Kilimo cha alizeti na biashara ya mafuta

Truthg

Member
Sep 3, 2015
54
16
Wadau Habarini.

Naomba kujuzwa machache kuhusu kilimo cha alizeti.
Katika ekari moja yanapatikana mazao gunia ngapi?

Je, kama nahitaji kufanya biashara ya mafuta kipi ni bora kati ya kununua alizeti au kulima mimi mwenyewe.
Natanguliza shukurani zangu kwa kila atakayechangia
 
Mm nawez kukushauri kidogo kuhusu Hilo zao! Lina vitu vngi mno, but generally, nivyema ukawa unanunua mbegu/nafaka tu then unakamuaa!
 
Wadau Habarini.
Naomba kujuzwa machache kuhusu kilimo cha alizeti.
Katika ekari moja yanapatikana mazao gunia ngapi?
Je, kama nahitaji kufanya biashara ya mafuta kipi ni bora kati ya kununua alizeti au kulima mimi mwenyewe.
Natanguliza shukurani zangu kwa kila atakayechangia
Mkuu kilimo cha Alizeti kipo simple sana, ni palizi moja tu mambo bwerere.

Ili uweze kupata mavuno mazuri lazima uzingati haya:
-Ardhi, inatakiwa iwe ni ardhi zuri yenye rutuba japo alzeti huwa haisumbui sana kwenye ardhi nyingi.

-Kiwango cha Mvua, mvua iwe ya kuridhisha japo mvua ya kawaida inatosha kabisa

Idadi ya gunia kwa ekari siwezi kujua idadi kamili ila itategemeana na jinsi zao litakavyonawiri na kuiva vizuri.

Kuhusu soko, soko bado lipo chini sana kwa miaka mingi hadi leo hii.

Kwa sasa wakati wa mavuno bei ni ndogo sana(30,000/= kwa gunia) ila baadae huwa inapanda hadi kufikia 50/55 elfu kwa gunia. Hapa hadi ikifika kipindi ambapo umeanza kuadimika kati mwezi November

Mimi nakushauri uwe unanunua na kukamua halafu uwe unauza mafuta.
 
Biashara ya kukununua Alizeti na kukamua iko poa sana lakini zingatia na alizeti yenyewe kwa kawaida alizeti hupakiwa debe 7@gunia moja hivyo inatakikana ktk debe saba upate dumu 1 la lita 20 na kidumu kidogo cha lita sio Chini ya lita Tatu kawaida dumu moja la mafuta huuzwa kuanzia 60k had 75k sometimes hadi 83_85k

Kwaiyo ukikamua alizeti ya debe 7 ikatoa lita 23-25 hapa utapiga hela lakini ukiona unakamua kuanzia debe 8-10 kwa Lita 20 Aisee acha kabisa utapata hasara Kubwa

Ushauri wangu

Ukitaka kupiga hela lima alizeti mwenyewe kisasa kisha ukivuna nenda ukakamue na kuuza mwenyewe kwa sehemu Kama Mbeya, Singida na Dodoma soko la mafuta ya alizeti liko vizuri sana maana utauza mafuta ya alizeti pamoja na mashudu
 
Mkuu kilimo cha Alizeti kipo simple sana, ni palizi moja tu mambo bwerere.

Ili uweze kupata mavuno mazuri lazima uzingati haya:
-Ardhi, inatakiwa iwe ni ardhi zuri yenye rutuba japo alzeti huwa haisumbui sana kwenye ardhi nyingi.

-Kiwango cha Mvua, mvua iwe ya kuridhisha japo mvua ya kawaida inatosha kabisa

Idadi ya gunia kwa ekari siwezi kujua idadi kamili ila itategemeana na jinsi zao litakavyonawiri na kuiva vizuri.

Kuhusu soko, soko bado lipo chini sana kwa miaka mingi hadi leo hii.

Kwa sasa wakati wa mavuno bei ni ndogo sana(30,000/= kwa gunia) ila baadae huwa inapanda hadi kufikia 50/55 elfu kwa gunia. Hapa hadi ikifika kipindi ambapo umeanza kuadimika kati mwezi November

Mimi nakushauri uwe unanunua na kukamua halafu uwe unauza mafuta.

Dodoma zao za la Alizeti lina stawi sana...

Kuna mashamba ya kukodi kule... yani wewe unampa mtu pesa za gharama tu...

Unafanyiwa kila kitu... ukiamua unauza alizeti kama alizeti au unaenda kuikamua na kupata mafuta alafu unauza mafuta...



Cc: mahondaw
 
Dodoma zao za la Alizeti lina stawi sana...

Kuna mashamba ya kukodi kule... yani wewe unampa mtu pesa za gharama tu...

Unafanyiwa kila kitu... ukiamua unauza alizeti kama alizeti au unaenda kuikamua na kupata mafuta alafu unauza mafuta...



Cc: mahondaw
N:B Wenyeji wengi wa Dodoma kwa maana ya wagogo, sio watu waaminifu hata kidogo!!
 
Wakuu habarini, mimi naomba kuuliza ni wapi naweza pata mashine za kukamua mafuta yq alizeti kwa hapa dar, tafadhali mjuzi naomba anijuze.
 
Mm nawez kukushauri kidogo kuhusu Hilo zao! Lina vitu vngi mno, but generally, nivyema ukawa unanunua mbegu/nafaka tu then unakamuaa!
Hivi unamshaurije mtu anunue akamue kama hana hela?? Yeye anataka akalime apate mtaji wewe unamuambia anunue akamue
 
Back
Top Bottom