Kilimo cha miti hakina faida kwa sasa. Ni biashara kichaa!

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,801
Bei ya miti hasa ya"Pine" imeporomoka mno mashambani, ingawa bei za mbao mijini hazijashuka. Huwezi amini ekari moja ya miti (Iliyostawi vizuri) ya miaka 10 ni kati ya mil.1.2 hadi 1.5. Siku za nyuma ekari moja ingeweza kuuzwa mil.5. au zaidi.

Visingizio vya wafanyabiashara ni kupanda kwa gharama za usafilishaji na miti kuwa mingi.

Ieleweke kuwa Miti ina gharama nyingi kuanzia ununuzi wa shamba, kusafisha shamba , kuandaa mashimo, ununuzi wa miche, gharama ya upandaji, na kusafisha miti hasa miaka 5 ya mwanzo. Hapo hapo kuna hatari (Risk) ya moto " Wild fire". Mfano msimu huu wa 2021baadhi ya maeneo ya Kilolo na Mufindi zaidi ekari 1000 zimeungua kwa moto.

Wale wazee wa kuaminishwa na "motivational speakers" kwamba miti ni utajiri tambueni kwa sasa kilimo cha miti ni umaskini tena wa muda mrefu. Fikiria unasubiri kwa miaka zaidi ya 10 aaafu unaambulia kijihela ambacho ni mshahara wa mtu wa mwezi mmoja. This is insane!
 
Mkuu nami mwaka huu nimepiga vi ekari kumi, mwaka jana nilipiga nane. So long watu wanaongezeka na kuendelea kujenga makazi bora. Kitaendelea kueleweka tu!
Ha ha ha ha ha. Hadi tujionee wenyewe.
Kama mashamba ni mengi , ni wazi miti imeongezeka , kwa hiyo, bei lazima ishuke maana ni maliggafi. Kama ni kupata faida lazima uuze mbao kama ilvyo kwa wakulima wa mahindi, anayepata faida ni muuza unga
 
IMG_0980.png

vp mchanganuo huu Mkuu
 
Mkuu nami mwaka huu nimepiga vi ekari kumi, mwaka jana nilipiga nane. So long watu wanaongezeka na kuendelea kujenga makazi bora. Kitaendelea kueleweka tu!
Ha ha ha ha ha. Hadi tujionee wenyewe.
Mkuu Unalima miti mkoa gani....Vipi kwa Morogoro kama unazoefu wowote wa mkoa huo?
 
Back
Top Bottom