Kilimo kiko hatarini, Vijana wamekimbilia mjini kuwa Wamachinga na Madereva bodaboda, Wazee ndio wanaozalisha

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,704
6,499
Ukiangalia trend za Kilimo Chetu ni kama kinashuka badala ya kupanda, kwa sababanu kuna baadhi ya takwimu ambako Tanzania zamani ilikuwa inaongoza kwa chai au Pamba ila leo hii hakuna Tena.

Umewahi fika Kilimanjaro siku za hivi karibuni? Vijijini hasa kwenye mashamba ya kahawa? Wanaolima ni wazeee sana na hao hata ndo unakuta wanakimbizana na KNCU chama cha chao cha Ushirika, Hakuna kijana mwenye shamba la kahawa, ni wazee na wengi wao kwa sababu nguvu zimepungua wameamua kutelekeza kahawa au wanalima kiasi fulani.

Nenda Meru kule Aruaha hali ni hiyo hiyo Wazeee ndio wanaolima kahawa na wamechoka wameamua hata kuuza mashamba na watu kujenga nyumba za kuishi au Mahoteli au Mashule. Nenda Bukoba kwenye kahawa wamebakia wazee.

Ukienda Mkoa wa Shinyanga kwenye Pamba, utaona kabisa uzalishaji unapungua sana, Kilimo cha Pamba Mikoa ya kanda ya Ziwa sio kama zamani ukiachana na mambo ya bei hata nguvu kazi ni Changamoto sana vijana wako Jiji la mwanza wanafanya Umachinga.

Nimewahi fanya kazi na Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula WFP kwenye mkoa wa Kigoma na Vikundi vyote vya wakulima sikuona kijana hata mmoja ni wazee tupu wa mama kwa Wababa. Vijana wamekimbilia miji kama Kahama, au miji yao kama Kasulu mjini na Kibondo mjini na kule wanafanya umachinga na kuendesha Pikipiki.

Ukiangalia Kanda ya Kaskazini, Vijana waliokuwa wakulima kule Singida kwenye alizeti sasa wako Arusha, wako Dar au wako Singida Mjini. Hali ni hivyo hivyo Morogoro, Tanga, Mbeya, Iringa, Songea na kwingineko.

Siku hizi ni kazi ngumu kupata vijana wa kukufanyia kazi shambani kwa sababu asilimia kubwa hawapo kabisa wamekimbili Mijini, waliobakia ni Wazee au vijana ambao ni addictade na pombe.

Serikali inapaswa kuja na mikakati thabiti sana kusaidia kupunguza hii hali.


Ushauri wangu kwa Serikali;

1. Serikali iweke ugumu sana wa vijana kufanya uchuuzi mijini, yaani mazingra ya kuwa Mchuuzi mjini yawe magumu sana na yasivutie kabisa vijana, Awamu ya 5 vijana walivutiwa sana na mazingira na kipindi hicho ndio mamia kwa maelfu ya Vijana walikimbilia Mijini kufanya uchuuzi na kuacha wazee wakilima.

Mazingira ya uchuuzi yanavuta sana vijana na hapo ndio Serikali inapokosea kabisa, the more unavyowavuta mjini ndio the more kilimo kina-lose.

2. Wazee ambao kwa sasa kweli ndo wazalishaji kule vijijini wasaidiwe basi, iangaliwe namna ya kuwasaidia wale wazee wanaokoa sana Taifa kwa Chakula lakini wanahitaji Sapoti ya kuwafuta Jasho, Fikiria mzee analima halafu ukame unapita unaangamiza kila kitu, hapo ndo kijana anaamua kukimbilia mijini make anaona hailipi. Linapokuja suala la kusapoti Wakulima Wazee wapewe kipaumbele hawa ndo wanaookoa kwa sasa.

3.Bila Motisha kwenye Kilimo vijana wataendelea kukimbia vijijini, Kilimo kinahitaji motisha sana, Moja ya sababu ya vijana kukimbia ni kwa sababu wanaona hakilipi na wako sahihi kabisa, Kilimo kinahitaji upendeleo special kwa kila nyanja, Upendeleo wa Serikali kwenye Kilimo unaweza wavutia sana Vijana kubakia kwenye Kilimo.
Kwa sasa Motisha ziko tu kwenye makaratasi hakuna uhalisia wala jitihada

- Kuwe na motisha special kwa vijana wao lima hasa vijijini.

4. Maeneo ya Kilimo pia ni bora yakawekewa mazingira kidogo yafanane na Mijini, ingawa kidogo kwenye Umeme wanajitahidi sana, pia huduma za kijamii jama Maji, Afya na kadhalika, Kunapo kuwa na huduma bora vijijini angalau inapunguza asilimia kiasi ya vijana wanaokimbilia mjini.

Serikali iweke mazingira magumu mjini na wakati huo huo mazingira rafiki ya kuendesha kilimo vijijini, na kwa wale vijana wa Vijijini ambao wamekubali kubakia na kulima wale wasaidiwe sana ili wawavutie wenzao waingie kwenye kilimo pia. Hatuwezi kuwa Taifa la uchuuzi pekee, tunahitaji sana kuzalisha mazao ya chakula na ya Biashara, lakini hii haitawezekana bila hatua kubwa.

Kanda ya Ziwa Jiji la Mwanza limemeza nguvu kazi yote ya ile kanda ukangalia Kaskazini ni Arusha imemeza wote, Dar imemeza nchi nzima.

Ukiangalia baadhi ya maeneo tayari hali ishakuwa mbaya, kama Moshi kwenye kahawa, Arusha kahawa na Ngano kama kule Karatu, Bukoba kahawa, Kanda ya ziwa pamba.

Na sisi wasomi tuache kubanana mijini twende tukawekeze kwenye kilimo huko vijijini kuokoa jahazi labda vijana watatuiga na wao watulie.

Serikali weka mazingira magumu sana mijini, Sheria kali za mambo ya Mipango miji, Usafi wa miji na ufanyaji biashara holela.

Nakaribisha michango.
 
Bank za Kilimo na Biashara hazipo maeneo ya uzailishaji wa Kilimo na kama ikiwepo ata moja ina msululu mkubwa wa vigezo kwa Vijana kukopesheka. Hari hiyo inafanya Vijana kuona kilimo ni zao la chakula katika familia na mazoea tu ili siku ziende si zao la biashara, ndio maana wanaamua waende mjini kufanya biashara. Kiufupi ( Mfano Moro) kijana una shamba na umelima kwa miaka 10 lakini bank inakuzungusha kukupa mkopo, ili utoke pale ulipo, ndio maana tunaamua kuja kushinda mjini na kuwaacha wazee waendelee kulima maboga.
 
Vijana wapo mijini wanalalamika serikali kuruhusu kuuza mazao ya baba/babu zao nje huku wao wana njaa.
Shida kubwa ni kwamba Mazingira ya mjini yana wavutia sana kwenda mjini na mazingira ya Vijijini mashambani yanawakimbiza, hivyo bila jitihada za kwanza kufanya mazingira ya mjini yasiwavutie san na pili kufanya mazingira ya Vijijini yawe rafiki kwao. Zaidi ya hapo tutaendelea kuona wanao bakia kulima ni wazee na wakisha kata nguvu basi mashamba wanauza au yanatelekezwa
 
Bank za Kilimo na Biashara hazipo maeneo ya uzailishaji wa Kilimo na kama ikiwepo ata moja ina msululu mkubwa wa vigezo kwa Vijana kukopesheka. Hari hiyo inafanya Vijana kuona kilimo ni zao la chakula katika familia na mazoea tu ili siku ziende si zao la biashara, ndio maana wanaamua waende mjini kufanya biashara. Kiufupi ( Mfano Moro) kijana una shamba na umelima kwa miaka 10 lakini bank inakuzungusha kukupa mkopo, ili utoke pale ulipo, ndio maana tunaamua kuja kushinda mjini na kuwaacha wazee waendelee kulima maboga.
Unashangaa Benki za Kilimo ziko Mjini city Centre, Haya ndo mambo yanawakimbiza vijana vijijini wanabakia wazeee pekee, haingii akilini Taasisi za kilimo ziko mjini kati kati, huko ndo wana oparate kutoka
 
Shida kubwa ni kwamba Mazingira ya mjini yana wavutia sana kwenda mjini na mazingira ya Vijijini mashambani yanawakimbiza, hivyo bila jitihada za kwanza kufanya mazingira ya mjini yasiwavutie san na pili kufanya mazingira ya Vijijini yawe rafiki kwao. Zaidi ya hapo tutaendelea kuona wanao bakia kulima ni wazee na wakisha kata nguvu basi mashamba wanauza au yanatelekezwa
Sahihi
 
Utakuta mleta mada naye yupo mjini

Sent using Jamii Forums mobile app
Nalimia mjini kusapoti kile kinacho toka Vijijini, huku nilipo tuna space za kutosha mjini tunafanya Urbun Farming, ni kwa % ndogo ingawa some how ina saidia sana kusapoti.

Mjini pia unaweza lima ingawa ni % ndogo mno na si kwa mazao makuu kama Mandi, au Pamba au Kahawa au alzeti au Tumbaku.

Unaweza lima mjini kwa sana matunda na vegitables, nalima starwbery nje kidogo sana ya mjini na pia nature ya hili zao hiwezi safirisha umbali mrefu na halitaki mitikisiko.

Karibu sana tulime mkuu
 
Mjini unaweza lima yes, ila kwa vijana wanao kimbilia mjini moja kwa moja wanakuja kufanya umachinga.
 
Mimi sikubaliani na hoja yako kwa sababu nimekuja wilaya ya malinyi huku kijiji cha Itete siku ya 5 leo. Nilichokiona ni kwamba vijana wengi wanalima na pia kuna scheme nzuri tu ya umwagiliaji na vijana wanapanda mpunga wa kiangazi.
Mtu mwenye mtaji wa wastani akiingia bonde hili (mzee,kijana) akakomaa kwa misimu minne ambayo ni miaka miwili ,atakua better off kuliko angefungua duka manzese au sinza.

Tanzania ina watu zaidi ya milioni 60 na wakazi wa miji mikubwa mitatu ya Arusha ,Mwanza na dar haifiki milioni 12.

Serikali ije na Sera nzuri za kilimo,watu wapate elimu waingie kwenye kilimo especially kwenye hizi schemes za umwagiliaji. Pls usithubutu kufanya kilimo cha simu.
 
Mimi sikubaliani na hoja yako kwa sababu nimekuja wilaya ya malinyi huku kijiji cha Itete siku ya 5 leo. Nilichokiona ni kwamba vijana wengi wanalima na pia kuna scheme nzuri tu ya umwagiliaji na vijana wanapanda mpunga wa kiangazi.
Mtu mwenye mtaji wa wastani akiingia bonde hili (mzee,kijana) akakomaa kwa misimu minne ambayo ni miaka miwili ,atakua better off kuliko angefungua duka manzese au sinza.

Tanzania ina watu zaidi ya milioni 60 na wakazi wa miji mikubwa mitatu ya Arusha ,Mwanza na dar haifiki milioni 12.

Serikali ije na Sera nzuri za kilimo,watu wapate elimu waingie kwenye kilimo especially kwenye hizi schemes za umwagiliaji. Pls usithubutu kufanya kilimo cha simu.
Scheme za umwagiliaji bila pesa huwezi, lazima uanze kuwezeshwa ata laki 5, ya kuanzia kama mpunga, benki inaweza kukukopesha na ukalipa mwisho wa msimu, pia benki zina bima kwenye mkopo ambapo ukianguka, wanafidia mwaka mwingine. Hakuna mtu anaekukopesha alafu ukae na ela yake miezi 12, zaidi ya benki tu. Lakini angalia scheme Morogoro zinavyoteseka, Scheme za kuwa Kilombero mkopo ulishindwa kutoka mpaka Waziri aliingiria Kati. Scheme za Mvomero pesa zinasumbua. Wakulima mmoja ambao ni wengi pa kukopa hakuna. Kwa nyakati hizi bila pesa huwezi lima, bora uje ukae mjini tu.
 
Ukiangalia trend za Kilimo Chetu ni kama kinashuka badala ya kupanda, kwa sababanu kuna baadhi ya takwimu ambako Tanzania zamani ilikuwa inaongoza kwa chai au Pamba ila leo hii hakuna Tena.

Umewahi fika Kilimanjaro siku za hivi karibuni? Vijijini hasa kwenye mashamba ya kahawa? Wanaolima ni wazeee sana na hao hata ndo unakuta wanakimbizana na KNCU chama cha chao cha Ushirika, Hakuna kijana mwenye shamba la kahawa, ni wazee na wengi wao kwa sababu nguvu zimepungua wameamua kutelekeza kahawa au wanalima kiasi fulani.

Nenda Meru kule Aruaha hali ni hiyo hiyo Wazeee ndio wanaolima kahawa na wamechoka wameamua hata kuuza mashamba na watu kujenga nyumba za kuishi au Mahoteli au Mashule. Nenda Bukoba kwenye kahawa wamebakia wazee.

Ukienda Mkoa wa Shinyanga kwenye Pamba, utaona kabisa uzalishaji unapungua sana, Kilimo cha Pamba Mikoa ya kanda ya Ziwa sio kama zamani ukiachana na mambo ya bei hata nguvu kazi ni Changamoto sana vijana wako Jiji la mwanza wanafanya Umachinga.

Nimewahi fanya kazi na Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula WFP kwenye mkoa wa Kigoma na Vikundi vyote vya wakulima sikuona kijana hata mmoja ni wazee tupu wa mama kwa Wababa. Vijana wamekimbilia miji kama Kahama, au miji yao kama Kasulu mjini na Kibondo mjini na kule wanafanya umachinga na kuendesha Pikipiki.

Ukiangalia Kanda ya Kaskazini, Vijana waliokuwa wakulima kule Singida kwenye alizeti sasa wako Arusha, wako Dar au wako Singida Mjini. Hali ni hivyo hivyo Morogoro, Tanga, Mbeya, Iringa, Songea na kwingineko.

Siku hizi ni kazi ngumu kupata vijana wa kukufanyia kazi shambani kwa sababu asilimia kubwa hawapo kabisa wamekimbili Mijini, waliobakia ni Wazee au vijana ambao ni addictade na pombe.

Serikali inapaswa kuja na mikakati thabiti sana kusaidia kupunguza hii hali.


Ushauri wangu kwa Serikali;

1. Serikali iweke ugumu sana wa vijana kufanya uchuuzi mijini, yaani mazingra ya kuwa Mchuuzi mjini yawe magumu sana na yasivutie kabisa vijana, Awamu ya 5 vijana walivutiwa sana na mazingira na kipindi hicho ndio mamia kwa maelfu ya Vijana walikimbilia Mijini kufanya uchuuzi na kuacha wazee wakilima.

Mazingira ya uchuuzi yanavuta sana vijana na hapo ndio Serikali inapokosea kabisa, the more unavyowavuta mjini ndio the more kilimo kina-lose.

2. Wazee ambao kwa sasa kweli ndo wazalishaji kule vijijini wasaidiwe basi, iangaliwe namna ya kuwasaidia wale wazee wanaokoa sana Taifa kwa Chakula lakini wanahitaji Sapoti ya kuwafuta Jasho, Fikiria mzee analima halafu ukame unapita unaangamiza kila kitu, hapo ndo kijana anaamua kukimbilia mijini make anaona hailipi. Linapokuja suala la kusapoti Wakulima Wazee wapewe kipaumbele hawa ndo wanaookoa kwa sasa.

3.Bila Motisha kwenye Kilimo vijana wataendelea kukimbia vijijini, Kilimo kinahitaji motisha sana, Moja ya sababu ya vijana kukimbia ni kwa sababu wanaona hakilipi na wako sahihi kabisa, Kilimo kinahitaji upendeleo special kwa kila nyanja, Upendeleo wa Serikali kwenye Kilimo unaweza wavutia sana Vijana kubakia kwenye Kilimo.
Kwa sasa Motisha ziko tu kwenye makaratasi hakuna uhalisia wala jitihada

- Kuwe na motisha special kwa vijana wao lima hasa vijijini.

4. Maeneo ya Kilimo pia ni bora yakawekewa mazingira kidogo yafanane na Mijini, ingawa kidogo kwenye Umeme wanajitahidi sana, pia huduma za kijamii jama Maji, Afya na kadhalika, Kunapo kuwa na huduma bora vijijini angalau inapunguza asilimia kiasi ya vijana wanaokimbilia mjini.

Serikali iweke mazingira magumu mjini na wakati huo huo mazingira rafiki ya kuendesha kilimo vijijini, na kwa wale vijana wa Vijijini ambao wamekubali kubakia na kulima wale wasaidiwe sana ili wawavutie wenzao waingie kwenye kilimo pia. Hatuwezi kuwa Taifa la uchuuzi pekee, tunahitaji sana kuzalisha mazao ya chakula na ya Biashara, lakini hii haitawezekana bila hatua kubwa.

Kanda ya Ziwa Jiji la Mwanza limemeza nguvu kazi yote ya ile kanda ukangalia Kaskazini ni Arusha imemeza wote, Dar imemeza nchi nzima.

Ukiangalia baadhi ya maeneo tayari hali ishakuwa mbaya, kama Moshi kwenye kahawa, Arusha kahawa na Ngano kama kule Karatu, Bukoba kahawa, Kanda ya ziwa pamba.

Na sisi wasomi tuache kubanana mijini twende tukawekeze kwenye kilimo huko vijijini kuokoa jahazi labda vijana watatuiga na wao watulie.

Serikali weka mazingira magumu sana mijini, Sheria kali za mambo ya Mipango miji, Usafi wa miji na ufanyaji biashara holela.

Nakaribisha michango.
Serikali ya kipumbav ya CCM imeua uchumi watu wamekuwa makapuku ,kilimo chenyewe kimedumazwa , masoko hamna na pembejeo na mitaji ya kuwekeza kwenye kilimo cha kisasa Hamna ,
Unafikiri kinachobaki hapo ni nini ? Kama sio watu kupigania kuwa bodaboda ,wasukuma mikokoteni ,machinga and other odd jobs zisizo na future ?

Hii nchi inahitaji serious reformation
 
Hivyo vyama vya ushirika vyenyewe vimeishia kuwa kama magenge ya over lords na miungu watu ambao kazi Yao ni kuterrorize wakulima na kuwadhulumu maslahi , Umasikini Tanzania ni mtaji WA chama tawala na si Kwa bahati mbaya , mkulima analima mazao strategic Tumbaku ,Kahawa ,Korosho , Pareto halafu anapangiwa pa kuuza hata kama maslahi ni ya kipuuz .Angalia jinsi kilimo cha Kahawa kilivyowahi kutajirisha watu miaka ya nyuma Kule Moshi nenda Leo uangalie na uwaulize wakulima waliokuwa wanalima Hilo zao pale Moshi sababu za kukata miti ya Kahawa na kuacha kulima kabisa ni nini ,Fanya hivyo hivyo Shinyanga na Mwanza kwenye pamba , Tumbaku Tabora , Kahawa pale Kagera wakulima wanazuiwa kuuza Uganda ambapo BEI ni double ya hapa ,sasa ni ujinga gani huo ?
 
Hivyo vyama vya ushirika vyenyewe vimeishia kuwa kama magenge ya over lords na miungu watu ambao kazi Yao ni kuterrorize wakulima na kuwadhulumu maslahi , Umasikini Tanzania ni mtaji WA chama tawala na si Kwa bahati mbaya , mkulima analima mazao strategic Tumbaku ,Kahawa ,Korosho , Pareto halafu anapangiwa pa kuuza hata kama maslahi ni ya kipuuz .Angalia jinsi kilimo cha Kahawa kilivyowahi kutajirisha watu miaka ya nyuma Kule Moshi nenda Leo uangalie na uwaulize wakulima waliokuwa wanalima Hilo zao pale Moshi sababu za kukata miti ya Kahawa na kuacha kulima kabisa ni nini ,Fanya hivyo hivyo Shinyanga na Mwanza kwenye pamba , Tumbaku Tabora , Kahawa pale Kagera wakulima wanazuiwa kuuza Uganda ambapo BEI ni double ya hapa ,sasa ni ujinga gani huo ?
Kabisa mkuu inasikitisha kwamba Kahawa inakufa, na kikubwa Wale wakulima walisha zeeka na Vijana hawaoni tena ni kwa nini waingie kulima kahawa
 
Back
Top Bottom