Kilimo cha Mitiki: Utaalamu na biashara yenyewe

Mimi nilipanda mitiki miche 6000 mwaka 2010 ilikua kama najaribu tu na sina utaalamu sana sasa miti imekua mirefu sana ( kwa kudaria urefu ni zaidi ya jengo la gorofa mbili ) nataka mwenye ujuzi anifahamishe maana nimeambiwa ni muda muafaka kupunguzwa, je hiyo inayopunguzwa naweza pata soko wapi? Maana inayopunguzwa ni zaidi ya miti 2000
Hlw mkuu
 
Mkuu Contequil,

Ulini PM kuhusu kilimo cha mitiki hapa yupo mtaalamu Kisima atakusaidia mimi si mtaalamu japo nimeilima, lakini niatakachokupa kitakua ni uzoefu toka kwa watu mbalimbali, lakini hapa wapo wataalamu na ukitaka mbegu watakupatia

Cc Kisima
 
Salama mkuu!
Moro naishi Turiani karibu kabisa na mtibwa teak forest.
Mbegu zipo zakutosha kulingana na shehena ya uhitaji wako.
Bei yangu inavary kulingana na wingi wa miche(stamps) utakazo.
Mathalani kama order yako itafikia miche 3200(ambayo unaweza panda ekari5) ntakuuzia kwa sh250 kila mche na kutakuwa na offer ya miche 300 bure!
Ikiwa order yako ni zaidi ya miche 16000 bei itapungua hadi 200@mche na kutakuwa na nyongeza ya miche 1000.
Utaratibu ni unalipia 50% ya mzigo na 50% nyingine utamalizia on delivery day.
Kama utahitaji huduma ya kupandiwa kitaalam, mimi na team yangu tupo tayari kukuhudumia popote lilipo shamba.
Karibu sana mkuu!
Mkuu kisima iyo bei 250 kwa 3200 pcs, ni mche ambao utaenda pandwa shambani au ni stump inayohitaji kuoteshwa ktk mfuko then ndo iende shamba baadae, na unahisi nikiandaa shamba na mashimo kila kitu upandaje na timu yako inaweza kuwa bei gani, kwa mfano shamba likiwa kilombero
 
Mkuu kisima iyo bei 250 kwa 3200 pcs, ni mche ambao utaenda pandwa shambani au ni stump inayohitaji kuoteshwa ktk mfuko then ndo iende shamba baadae, na unahisi nikiandaa shamba na mashimo kila kitu upandaje na timu yako inaweza kuwa bei gani, kwa mfano shamba likiwa kilombero
Hiyo ni bei ya stumps mkuu.
Binafsi mashamba yangu nilipanda stumps direct pasipo kuweka kwenye viriba vya nylon.
Kikubwa tu ni kuhakikisha unapanda stumps zilizo komaa na ardhi ya eneo utakalopanda udongo wake uwe umetifuliwa kiasi cha kuruhusu mizizi kupenya haraka na itasaidia kutunza unyevu kwa muda mrefu.

Mimi na team yangu tutakupandia kwa sh50,000/acre. Bei itapungua kulingana na wingi wa ekari.

Karibu sana tukuhudumie mkuu!
 
Un
Mimi natafuta mbao za ujenzi. Ofcourse Kama ningeweza ningetamani nipate mbao za mitiki. Sasa kuna mwenye uzoefu na mbao za mitiki? Kuna Hawa wazungu WA Kilombero Valley Teakwood. Nimetembelea website Yao na kuongea na one of their managers inaonekana focus Yao in export. Anybody anayewajua? Atupie neno hapa. Vile vile Kama kuna mtu anayejua sehemu nyingine wanauza teakwood mbao in large quantity humu humu Tz.

Asanteni in advance.[/QUOTE Unataka mbao size gn npgie 0784616544
 
Kwa sasa, soko la uhakika ni nje ya nchi zaidi, kiwanda cha kusindika mazao ya mitiki kinajengwa huko Kilombero. Kwa hiyo kwa mtu wa small scale ni kasheshe kupata soko la ndani, lakini kama unaweza kuuza kama nguzo za umeme,hilo linawezekana.[/QUOTE]

Kuna baadhi ya maeneo kama kule Mahenge na Ifakara wakulima wakubwa ambao ni wawekezaji wananunua pia mitiki kutoka kwa wakulima wadogo. Pia, huwa kuna minada inafanyika na wafanyabiashara wakubwa kama Mohamed Enterprises huwa wananunua. Anaweza pia kuchana mbao na akauza kama wanavyofanya wengine. Fursa bado ni nyingi.
 
Mkuu Kisima msila ndio mti gani huo? Je, unakubali maeneo ya mkoa wa Pwani kama vile Mkuranga? Jibu tafadhali ili niangalie uwezekano wa kuagiza mbegu toka kwako.
 
Stumps ndio njia rahisi sana kuliko kununua miche au mbegu.
Stumps kuna jamaa moja anaitwa kisima mtafute humu utampata.
Muagizie akuletee stumps nene na nzuri atakuletea.
Mimi stumps 5000 aliniuzia kwa milioni moja.
Akikuletea hesabu kabla ya kummalizia pesa.
Chukua udongo wenye rutuba au inaweza changanya na mbolea ya ngombe .
Kisha mchanganyo huo changanya na fungicides then pakia kwenye viroba.
Wakati wa kupanda stumps
Stumps huwa ni ndefu zikate kwa chini kidogo.kisha zichomeke kwenye vifuko.
Zichomeke hadi ziwe na usawa sawa na udongo ukiojaza kwenye mfuko.
Hapo ni kumwagia tu ndani ya miezi miwili unapori la miti kwenye kitalu chako.
Jitahidi kuilinda na wadudu kwa kumwagia insectcides.
stumps ndio nini mkuu?
 
Kila siku naona makala na thread zikizungumzia kilimo cha mitiki na jinsi inavyohitajika sana. Ila sijawahi kuona mtu akitoa kuhusu bei hasa ya mitiki ikishakuwa mikubwa iwe ni kwa mti mmoja mmoja au kwa eka ili kutuhamasisha kulima na pia kutufanya kufanya cost-profit analysis kabla ya kulima. Pia sionagi mtu akieleza ni wapi hasa soko la mitiki lipo au ni kampuni zipi hasa zinanunua mitiki.

Sio kwamba napinga kulima mitiki, ila inakuwa kama hakuna mtu mwenye uhakika hasa wa ni faida kiasi gani (hata kwa makadirio ya wastani, maana bei ni maelewano) mtu anaweza kupata baada yabkuwekeza kwa hiyo miaka 15-20.

Kama yupo mtu wa namna hii naomba atusaidie kutuelewesha zaid. Asante

Hate me at your own risk
 
Mkuu Kisima msila ndio mti gani huo? Je, unakubali maeneo ya mkoa wa Pwani kama vile Mkuranga? Jibu tafadhali ili niangalie uwezekano wa kuagiza mbegu toka kwako.
Samahani sana mkuu kwa kuchelewa kupata notification ya post hii.
Msila upo kwenye jamii ya msedela au mkangazi, isipokuwa hurefuka zaidi na hujipogolea wenyewe na ni imara zaidi.
Matawi yake huota kwa mpangilio kwa seti maalum kama ilivyo miti ya uzazi wa mpango.
Miti hii mbao zake hutumika kwa kupaulia na pia kama fenicha.
Haubunguliwi na wadudu.

Sifa kuu ya msila ni kwamba inakuwa haraka kuliko carribeae pine, ndani ya miaka7 inakuwa tayari kwa kuvuna.
Inastawi zaidi ukanda wenye mwinuko wa wastani na pawe na joto la wastani.

Kwa ukanda wa pwani miti hii inastawi bila shida yoyote.
Mahala panapo stawi mkangazi au msedelela, hata msila unastawi.

Msila kwa jina jingine huko kanda ya ziwa inajulikana kama "mihumula" tafasiri yake ni "mti tulivu"

Kama utahitaji mbegu za miti hii nicheck
 
Samahani sana mkuu kwa kuchelewa kupata notification ya post hii.
Msila upo kwenye jamii ya msedela au mkangazi, isipokuwa hurefuka zaidi na hujipogolea wenyewe na ni imara zaidi.
Matawi yake huota kwa mpangilio kwa seti maalum kama ilivyo miti ya uzazi wa mpango.
Miti hii mbao zake hutumika kwa kupaulia na pia kama fenicha.
Haubunguliwi na wadudu.

Sifa kuu ya msila ni kwamba inakuwa haraka kuliko carribeae pine, ndani ya miaka7 inakuwa tayari kwa kuvuna.
Inastawi zaidi ukanda wenye mwinuko wa wastani na pawe na joto la wastani.

Kwa ukanda wa pwani miti hii inastawi bila shida yoyote.
Mahala panapo stawi mkangazi au msedelela, hata msila unastawi.

Msila kwa jina jingine huko kanda ya ziwa inajulikana kama "mihumula" tafasiri yake ni "mti tulivu"

Kama utahitaji mbegu za miti hii nicheck

Mkuu nitakucheki ngoja hali ya usalama itengemae kule maana hivi sasa maeneo yale hajulikani nani mkulima nani mhalifu. Niangalie uwezekano wa kupanda miche kadhaa.
 
Kila siku naona makala na thread zikizungumzia kilimo cha mitiki na jinsi inavyohitajika sana. Ila sijawahi kuona mtu akitoa kuhusu bei hasa ya mitiki ikishakuwa mikubwa iwe ni kwa mti mmoja mmoja au kwa eka ili kutuhamasisha kulima na pia kutufanya kufanya cost-profit analysis kabla ya kulima. Pia sionagi mtu akieleza ni wapi hasa soko la mitiki lipo au ni kampuni zipi hasa zinanunua mitiki.

Sio kwamba napinga kulima mitiki, ila inakuwa kama hakuna mtu mwenye uhakika hasa wa ni faida kiasi gani (hata kwa makadirio ya wastani, maana bei ni maelewano) mtu anaweza kupata baada yabkuwekeza kwa hiyo miaka 15-20.

Kama yupo mtu wa namna hii naomba atusaidie kutuelewesha zaid. Asante

Hate me at your own risk
Kaina, mawazo yako ni kama yangu.

Kuna jamaa yangu amelima mitiki heka 50 na. Nilimuuliza hayo maswali na alishindwa kujibu.

Sipingi kulima mitiki, ila nadhani ulimaji wake umekuwa exagorrated. Ni kama ukuzaji wa sungura. Poleni kusema haya.

Cut point niliyoiona, ni kwamba mitiki inakomaa baada ya miaka 25 na.... Kwa maana hiyo, hii investment sio yako tena, ni ya wanao.

Kwa maana hiyo, kulima mitiki ni excess wakati una mambo mengine ya kufanya. Maana yake hutategemea mitiki kuishi.
 
Kila siku naona makala na thread zikizungumzia kilimo cha mitiki na jinsi inavyohitajika sana. Ila sijawahi kuona mtu akitoa kuhusu bei hasa ya mitiki ikishakuwa mikubwa iwe ni kwa mti mmoja mmoja au kwa eka ili kutuhamasisha kulima na pia kutufanya kufanya cost-profit analysis kabla ya kulima. Pia sionagi mtu akieleza ni wapi hasa soko la mitiki lipo au ni kampuni zipi hasa zinanunua mitiki.

Sio kwamba napinga kulima mitiki, ila inakuwa kama hakuna mtu mwenye uhakika hasa wa ni faida kiasi gani (hata kwa makadirio ya wastani, maana bei ni maelewano) mtu anaweza kupata baada yabkuwekeza kwa hiyo miaka 15-20.

Kama yupo mtu wa namna hii naomba atusaidie kutuelewesha zaid. Asante

Hate me at your own risk

Kaina, mawazo yako ni kama yangu.

Kuna jamaa yangu amelima mitiki heka 50 na. Nilimuuliza hayo maswali na alishindwa kujibu.

Sipingi kulima mitiki, ila nadhani ulimaji wake umekuwa exagorrated. Ni kama ukuzaji wa sungura. Poleni kusema haya.

Cut point niliyoiona, ni kwamba mitiki inakomaa baada ya miaka 25 na.... Kwa maana hiyo, hii investment sio yako tena, ni ya wanao.

Kwa maana hiyo, kulima mitiki ni excess wakati una mambo mengine ya kufanya. Maana yake hutategemea mitiki kuishi.

Haya mnataka bei za mtiki ni hizi hapa

813f9f7a64b2f17b618c0b3823ff3db4.jpg



Kuhusu soko: Nenda Turiani morogoro kuna Viwanda vitano vinauza nje hii miti. Pia nilisikia kilombero kipo kimoja

Nenda pia NMB wanakupa mkopo mzuri ukiwa na shamba la miti. Hapa ndio wajanja wengi wanatokea, wananunua kwa bei rahisi halafu wanachukulia mkopo mkubwa.

Ukitaka kuamini zaidi tembele wakala wa miti ofis zao zipo Morogoro njia ya kwenda Dodoma , nenda wakakupe ushuhuda.


Ushuhuda: kuna mtu kakataa 60M kwa ekari mbili zenye miti isiyozidi 800 ya mitiki ya miaka 8. Yupo morogoro sehemu inaitwa mngazi. Mwingine Turiani alitakataa 40M kwa nusu ekari ya mitiki. Hizi sio stori bali nimejionea

Taarifa mnazo sasa kimbieni shamba haraka msichelewe

NB: mitiki inaweza kuuzwa ukiwa na miaka 8, kwahiyo ondoeni fikira za kwamba watafaidi watoto.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom