tatizo watu wanaenda lima then hawaleti humu ndani matokeo watu tupate jua,naleta nguvu mtu akikupa ushauri ukaja na matokeo kwa faida ya wengineJamani hata nyanya inalipa sna.chakuzingatia nikanuni yake
Jamani hata nyanya inalipa sna.chakuzingatia nikanuni yake
kilimo kinalipa sana lakini ni bahati nasibu,nililima vitunguu,nyanya,tikiti,maharage na kufuga layers,mabadiliko ya tabia nchi, nyanya zikaharibiwa na mvua wiki la kwanza kuanza kuchuma,vitunguu hakuna uhakika wa kuvuna kwani huenda vikaenda na maji,vitakuwa tayari machi 20,tikiti zilioza baada ya mvua kujaza maji shamba,mahagwe ekari tatu yamekomaa,mvua inanyesha kupita kiasi-yataoza mengi,ekari mbili yanakaribia kukomaa pia. kuku wako wiki ya kumi;zaidi ya milioni saba zimetumika,hasara tupu but najipanga upya kulima ekari tatu za nyanya(nimeshamwaga mbegu na kukodisha shamba) name kufuka broilers 300(wanakuja next wiki) ili kukuza mtaji. ukiingia kwenye kilimo jipange,vinginevyo utakufa kwa pressure.
Msada kw wanaolima morogoro n maeneo gani yanalimwa?
Please ndugu zangu ambao mnabweteka na kutafuta kazi kuna kilimo cha vitunguu, two years unakuwa mtu mwingine kabisa na huta penda kuajiriwa na kama utakuwa kwenye ajira unaweza acha kabisa na kuamua kuwa mkulima. Tusiwaze kuajiriwa tu tutakufa maskin mwisho wa siku. Mimi nimejaribu na sasa nataka niache kazi na kuwa moja ya wakulima na wafanyabiashara wakubwa wa vitunguu na mazao yote ya shamba kwa ujumla ila pamoja na hilo bado nahitaji muongozo mkubwa kwa watu waliobobea kwenye ukulima pamoja na biashara ya mazao ya shambani ili waweze kunishauri zaidi. Mimi napatikana moshi pamoja na arusha ndiko napofanyia biashara zangu. Please kwa yoyote ambaye amebobea kwenye biashara hii zaidi naomba ani PM ili tuweze kupeana contact ili mkukuza network na bidae kuweza kuanzisha kitu flani kwa manufaa yetu asanteni sana na wakilisha.
Mkuu npo sehemu moja inaitwa malolo mpakan na iringa, ni kilimo cha umwagiliaji means kuvuna ni uhakika 100% halafu pia uzuri wa kitunguu huwa hakikosi soko mara baada ya kuvuna sema tu kama soko sio zuri utakiuza kwa bei ya chini na si kukosa soko na wateja huwa wanakuja wenyewe shamban kuvitafuta na si wewe kuwatafuta.
Kingine mkuu kuhusiana na uzuri wa kilimo cha vitunguu ni kwamba utapata hasara kama hutavuna lakin ukivuna huwez kupata hasara hata bei iwe mbaya vip au soko liwe baya vip mtaj wako lazima urudi huwez kupata hasara had ukapoteza na mtaji kwa kitunguu hicho kitu ni never!!!
Nimejifunza mengi sana kutoka kwenye huu mjadala wadau, Natanguliza shukrani zangu. Naomba kuuliza swali kwa wale wenye uzoefu...nasikia maeneo yanayohusika na kilimo cha mazao mbali mbali kuna biashara pia ya kukodisha mashamba kwa wamiliki wa mashamba, ningependa kujua huwa yanakodishwa kwa bei kiasi gani kwa heka na kama huwa yanakodishwa kwa mwaka au kwa msimu wa kilimo??
kwa igawa wanapima vidole ktk upandaji.pato niguni mia hdi mia20kw eka.soko ni msimu unaotoa mazao.mwez1 hd7 soko nzur
Sehemu nyingi wanachofanya kilimo cha vitunguu huwezi kuta wanauza mashamba ila wanakodisha. Gharama ya kukodi huwa inategemeana na sehemu, kwa Lumuma jaruba moja linakodishwa kwa elfu 2 kwahiyo zidisha jaruba 100*2000 ndo gharama ya acre moja kukodi. Kwa Magulu wanakodisha kwa acre na huwa ni laki 3 na nusu kwa acre. Pia mashamba hukodishwa kabla ya msimu kuanza, kwa mfano umeplan kulima msimu wa mwezi wa 3 mwakani, shamba unakodi mwaka huu mwezi wa 7 na huwa ni kwa msimu mmoja tu unarudisha shamba kwa mmiliki. Nadhan nimeeleweka kwa kiasi flan.
Sent from my BlackBerry 9930 using JamiiForums