwa wadau muhimu watakaokuwemo kwenye mchakato wa kupata katiba tuitakayo?.
Siasa za lawama, kejeli, kunyoosheana vidole, hazijawa na msaada wa kuipeleka mbele Tanzania hata kwa hatua moja ya kimaendeleo. Tunajipanga vipi kuwa sehemu ya Afrika yenye maendeleo na wakati huo huo kilio cha wenye kutaka katiba mpya kikafanyiwa kazi?.
Tukumbuke kuwa uwepo wa katiba mpya na yenye kuridhiwa na wengi ni sehemu tu ya mapambano ya kuuinua uchumi wa nchi. Hapo kwenye balance kati ya siasa na uchumi ndipo mahali muhimu sana kwa sasa.