Kilimo cha Parachichi - Fahamu Aina, Namna ya Kulima na Masoko

Ha ha ha! huko sawa mkuu wacha tulime parachichi. Umeniacha hoi sehemu hizo wanaishi wajanja.
 
Ha ha ha huko sawa mkuu wacha tulime parachichi. Umeniacha hoi sehemu hizo wanaishi wajanja
Ndio, maeneo yanayokubali parachichi wanaishi Wajanja, mfano. Bukoba parachichi linakubali, je wakuja unaweza pata eka 1000 hivi upige parachichi?

Au njoo Mby, hivi unaweza pata eka 500 sehemu zimekaa tu na wale wakakuangalia hivi hivi !, Hivi ukienda Moshi unatafuta eka kumi za kulima parachichi utapata wapi ambako jamaa zangu hawajapaona? Njombe usije, sababu kumejaa kabisa. Ukishuka Mbinga, ni kasheshe nyingine, avocado inakubali, sasa Wamatengo wale sijui kama wanaweza kukupa eka 100 bila mushikeli. Iringa pande za Kilolo na Mufindi pamejaa. Ukienda Songwe hali kadharika.

Upooooooo
 
Ndio, maeneo yanayokubali parachichi wanaishi Wajanja, mfano. Bukoba parachichi linakubali, je wakuja unaweza pata eka 1000 hivi upige parachichi?

Au njoo Mby, hivi unaweza pata eka 500 sehemu zimekaa tu na wale manyambala wakakuangalia hivi hivi !, Hivi ukienda Moshi unatafuta eka kumi za kulima parachichi utapata wapi ambako jamaa zangu hawajapaona? Njombe usije, sababu kumejaa kabisa. Ukishuka Mbinga, ni kasheshe nyingine, avocado inakubali, sasa Wamatengo wale sijui kama wanaweza kukupa eka 100 bila mushikeli. Iringa pande za Kilolo na Mufindi pamejaa. Ukienda Songwe hali kadharika.

upooooooo
Nipo yanalipa maparachichi sana tu.
 
Kuna miparachichi ya kisasa? Au unatuhamasisha kulima hii miparachichi ya kumaliza miaka 7 kabla ya kuanza kuzaa (kutoa matunda)
 
Chachu Ombara

Kiongozi heshima yako

Nakupa tu taarifa kwamba, siku nyingine unapokopi material toka sehemu moja si mbaya uka aknowledge source

Hii umekopa partlly toka katika hii blog yangu..KILIMO MAARIFA: KILIMO CHA PARACHICHI (AVOCADO), na content hizo hizo zilikuwa katika uzi wangu mama hapa jf kabla moderators hawajaubadilisha content zake Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane

Agronomy ya Parachichi

Hali ya hewa


-Ni tunda linalopenda sana sehemu za baridi, maeneo kama ya Rungwe-Mbeya, Njombe, Makete, linastawi vizuri sana, na huwa na Fatty Contenty kubwa

Joto

Nyuzi 15-25 Sentigrade

Muinuko
Mita 1200-1800 kutoka usawa wa baridi

Udongo
-Uwe kichanga tifutifu (Sandy loam), usiotuamisha maji

Aina za Parachichi
1. Zipo aina za kiasiliKila sehemu kuna iana za parachichi ambazo ni za asili ya eneo husika, parchichi hizi, huwa ndefu sana, na mavuno machache

2. Zipo aina za kisasa (Chotara)
Ziko aina nyingi sana za Parachichi chotara, na hizi hapa chini ni baadhi ya zile maarufu hapa tanzania

i. Hass
-Hii ni aina maarufu sana katika aina za parachichi

View attachment 332265

- Ni tunda linalokuwa na vipere vipere
-Limechongoka juu na chini
-Linahifadhika kwa urahisi

ii. Aina ya pili ni Fuerte

View attachment 332266

-Hili ni aina ya parachichi lenye ngozi laini saini, ngozi yake inateleza kama imepakwa mafuta
-liko na mafuta mengi ila linawahi kuoza
-Ni zuri kwa matumizi ya kawaida , si kwa kusafirisha umbali mrefu
-Aina hii ikilimwa sehemu za miinuko na baridi sana, inafaa sana kutoa mafuta mengi yanayoweza kutumika kutengeza lotion na baadhi ya vyakula vya mifugo

iii. Aina ya tatu maarufu hapa tanzania -inaitwa X-ikulu
-Ana hii ni maarufu sana kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya na Ruvuma)
-Mti wa aina hii huwa na majani mapana kama mti wa embe
-Mti huu huchukua muda mrefu sana kustawi
-Tunda lake huwa ni kubwa, na lina gharama sana

Upandaji wa Parachichi

Nafasi kati ya shimo na shimo


-Umbali wa kutoka shimo hadi shimo ni MITA 7
-UMbali wa kutoka mstari hadi mstari ni MITA 7

Lakini kipimo hicho hapo juu kitategemea sana na aina ya udongo wa shamba lako , kwa udongo wenye Phosphorus kwa wingi (P), kipimo hicho hakifai, maana baada ya mika 3-5 miche ya mistari miwili inayofuatana itakuwa imekuatana katikati

-Hivyo nafasi yaweza kuwa

8M X 8M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 63 KWA EKA 1
AU 9M X 9M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 49 KWA EKA 1
AU 10M X 10M- KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 40 KWA EKA 1

Ukubwa wa shimo-Shimo laweza kuwa futi 2.5 x futi2.5 x futi 2.5 = (sm 75 x sm 75 x sm 75) (Kimo x upana x urefu)

-Au kipimo cha futi 3 x futi 3 x futi 3= sm 90 x sm 90 x sm 90

Mbolea

-Mbolea za kupandia zitakazohitajika , ni moja wapo kati ya hizi
-Samadi, Mboji, DAP, au TSP-Lakini ni muhimu kupandia mbolea asilia kama samadi ukachanganya kidogo na TSP au DAP

Kipimo cha mbolea,
-Kama ni mbolea za asili (Samadi au Mboji)-Kiasi cha kilo 16 hadi 20 kinapaswa kiwekwe katika shimo miezi 3 kabla ya kupanda mche

-Kama utapandia mbolea za viwandani (TSP, DAP, Minjingu, NPK etc)
kiasi cha gramu 100 hadi 200 kiwekwe kwa kila shimo, ichanganywe vizuri na udongo, kisha mmea uwekwe na kumwagiliwa

KUKOMAA NA KUTOA MAVUNO
-Parachichi hasa hizi za kisasa, hukomaa baada ya miezi 18 hadi 24

MAVUNO
-Kwa mara ya kwanza mti mmoja wa parachichi unaweza kukupa kati ya matunda 50 hadi 100 kwa mche mmoja.
-Mavuno hueongezeka kadri umri unavyoongezeka
-Mti wa parachichi ukifikia umri wa miaka 4 hadi 5, unakuwa full maturity, na hivyo mti mmoja unaweza kukupa hadi matunda 1200 kwa mwaka mzima '

FAIDA
kwa kipimo cha mita 10 x mita 10, katika eka mmoja utakuwa na mita 40
-Kila mti baada ya mika 5 unaweza kukupa wastani wa matunda 1000
-Hivyo kwa miti 40, utakuw na jumla ya matunda 40 x 1000= 40,000
-Kila tunda kwa bei ya shambani uuze tsh 250, na unamatunda 40,000
-Hivyo utapata jumla ya tsh 250 x matunda 40,000= 10,000,000tsh (MILIONI 10)

Magonjwa ya parachichi


Parcahichi kama mimea mingine inashambuliwa sana hasa upande wa majani pamoja na matunda.

1. Yapo magonjwa ya majani, yanayosababishwa na fangasi/Ukungu, Algae, pamoja na wadudu, pamoja na lishe duni.


View attachment 332289
Jani lililoshambuliwa na Alga


View attachment 332290
Mite-Utitiri mweupe Avocado lililoshambuliwa na Utitiri

2.Magonjwa ya matunda

View attachment 332291 View attachment 332291

View attachment 332292

-Tatizo la Scab, husababishwa na Ukungu/Fangasi hasa wakati wa baridi/unyevu mwingi

View attachment 332293
Thrips wa avocado Matunda yaliyoathiriwa na Thrips

DAWA
-Dawa za kutibu wadudu kama Karate, Matchi, Actellic 50 EC, za faa sana kumaliza wadudu katika mmea wa parachichi

-Dawa za Ukungu kama Ridomil Gold, Ebony 72 WP (Mancozeb na Metalaxyn), Ivory, na Nordox zaweza kutumika kumaliza matatizo ya ukungu

-Lishe ya mmea

Mbolea za kukuzia kama CAN, UREA NA SA (hasa kwenye maeneo yenye magadi kwa wingi, na chumvi nyingi) yaweza kutumika kubalane PH YA Udongo.

-Booster=Mbolea za majani, maua na matunda kama vile Polyfeed Starter, Polyfeed finisher, Wauxal macro mix, Potphos, au Multi K , Ni muhimu sana zikatumika wakati wa maua, na matunda ili kuzuia matunda ya parachichi kuabort (Fruit abortion) yakiwa machanga, pamoja na kuzuia matunda kudondoka yakiwa machanga.

Hitimisho
Parachichi-Kama matunda mengine, ukililima kitaalamu, na ukaweka juhudi na maarifa linakutoa katika umaskini
 
Wakuu kilimo cha parachichi aina ya hass kwa sasa kinachukua umaarufu hasa kwa mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa, Arusha, Songea na kwingineko.

Mwenye kujua masoko yake hasa nje ya nchi na makampuni yanayonunua tujuzane please.
 
Maneno machache niliyochukua hapo juu. kama unafanya kazi sasa panda parachichi na itakulea zaidi ya pension yako ya kustaafu.
Aksante mdau naendelea kufuatilia kwa ukaribu inaonekana kilimo hiki kina tija faida yake kama unavyosema ni zaidi ya pension.
 
Wakuu, kilimo cha parachichi aina ya hass kwa sasa kinachukua umaarufu hasa kwa mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa, Arusha, Songea na kwingineko mwenye kujua masoko yake hasa nje ya nchi na makampuni yanayonunua tujuzane please
80% ya parachichi zinatoka Kilimanjaro hata Arusha wanatoa Moshi - Dar msimu wake hutokea Kilimanjaro, msimu ukiisha yanaenda fatwa Burundi na mnufaikaji mkubwa sio mkulima ni mtu wa kati na hata ukipanda miti 20 leo hadi ije kuzaa na hata ikizaa siokuja kukupa pensheni mzee.

Gunia la parachichi za Rombo baada ya kufika Dar ni 60,000 hadi 75,000 inategemea na msimu. Sasa kula hesabu gharama ya kutoa shamba hadi Dar na anaeleta Dar ananunua sokoni kwa anaetoa shamba. Kuna za Machame sasa ambazo ndio zinafanana na za Mbeya izo kuiva ni siku 1 tu ukijitekenya zinaivia njiani zinaharibika, ndio maana kuzitoa Mbeya ni jau sana na sio nzuri kama za Rombo na gunia lake ni 45000-50000 zikifika Dar. Sasa jiulize unazopanda ni zipi, Je, zitakupa pensheni?
 
80% ya parachichi zinatoka Kilimanjaro hata Arusha wanatoa Moshi - Dar msimu wake hutokea Kilimanjaro, msimu ukiisha yanaenda fatwa Burundi na mnufaikaji mkubwa sio mkulima ni mtu wa kati na hata ukipanda miti 20 leo hadi ije kuzaa na hata ikizaa siokuja kukupa pensheni mzee.

Gunia la parachichi za Rombo baada ya kufika Dar ni 60,000 hadi 75,000 inategemea na msimu. Sasa kula hesabu gharama ya kutoa shamba hadi Dar na anaeleta Dar ananunua sokoni kwa anaetoa shamba. Kuna za Machame sasa ambazo ndio zinafanana na za Mbeya izo kuiva ni siku 1 tu ukijitekenya zinaivia njiani zinaharibika, ndio maana kuzitoa Mbeya ni jau sana na sio nzuri kama za Rombo na gunia lake ni 45000-50000 zikifika Dar. Sasa jiulize unazopanda ni zipi, Je, zitakupa pensheni?
Mdau, ni sahihi unachozungumza isipokuwa maparachichi kuna varieties nyingi sana zaidi ya 60 lakini ninayozungumzia hapa tagert yake si soko la ndani, najaribu kupata idea tofauti tofauti hapa we nye kujua zaidi hasa aina hii ya parachichi aina ya HASS aina hii huwa haliuzwi kwenye soko la ndani kwasababu ya uhimilivu wa kukaa muda mrefu bila kuiva.

maxresdefault.jpg
 
Kama kuna mtu anategemea kupanda parachichi mwaka huu Wilaya ya Kilolo, basi tuwasiliane, tutakuletea seedlings mpaka shambani kwako, price yetu ni 2500/- kwa mchi. Ni-PM
 
wakuu kilimo cha parachichi aina ya hass kwa sasa kinachukua umaarufu hasa kwa mikoa ya Mbeya,Njombe,Iringa,Arusha,Songea na kwingineko mwenye kujua masoko yake hasa nje ya nchi na makampuni yanayonunua tujuzane please
Rungwe kuna kampuni inanunua na kuna mzungu kapanda shamba kubwa sana la Parachichi. Huko watu wanang'oa baadhi ya mazao na kupanda parachichi. Waliopanda zamani wanapiga sana hela. Hili zao lisipoingiliwa na mabodi ya mazao au makodi nyonyaji litawatoa sana watu. Mexico parachichi zina hela hadi mashamba yanawekewa walinzi wenye bunduki.
 
Wadau,

Nahitaji kulima maparachichi. Kwa mwenye ufahamu zaidi naomba kujua changamoto na nini nifanyeje ili nieweze kufanikiwa.
2. Agronomy ya Parachichi
Hali ya hewa

-Ni tunda linalopenda sana sehemu za baridi, maeneo kama ya Rungwe-Mbeya, Njombe, Makete, linastawi vizuri sana, na huwa na Fatty Contenty kubwa

Joto

Nyuzi 15-25 Sentigrade

Muinuko
Mita 1200-1800 kutoka usawa wa baridi

Udongo
-Uwe kichanga tifutifu (Sandy loam), usiotuamisha maji

Aina za Parachichi
1. Zipo aina za kiasiliKila sehemu kuna iana za parachichi ambazo ni za asili ya eneo husika, parchichi hizi, huwa ndefu sana, na mavuno machache

2. Zipo aina za kisasa (Chotara)
Ziko aina nyingi sana za Parachichi chotara, na hizi hapa chini ni baadhi ya zile maarufu hapa tanzania

i. Hass
-Hii ni aina maarufu sana katika aina za parachichi

View attachment 332265

- Ni tunda linalokuwa na vipere vipere
-Limechongoka juu na chini
-Linahifadhika kwa urahisi

ii. Aina ya pili ni Fuerte

View attachment 332266

-Hili ni aina ya parachichi lenye ngozi laini saini, ngozi yake inateleza kama imepakwa mafuta
-liko na mafuta mengi ila linawahi kuoza
-Ni zuri kwa matumizi ya kawaida , si kwa kusafirisha umbali mrefu
-Aina hii ikilimwa sehemu za miinuko na baridi sana, inafaa sana kutoa mafuta mengi yanayoweza kutumika kutengeza lotion na baadhi ya vyakula vya mifugo

iii. Aina ya tatu maarufu hapa tanzania -inaitwa X-ikulu
-Ana hii ni maarufu sana kwa mikoa ya nyanda za juu kusini (Mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya na Ruvuma)
-Mti wa aina hii huwa na majani mapana kama mti wa embe
-Mti huu huchukua muda mrefu sana kustawi
-Tunda lake huwa ni kubwa, na lina gharama sana


Upandaji wa Parachichi

Nafasi kati ya shimo na shimo


-Umbali wa kutoka shimo hadi shimo ni MITA 7
-UMbali wa kutoka mstari hadi mstari ni MITA 7

Lakini kipimo hicho hapo juu kitategemea sana na aina ya udongo wa shamba lako , kwa udongo wenye Phosphorus kwa wingi (P), kipimo hicho hakifai, maana baada ya mika 3-5 miche ya mistari miwili inayofuatana itakuwa imekuatana katikati

-Hivyo nafasi yaweza kuwa

8M X 8M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 63 KWA EKA 1
AU 9M X 9M-KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 49 KWA EKA 1
AU 10M X 10M- KWA NAFASI HII UTAKUWA NA MICHE 40 KWA EKA 1

Ukubwa wa shimo-Shimo laweza kuwa futi 2.5 x futi2.5 x futi 2.5 = (sm 75 x sm 75 x sm 75) (Kimo x upana x urefu)

-Au kipimo cha futi 3 x futi 3 x futi 3= sm 90 x sm 90 x sm 90

Mbolea

-Mbolea za kupandia zitakazohitajika , ni moja wapo kati ya hizi
-Samadi, Mboji, DAP, au TSP-Lakini ni muhimu kupandia mbolea asilia kama samadi ukachanganya kidogo na TSP au DAP

Kipimo cha mbolea,
-Kama ni mbolea za asili (Samadi au Mboji)-Kiasi cha kilo 16 hadi 20 kinapaswa kiwekwe katika shimo miezi 3 kabla ya kupanda mche

-Kama utapandia mbolea za viwandani (TSP, DAP, Minjingu, NPK etc)
kiasi cha gramu 100 hadi 200 kiwekwe kwa kila shimo, ichanganywe vizuri na udongo, kisha mmea uwekwe na kumwagiliwa

KUKOMAA NA KUTOA MAVUNO
-Parachichi hasa hizi za kisasa, hukomaa baada ya miezi 18 hadi 24

MAVUNO
-Kwa mara ya kwanza mti mmoja wa parachichi unaweza kukupa kati ya matunda 50 hadi 100 kwa mche mmoja.
-Mavuno hueongezeka kadri umri unavyoongezeka
-Mti wa parachichi ukifikia umri wa miaka 4 hadi 5, unakuwa full maturity, na hivyo mti mmoja unaweza kukupa hadi matunda 1200 kwa mwaka mzima '

FAIDA
kwa kipimo cha mita 10 x mita 10, katika eka mmoja utakuwa na mita 40
-Kila mti baada ya mika 5 unaweza kukupa wastani wa matunda 1000
-Hivyo kwa miti 40, utakuw na jumla ya matunda 40 x 1000= 40,000
-Kila tunda kwa bei ya shambani uuze tsh 250, na unamatunda 40,000
-Hivyo utapata jumla ya tsh 250 x matunda 40,000= 10,000,000tsh (MILIONI 10)

Magonjwa ya parachichi


Parcahichi kama mimea mingine inashambuliwa sana hasa upande wa majani pamoja na matunda.

1. Yapo magonjwa ya majani, yanayosababishwa na fangasi/Ukungu, Algae, pamoja na wadudu, pamoja na lishe duni.


View attachment 332289
Jani lililoshambuliwa na Alga


View attachment 332290
Mite-Utitiri mweupe Avocado lililoshambuliwa na Utitiri

2.Magonjwa ya matunda

View attachment 332291View attachment 332291

View attachment 332292

-Tatizo la Scab, husababishwa na Ukungu/Fangasi hasa wakati wa baridi/unyevu mwingi

View attachment 332293
Thrips wa avocado Matunda yaliyoathiriwa na Thrips

DAWA
-Dawa za kutibu wadudu kama Karate, Matchi, Actellic 50 EC, za faa sana kumaliza wadudu katika mmea wa parachichi

-Dawa za Ukungu kama Ridomil Gold, Ebony 72 WP (Mancozeb na Metalaxyn), Ivory, na Nordox zaweza kutumika kumaliza matatizo ya ukungu

-Lishe ya mmea

Mbolea za kukuzia kama CAN, UREA NA SA (hasa kwenye maeneo yenye magadi kwa wingi, na chumvi nyingi) yaweza kutumika kubalane PH YA Udongo.

-Booster=Mbolea za majani, maua na matunda kama vile Polyfeed Starter, Polyfeed finisher, Wauxal macro mix, Potphos, au Multi K , Ni muhimu sana zikatumika wakati wa maua, na matunda ili kuzuia matunda ya parachichi kuabort (Fruit abortion) yakiwa machanga, pamoja na kuzuia matunda kudondoka yakiwa machanga.


Hitimisho
Parachichi-Kama matunda mengine, ukililima kitaalamu, na ukaweka juhudi na maarifa linakutoa katika umaskini[/QUOT
Document imeshiba
 
Kama kuna mtu anategemea kupanda parachichi mwaka huu Wilaya ya Kilolo,
Basi tuwasiliane, tutakuletea seedlings mpaka shambani kwako, price yetu ni 2500/- kwa mchi,
Ni PM
Mkuu vipi hiyo Miche ya parachichi ni ya aina gani unauza, funguka hapa nijue, maana mi sipo kilolo huko iringa, ila nipo Kilimanjaro na nimeona Bei yako ni nzuri tu.
 
Nipo Kilimanjaro nataka nijaribu hii project kwa bidii sana, so na Mimi naangalia ni jamii gani sokoni inaweza kufika maana hii oviusly ni mali kuoza na production yake ni ya kiasi gani au yield per cultivation over area, hivyo nimefurahi kuona hii thread na ninapenda kuona maoni zaidi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom