Kilimo cha Alizeti (Sunflower): Masoko, Mbinu na Ushauri toka kwa wadau

Naomba msaada kwa wataalam waliokwisha kulima na zao la Alizeti wanapambana vipi na ndege, maana naona watamaliza juhudi zote nilizoweka mwaka huu.

Wako wengi na wanashambulia mazao kweli kweli.
Sijawahi kulima alizeti lakini nina wazo. Hivi ukinunua waya mrefu sana na kuunganisha spika sehemu zote za shamba halafu ukakaa kwenye kona na mic wakija unafoka ''toka toka, kamata kamata, piga piga'' haitasadia? Au gharama itakuwa kubwa?
Au unanunua drone unabana kwenye kona ya shamba, ukiona wanakuja unawafuatilia na drone na kuwakimbiza kama ndege mkali anavyofukuza wengine..
 
Sijawahi kulima alizeti lakini nina wazo. Hivi ukinunua waya mrefu sana na kuunganisha spika sehemu zote za shamba halafu ukakaa kwenye kona na mic wakija unafoka ''toka toka, kamata kamata, piga piga'' haitasadia? Au gharama itakuwa kubwa?
Au unanunua drone unabana kwenye kona ya shamba, ukiona wanakuja unawafuatilia na drone na kuwakimbiza kama ndege mkali anavyofukuza wengine..
hahahhaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna njia nyingi sana za kupambana nao. Wengi huwa wanahamia shambani na kufanya kazi ya kufukuza ndege, veta nahisi wana vifaa vinaweza fanya hivyo na njia nyingine hakikisha ukitaka kulima alizeti na wenye mashamba ya eneo hilo wanailima pia ili mgawane hao ndege kwenye mashamba yenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alizeti huwezi lima peke yako! Ukilima peke yako ndege wote ni wa kwako peke yako. Mkilima wengi ndege walewale mtagawana wengi na wengine hawawezi kufika huko shamba lako lilipo maana watakua wameshashiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aiseh pole sana
Mziki wa ndege unazidi ule wa viwavi
Kwenye mpunga au mtama ungekubali
 
Naomba msaada kwa wataalam waliokwisha kulima na zao la Alizeti.

wanapambana vipi na ndege maana naona watamaliza juhudi zote nilizoweka mwaka huu maana wako wengi na wanashambulia mazao kweli kweli.
Hii nilioona nanenane mby.Tafuta net zilizochoka funga kila tunda lililoanza kukomaa.Ubunifu wangu binafsi maana nimepanga kulima ntakapotulia.Nitatafuta vifungashio laaini vyeupe,ntatoboa matundu na kuvifunga.Naomba ujaribu kidogo ila net uhakika imefanyiwa utafiti uyole Ila kuzipata net ndio ishu naomba ujaribu vifungashio.Mi ntajaribu miche michache ya majaribio, ninashamba porini kuna rutuba hatari najionea wivu rasimali imelala tu naogopa ndege.
 
Nashukuru sana kwa hiyo topic naomba hata mie nichangie, Kilimo cha Alizeti sina uzoefu nacho ila ninachoweza kukusaidia tu ni uzoefu nilionao wa mwaka mmoja nikiendesha kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti hapa Dar es salaam.

Uzalishaji wa mbegu za alizeti kwa maeneo ya Iringa, Singida, Dodoma, n.k bado upo chini ukilinganisha ni demand ya mafuta yatokanayo na mimea ambayo yanakiwango kidogo cha LEHEMU (low level of cholestrol), ukiangalia mfano importation ya edible oil from indonesia, and other Asian country is almost 80% ya demand ya edible oil kwa nchi nzima, wakati mafuta haya yanakiwango kikubwa cha LEHEMU, na ukisoma machapisho (articles za PWC,World Bank na RLDC - ambazo zinaelezea Alizeti, utaona hiyo shortfall na kuwa inchi yetu inatumia fedha nyingi sana za kigeni kwenye ununuzi wa mafuta ghafi kutoka Asian country).

Ukitoa mafuta ya disel, petrol na mafuta ya taa, mafuta ghafi ya kula yanachukua nafasi ya pili kwa kutumia fedha za kigeni kwenye uagizaji wake nje ya nchi.

Hivyo basi demand ya mbegu kwa viwanda vidogo vidogo na vikubwa vya kukamua mafuta hayo ni kubwa na inasababisha kuwepo na shortage ya hizo mbengu. Mfano mwaka huu ngunia moja la kg 65-70 kwa sasa linauzwa kati ya Tsh36,000/= hadi 45,000/=(the current price is 45,000 - 60,000 per kg January 2011)) kutegemea na eneo wakati huo huo kwa mwaka jana ngunia hilo hilo liliweza kuuzwa kwa Tsh 22,000/= hadi 35,000/= kwa kipindi hicho hicho.

Point nayotaka ku-raise hapa ni kuwa ongezeko kubwa la viwanda vidogo vidogo limeongeza demand ya mbegu, na awareness ya watu kuhusu mafuta yenye kiwango kidogo cha LEHEMU imesababisha kuwepo na demand ya mafuta hayo.
Kwa mantiki hiyo basi kama unataka kulima kilimo cha KIBEPARI na cha KISASA kwa kuangalia ile opened window kwa ajili ya KILIMO KWANZA, that is a great opportunity, go for it!!!

My take: Ila kama tu unataka kwa ajili ya ku access ile mikopo ya TIB then upeleke pesa kwingine then i don't have any comment.

Mimi ni mdau naomba tushirikiane.
Mkuu bado unaendelea na hii shughuli?
 
Jamani nilikuwa naomba kujua bei ya machine za kukamulia alizeti kupata mafuta mpaka ku purify, nimeona uko juu kua za india ndo ziko vizuri zaidi, ningependa kwa anaejua anipe bei zake, full set na za sido pia full set. natanguliza salam namaliza na shukrani.
 
Hii nilioona nanenane mby.Tafuta net zilizochoka funga kila tunda lililoanza kukomaa.Ubunifu wangu binafsi maana nimepanga kulima ntakapotulia.Nitatafuta vifungashio laaini vyeupe,ntatoboa matundu na kuvifunga.Naomba ujaribu kidogo ila net uhakika imefanyiwa utafiti uyole Ila kuzipata net ndio ishu naomba ujaribu vifungashio.Mi ntajaribu miche michache ya majaribio, ninashamba porini kuna rutuba hatari najionea wivu rasimali imelala tu naogopa ndege.
Alafu pimbi 1 anajitokeza eti kufuta maonesho ya nane nane sijui huwa wanatumia nini kufikiria
 
Back
Top Bottom