MJADALA: Maswali, majibu na ushauri kuhusu Kilimo cha Mpunga cha kitaalam pamoja na masoko yake

Memory

Senior Member
Jun 29, 2011
106
37
1584085226432.png
MASWALI MBALIMBALI YALIYOULIZWA KUHUSU KILIMO HIKI

Ndugu wana JF,

Naomba kama kuna mtaalamu wa kilimo anisaidie ili nifahamu makadirio ya kiasi cha mavuno ya mpunga katika ekari moja katika kilimo cha kisasa ili tujipange kutekereza sera ya kilimo kwanza!

Naomba pia kufahamu sehemu ambazo unaweza ukapata washauri wazuri wa kilimo cha mpunga ambao si tu wanatumia makaratasi bali wana uzoefu na hii kazi kwa vitendo kwa muda sasa.

Asanteni.
---
Naomba ushauri jinsi ya kuanzisha shamba dogo la kilimo cha mpunga; maelezo yangu ya awali ni kama ifuatavyo

  1. lengo ni kujiongezea kipato
  2. eneo ni eka 2.5
  3. aina ya mbegu : za muda mfupi zinazonukia , kwa ajili ya kuvutia wateja
  4. aina ya kilimo : ningependa kununua pampu ya kutumia petrol/diesel ili niongezee maji wakati pakiwa na upungufu wa mvua; niwe namwagilia ndani ya vijaruba vidogo; naomba pia ushauri kuhusu aina ya pampu
  5. nitaajiri kibarua 1; atafanya kazi za ulinzi na palizi
  6. Ardhi ni ya kununua ( Tshs 50000 kwa eka), maji yapo ndani ya mita 50 na ni ya kudumu
  7. Mtaji nitategemea mkopo kutoka benki nitakaorejesha ndani ya miaka 4
Naomba ushauri wa hali halisi ya kilimo hiki, je bajeti yangu inatakiwa iewje(kiasi gani), je eneo linatosha au halitaweza kulipa gharama za uendeshaji?, nitaweza kubreak even baada ya muda gani

nawasilisha
---
kasopa,
Thanks kwa ushauri,

Naomba kama una data za maeneo mhimu kwa kilimo cha mpunga katika mkoa wa Morogoro uwe wa kwanza kunipatia hapa ili niweke plan yangu vizuri kwa ajili ya kuyatembelea nikianza na Dakawa kama ulivyo nitajia hapo awali.

Ahsante!
---
Hellow wana jf,

Katika kupambana na Hali ya uchumi, ninajipanga kwenda kulima mpunga huko ifakara na Kwa utafiti kidogo nilioufanya nimeona naweza kutumia km sh 350,000/=, Kutoka kukodisha shamba mpaka kuvuna na nakadilia eka moja.

itatoa gunia km kumi na nitahifadhi mpaka bei iwe km 90000 Kwa gunia la mpunga ndipo niuze hivyo eka moja naweza kupata faida ya sh 550000.

Natazamia kuanza na heka hamsini, naomba waliowahi kulima huko wanipe ushauri kwani nataka kuanza kulima kuanzia mwezi wa tisa.
---
Habari wadau, natarajia kulima mpunga msimu wa masika, lakini kabla hujaingia LAZIMA ufanye udadis ili kujiridhisha!

Ukiwauliza wakulima wenyewe wanakuambia heka moja inatoa magunia 20-30
Wengine magunia 15-20

Sasa UPI ukweli?

Naomba mwenye maelezo ya kina, kama inawezekana anieleze ni aina gani ya mbegu ya mpunga inayovumilia hali ya hewa na yenye mavuno mengi /mazuri!

Naomba kuwasilisha wakuu!

Karibuni nyote!

Sent using Jamii Forums mobile app
---
Jamani naomba kufahamu ukweli kuhusu Kilimo cha umwagiliaji cha mpunga nimepata taarifa sasa nahitaji kujua zaidi taarifa nilizopata nikwamba.kukodi hekta 1 ni 800,000/=Kulima 100,000/=,kurudia kulima 80000/=, Kupanda 180000, Mbolea 300000, kuvuna na mashine 180000 JUMLA ni kama 1700000.kwa kila hekta na Mavuno yanakisiwa 7.5 tani, Je hapa kuna ukweli naomba kama kuna mzoefu atupe ukweli wa hii skim

Sent using Jamii Forums mobile app
===

BAADHI YA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU

Mkuu Sendoro Mbazi

eka 2.5 ni sawa na hekta 1, hapo unapata vijaruba 25 vya 20 x 20
kulima kila kijaruba sh 3000(makadirio kibarua), jumla 75000
kwa trekta 50,000 x 2.5 = 125,000
kusawazisha/ harrowing 30 x 2.5 = 75000.

Mbegu tafuta kwa wakulima ndio za uhakika zaidi japo madukani ni kati ya 2500 mpaka 3500
ukisambaza mbegu/broadcasting utahitaji kg 20 x 2.5 = 50 x 3000 = 150,000
ukipanda kitaluni kg 3 x 2.5 = 7.5 x 3000 = 22500 (kuna gharama za kuotesha miche)

Palizi 2, (25 x 3000)2 = 150,000.

niishie hapo kwanza..
sijataja gharama za kuvuna kupiga na kuhifadhi na vingine kama nimesahau

NB: kijana mmoja hawezi palilia peke yake kama hujapanda kwa mistari itamgharimu muda mwingi sana
---
Mkuu Sendoro Mbazi, hongera kwa kuingia kwenye Kilimo cha mpunga mchango wangu ni huu hapa, utanijulisha iwapo utakuwa ni msaada kukidhi haja yako.

Aina za mbegu
Tumia mbegu iliyothibitishwa na wataalamu iitwayo SARO (TXD 306), inazaa sana gunia 32 kwa ekari moja.
Mbegu hii inaradha nzuri na inakubalika kibiashara. Ekari moja hutumia kilo 10 kwa mpunga wa kupandikiza.
Andaa sh 2500 x 2.5 jumla sh 6250 kama itabidi uzifuate mbali ongeza nauli na gharama za safari zote.

Pump
Tumia pump ya inchi 3 sawa na horse power 5 hadi 6. Ninauzoefu na pump ya JD ni ya petrol. Ekari moja petrol ni lita 5 lakini kwa mpunga itabidi uloweshe shamba mara mbili kwa wiki!

Pump 450,000/= mipira inategemea na umbali toka source ya maji, Pipe ya kunyonyea maji kwenye source 1m sh 8000, utahitaji at least mita 4, (32,000/=), pipe ya kupelekea shambani roll moja urefu wa mita 100 kama litatosha mita 1 sh 2000 ( 200,000/=) dumu la lita 20 kuhifadhia mafuta 3,000 dumu dogo la kupelekea mafuta shamba 1500/=, Petrol lita 4 kwa ekari moja x eka 2.5 x 2 kwa wiki x wiki 6 (assume 6 weeks rain, 6 weeks no rain) x bei ya petrol lita moja 2300/=, service ya pump lita moja ya oil inatosha hadi unavuna, tenga pembeni shs 10,000/= kwa service. Usafiri wa kupeleka na kurudisha pump kama huna baiskeli tenga 2000 kila siku ya kumwagilia kwa umbali ndani ya kilometer 5.
Hapa andaa jumla ya shillingi 974,500/=.

Kama ni shamba jipya
Kutengeneza majaruba idadi yake inategemea mtelemko wa shamba - andaa 50,000/= kwa ekari
kusawazisha ndani ya majaruba (hii ni kazi ngumu na kubwa sana kutegemea na slope ya shamba) andaa angalau laki 3 kwa kila ekari moja. Shamba la mpunga sharti liwe level ili kumwagilia kwa urahisi, hii ni very expensive operation, kutengeneza shamba la mpunga ni kama ujenzi wanyumba, ukishatengeneza unabaki ukarabati tu.
Andaa 350,000/= x 2.5 jumla 875,000

Bei ya shamba 50,000 x 2.5 jumla 125,000/=

Gharama zingine za shambani zote kwa ujumla hadi unarudisha mzigo tenga pembeni sh 700,000/= kwa ekari moja kwa hiyo jumla gharama 1,750,000/=

Jumla ghafi 3,730,750/= ongezea 10% tahadhari (373,075/=)

Jumla kuu 4,103,825/=


Ukifuata utaalamu utavuna gunia 32 kwa ekari lakini kwa kuwa na uhakika assume mavuno gunia 25 kwa ekari. Uza bei ikifikia 80,000/= kwa gunia la kilo 100/=
Mapato itakuwa 5,000,000/=
Faida 5,000,000/= kutoa 4,103,825/= inabaki 896,175/=

Mahesabu yanaonesha kuwa utarudisha pesa uliyowekeza na kupata faida
Faida kubwa zaidi ni shamba ambalo utakuwa umeshali-level tayari itakusaidia kuwa na gharama kidogo za umwagiliaji na level inafaida nyingi sana, hutaingia garama hii ya levo miaka ijayo bali ni kufanya usawazishaji mdogo tu.

Nakushauri ukitaka kufanikisha kilimo cha mpunga hakikisha unaweka shamba lako level, yaani ukiweka maji kwa kina cha sm 1 au 2 yasambae jaruba lote kwa kina cha sm1 au 2. Level kweye shamba la mpunga haina mbadala, kutengeneza jaruba na kuweka level ni mambo ya LAZIMA kwenye shamba la mpunga!
Nimewasilisha!
---
Maandalizi sahihi ya shamba ni jambo la msingi katika kuboresha kilimo cha umwagiliaji wa mpunga. shamba lisipoandaliwa vema husababisha mbinu bora zinazoshauriwa kutoonyesha matokeo katika kiwango kinachotarajiwa hasa katika uzalishaji. Kimsingi maandalizi ya shamba yanatakiwa yafanyike kwa usahihi na kwa wakati katika mtiririko unaotakiwa. Zifuatazo ni hatua saba muhimu na za msingi katika kilimo cha mpunga.

1.KUSAFISHA SHAMBA
Safisha shamba mapema kabla ya msimu kuanza. Kusanya na kuangamiza visiki na takataka nyingine zote. Masalia ya mazao yanaweza kutumika kutengeneza mbolea ya mboji. Inapobidi tumia moto kwa uangalifu sana maana moto unaweza kuharibu mazingira, unaua wadudu rafiki, unaharibu udongo na kuteketeza mboji.

2.KULIMA
Kulima husaidia kupunguza kiasi cha magugu, huruhusu mzunguko mzuri wa hewa na maji, hurahisisha mizizi kupenya na kuchanganya masalia ya mazao kwenye ardhi. Wakati wa kulima uangalifu unahitajika ili kuzuia kuharibu usawa wa ardhi. Kina cha kulima kiwe kati ya sentimeta 10 na 15. Ili kurahisisha na kuharakisha kazi ya kulima ni vema kutumia zana/mashine rahisi kama Trekta la mkono na wanyamakazi

3.KUKARABATI/KUJENGA MAJARUBA
Baada ya kulima hakikisha kuwa kingo za jaruba zimekarabatiwa ili kuweza kuhifadhi maji vema. Kama ni shamba jipya, ujenzi wa kingo za jaruba ufanyike kwa kufuata utaalamu unaotolewa. Kingo imara ni muhimu kudhibiti vema maji shambani.

4. KUVURUGA
Weka maji shambani kiasi cha sentimeta 3 hadi 5 juu ya usawa wa ardhi ili kukamilisha vema uvurugaji. Jembe la mkono linatumika lakini ili kurahisisha na kuharakisha kazi hii ni vema kutumia trekta la mkono au wanyamakazi. Unapotumia wanyamakazi au trekta la mkono weka maji shambani si zaidi ya siku moja kabla. Shamba lililovurugwa vema huiwezesha mizizi ya miche kupenya vema ardhini.

5. KUSAWAZISHA SHAMBA
Baada ya kuvuruga ni lazima kuhakikisha kwamba shamba limesawazishwa vema. Shamba lililosawazishwa vema linaruhusu usambaaji mzuri wa maji. Wakati wa kusawazisha kina cha maji kiwe kiasi cha sentimeta 3-5 juu ya usawa wa ardhi Ili kurahisha kazi hii tumia reki ya ubao ili kuvuta udongo kutoka sehemu zilizoinuka kuelekea sehemu zilizo bondeni

6.VYANZO NA ATHARI ZA UPOTEVU WA MAJI YA UMWAGILIAJI
Ili kupata maji ya kutosha inabidi kuhakikisha kwamba upotevu wa maji ya umwagiliaji unapungua kwa kiwango kikubwa na wakulima wanamwagilia maji kwa kiasi kinachohitajika bila kuzidisha kiwango.

Vyanzo vya upotevu wa maji ya umwagiliaji katika skimu za mfano ni pamoja na:
• Maji yanayopotea kwenye mifereji mikuu, ya kati na ile midogo ya kusambaza maji mashambani.
• Maji yanayopotea mashambani wakati wa kumwagilia.

Upotevu wa maji kwenye mifereji mikuu, ya kati na ile ya kusambaza maji unasababishwa na aina ya udongo uliotengeneza kingo za mfereji, uchafu na matengenezo hafifu ya mifereji. Katika baadhi ya skimu upotevu wa maji kwenye mfereji mkuu uliosababishwa na kuvuja maji kwenye tuta la mfereji mkuu na kunywea chini ya ardhi ulikuwa mkubwa kiasi cha kuathiri upatikanaji wa maji kwenye mashamba yaliyoko mbali na banio.Vilevile athari nyingine ilikuwa ni maji mengi kuingia sehemu yasikohitajika na kusababisha tatizo la maji kutuama kwa muda mrefu.

Hivyo wakulima wanashauriwa kupunguza upotevu huu wa maji kwenye mfereji kwa kujengea na kusakafia. Upotevu wa maji mashambani wakati wa kumwagilia unasababishwa na kuvuja kwenye tuta linalozunguka jaruba, kunywea chini na kuzidisha kiwango cha maji ya kumwagilia kinachotakiwa. Hii mara nyingi inasababishwa na utengenezaji mbovu wa jaruba. utengenezaji wa majaruba na uimarishaji wa kingo za jaruba umesaidia kupunguza upotevu wa maji kwa kiwango kikubwa na hatimaye kuongeza mavuno na kipato cha mkulima.

7. UPANDIKIZAJI MPUNGA
Ili kupata mavuno mengi na kukifanya kilimo cha mpunga kuwa cha faida ni muhimu wakulima kuzingatia mbinu hii muhimu na kuachana na kilimo cha kiholela kwa kumwaga mbegu moja kwa moja shambani. Aidha kwa wakulima wanaofuata kanuni hii wamepata mafanikio makubwa.

Faida zinazopatikana kwa kupandikiza mpunga
• Mkulima huweza kuchagua miche bora na mizuri ikiwa kitaluni.
• Miche hukua haraka na yenye afya .
• Kiasi kidogo cha mbegu huhitajika.
• Mavuno huwa mengi.

Njia za kupandikiza miche ya mpunga
Zipo njia kuu mbili za kupandikiza miche ya mpunga, nazo ni:
• Kupandikiza kwa mistari
• Kupandikiza bila ya kufuata mistari (Mchaka mchaka).

Aidha kati ya njia hizi mbili, njia ya kupanda kwa mistari ndiyo inayopendekezwa.zaidi. Pamoja na kwamba upandikizaji wa mistari unahitaji nguvu kazi zaidi, njia hii imeonyesha kuwa na mafaniko mengi ikilinganishwa na kupandikiza kiholela. Shamba lililopandwa kwa mistari ni rahisi kupalilia kwa kutumia kipalizi cha kusukuma kwa mkono. Pia ni rahisi kwa mkulima kupanga idadi ya mashina/mimea kwa eneo kwa uchagua nafasi aitakayo itakayompa mazao mengi.

Uandaaji wa miche
Kabla ya kupandikiza miche shambani ni muhimu kufanya maandalizi yafuatayo:
• Inashauriwa kumwagilia miche kwanza ili kupata urahisi wa kungo’a
• Ili kuzuia miche isikatike ovyo, miche ing’olewe kwa kushikwa chini zaidi ya shina
• Epuka kung’oa miche mingi kwa wakati mmoja
• Miche ifungwe kwenye mafungu madogo madogo ili kurahisisha usafirishaji na upandikizaji shambani
• Miche bora tu ndio ichaguliwe. Sifa za miche bora
• Iwe na kimo kinacholingana,
• Iwe na majani mafupi yaliyosimama, yenye mizizi mingi na yenye afya, isiyoshambuliwa na wadudu wala magonjwa,

Jinsi ya kupandikiza miche
• Miche ishikwe kwa vidole vitatu kama inavyoosha kweye picha chini
• Pandikiza kati ya miche 2 -3 kwa kila shina
• Kwa mafanikio zaidi, miche ipandikizwe katika kina cha sentimita 2-3.

Chanzo: Mitiki
---
Mkuu ni wazo zuri sana hili na mimi ningekushauri utoe kabisa mchanganuo uno onyesha utatumia kiasi fulani na utapata faida kiasi hiki, make unaweza kuwa una ashumu kutumia hicho kiasi ukaja kujikuta kimepanda juu au kimeshuka chini, Na vile vile Usipende sana kuuza mpunga tu.

Cha kufanya ni kujipanga na kuwa na mashine yako unakoboa una gred unapali na kuuza mifuko ya kilo tano hadi 10, ungeweza kufanya hivyo mwaka mzima tatizo linakuja kwamba Watanzania wengi mashamba tuliyo nayo yaani mtu mmoja mmoja haitoshi kulisha hata Kata moja mwaka mzima,

Kwa nchi za wenzetu utakuta mtu shamba lake moja lina tosha kulisha hata mikoa mtatu mwaka mzima hapo ndo inakuwa raha kuweka mitambo yako ya kuprocess kwa sababu malighafi unayo,

OK KAZI NJEMA NA UKIFANIKIWA URUDU KUTUKUZA NA UKISHINDWA NAPO URUDI KUTUJUZA ILI TUTUMIE KAMA CASE STUDY
---
Zar,

Habari yako ndugu yangu.

Mimi sijalima huko lakini ninaye mtu wangu wa karibu ambaye alikuwa analima huko na bado anaendelea lakini anakatishwa tamaa sana na mambo yanayotokea pale. Kwanza wenyeji wenyewe ni choka mbaya hawana uwezo wa kulima pale kwakuwa kilimo cha Pale ni cha umwagiliaji na kinahitaji pesa ili kuweza kuchangia mafuta ndio Pump ifanye kazi ya ku push maji kutoka mtoni yaingia mashambani. Sasa wenyeji hawapendi sana kuona watu kutoka Dsm na sehemu nyingine wanalima pale. So kama unaenda ulifahamu hili swala lipo.Nadhani wenyeji wana wish ile sehemu ikae pori kama ilivyoachwa na wachina kuliko kuona wageni wanakuja kulima.

Huyu jamaa alipoanza kulima alipewa sehemu pori na uongozi (kamati ambayo imeteuliwa pale kusimamia) akalima visiki akaanza kulima mpunga kwenye hivyo vi Plot vyake. Lakini jambo la ajabu baadae wakamnyang'anya wakamgawia mtu mwengine. Kwa kisingizio eti amechukua sehemu kubwa so wakampunguzia na hakupewa compensation yeyote.

Sometimes maji nayo yanakuwa changamoto kwakuwa si wakati wote mpunga unahitaji maji. Ili uweze kuvuna mpunga inabidi shamba liwe kavu kabisa. Sasa hapo lazima wote muende sawa wakati wa kumwagia pampu ikiwashwa inabidi wote muwe kwenye stage ya kuhitaji maji shambani.

Kuna changamoto nyingi za ki menejimenti pale mahala , hilo lazima ulifahamu.
---
Mi ningemshauri mtu yeyote anayetaka kuanzisha mradi wowote asianzishe kwa majaribio au kama part time inayokosa proper concentration, vinginevyo ataishia kukiri kutofaidika na mardi na kisha kutoa mchango hasi juu ya mradi huo.

Naona walio wengi katika Jf wanataka kufanyia kazi habari za kusikia sikia tu bila kuzifanyia upembuzi yakinifu yaani kujishughulisha kwa kina kujua kila kitu kuhusu mradi.

Kwa Ifakara, Mang'ula, Kiberege, Mkula nk, ni bora mjasiriamali wa kuja akanunua mchele na kuuza mbali badala ya kulima mpunga. Katika kipindi cha mavuno, yaani june,julai mpaka August watu huvuna mpunga na kuuza kwa bei ndogo sana, hasa sehemu za Chita, Mngeta na Mlimba, na kisha mchele huohuo huuzwa kwa bei karibia mara tatu yake baada ya muda mfupi wa miezi mitatu tu yaani November,december mpaka march.

Sasa mdau, kama kweli unataka kukwepa adha ya kulima mpunga,na kupata faida ya muda mfupi fanya kununua mchele badala ya kulima mpunga. kule ni bondeni, kuna mito mingi which means pia kuna malaria nk, mdau kash kash hizo baba utazimudu?

Halafu kuna vishawishi vya ndogondogo kama alivyosema mdau hapo juu, si utamalizia mtaji huko? Naomba ufikirie mara mbili mdau kabla hujaamua!
---
@Robbinhood,
Robbinhood, kilimo cha mpunga wa umwagiliaji ni cha uhakika. Risk zake ni pale serikali inapozuia uuzaji mchele nchi za nje, hapo bei hudoda kabisa! Risk nyingine ni kulima eneo lenye mkondo wa mafuriko, huko watu hupata hasara!

Na risk nyingine ni ndege na panya kuna misimu hutokea mlipuko wa hao viumbe ambapo wakulima hukimbia mashamba. Ndege wakiwa wengi hata watu 3 kwa ekari moja huweza kutoka povu mdomoni kwa kukimbia huku na kule kufukuza ndege!

Ukilima kiangazi peke yako kwa umwagiliaji maeneo yenye wafugaji wa Kimasai jua unawatayarishia malisho! Watakuja kuingiza mifugo yao mchana kweupe na mwenyewe ukishuhudia kwa macho yako! Chezea masai wewe!!??

Mpunga unafaida kubwa hasa ukiangalia bei ya mchele sokoni hivi sasa, ukistawisha ipasavyo kwenye mashamba ya umwagiliaji kwa kufuata maelekezo ya wataalamu unapaswa upate kuanzia gunia 25 kwa ekari moja!

Kila gunia ukikoboa ukapata kilo 70 za mchele ukauza bei ya jumla 1500/= wakati wa uhaba, ekari moja unapata sh 2.6 Millioni!

Gharama ya kutunza shamba hadi kuingiza nyumbani Dakawa Morogoro ilikuwa sh 550,000/= mwaka 2011! Sijui msimu uliopita hali ilikuwaje! Kwa hiyo utaona faida ni kubwa tu hasa ukilima eneo kubwa!!

Wengi tunafahamu kuwa mchele umekuwa ukiuzwa sokoni rejareja kwa bei kubwa tu! Inawezekana kabisa kuvuna hata zaidi ya magunia 35 kwa ekari iwapo utaalamu utatumika na kutambua misimu yenye mavuno makubwa!

Wakulima wazoefu kutoka maeneo ya umwagiliaji watakubaliana kabisa na maelezo haya!!! Hii siyo hadithi ya machungwa 4,000 kwa mchungwa wa miaka 3 nooo!!! It is real!!
---
Sendoro Mbazi,

Mkuu Sendoro Mbazi, hongera kwa kuingia kwenye Kilimo cha mpunga mchango wangu ni huu hapa, utanijulisha iwapo utakuwa ni msaada kukidhi haja yako.

Aina za mbegu
Tumia mbegu iliyothibitishwa na wataalamu iitwayo SARO (TXD 306), inazaa sana gunia 32 kwa ekari moja.
Mbegu hii inaradha nzuri na inakubalika kibiashara. Ekari moja hutumia kilo 10 kwa mpunga wa kupandikiza.
Andaa sh 2500 x 2.5 jumla sh 6250 kama itabidi uzifuate mbali ongeza nauli na gharama za safari zote.

Pump
Tumia pump ya inchi 3 sawa na horse power 5 hadi 6. Ninauzoefu na pump ya JD ni ya petrol. Ekari moja petrol ni lita 5 lakini kwa mpunga itabidi uloweshe shamba mara mbili kwa wiki!

Pump 450,000/= mipira inategemea na umbali toka source ya maji, Pipe ya kunyonyea maji kwenye source 1m sh 8000, utahitaji at least mita 4, (32,000/=), pipe ya kupelekea shambani roll moja urefu wa mita 100 kama litatosha mita 1 sh 2000 ( 200,000/=) dumu la lita 20 kuhifadhia mafuta 3,000 dumu dogo la kupelekea mafuta shamba 1500/=, Petrol lita 4 kwa ekari moja x eka 2.5 x 2 kwa wiki x wiki 6 (assume 6 weeks rain, 6 weeks no rain) x bei ya petrol lita moja 2300/=, service ya pump lita moja ya oil inatosha hadi unavuna, tenga pembeni shs 10,000/= kwa service. Usafiri wa kupeleka na kurudisha pump kama huna baiskeli tenga 2000 kila siku ya kumwagilia kwa umbali ndani ya kilometer 5.
Hapa andaa jumla ya shillingi 974,500/=.

Kama ni shamba jipya
Kutengeneza majaruba idadi yake inategemea mtelemko wa shamba - andaa 50,000/= kwa ekari
kusawazisha ndani ya majaruba (hii ni kazi ngumu na kubwa sana kutegemea na slope ya shamba) andaa angalau laki 3 kwa kila ekari moja. Shamba la mpunga sharti liwe level ili kumwagilia kwa urahisi, hii ni very expensive operation, kutengeneza shamba la mpunga ni kama ujenzi wanyumba, ukishatengeneza unabaki ukarabati tu.
Andaa 350,000/= x 2.5 jumla 875,000

Bei ya shamba 50,000 x 2.5 jumla 125,000/=

Gharama zingine za shambani zote kwa ujumla hadi unarudisha mzigo tenga pembeni sh 700,000/= kwa ekari moja kwa hiyo jumla gharama 1,750,000/=

Jumla ghafi 3,730,750/= ongezea 10% tahadhari (373,075/=)

Jumla kuu 4,103,825/=


Ukifuata utaalamu utavuna gunia 32 kwa ekari lakini kwa kuwa na uhakika assume mavuno gunia 25 kwa ekari. Uza bei ikifikia 80,000/= kwa gunia la kilo 100/=
Mapato itakuwa 5,000,000/=
Faida 5,000,000/= kutoa 4,103,825/= inabaki 896,175/=

Mahesabu yanaonesha kuwa utarudisha pesa uliyowekeza na kupata faida
Faida kubwa zaidi ni shamba ambalo utakuwa umeshali-level tayari itakusaidia kuwa na gharama kidogo za umwagiliaji na level inafaida nyingi sana, hutaingia garama hii ya levo miaka ijayo bali ni kufanya usawazishaji mdogo tu.

Nakushauri ukitaka kufanikisha kilimo cha mpunga hakikisha unaweka shamba lako level, yaani ukiweka maji kwa kina cha sm 1 au 2 yasambae jaruba lote kwa kina cha sm1 au 2. Level kweye shamba la mpunga haina mbadala, kutengeneza jaruba na kuweka level ni mambo ya LAZIMA kwenye shamba la mpunga!
Nimewasilisha !!!
 
Mkuu wewe upo maeneo gani na unashamba au unategemea kukodi mashamba kama unaweza kwenda dakawa kunawanakijiji wanakodisha mashamba na kama utabahatisha kwenye block za iliyokuwa nafco kunawatu hukodisha block zao utapata watala hukohuko.
 
Ni kigumu kinahitaji kujitoa na usimamizi wa kutosha unaweza ukapata gunia 30 kwa eka inategemea unalima wapi unatumia nini na umejitumaje hili ni shamba la watani zangu wapogoro hawa hawtumii mbolea wala planter.
 
Mkuu wewe upo maeneo gani na unashamba au unategemea kukodi mashamba kama unaweza kwenda dakawa kunawanakijiji wanakodisha mashamba na kama utabahatisha kwenye block za iliyokuwa nafco kunawatu hukodisha block zao utapata watala hukohuko

kasopa nashukuru sana kwa msaada wako japo bado nategemea kupata estimates of maximum yield katika ekari moja kama kilimo kimefanyika kitaalam ili nifanya maamuzi ya mwisho ya kujua kiasi/ukubwa wa eneo ninalotakiwa kutafuta.

Ninafanya utafiti wa kupata maeneo ya kilimo kanda ya Ziwa victoria na Mbeya. Jana kuna mtu amenipatia data za Kilombero hivyo nafikiria pia kufuatilia ikiwa ni pamoja na Dakawa kama ulivyoniambia. Haya ni maandalizi ya kazi ya Mwakani.
 
ni kigumu kinahitaji kujitoa na usimamizi wa kutosha unaweza ukapata gunia 30 kwa eka inategemea unalima wapi unatumia nini na umejitumaje hili ni shamba la watani zangu wapogoro hawa hawtumii mbolea wala planter
Chiwa,
Nashukuru kwa ushauri wako ila naomba ufahamu kuwa hakuna kitu kirahisi hapa Duniani na kadri kitu kinapokuwa kigumu kupatikana ndivyo faida kubwa inavyozidi kupatikana. Dhahabu ni ngumu sana kupatikana na ndiyo maana inalipa zaidi n.k.

Tunachotakiwa watanzania ni kufanya kazi kwa bidii zote ili kuongeza vipato vyetu, hii ndiyo siri pekee ya mafanikio. Hata China ya leo imefikiwa baada ya wananchi kujituma katika kazi na biashara na kupata security za mikopo.

Kama ungenipatia analysis ya prifit margin katika kilimo cha mpunga ingenisaidia zaidi lakini kama hoja ni kujituma, hilo lisikupe shaka.
 
Mkuu mimi kwa maono yangu mpunga unalipa sana tu wala usihofu ispokuwa tafuta eneo lenye maji yakutosha yani usitegemee mvua hasakama utapata maeneo ya mkoa wa morgoro ni nzuri zaid kwakuwa huku gharama za undeshaji ni ndogo ukilinganisha na bara.

Na bei pia huku ni nzuri huduma za madawa beipoa na zinapatkana vinginevyo laba uwe na unyeji wahuko nyanza lakini mimi nakushauri utafute shamba sehem za huku hata samani yake ni tofauti na nyanza kila mwaka linapanda marambili mikopo pia inakubalika kiurahisi kama utakim nyaraka zinazo takiwa

Mungu akubariki ufanikiwe ndotoyako mkuu. Memory,
 
Mwaka jana nililima Ifakara ikala kwangu japo nisiwe mnafki sikuweza kusimamia vizuri na resource hazikutosha sana kwa kifupi kulikuwa na uzembe mwaka huu najipanga tena kulima na nimejaribu kufanya gharama za awali ili nione ina kuwaje kama ninavyo kutumia nadhani kwa mchanganuo huu.

Tutawachokonoa wadau watusaidie zaidi kwani nina plan ya miaka mitatu kwa kila mwaka kuongeza eneo na pia nina mpango wa kuwasaidia wakulima wadogo wadogo kwa kuanzisha umoja wao na kupata bei nzuri zaidi
 
Kuna garama za chini za mahitaji hizo huwa zinarudi kwa kila kitu tunawauzia wasaidizi wa shamba kwa mfano umenunua jiko shs 70000 wanfanya kazi inayofanana na hiyo wakati wa kuondoka unawapa jiko japo mimi nimeamua kutoa hizo bidhaa kwa bei nafuu kwa kiasi fulani ili wasiumie sana.
 
Mkuu mbona kuna mapunguf mengi kwenye mchakato wako napia umepanda gunia tatu 3 katika heka 15 ulitakiwa upande gunia4 napia ni aina gani ya mbegu uliyopanda na unaweza kutujuza ni kiasi gani ulivuna kwa sababu haiwezekani ule hasara kwa heka 15 hata iweje labda mpunga ufe ama hukuzingatia mbegu bora nayo pia ni ngumu sana kupiga chini kwa hesabu hata kamaulilima kienyeji basi ungeambulia hata 6m sio ukose kabisa.

Kwa heka 15 matarajio ya mavuno ni gunia30 kwa heka mbegu bora na matunzo usitegemee mvua utaumia mtalam lazima uwe nae Chiwa,
 
Unachosema ni kweli hiyo kwanza ni plan ya mwaka huu bado inamarekebisho sio gharama halisi mwaka jana nililima eka kumi nikapata gunia 22 usiogope ndio ukweli nilitumia kama 2M kwa kilimo chote kuna mambo mengi lakini kubwa ni usimamizi mbovu kwa kumuamini mtu nilivyoenda kwenye mavuno nikakuta aibu yangu.

Lakini mwaka huu sitaki utani mbaya zaidi hata mbegu walinichanganyia kwa wastani kama usimamizi umekwenda vizuri kulingana na mashamba ya majirani umekosa kabisa basi gunia sita kwa heka japo kuna ugojwa wenyeji wanauita kimyanga huo unaweza kula shamba zima.

Nakushauri tafuta fedha ingia utajua vizuri hapa kweye computa hakuna kitu gharama muhimu ndo hizo maelekezo mengine mbele kwa mbele.tuache uwoga.

Hasara inawezekana wako walio panda hekari 100 na kupata gunia mbili acha wali uwe mtamu muhimu ni kufanya na kurekebisha makosa kadri unavyozoea shamba.
 
kasopa,
Thanks kwa ushauri,

Naomba kama una data za maeneo mhimu kwa kilimo cha mpunga katika mkoa wa Morogoro uwe wa kwanza kunipatia hapa ili niweke plan yangu vizuri kwa ajili ya kuyatembelea nikianza na Dakawa kama ulivyo nitajia hapo awali.

Ahsante!
 
Bilashaka mkuu kidogo nipo nje ya eneo nategemea kurudi tareh28 nikifika ntaku pm kama vip twende ukaonane na wenyeji mojkwamoja
Thanks kwa ushauri

Naomba kama una data za maeneo mhimu kwa kilimo cha mpunga katika mkoa wa Morogoro uwe wa kwanza kunipatia hapa ili niweke plan yangu vizuri kwa ajili ya kuyatembelea nikianza na Dakawa kama ulivyo nitajia hapo awali.

Ahsante!
 
Desa la nguvu ili Tz hasa kyela,ifakara,Mangula,mbarali wengi hutumia system ya kumwaga mpunga badala ya kupanda.
 
Mkuu nimejaribu kufuatilia hii kitu nimeona ina tija sana. Nitaenda kuongea na mshauri wangu wa kilimo kuona kama nitaweza kuapply shambani kwangu. Tatizo ni kwamba wataalamu wetu wakilimo wapo outdated sana na vitu kama kama hivi. Wao na internet ni vitu viwili tofauti
 
Hellow wana jf,

Katika kupambana na Hali ya uchumi, ninajipanga kwenda kulima mpunga huko ifakara na Kwa utafiti kidogo nilioufanya nimeona naweza kutumia km sh 350,000/=, Kutoka kukodisha shamba mpaka kuvuna na nakadilia eka moja.

itatoa gunia km kumi na nitahifadhi mpaka bei iwe km 90000 Kwa gunia la mpunga ndipo niuze hivyo eka moja naweza kupata faida ya sh 550000.

Natazamia kuanza na heka hamsini, naomba waliowahi kulima huko wanipe ushauri kwani nataka kuanza kulima kuanzia mwezi wa tisa.
 
Mkuu ni wazo zuri sana hili na mimi ningekushauri utoe kabisa mchanganuo uno onyesha utatumia kiasi fulani na utapata faida kiasi hiki, make unaweza kuwa una ashumu kutumia hicho kiasi ukaja kujikuta kimepanda juu au kimeshuka chini, Na vile vile Usipende sana kuuza mpunga tu.

Cha kufanya ni kujipanga na kuwa na mashine yako unakoboa una gred unapali na kuuza mifuko ya kilo tano hadi 10, ungeweza kufanya hivyo mwaka mzima tatizo linakuja kwamba Watanzania wengi mashamba tuliyo nayo yaani mtu mmoja mmoja haitoshi kulisha hata Kata moja mwaka mzima,

Kwa nchi za wenzetu utakuta mtu shamba lake moja lina tosha kulisha hata mikoa mtatu mwaka mzima hapo ndo inakuwa raha kuweka mitambo yako ya kuprocess kwa sababu malighafi unayo,

OK KAZI NJEMA NA UKIFANIKIWA URUDU KUTUKUZA NA UKISHINDWA NAPO URUDI KUTUJUZA ILI TUTUMIE KAMA CASE STUDY
 
chodoo,

Salaam Chonde,

Nashukuru kwamba umeonyesha nia ya kulima mpunga ila kabla sijatoa ushauri wangu..Ningependa kujua yafuatayo:

1. Ulishawahi kulima mpunga tofauti na ifakara?
2. Unategemea kukodi shamba maeneo gani? Ie mgeta,chita,malinyi
3.Nafasi yako ya kusimamia shamba ikoje?

Maana nina uzoefu kidogo ktk maeneo hayo nadhan ungenijubu basi ningekushaur kadir niwezavyo!
 
John Deer,
kuhusu kulima mpunga Ndiyo kwanza naanza sijawahi lima sehemu nyingine , na maeneo ni kijiji cha namawala, sitakuwa full time shamba lakini naplan kuwa na visit mara mbili kwa mwezi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom