Fisadi.Jones
Senior Member
- Aug 15, 2008
- 110
- 7
Nimeambiwa kinachotokea huko vijijini kwetu, nikasikitika sana. Inawezekana kabisa tulilogwa.
Mkulima anaambiwa atoe 70,000 ili apewe pembejeo za 600,000. Lakini hali yao ni mbaya mwaka huu kwa kuwa mvua hazikunyesha. Na huu si mda ambao wakulima kwa kawaida wanakuwa safi mfukoni. Na pia huu si mda wa kutayarisha mashamba pia.
Basi mkulima anaomba kwamba hiyo 70,000. Anaambiwa basi saini haya makaratasi tukupe 10,000. Mkulima anasaini, anapewa 10,000 akalinde njaa angalau kuliko akose kila kitu, watu wanaondoka na pembejeo za 600,000. Inasikitisha kwamba kuna ambao wanapewa mpaka 5,000.
Kuna mtandao umejengwa kati ya watendaji wa vijiji na mawakala wa pembejeo kupora wakulima hizi pembejeo. Na kwa kuwa mkulima inabidi aje na barua ya mtendaji, basi ukijifanya mjuaji mtendaji anakuwekea ribiti.
Matokeo yake pembejeo wakulima hawpati. Na hata wale wenye 70,000 inakuwa ngumu kuzipata kwa sababu priority wanaamua watendaji na mawakala ambao wana ajenda yao tofauti.
Na wakulima wakishatapeliwa hivyo, pembejeo hizo (mbolea, etc) zinapelekwa kuuzwa Kenya.
Sasahivi watendaji na mawakala walio kwenye mtandao huo huko neema tupu. Magari ya kifahari ndio yanaingia kwa kwenda mbele. Watu wanakuwa matajiri from no where.
Jitayarisheni na EPA nyingine. Ila hii ni ngumu maana watuhumiwa watakuwa wengi mno.
Mkulima anaambiwa atoe 70,000 ili apewe pembejeo za 600,000. Lakini hali yao ni mbaya mwaka huu kwa kuwa mvua hazikunyesha. Na huu si mda ambao wakulima kwa kawaida wanakuwa safi mfukoni. Na pia huu si mda wa kutayarisha mashamba pia.
Basi mkulima anaomba kwamba hiyo 70,000. Anaambiwa basi saini haya makaratasi tukupe 10,000. Mkulima anasaini, anapewa 10,000 akalinde njaa angalau kuliko akose kila kitu, watu wanaondoka na pembejeo za 600,000. Inasikitisha kwamba kuna ambao wanapewa mpaka 5,000.
Kuna mtandao umejengwa kati ya watendaji wa vijiji na mawakala wa pembejeo kupora wakulima hizi pembejeo. Na kwa kuwa mkulima inabidi aje na barua ya mtendaji, basi ukijifanya mjuaji mtendaji anakuwekea ribiti.
Matokeo yake pembejeo wakulima hawpati. Na hata wale wenye 70,000 inakuwa ngumu kuzipata kwa sababu priority wanaamua watendaji na mawakala ambao wana ajenda yao tofauti.
Na wakulima wakishatapeliwa hivyo, pembejeo hizo (mbolea, etc) zinapelekwa kuuzwa Kenya.
Sasahivi watendaji na mawakala walio kwenye mtandao huo huko neema tupu. Magari ya kifahari ndio yanaingia kwa kwenda mbele. Watu wanakuwa matajiri from no where.
Jitayarisheni na EPA nyingine. Ila hii ni ngumu maana watuhumiwa watakuwa wengi mno.