Kilimo cha Vanilla nchini Tanzania

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
1578983678128.png


1578983960656.png


Zao hili lilianza kuingia nchini kutoka Uganda mnamo mwaka 1954 kupitia kwa mkulima mmoja wa kijiji cha Kiilima wilaya ya Bukoba Vijijini.

UTANGULIZI
Zao la vanilla ni moja ya zao la viungo ambalo asili yake ni Kusini Mashariki ya Mexico na sehemu nyingine za Amerika ya Kati. Vanilla hulimwa katika nchi mbalimbali duniani. Nchi zinazolima kwa wingi ni pamoja na Madagascar, Comoro, Tahiti, Uganda, India na nchi nyingine za Amerika ya Kati.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazolima vanilla katika Afrika. Zao hili lilianza kuingia nchini kutoka Uganda mnamo mwaka 1954 kupitia kwa mkulima mmoja wa kijiji cha Kiilima wilaya ya Bukoba Vijijini. Vanilla imeanza kulimwa kibiashara hasa katika mkoa wa Kagera mwaka wa 1992.

Katika mkoa wa Kagera, kilimo cha Vanilla kimehamasishwa zaidi na Chama cha Maendeleo Ya Wakulima kinachofahamika kama MAYAWA. Chama hiki kimekuwa kikihimiza uzalishaji na usindikaji wa Vanilla ambayo huuzwa kupitia kampuni zilizopo Uganda.

Mmea wa Vanilla huzaa maharage (mapodo) ambayo hukaushwa kwa njia maalum inayowezesha kupatikana kwa Kemikali inayoitwa Vanillini. Kemikali hiyo hutumika katika kuongeza laadha na harufu nzuri kwenye vyakula na vinywaji mbalimbali. Pia hutumika katika viwanda vinvyotengeneza Vipodozi na Dawa za matibabu ya binadamu.

Kwa matumizi ya kawaida, Vanilla huweza kutumika katika vinywaji kama Chai, Maziwa na kama kiungo kwenye mapishi ya Vyakula mbalimbali.

Maeneo mengine ya Tanzania yanayoweza kulima zao la vanilla ni pamoja na wilaya za Mbeya Vijijini, Tukuyu, Morogoro Vijijini, Mvomero, Muheza, Arumeru na Ukerewe.

UMBILE LA MMEA NA MAZINGIRA YANAYOFAA
Mmea wa Vanilla upo katika familia ya Okidi (Orchidaceae) ambayo ina genera zipatazo 700. Kati ya hizo, genera moja itwaayo vanilla ndio yenye umuhimu wa kiuchumi. Genera ya Vanilla ina aina au jamii zipatazo 110, kati ya hizo ni mbili ambazo huzalishwa kibiashara. Aina hizo ni Bourbon ya nchini Mexico na Tahitian ya visiwa vya Tahiti.

Umbile la Mmea wa Vanilla
Mmea wa Vanilla ni rando teke linalotambaa ambalo ni la kudumu. Mmea huu hukua na kutambaa katika mti mwingine hadi kufikia urefu wa mita 10 hadi 15 na zaidi kutegemea na mazingira.

Mizizi
Mizizi ya mmea huu ni mirefu ina rangi nyeupe, myembamba yenye kipenyo cha milimita mbili. Mizizi hutokea kwenye fundo la shina lililo ndani ya udongo na hutambaa sambamba na tabaka la udongo wenye rutuba. Pia hutokea katika vifundo vya shina sambamba na majani ambayo hujishikiza katika miti ya kuegemea.

Shina
Shina la vanilla lina rangi ya kijani, refu lenye vifundo na kipenyo cha sentimeta moja hadi mbili. Nafasi kati ya fundo na fundo ni sentimita tano (5) hadi 15.

Majani
Majani yana rangi ya kijani iliyokolea, yenye umbile la bapa, lenye ncha, nene na kubwa. Huota kwa kupishana katika shina, yana urefu wa sentimita nane hadi 25 na upana wa sentimita mbili hadi nane, na yana rangi ya kijani iliyokolea.

Maua
Maua yana rangi mchanganyiko wa kijani na njano na kipenyo cha sentimita 10. Huota katika vifungu vyenye maua kati ya 18 hadi 30.

Matunda
Matunda yana umbile la podo la harage lenye rangi ya kijani likiwa changa. Hubadilika kuwa rangi ya njano, hatimaye kahawia kadri linavyokomaa. Podo lina urefu wa sentmeta 10 hadi 25, kipenyo cha sentimeta nane hadi 15 na lina mbegu ndogo sana ambazo huonekana linapokomaa.

Mazingira Yanayofaa katika Uzalishaji wa Zao la Vanilla
Mmea wa vanilla una asili ya msituni hivyo huhitaji kuoteshwa katika sehemu yenye kivuli na mvua ya kutosha. Ili zao hili liweze kukua vizuri linahitaji mazingira yafuatayo:

Mvua
Mmea wa Vanilla huhitaji kiasi cha mvua cha milimita 1250 hadi 2500 kwa mwaka. Pia zao hili huhitaji kipindi cha miezi mawili cha ukame ili kuweza kusisisimka na kutoa vitumba vya maua.

Joto
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye nyuzi joto 20 hadi 30 za Sentigredi. Pia huweza kustahimili nyuzi joto 32 za Sentigredi. Lakini hukua vizuri zaidi katika kiwango cha nyuzi joto 27 za Sentigredi.

Mwinuko
Zao hili hustawi vizuri katika maeneo yenye mwinuko wa mita 0 hadi 600 kutoka usawa wa bahari. Pia hustawi katika maeneo yenye mwinuko unaofikia mita 1500 katika nchi za joto (tropiki).

Udongo
Mmea wa vanilla una mizizi ambayo hutambaa katika sehemu ya juu ya udongo. Hivyo, huhitaji udongo mwepesi wa tifutifu, wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji.

Mwanga
Mmea wa vanilla huathirika kwa jua na husababisha kuungua kwa majani, hivyo huhitaji kivuli cha asilimia 50 hadi 75 ili uweze kukua vizuri. Kivuli kinaweza kupatikana kwa kupanda miti au kwa kutengenezwa kitaalamu.

UZALISHAJI WA ZAO LA VANILA
Vanilla huzalishwa kwa kupandikiza marando moja kwa moja shambani au kwa kukuzwa kwanza kwenye kitalu na baadaye kupandikizwa shambani. Kabla ya kupanda inatakiwa kuzingatia yafuatayo:

Uchaguzi wa Shamba
Shamba la kupanda vanilla inafaa liwe mahali pasipo na upepo mkali ili kuepuka kuanguka kwa miti ya kuegemea na kukatika kwa mimea. Ni muhimu kupanda miti ya kuzuia upepo ikiwa mahali hapo pana upepo mkali. Shamba hilo pia liwe na udongo usiotuamisha maji, mwepesi na ambao unaruhusu mizizi kupenya kwa urahisi.

Aidha, shamba lisiwe na magugu mabaya (kwa mfano kwekwe/sangare) ambayo hulazimu kutumia jembe mara kwa mara wakati wa palizi. Kutumia jembe huweza kusababisha kukatika au kuharibu mizizi na kuhatarisha ukuaji wa mmea.

Utayarishaji wa Shamba
Utayarishaji wa shamba huhusisha shughuli mbalimbali kama vile usafishaji wa shamba, utayarishaji wa mashimo na uwekaji wa mbolea.

Kusafisha Shamba
Shamba lisafishwe kwa kulima, kungíoa visiki, magugu mabaya na kutifua hadi kina kisichopungua sentimita 30.

Kutayarisha Mashimo
Mashimo yatayarishwe miezi miwili hadi mitatu sambamba na usafishaji wa shamba. Yawe na kina cha sentimita 30 na upana wa sentimita 60 hadi 90. Nafasi kati ya mstari na mstari iwe mita mbili na nusu hadi mita tatu na kati ya shimo na shimo iwe mita moja na nusu hadi mbili. Udongo wa juu utengwe na ule wa chini.

Uwekaji wa Mbolea
Mbolea za asili kama mboji, vunde au samadi ichanganywe vema na udongo wa juu na kujazwa kwenye shimo kwa kipimo cha debe moja hadi mbili kwa kila shimo.

Mifumo ya Upandaji
Zao la vanilla huweza kupandwa shambani kwa kutumia mifumo mikuu mitatu ifuatayo:

(i) Vanilla Pekee
Mfumo huu unahusisha upandaji wa mmea wa vanilla na miti ya kuegemea tu ambayo hutoa kivuli kwa mimea.

(ii) Vanilla na Migomba
Mfumo huu unawezesha kuotesha vanilla katika shamba la migomba, ambapo rando hupandwa pamoja na mti wa kuegemea ndani ya shamba la migomba. Na hivyo kukuwezesha kufanya kilimo cha migomba na vanilla katika shamba moja kwa wakati mmoja

(iii) Vanilla na Miti ya Kivuli
Katika mfumo huu vanilla huoteshwa katika shamba la miti ya kivuli, ambapo mmea hupandwa na miti ya kuegemea katikati ya miti ya kivuli.

Kumbuka: Mfumo wa pili na wa tatu unapendekezwa zaidi kutokana na matokeo yake mazuri.

Upandaji wa Miti ya Kuegemea (miega)
Miti ya kuegemea hupandwa miezi miwili hadi mitatu kabla ya kupanda rando la vanilla ili iweze kuchipua, kutoa kivuli na kuwa na uwezo wa kuhimili mimea.

(i) Sifa za Miega
Miti inayofaa kutumika kwa kuegemea iwe na sifa zifuatazo:
  • Uwezo wa kukua haraka bila kuathiri mmea wa vanilla.
  • Uwezo wa kutoa kivuli kinachofaa.
  • Uwezo wa kuchipua haraka inapopunguzwa.
  • Uwezo wa kuchipua matawi kwa chini ili kupandishia marando kwa urahisi.
  • Uwezekano wa kuoteshwa kwa urahisi.
Miti yenye sifa hizo ni pamoja na mibono (Jatropha carcus) na Gilirisidia. Miti mingine inayoweza kutumika kwa kivuli na kuegemea ni pamoja na Erythrina spp na Bauhania spp.

(ii) Kupanda Miega ya Mibono
Miti inayotumika zaidi katika mashamba ya vanilla ni jamii ya Jatropha. Miti hii huoteshwa kwa kutumia mbegu au kipande cha tawi kwa umbali wa sentimita 30 kutoka katika shimo la kupandia vanilla. Tawi la mbono lenye urefu wa sentimita 120 hadi 150 hupandwa katika kina cha sentimita10 hadi 15.

Upandaji wa Vanilla
Mmea wa vanilla hupandwa mwanzoni mwa msimu wa mvua ili kuhakikisha upatikanaji wa unyevu ardhini. Hupandwa kwa kutumia rando lenye urefu wa kati ya sentimita 100 hadi 150 (futi tatu na nusu hadi tano) kutoka kwenye mmea unaokuwa vizuri, usio na magonjwa na wenye pingili ndefu. Rando lenye sifa hizo hukua haraka na kutoa maua mapema (miaka 2). Rando fupi halikui haraka na huchukua muda mrefu kutoa maua (miaka 2 hadi 3).

Kutayarisha Marando
  • Kata rando kwa kutumia kisu kikali kwa kufuata vipimo (sentimita 100 hadi 150).
  • Ondoa majani matatu hadi matano katika sehemu ya chini ya rando itayofukiwa kwenye udongo.
  • Ning'iniza rando lililokatwa kwenye kivuli kwa muda wa siku saba hadi 10 kabla ya kupanda ili kupunguza utomvu na kulipa nguvu ya kuchipua na kuhimili hali ya shambani.
Jinsi ya Kupanda
Upandaji wa vanilla hufanywa kwa kutumia hatua zifuatazo:
  • Andaa nyasi kavu (matandazo) ambazo zitatumika mara baada ya kupanda.
  • Tengeneza kifereji chenye kina cha sentimita 10 hadi 12 katikati ya shimo lenye mbolea lililokwisha tengenezwa.
  • Laza sehemu ya rando iliyotolewa majani katika kifereji hicho, acha sehemu yenye majani juu ya ardhi.
  • Fukia rando kwenye kifereji kwa udongo na gandamiza taratibu ili lishikamane na udongo.
  • Funga sehemu ya juu ya rando kwa kutumia kamba katika umbile la nane kwenye mti wa kuegemea.
  • Weka matandazo kuzunguka kila shina lililopandwa.
Kumbuka:
  • Utaratibu huu wa kupanda hutumika katika aina zote za mifumo ya kuzalisha vanilla, na hutofautiana kwa nafasi za upandaji kati ya mfumo mmoja na mwingine.
  • Shamba la vanilla pekee katika miaka ya mwanzoni, huweza kuchanganywa katikati ya mistari na mazao mengine ya muda mfupi kama mazao ya jamii ya mikunde.
Utunzaji wa Shamba
Vanilla huhitaji kutunzwa vizuri ili iweze kukua vizuri na kutoa mavuno yenye ubora wa hali ya juu. Huduma muhimu katika uzalishaji wa vanilla ni kama ifuatavyo:

Kutengeneza Kivuli
Mmea wa vanilla huhitaji kivuli ili uweze kukua vizuri. Hivyo ni muhimu kupanda miti ya kivuli kabla ya kustawisha vanilla. Katika ukuaji wake kuanzia inapopandwa hadi inapokaribia kutoa maua huhitaji kivuli cha kutosha kinachoweza kuzuia jua kali na kuruhusu mwanga (asilimia 60 hadi 70).

Kipindi cha kusisimua kivuli kipunguzwe zaidi na kufikia asilimia 55 hadi 50. Kivuli kitengenezwe kwa kupunguza matawi ya miti ya miega na ya kivuli ili kupata kivuli kinachofaa.

Kumbuka: Kivuli kizito huathiri ukuaji wa mmea.

Kuweka Matandazo
Utandazaji wa nyasi ni muhimu katika shamba la vanila kutokana na tabia ya ukuaji wa mizizi ambayo huota katika kina cha sentimita 5 hadi 10, hivyo huhitaji kulindwa isiharibiwe. Matandazo yawekwe kuzunguka mashina ya mimea ili kuhifadhi unyevu, kuzuia uotaji wa magugu, na kulinda mizizi isiharibiwe wakati wa palizi.

Kumbuka: Matandazo yawe makavu na yasiwe na mbegu za magugu.

Palizi
Palizi hufanyika wakati wowote magugu yanapoota shambani. Inashauriwa kufanya palizi kabla ya mvua kunyesha ili mmea uweze kutumia maji ya mvua ipasavyo. Palizi ifanyike wakati wowote magugu yanapoota shambani, kwa kungíoa magugu kutumia mikono ili kuepuka kujeruhi mizizi jembe linapotumika.

Kuning’iniza Marando
Mmea wa vanilla uliokua vizuri huota matawi (marando) mengi na marefu. Marando hayo huelekezwa kwenye matawi ya miti ya kuegemea na kuningíinizwa. Rando linapofikia urefu wa sentimita 150 hadi 180 liningíinizwe katika matawi ya miega ili liendelee kukua kuelekea chini. Endapo kuna upepo mkali, marando yafungwe kwenye miega kwa muda ili yasivunjike.

Kulisha Marando
Kulisha marando ni kitendo cha kufukia ardhini sehemu ya kipande cha rando ili kiweze kutoa mizizi na kuongeza nguvu ya kuchukua chakula kutoka kwenye udongo. Kazi hii hufanywa baada ya rando lililoningíinizwa kurefuka sana kiasi cha kutambaa ardhini, katika hatua hii mmea huweza kuwa na umri wa miezi sita hadi tisa kutegemea na utunzaji.

Jinsi ya Kulisha
  • Ondoa majani matatu hadi manne kwenye rando lililoingíinizwa na kurefuka sana.
  • Fukia kwenye udongo, karibu na shina sehemu iliyoondolewa majani.
  • Weka matandazo katika sehemu iliyofukiwa ili kuhifadhi unyevu.
  • Funga sehemu ya juu ya rando katika mti wa kuegemea ili liendelee kukua.
  • Marando mawili hadi mitatu yalishwe kwa wakati mmoja na mengine yaachwe kwa ajili ya kutoa maua na kupata marando ya kupanda.
Kumbuka: Kulisha kufanyike wakati wa mvua ili marando yaweze kutoa mizizi kwa urahisi. Kazi hii irudiwe kila wakati ili rando mama litakapokatika machipukizi yake yaendelea kukua.

Kusisimua
Kusisimua ni kitendo cha kuufanya mmea kuwa katika hali ya kuweza kutoa maua. Kitendo hiki kifanywe wakati mmea ukiwa umefikia umri wa mwaka 1 na nusu au zaidi, na hufanywa wakati wa kiangazi ili kuepuka kupata matawi mengi badala ya vitumba vya maua. Mmea usiosisimuliwa hautoi maua au hutoa maua machache na kusisimua mapema kunaweza kuuchosha mmea.

Jinsi ya Kusisimua
  • Chagua matawi matatu hadi matano yanayoningíinia. Kusisimua matawi mengi kunaweza kuudhoofisha mmea au kuzaa maharage madogo.
  • Kata ncha ya rando ili kuwezesha vitumba vya maua kukua na kuwa tayari kufunguka au kutoa maua.
Ukataji wa ncha huweza kufanyika kama ifuatavyo:
  • Kukata ncha ndogo (mdomo wa rando) kwa mkono. Hii hufanyika kwa rando fupi linaloningínia.
  • Kukata rando kwa kisu kikali, kwa rando linaloningínia ambalo halijafikia urefu wa kupanda.
  • Kukata rando kwa kisu kikali kwa rando refu linaloningíinia (lenye urefu wa kuweza kupandwa, sentimita100-150).
Uchavushaji
Ni kitendo cha kuunganisha chavua kutoka katika sehemu dume ya ua na kuweka katika sehemu jike ya ua, hufanyika baada ya maua kuchanua.

Uchanuaji wa Maua
Mmea wa Vanilla hutoa maua miezi miwili hadi mitatu baada ya kusisimuliwa. Maua huchanua kwa kipindi cha masaa matatu hadi manne kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu kutegemea unyevu uliopo kwenye udongo na kiwango cha Jua.

Ua huchanua kwa muda huo na hudondoka baada ya siku 1 ikiwa halikupata chavua. Hivyo ni muhimu uchavushaji ufanyike kwa haraka na kwa uangalifu mkubwa.

Jinsi ya Kuchavusha
Mmea wa vanilla, ili uweze kutoa matunda inabidi uchavushwe. Ua la vanilla kwa kawaida huchavushwa na nyuki jamii ya melapona ambao hawapo hapa nchini. Nyuki hao hupatikana Mexico na katika nchi nyingine za Amerika ya Kati. Hivyo uchavushaji hufanywa kwa mikono kwani umbile la ua haliruhusu nyuki wa aina nyingine kufanya uchavushaji.

Uchavushaji hufanywa kwa kufuata hatua zifuatazo:
  • Gawa petali ya ua la vanilla katika sehemu mbili kwa kutumia pini, sindano, au mwiba. Hakikisha vifaa hivyo ni safi.
  • Kunjua sehemu jike ya ua (stigima) kwa kuelekea juu ili kuwezesha kulala sambamba kwenye sehemu dume ya ua (stameni).
  • Unganisha stameni na stigima na kubana taratibu kwa dole gumba kwa nusu dakika ili kuruhusu chavua kuingia kwenye stigima.
Ua lililochavushwa vizuri, hubaki likiningíinia kwenye kikonyo chake. Ikiwa uchavushaji haukufanikiwa, ua hudondoka baada ya siku moja au mbili. Kiasi cha maua au mapodo nane hadi 12 yaachwe katika kila kitumba. Aidha vitumba vinne hadi nane viruhusiwe kukua katika kila rando na visizidi 20 kwa mmea.

Ndugu yangu mkulima hivi ndivyo vanilla inavyolimwa, ni shughuri nzito sana lakini inalipa sana, kama ilivyo kawaida: mvumilivu hula mbivu. Sasa badilishana nasi uzoefu wako wa kilimo hiki kwa ku-coment hapa chini huku ukisubiri muendelezo wa kilimo cha vanilla.

MAGONJWA, WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU
Mmea wa vanilla kwa kawaida haushambuliwi mara kwa mara na magonjwa au wadudu waharibifu kama shamba limetunzwa vizuri. Mashambulizi ya magonjwa na wadudu waharibifu ni dalili ya utunzaji duni wa shamba.

Ili kuepuka hali hiyo, ni muhimu kukagua shamba kila wakati kubaini na kurekebisha yafuatayo:
  • Nafasi kati ya mmea na mmea ni ya kutosha kuruhusu mzunguko wa hewa safi na hivyo kupunguza hali inayoruhusu vimelea vya magonjwa kuishi na kuzaliana.
  • Kivuli kisiwe kizito ili kuepuka giza linalowavutia wadudu waharibifu na kuruhusu vimelea vya magonjwa.
  • Kivuli chepesi husababisha kuungua kwa majani na kufanya mmea kutokua vizuri
  • Afya ya mmea ikaguliwe kwa makini.
Kulisha marando kila mara kunaongeza uwezo wa mizizi kuchukua chakula ardhini hivyo mmea hukua vizuri. Mmea wenye afya nzuri haushambuliwi na magonjwa pia hustamilii mashambulizi ya wadudu waharibifu.

Magonjwa
(i) Kuoza kwa Mizizi (Root rot)
Ugonjwa huu husababishwa na kuvu inayoitwa Fusarium batatis Woollenw.var. vanillae Tucker.

Dalili
  • Mmea kunyauka na majani kuningíinia.
  • Majani kubadilika rangi na kuanza kuwa ya manjano na hatimaye kukauka.
  • Mmea kunyauka sehemu ya chini iliyo kati ya shina na mizizi. Zao la vanilla lina thamani kubwa sana sokoni, lakini ni vizuri ufanye utafiti juu ya bei na soko lake kabla hujaanza uzalishaji. Hii itakupa uhakika na matumaini ya kukifanya kilimo hiki kwa moyo zaidi!
Kudhibiti
  • Ondoa maji yaliyotuama.
  • Epuka kujeruhi mizizi.
  • Tumia dawa za ukungu kama Bordeaux mixture 5%.
(ii) Chule ya Majani, Matunda (Anthracnose)
Ugonjwa huu husababishwa na aina ya kuvu inayojulikana kama Calospora vanillae Massee.

Dalili
  • Mapodo na majani kuwa na madoa ya rangi ya kahawia.
  • Majani na ncha ya juu ya shina hunyauka.
  • Mizizi na mapodo na hunyauka
  • Mapodo hudondoka
Kudhibiti
  • Kuzuia maji yasituame ardhini
  • Kutengeneza kivuli chepesi,
  • Kupunguza matawi
  • Kuzingatia nafasi kati ya mmea na mmea ili kuruhusu hewa safi kupita vizuri.
  • Kunyunyizia dawa aina ya Bordeaux mixture (1%) au Captafol 0.1% kabla ya mimea kuchanua.
(iii) Ubwiri Vinyoya (Downy mildew)
Husababishwa na kuvu aina ya Phytophthora jatrophae Jens ambao hushambulia mti wa Jatropha unaotumika kama muega. Pia hushambulia mapodo yakiwa shambani na baada ya kuvunwa.

Dalili: Mapodo ya vanilla na majani ya jatropha huwa ukungu mweupe.

Kudhibiti
  • Kufuata kanuni bora za utunzaji wa shamba.
  • Kutumia dawa za ukungu kama Nitrophenol 0.518
Wadudu, Ndege na Wanyama Waharibifu

(i) Wadudu
Wadudu wanaoweza kushambulia vanilla ni pamoja na katapila na jongoo.
  • Katapila: Hukata ncha ya mmea inayokua
Kudhibiti: Kagua shamba mara kwa mara ili kutambua kuwepo kwa wadudu hao na kuwaua.
  • Jongoo: Hukwangua shina na kuacha michubuko
Kudhibiti: Kagua shamba mara kwa mara na kuwaua.

(ii) Ndege: Kuku
Huharibu mmea kwa kuparura juu ya ardhi na kusababisha kujeruhi na kukata mizizi. Uharibifu huu husababisha mmea kuwa katika mazingira rahisi ya kushambuliwa na vimelea kama Fusarium batatis ambao huozesha mizizi ya mmea.

Kudhibiti: Zuia kuku wasiingie shambani.

(iii) Konokono
Husababisha uharibifu zaidi kipindi cha mvua. Wanapotambaa kwenye mmea huacha utando, hasa katika sehemu inayochipua na kusababisha mmea kudumaa.

Kudhibiti
  • Kagua shamba mara kwa mara na kuwaondoa.
  • Weka mchanganyiko wa mbolea ya samadi na majivu kuzunguka shina la mmea ili kuzuia wasiweze kupanda juu ya mimea.
UVUNAJI
Mapodo ya vanilla hukomaa na kuwa tayari kuvunwa baada ya miezi sita hadi tisa tangu maua kuchavushwa.

Hatua za Kukomaa kwa Vanilla

Ukomaaji wa podo (harage la Vanilla) la vanilla hupitia hatua tano zifuatazo:
  1. Podo hurefuka na kuwa na rangi ya kijani iliyokolea.
  2. Ncha ya podo hubadilika na kuwa njano.
  3. Rangi ya njano husambaa taratibu katika podo.
  4. Ncha ya podo hubadilika rangi na kuwa ya kahawia
  5. Podo hupasuka kuanzia chini.
Jinsi ya kuvuna

Uvunaji wa zao la vanilla huzingatia hatua za ukomaaji wa podo na njia ya ukaushaji itakayotumika. Mapodo huvunwa kwa kukata kikonyo kutumia kisu kidogo.
  • Katika hatua ya kwanza ya ukomaaji, mapodo hayana vanillin ya kutosha hivyo yasivunwe katika hatua hiyo.
  • Mapodo yanaweza kuvunwa yakiwa katika hatua ya pili na ya tatu endapo yatakaushwa kwa njia ya Bourbon.
  • Mapodo yanayokaushwa kwa njia ya kukata na kukausha haraka huvunwa yakiwa katika hatua ya pili, ya tatu na ya nne. Mapodo yasiachwe hadi kufikia hatua ya tano ya ukomaaji kwani ubora wake hupungua.
  • Uvunaji ufanyike kila baada ya siku moja hadi mbili ili kuepuka kupasuka kwa mapodo.
  • Uvunaji huendelea kwa muda wa miezi miwili mfululizo au zaidi kulingana na ukomaaji wa mapodo.
  • Marando yaliyosisimuliwa na kutoa mapodo yakatwe na kuondolewa shambani baada ya kuvunwa.
Mavuno
Mavuno ya zao la vanilla hutofautina kulingana na umri wa mmea na utunzaji wa shamba. Mavuno ya kwanza huanza kati ya miaka miwili na nusu hadi mitatu kwa wastani wa kilo moja sawa na mapodo 50 hadi 60. Mmea unapofikia umri wa miaka minne hadi nane, mavuno huongezeka kufikia kilo tatu hadi tano kwa mmea. Hata hivyo mavuno huweza kupungua mmea unapofikia miaka 15 na kuendelea. Hekta moja ya shamba la vanilla lililotunzwa vizuri hutoa mavuno tani tatu hadi tano za mapodo mabichi sawa na wastani wa kilo 500 hadi 800 za mapodo yaliyokaushwa kwa mwaka.

UKAUSHAJI NA UHIFADHI

Mapodo ya vanilla hukaushwa kwa njia mbalimbali kulingana na utaalamu unaotumika, vifaa vilivyopo na matakwa ya mnunuzi. Ili kupata ubora unaotakiwa, mapodo yakaushwe mara baada ya kuvunwa. Njia za ukaushaji zinazotumika zaidi ni Bourbon na Mexico. Njia hizi huhitaji uangalifu na utaalamu wa kutosha ili kupata madaraja mbalimbali, ladha, na harufu inayohitajika. Njia zote mbili hupitia katika hatua kuu nne za ukaushaji. Hapa nchini, njia ya ukaushaji inayotumika kwa sasa ni Bourbon.

Ukaushaji kwa Njia ya Bourbon

Njia hii ya ukaushaji huhusisha hatua zifuatazo:

Kuchovya Mapodo kwenye Maji moto (Blanching)

Hatua hii huyazuia mapodo yasiendelee kukomaa na kuanza kutoa ladha.
  • Mapodo mabichi hupangwa kulingana na ukubwa na hatua za ukomaaji.
  • Mapodo hayo hupangwa katika mafungu yasiyozidi uzito wa kilo 30 ili kurahisisha uchovyaji.
  • Mapodo huwekwa na kufungwa katika mifuko ya vitambaa maalumu vinavyoruhusu joto la maji kupenyeza kwa urahisi.
  • Mapodo yaliyovunwa katika hatua ya pili, tatu, na nne ya ukomaaji, yatumbukizwe katika maji yenye joto la nyuzi 60 hadi 65 za Sentigredi kwa muda wa dakika tatu hadi tatu na nusu.
  • Mapodo yaliyovunwa katika hatua ya tano ya ukomaaji, yatumbukizwe kwenye maji ya moto kwa muda usiozidi dakika moja.
  • Mapodo yaliyochovywa kwenye maji ya moto vizuri, huwa na rangi ya kijani iliyokolea hadi kahawia.
Kuhifadhi Joto (sweating)

Lengo la hatua hii ni kuongeza joto katika mapodo ili kuruhusu vimengíenya (enzymes) kufanya kazi ya kutoa kemikali ya vanillin ambayo huongeza ladha na harufu inayohitajika.
  • Mapodo yaliyochovywa maji moto hutolewa maji na kufungashwa katika vitambaa vyeupe na mablanketi yanayoweza kuhifadhi joto.
  • Mapodo huwekwa kwa muda wa siku moja hadi mbili (saa 24 hadi 48) katika makasha maalumu yanayohifadhi joto.
  • Mapodo hutolewa kwenye makasha baada ya siku moja au mbili na kutandazwa ili kuondoa yasiyo na rangi ya kahawia.
  • Katika hatua hii, mapodo huwa na rangi ya kahawia iliyokolea.
Kukausha

Katika hatua hii, mapodo huanikwa asubuhi au jioni wakati jua sio kali.
  • Mapodo yaliyofungashwa kwenye vitambaa vyeupe na mablanketi hutandazwa juu ya vichanja na kuanikwa kwa muda wa saa moja au mbili.
  • Baada ya saa moja au mbili, mapodo hufungashwa tena kwenye mablanketi na kurudishwa ndani. Kazi hii huendelea kwa muda usiopungua wiki tatu.
  • Baada ya wiki tatu, mapodo hutandazwa ndani, juu ya vichanja vinavyoruhusu hewa ya kutosha.
  • Ukaushaji wa ndani huchukua muda wa miezi mawili au mitatu.
  • Ukaguzi ufanywe mara kwa mara ili kuondoa mapodo yenye hitilafu na kutenga yaliyowahi kukauka.
Kuhifadhi Ladha
Hii ni hatua ya mwisho katika mtiririko mzima wa ukaushaji. Katika hatua hii, mapodo huwekwa katika makasha maalumu kwa muda wa miezi mitatu hadi mitano ili kuongeza ladha ya vanilla.

Kufungasha
Vanilla iliyokwisha kaushwa vizuri hufungashwa kulingana na madaraja. Uzito wa kila kifungu na aina ya ufungashaji hutegemea mahitaji ya soko.
 
Mnunuzi wa hili zao ni Nani?
Kuna makampuni kadhaa yananunua vanilla. Makampuni ya chai, biscuit, ice cream na baadhi wanaoprocess maziwa wanahitaji vanilla. Lakni huwezi kwenda kumuuzia vanilla ukiwa peke yako. Namaanisha muwe kwenye group, hapo mtauza in bulk. Moshi wanalima, bukoba pia. Kwa Bukoba kuna MAYAWA na Maruku farming&processing na KAVANIFA wilayan Muleba wananunua vanilla
 
Kuna makampuni kadhaa yananunua vanilla. Makampuni ya chai, biscuit, ice cream na baadhi wanaoprocess maziwa wanahitaji vanilla. Lakni huwezi kwenda kumuuzia vanilla ukiwa peke yako. Namaanisha muwe kwenye group, hapo mtauza in bulk. Moshi wanalima, bukoba pia. Kwa Bukoba kuna MAYAWA na Maruku farming&processing na KAVANIFA wilayan Muleba wananunua vanilla


Mkuu kuna factors nyingi nyingi za kuconsider.Tukianza na mfano ni mikoa IPI labda ili zao linastawi.Manake Kwa ufatiliaji wangu Kwa Africa mainland ni nchi ya Uganda tu ambayo imejikita kwenye kilimo cha zao hili.Na Uganda wao wapo kwenye Tropic region.

Suala LA msingi linakuja je mi mikoa IPI hapa Tanzania zao hili linaweza kustawi?
 
Mkuu kuna factors nyingi nyingi za kuconsider.Tukianza na mfano ni mikoa IPI labda ili zao linastawi.Manake Kwa ufatiliaji wangu Kwa Africa mainland ni nchi ya Uganda tu ambayo imejikita kwenye kilimo cha zao hili.Na Uganda wao wapo kwenye Tropic region.

Suala LA msingi linakuja je mi mikoa IPI hapa Tanzania zao hili linaweza kustawi?
Mikoa ya Kagera, Kilimanjaro, Mbeya, Morogoro wanalima mpaka leo. Infact mikoa yenye hali ya mvua nyingi na milima vanilla inastawi.
 
Mikoa ya Kagera, Kilimanjaro, Mbeya, Morogoro wanalima mpaka leo. Infact mikoa yenye hali ya mvua nyingi na milima vanilla inastawi.

Nimekupata vizuri mkuu.


Sisi wajasiriamali tunapoangaza kwenye kazi mbali mbali huwa tunaanza kuanalyse key points/hints za biashara husika kabla ya kuchimbua zaidi.

Kwa taarifa za awali nilizopata ni kuwa hili zao ni labour intensified throughout the year.Kwa hapa Africa nchi inayoongoza Kwa uzalishaji wa vanilla ni Madagascar.

Katika kufuatilia zaidi inadaiwa kuwa hili zao lina mahitaji makubwa ya nguvukazi.
Na huko Madagascar wamefanikiwa kufikia uzalishaji mkubwa sababu kuna very cheaper labor costs (kibarua wa huko analipwa 1.5 US$ Kwa siku).

Ndio maana inabidi tujiulizie hivi Kwa bei nzuri ya zao hili na soko linavovutia inakuwaje nchi inayoongoza iwe kutoka Africa na sio Asia ambao huwa hawaachii fursa?

Hivi kibarua gani wa TZ atakubali malipo ya shilingi elfu tatu(US$1.5) Kwa siku?

Inabidi kukaa chini na kuchimbua zaidi kama sisi ni GT's kweli wa JF.Otherwise naweza kusema hili zao ni fursa mpya sababu linasoko zuri na la uhakika zaidi.Ila kujiingiza katika kilimo cha zao hili bila mipango sahihi unaweza kukuta mi kama unaweka hela kwenye kibubu.

Ciao!!!!!!!
 
Middlemen wabaya sana wananunua kwa wakulima ikiwa bado kijani halafu wanaenda kui process ingawa inakuwa low quality.
Wakulima wameamua wengi wao kuyachoma moto na kujikita kwenye mazao mengine.

Vanilla kwa kg inaweza fika $500.
Ni zao lenye faida sana lakini mda mwingi bei hushuka kwa kasi you can't predict
 
Nimekupata vizuri mkuu.


Sisi wajasiriamali tunapoangaza kwenye kazi mbali mbali huwa tunaanza kuanalyse key points/hints za biashara husika kabla ya kuchimbua zaidi.

Kwa taarifa za awali nilizopata ni kuwa hili zao ni labour intensified throughout the year.Kwa hapa Africa nchi inayoongoza Kwa uzalishaji wa vanilla ni Madagascar.

Katika kufuatilia zaidi inadaiwa kuwa hili zao lina mahitaji makubwa ya nguvukazi.
Na huko Madagascar wamefanikiwa kufikia uzalishaji mkubwa sababu kuna very cheaper labor costs (kibarua wa huko analipwa 1.5 US$ Kwa siku).

Ndio maana inabidi tujiulizie hivi Kwa bei nzuri ya zao hili na soko linavovutia inakuwaje nchi inayoongoza iwe kutoka Africa na sio Asia ambao huwa hawaachii fursa?

Hivi kibarua gani wa TZ atakubali malipo ya shilingi elfu tatu(US$1.5) Kwa siku?

Inabidi kukaa chini na kuchimbua zaidi kama sisi ni GT's kweli wa JF.Otherwise naweza kusema hili zao ni fursa mpya sababu linasoko zuri na la uhakika zaidi.Ila kujiingiza katika kilimo cha zao hili bila mipango sahihi unaweza kukuta mi kama unaweka hela kwenye kibubu.

Ciao!!!!!!!
Kuna vibarua wanalipwa 75,000 kwa mwezi sawa na 2,500 kwa siku.
 
hiti, Madagascar, Indonesia, and other tropical locations. Growing vanilla at home does require some time and effort, but it’s worth the reward of fragrant and delicious vanilla beans!



Part 1
Creating the Right Environment

  1. Image titled Grow Vanilla Step 1
    1
    Construct a greenhouse if you don’t live in a tropical climate. Vanilla orchids require a tropical environment, so you will need sunlight, heat, space, and humidity for the plants to grow. Choose a location with morning sun and build the structure yourself or from a greenhouse kit. Cover the structure with UV-stabilized polyethylene or fiberglass or add glass panels.[1]
    • If you live in a tropical climate, you may be able to cultivate vanilla outside. Check the temperature and humidity of your environment to determine if the conditions are suitable for a vanilla orchid.

  2. Image titled Grow Vanilla Step 2
    2
    Keep the temperature above 65 °F (18 °C). Vanilla orchids will thrive in climates with daytime temperatures between 80–85 °F (27–29 °C). At night, temperatures should remain between 65–75 °F (18–24 °C).[2] To decrease the temperature in a greenhouse, you can open vents or turn on fans. To increase the temperature in a greenhouse, you can add heat lamps or a heater.[3]


  3. Image titled Grow Vanilla Step 3
    3
    Maintain an 85% humidity level. Vanilla orchids need high humidity levels to grow properly. Use a hygrometer to measure the humidity in the greenhouse or planting location. If it is below 85%, add a humidifier to the area. If the humidity is above 85%, use a dehumidifier to reduce the humidity.[4]


Part 2
Planting the Cutting

  1. Image titled Grow Vanilla Step 4
    1
    Purchase a 15–20 in (38–51 cm) vanilla cutting. If you don’t have a local florist or garden center that sells cuttings from vanilla orchids, you may need to order them online. For best results, choose a cutting that is 15–20 inches (38–51 cm) long. It’s a good idea to purchase several cuttings in case some of them don’t make it.[5]
    • Cuttings are usually taken from mature plants that are 20 feet (6.1 m) or more in length.
    • Be sure to ask the supplier which end of the cutting is the top and which is the bottom if you are unsure. The top is the direction in which the plant has been growing. The leaves will point down toward the bottom of the cutting.

  2. Image titled Grow Vanilla Step 5
    2
    Fill a small pot with a mix of fir bark and peat moss. Fir bark and peat moss will ensure that the soil has good drainage. Alternatively, you could use a potting medium formulated for orchids. Keep in mind that orchids do better in small pots rather than in large ones or directly in the soil.[6]
    • All of these materials are available at garden shops and home improvement stores.

  3. Image titled Grow Vanilla Step 6
    3
    Test the potting medium to ensure it has a neutral pH. Vanilla orchids thrive in a potting medium with a neutral pH of 6.6 to 7.5.[7] To test the pH of the soil, you can use a commercial test probe or paper test strips, both of which are available at your local garden center and online. If you need to adjust the pH, add lime to increase the alkalinity or add organic matter (like more peat moss) to increase the acidity.

  4. Image titled Grow Vanilla Step 7
    4
    Plant the vanilla orchid cutting in the pot. Bury the bottom 2 leaf joints, or nodes, of the plant about 1 inch (2.5 cm) into the potting medium. Lightly tamp down the potting medium with your hands to stabilize the cutting.[8]

  5. Image titled Grow Vanilla Step 8
    5
    Water the orchid lightly with distilled water after planting. It’s important that you don’t oversaturate the orchid, which could lead to root rot. Water the orchid lightly, rather than deeply, just until the potting medium is moist. Always use distilled water, as the minerals in tap water aren’t good for plants.[9]

Part 3
Caring for the Vanilla Orchid

  1. Image titled Grow Vanilla Step 9
    1
    Place the pot in an area with 6 hours of indirect sunlight per day. Vanilla orchids will get scorched if you place them in direct sunlight. To prevent this, choose an area of the greenhouse with bright, but indirect, sunlight. A location with dappled, but not deep, shade that gets at least 6 hours of sun per day is ideal.[10]

  2. Image titled Grow Vanilla Step 10
    2
    Install a trellis next to the orchid to allow the vines to climb. Vanilla orchids are a climbing vine, so they’ll need a trellis to support them. Alternatively, you could position the pot near a stake or a tree so the vines can climb that. The vanilla orchid must be trained to grow vertically, so you’ll need to gently secure the plant to the the trellis, stake, or tree using plant ties or clips.[11]
    • You can purchase ties or clips online or at a gardening store.

  3. Image titled Grow Vanilla Step 11
    3
    Allow the potting medium to dry out between waterings or mist it daily. Wait until the top 2–3 inches (5.1–7.6 cm) of potting medium has dried before watering the orchid again. After watering, the soil should be moist but not soggy. Alternatively, you could mist the orchid daily with distilled water from a spray bottle. Lightly spray the soil, stem, and leaves of the plant.[12]

  4. Image titled Grow Vanilla Step 12
    4
    Apply liquid fertilizer to the plant “weakly, weekly.” To ensure your orchid will bloom and develop vanilla beans, you should fertilize it regularly. Fertilizing “weakly, weekly” means adding a diluted amount of fertilizer (about half as strong as the package directs) once every 7 days. When the plant is actively growing, use a high-nitrogen (30-10-10) liquid fertilizer. When the orchid is not in active growth, use a 10-10-10 fertilizer.[13]

  5. Image titled Grow Vanilla Step 13
    5
    Allow the vanilla orchid to grow and mature for 2-7 years. As the orchid grows, air roots (which are roots that grow above the soil) will attach upward to the support and others will reach down to the soil. It will take between 2-7 years for the plant to grow large enough to bloom, as it must reach 20–40 feet (6.1–12.2 m) in length. Don’t despair, though, the time and effort is worth it![14]
    • During this time, water and fertilize the vanilla orchid as before.

Part 4
Pollinating the Flowers

  1. Image titled Grow Vanilla Step 14
    1
    Pollinate the vanilla orchids when they develop clusters of flowers. The vanilla orchid only flowers for one 6-week period per year. Additionally, the flowers only last approximately 1 day! This means you’ll need to keep a close eye on the orchid, checking it daily for flowers. When it does flower, you will need to hand-pollinate the flowers in order to grow the vanilla beans.[15]

  2. Image titled Grow Vanilla Step 15
    2
    Push the anther up and place the pollen on the ridge. It’s best to pollinate the flowers in the morning, around 11 o’clock. Push the pollen mass out and hold it up with your right thumb and index finger. Use your middle finger to push the anther back and expose the cam underneath it, which serves as a shield. Place the pollen on the ridge. Push the ridge back into place with your left hand and pull the cap back down. Repeat with all the flowers.[16]
    • Sap from orchid roots and flowers can irritate the skin. Wear gloves and be cautious when replanting or pollinating the plant.[17]
    • Consider asking a local orchid grower to help you hand-pollinate the first few times as it is a very delicate process.

  3. Image titled Grow Vanilla Step 16
    3
    Look for stems that face downward to indicate successful pollination. Check the orchid the day after pollination. The flowers should not fall off, but they will wither and turn dark brown. If the stem begins to elongate instead of point up, it is pollinated. If you don’t see a change, you may need to re-pollinate the flower.[18]

Part 5
Harvesting Vanilla Beans

  1. Image titled Grow Vanilla Step 17
    1
    Pick the pods when they begin to turn yellow at the bottom. The pods will appear within 2 months of pollination, but they take 6-9 months to mature. During this time, care for the plant as you normally would. Then, when the pods, normally green, are just starting to turn yellow, carefully pluck them off the plant.[19]

  2. Image titled Grow Vanilla Step 18
    2
    Blanch the beans for 2-5 minutes in 158 °F (70 °C) water. Heat a pot of water to 158 °F (70 °C). Submerge the beans for 2-5 minutes, then carefully remove them. This kills any germs or bacteria, and also prepares the beans for curing.[20]

  3. Image titled Grow Vanilla Step 19
    3
    Sweat the beans for 36-48 hours in a blanket-lined box. After blanching the beans, transfer them to a box lined with a blanket. A bamboo box and woolen blankets are best, but you can use whatever you have on hand. Allow the beans to “sweat” inside the blankets and box for 36-48 hours before removing them.[21]
    • The beans will sweat out moisture due to the heat, helping them to dry out.

  4. Image titled Grow Vanilla Step 20
    4
    Alternate drying the beans in the sun and sweating them for 7-14 days. Spread your beans on trays and place them in direct sunlight for 3 hours each day. Then, fold them in a cloth or blanket and put them in a box to allow them to sweat overnight. Repeat the process of drying and sweating each day until the pods turn a deep brown.[22]
    5
    Allow the beans to air dry for 8-20 days at 95 °F (35 °C) and 70% humidity. To further remove moisture from the beans, they should be allowed to air dry fully. Hang them up or spread them out on trays in a drying room. Keep the room at 95 °F (35 °C) and 70% humidity for best results. The beans are done drying when they have a soft, leathery texture and lots of length-wise wrinkles.[23]

How to Grow Vanilla (with Pictures) - wikiHow
 
Back
Top Bottom