Kilimo cha Mihogo (Cassava): Mbinu, Ushauri, Changamoto na Masoko yake

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
4,992
istockphoto-179038063-612x612.jpg

Wakuu,

Kutokana na uhitaji wa kuwepo mjadala endelevu na wa tija kwa wajasiriamali, tumeona ni vema tukaweka hii thread kwa maslahi ya wengi.

Tunashauri Mjadala huu ujikitae kwenye maeneo yafuatayo:

1. Aina za mihogo na maeneo inakostawi vizuri
2. Misimu ambayo mihogo inapandwa ni miezi ipi? Inaweza kupandwa misimu yote ya mwaka?
3. Mihogo inashambuliwa na magonjwa yapi? Zipi mbinu za kukabiliana na maradhi hayo?
4. Mihogo inachukua muda gani tangu kupandwa hadi kuvunwa?
5. Hekari moja inaweza kutoa magunia mangapi ya mihogo?
6. Masoko ya mihogo na bidhaa zake ndani na nje ya nchi yapoje?
Asante


MICHANGO YA WADAU MBALIMBALI KUHUSU KILIMO CHA MIHOGO
KILIMO BORA CHA MIHOGO

Zao la muhogo ni muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini. Wakulima wengi huchanganya zao la muhogo na mazao mengine kama vile kunde, mbaazi, njugumawe, n.k. Umuhimu wa zao hili ni kutupatia cahakula na wakati mwingine kwa biashara. Kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula kikuu ambacho kinachukua asilimia 75 ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya pwani

Muhogo hustawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye maeneo ya mita 0 – 1500 kutoka usawa wa bahari. Vile vile muhogo hustawi vizuri kwenye maeneo yanayopata mvua ya wastani wa mm 750 - mm1200 kwa mwaka. Muhogo hustawi vizuri kwenye ardhi ya kichanga. Vili vile zao la muhogo ni maarufu sana kwa uvumilivu wa hali ya ukame.

TEKNOLOJIA ZILIZOPO
Mbegu bora za muhogo

Mpaka sasa hivi kuna aina mbili za mbegu bora ambazo zimathibitishwa kwa wakulima. Mbegu hizi huvumilia magonjwa, (batobato na matekenya), pia huzaa sana ukilinganisha na mbegu za kienyeji.
Naliendele
Huzaa tani 19 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

Kiroba
Huzaa tani 25 – 30 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

Mbinu bora za kilimo cha muhogo
Uandaaji wa shamba

Shamba liandaliwe kabla ya msimu wa kuanza. Uandaaji wa shamba bora hufuata hatua zifuatazo:
  • Kufyeka shamba
  • Kung’a na kuchoma visiki
  • Kulima na kutengeneza matuta

· Uchaguzi wa mbegu bora za kupanda
Mbegu zinatakiwa zisiwe na magojwa yeyote, pia chagua mashina ambayo yamelomaa vizuri

· Upandaji
Kuna njia tatu za upandaji wa muhogo:
  • Kulaza ardhini (Horizontal)
  • Kusimamisha wima (Vertcal)
  • Kuinamisha ( Inclined/Slunted)

Urefu wa kipande cha shina cha kupanda:
Inashauriwa urefu uwe sm 30; lakini urefu wa kipande cha kupanda unategemea sana idadi ya macho yaliyopo kwenye hicho kipande, inashauriwa kipande kiwe na macho (4 – 6).

Nafasi ya kupanda:
Kwa upandaji wa shamba muhogo tupu, shina hadi shina ni mita 1 na mstari hadi mstari ni mita 1.Kwa shamba la mchanganyiko na mazao mengine, inategemeana na zao linalochanganywa; mstari hadi mstari ni mita 2 – mita 4 na shina hadi shina ni mita 1.

· Palizi:
Palizi ya kwanza ifanyike mapema (mwezi 1) baada ya kupanda ili kuepukana na magugu yanayochipua haraka baada ya mvua kunyesha. Ndani ya miezi mine ya mwanzo mihogo haitakiwi kuwa na magugu ili kuepuka ushindni wa mahitaji muhimu (mwanga, mbolea, maji, n.k) kati ya muhugo na magugu.
  • Palizi hufanyika kwa kutumi jebe la mkono au dawa ya kuuwa magugu.
  • Wakati mwingine udhibiti wa magugu kufanyika kwa kutumia majani kwa kutandazwa juu ya udongo.
  • Plaizi hufanyika mara 2 – 3 hadi muhugo kukomaa.

· Uvunaji:
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 – 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvuna katika katika kipindi cha jua; kwani wakati wa mvua kiwango cha wanga kwenye muhogo hupungua.

· Usindikaji bora
Usindikaji bora wa muhogo unafanyika kwa sababu kuu mbili:
  • Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji
  • Kuondoa sumu (cyanide) ilyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo
  • Kuongeza ubora wa unga utokanao muhogo wenyewe.

Njia bora za usindikaji
- Kwa kutumia mashine aina ya Grater
Hii hutoa chembechembe laini za muhogo, ambazo baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kingine kiitwacho “presser” ili kuondo sumu iliyoko kwenye muhogo. Mashine hii hutumika hususani kwa muhogo mchungu.
  • Kwa kutumia mashine aina ya chipper
  • Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo (chips). Mashine hii hutumika hasa hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.

Matumizi ya Muhogo
  • Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga
  • Unga wa muhogo unaweza kutengeneza vitu vyotekama vinavyotengenezwa na unga wa ngano kama vile biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k.
  • Pia muhogo huweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa nyingine kama vile wanga.
ZAO LA MUHOGO

Utangulizi
Mihogo hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Mara, Mwanza, Kigoma, Mtwara, Lindi, Pwani, Ruvuna, Tanga, Morogoro, Mbeya, na Shinyanga. Muhogo una kiwango kikubwa cha wanga ukilinganisha na nafaka (zaidi ya asilimia 40 kuliko mchele, na zaidi ya asilimia 25 kuliko mahindi). Majani yake hutumika kama mboga na yana virutubishi muhimu hususan vitamini B na protini.
Uzalishaji wake ni wastani wa tani 1,292,000 kwa mwaka. Ili kupata mazao mengi na bora ni muhimu kuzingatia kanuni za kilimo bora cha mihogo hasa zifuatazo:

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Katika Uzalishaji
Kuchagua aina ya mbegu

  • Chagua mbegu kufuatana na mahitaji ya soko, zilizo safi zinazostahimili magonjwa, wadudu waharibifu na zenye uwezo wa kutoa mazao mengi na bora.
Palizi
  • Palilia ili kupunguza ushindani wa virutubishi kati ya mmea na magugu.
  • Palilia na kupandishia udongo kwenye mashina.
  • Palizi ifanyike mara kwa mara mpaka mihogo inapokomaa.
Kudhibiti magonjwa na wadudu
Muhogo hushambuliwa na wadudu waharibifu kama vidung’ata, vidugamba, mchwa na magonjwa kama batobato na ugonjwa wa michirizi ya kikahawia. Visumbufu hawa wanaweza kusababisha upotevu wa mazao kwa zaidi ya asilimia 90. Hivyo ni muhimu kukagua shamba mara kwa mara ili kuona kama kuna mashambulizi na kuchukua tahadhari mapema.

Maandalizi kabla ya kuvuna
Kukagua shamba

  • Kagua shamba ili kuhakikisha kama muhogo umekomaa. Kwa kawaida muhogo hukomaa katika kipindi cha miezi 9 hadi 24 tangu kupanda kutegemea aina na hali ya hewa. Wakati huo muhogo huwa na unyevu wa asilimia 60 na wanga asilimia 35.
Dalili za muhogo uliokomaa
  • Udongo unaozunguka shina hupasuka.
  • Mti wa muhogo huonekana kupevuka.
  • Muhogo uliokomaa ni mnene na ukiutafuna utahisi wanga mwingi na maji kidogo.
Kuandaa vifaa vya kuvunia, kubeba, vyombo vya usafiri, na vifungashio

Vifaa vya kuvunia na kubeba

  • Jembe, Panga, Vikapu, Matenga, na Magunia
Vifaa vya kufungashia
  • Maboksi ya mbao/plastiki, viroba, Matenga
Vyombo vya usafiri
  • Baiskeli, Matoroli, Mikokoteni, Magari na matela ya matrekta.
Kuvuna
Ni muhimu kuvuna mapema ili kupunguza uharibifu unaoweza kusababishwa na mashambulizi ya magonjwa na wadudu waharibifu. Kabla ya kuvuna matawi yote yakatwe ili kurahisisha uvunaji.

Njia ya kuvuna muhogo
Chimbua shina la muhogo kwa kutumia jembe na ng’oa muhogo wote kutoka ardhini. Tenganisha muhogo na shina kwa kutumia panga kali.

Utayarishaji, Hifadhi na Usindikaji wa Mazao ya Mizizi baada ya Kuvuna

Tahadhari

Epuka kukata muhogo wakati wa kuvuna kwani mihogo iliyokatwa au kuwa na majeraha huharibika mapema, kutokana na kuingiwa kwa urahisi na vimelea vya magonjwa.

Kuchambua Na Kusafisha

Kuchambua

Lengo la kuchambua ni kuondoa mihogo isiyofaa, iliyooza na iliyokatwa vibaya na kuharibika.
  • Mihogo iliyooza isitumike kwa chakula bali ifukiwe.
  • Mihogo iliyokatwa au yenye michubuko itumike kwa chakula mapema iwezekanavyo au ioshwe vizuri na isindikwe mara moja.
  • Mihogo iliyodumaa itumike kwa chakula cha mifugo.
Kusafisha na kuimarisha maganda

Kusafisha

Mihogo iliyovunwa huoshwa mara tu baada ya kuvuna ili kuondoa udongo na uchafu mwingine. Mihogo ambayo haikuoshwa vizuri hupunguza ubora wakati wa kukausha na kusindika. Mihogo huoshwa kwa maji na kurudiwa hadi maji yanapokuwa safi na kuona kuwa mihogo imetakata.

Kwa maelezo au mazao mengine unaweza tembelea
FAHAMU KILIMO CHA ZAO LA MUHOGO

Zao la muhogo ni muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini. Wakulima wengi huchanganya zao la muhogo na mazao mengine kama vile kunde, mbaazi, njugumawe, n.k. Umuhimu wa zao hili ni kutupatia cahakula na wakati mwingine kwa biashara. Kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula kikuu ambacho kinachukua asilimia 75 ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya pwani.

Muhogo hustawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye maeneo ya mita 0 – 1500 kutoka usawa wa bahari. Vile vile muhogo hustawi vizuri kwenye maeneo yanayopata mvua ya wastani wa mm 750 - mm1200 kwa mwaka. Muhogo hustawi vizuri kwenye ardhi ya kichanga. Vili vile zao la muhogo ni maarufu sana kwa uvumilivu wa hali ya ukame.

TEKNOLOJIA ZILIZOPO

Mbegu bora za muhogo

Mpaka sasa hivi kuna aina mbili za mbegu bora ambazo zimathibitishwa kwa wakulima. Mbegu hizi huvumilia magonjwa, (batobato na matekenya), pia huzaa sana ukilinganisha na mbegu za kienyeji.
Naliendele Huzaa tani 19 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

Kiroba
Huzaa tani 25 – 30 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9toka ipandwe.

Mbinu bora za kilimo cha muhogo
Uandaaji wa shamba

Shamba liandaliwe kabla ya msimu wa kuanza. Uandaaji wa shamba bora hufuata hatua zifuatazo:
  1. Kufyeka shamba
  2. Kung’a na kuchoma visiki
  3. Kulima na kutengeneza matuta
  4. Uchaguzi wa mbegu bora za kupanda
  5. Mbegu zinatakiwa zisiwe na magojwa yeyote, pia chagua mashina ambayo yamelomaa vizuri.
  6. Upanadaji
  7. Kuna njia tatu za upandaji wa muhogo:
  8. Kulaza ardhini (Horizontal)
  9. Kusimamisha wima (Vertcal)
  10. Kuinamisha ( Inclined/Slunted)
Urefu wa kipande cha shina cha kupanda:
Inashauriwa urefu uwe sm 30; lakini urefu wa kipande cha kupanda unategemea sana idadi ya macho yaliyopo kwenye hicho kipande, inashauriwa kipande kiwe na macho (4 – 6).

Nafasi ya kupanda:
Kwa upandaji wa shamba muhogo tupu, shina hadi shina ni mita 1 na mstari hadi mstari ni mita 1.Kwa shamba la mchanganyiko na mazao mengine, inategemeana na zao linalochanganywa; mstari hadi mstari ni mita 2 – mita 4 na shina hadi shina ni mita 1.

Palizi:
  • Palizi ya kwanza ifanyike mapema (mwezi 1) baada ya kupanda ili kuepukana na magugu yanayochipua haraka baada ya mvua kunyesha. Ndani ya miezi mine ya mwanzo mihogo haitakiwi kuwa na magugu ili kuepuka ushindni wa mahitaji muhimu (mwanga, mbolea, maji, n.k) kati ya muhugo na magugu.
  • Palizi hufanyika kwa kutumi jebe la mkono au dawa ya kuuwa magugu.
  • Wakati mwingine udhibiti wa magugu kufanyika kwa kutumia majani kwa kutandazwa juu ya udongo.
  • Plaizi hufanyika mara 2 – 3 hadi muhugo kukomaa.

Uvunaji:
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 – 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvuna katika katika kipindi cha jua; kwani wakati wa mvua kiwango cha wanga kwenye muhogo hupungua.

Usindikaji bora
Usindikaji bora wa muhogo unafanyika kwa sababu kuu mbili:
  • Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji
  • Kuondoa sumu (cyanide) ilyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo
  • Kuongeza ubora wa unga utokanao muhogo wenyewe.
Njia bora za usindikaji
  • Kwa kutumia mashine aina ya Grater
  • Hii hutoa chembechembe laini za muhogo, ambazo baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kingine kiitwacho “presser” ili kuondo sumu iliyoko kwenye muhogo. Mashine hii hutumika hususani kwa muhogo mchungu.
  • Kwa kutumia mashine aina ya chipper
  • Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo (chips). Mashine hii hutumika hasa hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.
Matumizi ya Muhogo
  • Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga
  • Unga wa muhogo unaweza kutengeneza vitu vyotekama vinavyotengenezwa na unga wa ngano kama vile biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k.
  • Pia muhogo huweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa nyingine kama vile wanga.
iii MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
Magonjwa
Kuna magonjwa mawili ambayo ni muhimu sana na yanapunguza uzalishaji wa zao la muhogo.

a) Ugonjwa wa Matekenya au Ugonjwa wa michirizi ya kahawia katika muhogo
Ugonjwa huu ni maarufu kwenye sehemu zenye miinuko iliyo na urefu chini ya mita 300 na unapatikana kidogo sana kwenye miinuko ya mita 500 na kuendelea ambako uenezaji wake wa kawaida hautokei kabisa.

Visababishi:
Matokeo ya uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba ugonjwa huu ulienezwa na mdudu mweuupe au inzi mweupe (whitefly) mwenye mabawa madogo.

Dalili za Ugonjwa
Sehemui zote za muhogo zinaweza kuonyesha dalili za uambukizo wa ugonjwa huu lakini ni vipengele gani vya ugonjwa na ni kwa kiwango gani hutegemea hali ya mzingira, hatua ya kukua kwa mmea kwa kulinganisha.

Kwenye majani
  • Dalili ya kwanza: Chlorosis rangi ya njani hutokea kwanza pembezoni mwa vena ndogo baadae huathtiri vena ndogo zaidi na inaweza kuwa doa (chlorosis) la rangi ya njano.
  • Dalili ya pili: Rangi ya njano ambayo haihusishwi vizuri na vena isipokuwa katika mbaka ya mviringo kati ya vena kuu kwenye hatua za mwisho za ugonjwa sehemu kubwa ya lamin inaweza isiathirike, majni yenye ugonjwa hubaki yameshikilia kwenye mmea kwa muda wa wiki kadhaa.
Kwenye shina
Huonekana kwenye tisu ya shina changa la kijani, jeraha la zambarau au kahawia linweza kuoneakan nje na kuingia ndani hadi kwenye gamba baaada ya kubandua gome la nje. Pia jeraha la nekrotiki kwenye kovu la shina hutokea baada ya majni kudondoka kutokana na umri wa mmea. Tawi/shina hufa kuanzia kwenye nch kuelekea chini na kusababisha kufa kwa mmea wote.


Kwenye mizizi

Kwa kawaida hutokea baada ya dalili za majani na wakati wa kipindi kati ya uambukizo na kufa, amabpo kifo cha mizizi hutokea kuanzia miezi 5 toka kupandwa. Dalili za mizizi zinabadilika nje ya mizizi na zinaweza kuwa kamakizuizimwanga au shimo au kufa kwenye gome.

Tishu inayo zunguka mshins ina doa la rangi ya kahawia au nyeusi. Wakati mwingine mizizi huonekana kuwa yenye afya kwa nje bila kuwa na matatizo yaliyowazi au bila kupungua ukubwa, lakini ikikatwa huonekana kufainakufa au rangi ya njano.
Uambukizaji na ueneaji

Ugonjwa wa CBSD unaambukizwa kwa njia ya vipandikizi vinavyotokea kwenye mimea iliyoathiriwa vinavyosababisha mmea kuonesha kwenye majani dalili za ugonjwa.

Kwa kuwa muhogo kwa kawaida huzalishwa kwa njia ya vipandikizi ugonjwa huu huingizwa kwenye sehemu mpya zilizopandwa kwa kutumia vipandikizi vilivyoambukizwa.
Kwa aina zinazovumilia sana kwenye hali za mabondeni, dalili mbaya sanahutokea wakati ugonjwa ukigundulika katika hatua za mwanzo.

Uchunguzi umeonesha kwamba Bemisia afer ni mdudu/kisababishi ambacho ndicho kinachohusiana na maendeleo ya hivi karibuni kuhusu uhamishaji wa visababishi kama “ipomovirus”. Mara nyingine inaonesha nzi weupe (White flies) na kutokana na hali hiyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.

Udhibiti/Kuzuia
  • ü Njia ya msingi ya kuzuia/kudhibiti ugonjwa wa CBSD ni kuchagua mbegu kutoka kwenye mimea isiyo na dalili ya ugonjwa.
  • ü Ubora wa mashina unahitaji kutunzwa kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza ile iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.
  • ü Hakikisha kuwa unapanda mbegu bora za mhogo ambazo zinastahimili uambukizo wa magonjwa.
  • ü Hakikisha kuwa wakati wa uvunaji uonapo hali ya kuoza kwa mizizi ya mhogo ichome moto ili kutokomeza ugonjwa huo.
  • ü Kuelewa dalili za ugonjwa wa CBSD kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya kutokomeza ugonjwa huu.
  • ü Hakikisha kuwa unaendelea kutunza mbegu bora zinazoonekana kuvumilia magonjwa sana.
  • ü Hakikisha kuwa shamba la mhogo linakuwa safi kwa ajili ya kupunguza visababishi vya ugonjwa wa CBSD


b) Ugonjwa wa batobato au ukoma wa majani
Ni ugonjwa ambao ulienezwa kwamara ya kwanza hapa Tanzani mwaka 1894, na baadae uliripotiwa katika nchi nyingine nyingi za Afrika Mashriki, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati na sasa unafahamika kuwa upo maeneo yote yanayolimwa muhogo Afrika.

Katika viwango vya kuwepo kwa ugonjwa wa CMD na katika uwingi wa hasara zinazopatikana kutokana na CMD ni kati ya 15% – 20%. Hii ni sawa na tani milioni 15 – 18 zikilinganishwa na makadirio ya shirika la kilimo na chakula duniani ya tani milioni 85 ya mwaka 1997.

Visababishi
Tangu ugonjwa wa CMD ulipoenezwa kwa mara ya kwanza, visababishi vilichukuliwa kuwa ni virusi kwa sababu ya kukosekana kisababishi kingine. Kwa hiyo kutokana na kuwa mtazamo huu unalingana na matokeo ya uchunguzi wa awali inaonesha kwamba ugonjwa huu huenezwa na nzi mweupe (white fly).

Pia uchunguzi wa mara kwa mara umesababisha utambuzi wa virusi vya aina mbalimbali na tofauti kama ifuatavyo:
  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Africa cassava mosaic virus
  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Afrika mashariki (East Africa cassava mosaic virus)
  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya India (Indian cassava mosaic virus)
  • Dalili za ugonjwa wa batobato (Cassava Mosaic Disease-CMD)

Dalili hutokea kwenye jani lenye uwaraza wa michirizi ambazo huathiri Sehemu zisizokunjamana za kutolea hewa na hufahamika katika hatua za Awali za ukuaji wa jani.

Sehemu za kloritiki hushindwa kutanuka hadi mwisho, hivyo mvutano unaji- tokeza kutokana na ukuaji usiolingana na jani au majani madogo yaliyoharibika.

Majani yaliyoathirika sana hupungua ukubwa wa umbo, na hujikunja na kujitenga kwa Sehemu zenye rangi ya njano na zenye rangi ya kawaida ya kijani.

Mmea hudumaa na majani machanga hupatwa na uvimbe.
Kloritiki ya jani inaweza kuwa ya rangi ya manjano nyepesi au rangi inayokaribia nyeupe yenye kijani kidogo au kupauka kuliko ilivyo kawaida.


Uambukizaji na uenezaji
  • Ukoma wa mhogo huambukizwa kwenye vipandikizi vya shina ambavyo kwa kawaida
  • hutumika kuzalishia mmea.
  • Pia huenezwa na inzi mweupe (white fly) aitwae Bemisia tabaci G. Aina mbili za inzi au
  • Mbu hao Bemisia (Preisner Hhosny na Aleorodius disperses R) pia huambukiza mihogo
  • katika nchi za Afrika na India
  • Usambazaji wa vipandikizi unaweza kusababisha kuenea kwa ugonjwa wa CMD katika
  • Maeneo mapya.
UHIBITI NA KUZUIA
  • Hatua ya msingi ya uzuia ugonjwa wa CMD ni kwa kuchagua vipandikizi kutoka kwa Mmea ambao hauna uambukizo wowote.
  • Ubora wa mashina unahitajika kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza kwa kung’oa ile
  • Mihogo iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.
  • Hakikisha kuwa wakati wa kuvuna mihogo kwa ile iliyoathirika na ugonjwa wa CMD
  • inaangamizwa kwa kuchomwa moto.
  • Hakikisha una elimu ya kutosha juu ya dalili za ugonjwa wa CMD>
WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU
Cassava Mealy Bug (CMB)



Wadudu hawa hushambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani ynadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana.


Cassava Green Mites (CGM)
Wadudu hawa hushambulia majani mapya sehemu za chini. Madhara yake sio makubwa.


White Scales
Hawa ni weupe na hujishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo. Vili vile wadudu hawa madhara yake sio muhimu.

Mchwa
Hawa hutafuna/hula mashina ya muhogo hasa wakati wa jua kali/kiangazi.
Wanyama waharibifu
Hawa hushambulia muhogo ukiwa shambani kwa kuula, kama vile nguruwe, panya, wezi, n.k

Udhibiti/Kuzuia
Kwa upande wa wadudu wanweza kudhibitiwa kwa njia zifuatazo:
ü Kutumia dawa za kuulia wadudu
ü Kutumia wadudu marafiki wa wakulima
iii Kwa upande wa wanyama ni kuweka walinzi.
UZOEFU WANGU KUHUSU KILIMO HIKI

Tuwe wakweli ndugu hayo mahesabu uliopiga hapo hayawezekani, mimi nina udhoefu na kilimo cha muhogo, isitoshe mimi mwenyewe nina shamba hukohuko Bungu.

Kusafisha shamba kwasasa ni 50,000 kwa heka, kumbuka shamba ppri lina hatua tatu za kusafisha 1. Kuvunja msitu, 2. Kukusanya mara ya kwanza, kukusanya mara ya pili baada ya kuchoma moto.

3. Kungoa visiki alafu na kuchoma moto tena au kutolewa nje ya shamba, mwisho ndio kulima.

Jambo jingine ni kuhusu mbegu ya muhogo kweli fungu ni 3000 lakini heka moja inaweza kuchukua mafungu hata zaidi ya kumi.

Ghalama nyingine za ziada ni kudhibiti panya na nguruwe huku swala hili limekuwa tatizo kubwa sana maana labda uweke wigo au mfanye ulinzi nyakati za usiku, fikiria muhogo unaotakiwa uwe mzito zaidi utakaa shambani kwa muda gani?

Mwisho wa yote bei iliokuwa inatolewa hapa ni 50 -100 @ kilo na wanataka upeleke muhogo uliomenywa baganda na bado gharama ya kuusafirisha kupeleka kiwandani.

hapo sijataja gharama za palizi kwahuku palizi kwa msimu mmoja tunafanya hata mara nne kutokana na nyasi na rutuba ya udongo, bado gharama za watu watakaovuna pia.

But kila lakheri.
 
Mzee umechungulia deal nasikia kilimo cha mihogo kinalipa vibaya mno na soko lake ni kubwa pia.

Mfano mzuri ulio hai nenda pale mbezi stendi mwisho utakuta wamama kibao wanapigania ikija fuso ya mihogo nusu saa nyingi inakua imekwisha,na unakuta wengine wanasubiria mpaka saa tano ya usiku.

Ngoja wataalamu wenye uzoefu nayo watupe data.
 
mzee umechungulia deal nasikia kilimo cha mihogo kinalipa vibaya mno na soko lake ni kubwa pia.<br />
<br />
Mfano mzuri ulio hai nenda pale mbezi stendi mwisho utakuta wamama kibao wanapigania ikija fuso ya mihogo nusu saa nyingi inakua imekwisha,na unakuta wengine wanasubiria mpaka saa tano ya usiku.<br />
<br />
Ngoja wataalamu wenye uzoefu nayo watupe data.
<br />
<br />
kweli mkuu nimeona hata naofisini wengi wanapiga mihogo badala ya chapat
 
Nadhani mtu yeyote aliye makini asingependa kuwekeza kwenye kilimo cha mhogo na kuuza bila kuongeza thamani, hasa kusindika. Ninajua very recently kuna watafiti wamegundua matumizi mengi zaidi ya unga wa mhongo mbali na chakula. Kama unaweza kutembelea ofisi za IITA unaweza kupata taarifa nzuri. Very recently pia kuna ka-mtandao ka mashirikia yanayopromote mhogo kameanzishwa nadhani naweza kukutautia details at some point
mzee umechungulia deal nasikia kilimo cha mihogo kinalipa vibaya mno na soko lake ni kubwa pia.

Mfano mzuri ulio hai nenda pale mbezi stendi mwisho utakuta wamama kibao wanapigania ikija fuso ya mihogo nusu saa nyingi inakua imekwisha,na unakuta wengine wanasubiria mpaka saa tano ya usiku.

Ngoja wataalamu wenye uzoefu nayo watupe data.
 
Nadhani mtu yeyote aliye makini asingependa kuwekeza kwenye kilimo cha mhogo na kuuza bila kuongeza thamani, hasa kusindika. Ninajua very recently kuna watafiti wamegundua matumizi mengi zaidi ya unga wa mhongo mbali na chakula. Kama unaweza kutembelea ofisi za IITA unaweza kupata taarifa nzuri. Very recently pia kuna ka-mtandao ka mashirikia yanayopromote mhogo kameanzishwa nadhani naweza kukutautia details at some point
Mkuu nazisubiria hzo more details, ubarikiwe sana.
 
Wanajf naomba mwenye ujuz/utaalam wa kilimo cha mihogo, nampango wakulima huko kisarawe kama heka 5,
Soko lake likoje, na garama za kilimo zkoje?

Mkuu naanza ujenzi wa kiwanda cha kusindika Rufiji kuanzia Sept na by Jan 2012 nitaanza kununua tani 20 kila siku mihogo aina zote so kama utakuwa na uwezo wa kufikisha tutanunua yote. Michungu na mitamu yote tutachukua kutengezea starch tuna masoko ya nje makubwa na tutanunua bei nzuri tu mkuu.

Maelezo mengi zaidi yapo hapa mkuu

https://www.jamiiforums.com/business-and-economic-forum/39210-project-funding-sources-10.html#post2118391
 
Wanajf naomba mwenye ujuz/utaalam wa kilimo cha mihogo, nampango wakulima huko kisarawe kama heka 5

Soko lake likoje, na garama za kilimo zkoje?
 
Mkuu naanza ujenzi wa kiwanda cha kusindika Rufiji kuanzia Sept na by Jan 2012 nitaanza kununua tani 20 kila siku mihogo aina zote so kama utakuwa na uwezo wa kufikisha tutanunua yote. Michungu na mitamu yote tutachukua kutengezea starch tuna masoko ya nje makubwa na tutanunua bei nzuri tu mkuu.<br />
<br />
Maelezo mengi zaidi yapo hapa mkuu <br />
<a href="https://www.jamiiforums.com/busines...0-project-funding-sources-10.html#post2118391" target="_blank"><br />
https://www.jamiiforums.com/busines...0-project-funding-sources-10.html#post2118391</a>
Nimekupata kiongozi tupo pamoja!
 
Mzee umechungulia deal nasikia kilimo cha mihogo kinalipa vibaya mno na soko lake ni kubwa pia.

Mfano mzuri ulio hai nenda pale mbezi stendi mwisho utakuta wamama kibao wanapigania ikija fuso ya mihogo nusu saa nyingi inakua imekwisha,na unakuta wengine wanasubiria mpaka saa tano ya usiku.

Ngoja wataalamu wenye uzoefu nayo watupe data.
Wataalam pia tuombe mtusaidie kujua aina gan ya mbegu ni bomba!, tayar niko kazini. Kuna watalaam weng hapa lakn naona msimu unakaribia wako shamban, akina malila, ngoshwe n.k! Hawasikk
 
nami nimefaidika mkuu! Asante, hv maeneo ya huko mbegu zinauzwa bei gan kwa fungu? Maana nimeambia kule maeneo ya kisarawe, fungu la mashina 7 urefu wa mita moja ni buku6.
Mkuu check na magereza ndo walipewa jukumu la kuandaa mbegu bora zinazohimili ukame na magonjwa na zenye amount kubwa ya starch. Pia check pale Kibaha kuna shamba la mbegu ambalo hata sisi tumeshauriwa na wizara ya Kilimo kuna wataalamu pal wanafanya utafiti na kubreed mbegu bora na nimesikia zipo za kutosha.
 
Mkuu check na magereza ndo walipewa jukumu la kuandaa mbegu bora zinazohimili ukame na magonjwa na zenye amount kubwa ya starch. Pia check pale Kibaha kuna shamba la mbegu ambalo hata sisi tumeshauriwa na wizara ya Kilimo kuna wataalamu pal wanafanya utafiti na kubreed mbegu bora na nimesikia zipo za kutosha.
Asante sana, wk hii nitafika kibaha, ni pale taasisi ya elimu? Au kwa afisa ugani wa wilaya? Nipe raman mkuu ili niende pale.
 
hivi mihogo inachukua muda gani tokea kulima hadi kuvuna,katika maeneo ya rufiji?

Inategemea aina ya mbegu. Kuna mbegu za muda mfupi (miezi 6) na za muda mrefu (mpaka mwaka mmoja). Halafu unataka mihogo kwa madhumuni gani - starch nyingi au chakula? Jaribu kuangalia aina ya mbegu ambayo itakufaa kwa aina ya matumizi yako.

Wengine huwa tunakula inapofika mwezi wa ramadhani.
 
Mkuu check na magereza ndo walipewa jukumu la kuandaa mbegu bora zinazohimili ukame na magonjwa na zenye amount kubwa ya starch. Pia check pale Kibaha kuna shamba la mbegu ambalo hata sisi tumeshauriwa na wizara ya Kilimo kuna wataalamu pal wanafanya utafiti na kubreed mbegu bora na nimesikia zipo za kutosha.
Thanks much mkuu, nimekupata vema vp maeneo ya mlandizi kibaha yamafaa kwa kilimo?
 
Mkuu check na magereza ndo walipewa jukumu la kuandaa mbegu bora zinazohimili ukame na magonjwa na zenye amount kubwa ya starch. Pia check pale Kibaha kuna shamba la mbegu ambalo hata sisi tumeshauriwa na wizara ya Kilimo kuna wataalamu pal wanafanya utafiti na kubreed mbegu bora na nimesikia zipo za kutosha.
Mkuu hii ni kibqha sehemu gani, ningependa kuwatembelea hawa na kuchukua mbegu.
 
<br />
<br />

Mkuu hii ni kibqha sehemu gani, ningependa kuwatembelea hawa na kuchukua mbegu.

Cassava research takes place in various research institutes that are based on the research zones. These include Agricultural Research Institute (ARI) Naliendele based in Mtwara (Southern zone), ARI Kibaha based in Kibaha (Eastern zone), ARI Ukiriguru based in Mwanza (Lake zone), ARI Maruku based in Kagera (Lake zone). Others are ARI Uyole based in Mbeya (Southern highlands zone), ARI Hombolo based in Dodoma (Central zone), ARI Tumbi based in Tabora (Western zone), ARI Tengeru based in Arusha (Northern zone) and ARI Kizimbani based in Unguja.

Sehemu zote hizi mkuu ndo nimeambiwa na wataalamu wa wizara mbegu zinapatikana na pia baada ya hawa jamaa kufanya utafiti wanatoa kwa Magereza kwa ajili ya kuzalisha ili wakulima wanunue kwa wingi sasa. So ukifika kwao japo sina address zao kamili utapata mbegu au maelekezo mazuri.

Mbegu ambazo zimethibitika kuwa na viwango kwa saa zinaitwa Kibaha, Mzungu na Kiroba ambazo ukilima kwa hali ya nchi yetu unweza kupata kati ya tani 10 hadi 20 kwa Hekta.

Nafikiri hii itatoa mwanga kidogo.
 
thanks much mkuu, nimekupata vema vp maeneo ya mlandizi kibaha yamafaa kwa kilimo??

Mkuu mikoa yote ya Pwani muhogo unakubali vizuri tu ila kama utapenda kuwa mdau kwa eneo letu au ungependa kuzalisha ili tununue ningeshauri ili kupunguza ghrama za usafirishaji ni nzuri kama utaelekea barabara ya Kilwa maeneo ya kuanzia Mkuranga kuelekea njia ya Mtwara hadi karibu na Mbuga ya Selous maeneo yapo wazi sana mkuu na yanakubali muhogo ile mbaya. Tutahitaji muhogo uingie kwenye mashine kabla ya kuzidi umri wa siku 3 tangu kuvunwa ambayo najua hiyo ni feasible kabisa kwa sehemu kubwa ya Tanzania kufikisha kiwandani.

So Mlandizi pia sio mbali nimeongelea kupanua profit margin kwa kupunguza transportation costs tu hapo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom