Fahamu kuhusu kilimo bora cha Hiliki

Iliki inapatikana sana maeneo ya Tanga wilaya muhuze kuna kijiji kinaitwa Amani nikama km 35 kutoka Muheza nabaadhi ya maeneo mengine ya juu yamilima ya usambara. Bei ya sasa naskia ni 34000 kwa iliki iliokauka kwakilo moja(huu sio msimu wailiki)
Changamoto kubwa nikuitoa kutoka huko milimani kuifikisha muheza ambapo ndo unaweza kupatia usafir wakuisafirsha mkoani.

Ubora wailiki unatagemea nakama iliki ilichumwa ikiwa imekomaa vzur na kama ilianikwa mahali pakavu yaan haikumwagikiwa namaji au mvua wakat ikiwa imeanikwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh,kana kilo tu Ni 34,000,gunia Ina maana 3,400,000,hii inataka mtaji na wateja wasiwe wa kubahatisha
 
Nilifanyaga research ya iliki siyo kulima ila ni wapi zinapatikana kwa wingi kwa bahati nilienda sehemu za lutindi,tanga huko nlizunguka vijiji kama 5 kieti,tamota,masangi,nguru,bungu kote huko nlikutana n'a zao la iliki na huko kg1 wanauza 14000 mpaka 16000 n'a kwa dar huku wanauza 25000 mpaka 26000 kwa kg wakomoro wananuua juu kidogo ya hapo......soon ntarudi tena huko kwa ajili ya kununua na kuwa supply watu wangu

Morogoro pia ipo sehemu fulani fulani ila iliki ya tanga wanasema ni the best hata iliki ya india haifikii

Soon nabadilisha tena gia angani mtamuona mrangi kwenye biashara ya mazao maana jiwe lishabuma mh kabana
Ila kwa wabishi kama sisi hata ukibana huku sisi tunapiga kule


OVA
Mwamba fanya assist kidogo.
Naomba kujua miezi gani ndiyo wanavuna na kuuza iliki huko Tanga na Morogoro?
 
Fursa zipo shambani, sio wote tubanane maofisini jamani.

Ngoja nifanye extensively research kuhusu Hiriki na Vanila

Na strawberry pia, nasikia zina pesa balaa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mwezi wa Sita na saba
Sahv mambo bado magumu
Ntakpa connection mpk jikoni tu
Usijali

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja mwamba, tuombeane uzima tuvuke salama haya magonjwa ya upumuaji siyo poa kabisa.
Hivi mwaka jana 1kg ilifikia bei gani?
Huko Tanga ni iliki nyeupe au ya kahawia(brown) ile?
Unaweza kunipa bei na aina ya iliki ya Morogoro pia.
 
shangazi tutajie mbegu yake na jinsi inavyopandwa, changamoto, umri wa kuvunwa toka kupanda, nk.

tendea haki jukwaa. umeeleza kana kwamba unawaelezea wakulima

Sent using Jamii Forums mobile app


Ozesha udongo na mbolea kutengeneza kitalu

Mwaga mbegu za iliki kwenye kitalu, wengi hufanya hivi kwenye beseni chakavu.

Miche ikifika urefu wa cent mita 5-7 hamishia kwenye vikopo au vifuu vya nazi. Hivi vitakusaidia wakati wa kuhamishia shambani kwani vifuu vinaoza

Hamishia miche shamani kipindi cha mvua, iliki inapenda maji na unyevu unyevy na haistamili jus kali hivyo shambani panda migomba kati kati ya iliki ili ilete kivuli.

iliki huzaa baada ya miaka mitatu
 
Kumbe sio miaka mingi sn ni sawa na miembe tu hii ya kisasa
Ozesha udongo na mbolea kutengeneza kitalu

Mwaga mbegu za iliki kwenye kitalu, wengi hufanya hivi kwenye beseni chakavu.

Miche ikifika urefu wa cent mita 5-7 hamishia kwenye vikopo au vifuu vya nazi. Hivi vitakusaidia wakati wa kuhamishia shambani kwani vifuu vinaoza

Hamishia miche shamani kipindi cha mvua, iliki inapenda maji na unyevu unyevy na haistamili jus kali hivyo shambani panda migomba kati kati ya iliki ili ilete kivuli.

iliki huzaa baada ya miaka mitatu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwema ndugu mwenye kujua bei ya iliki itembeavyo kwa sasa sokon tujuzane.!! (mkoa uliopo na bei husika ya ssa sokon)
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom