Wakulima wenzangu,ngoja nikili kuwa nililima kilimo cha kiswahili sana. Sikufanya utafiti wa soko kabla ya kulima, nililima tu kwakuwa nina ardhi na sikutaki ardhi ikae bure. Sasa natarajia kuvuna nanasi zaidi ya 200, 000 mwaka huu kuanzia Nov. Nahitaji yeyote anayefahamu soko la uhakika la nanasi na kama kuna mteja mkubwa tunayeweza kukubaliana katika reasonable price tuingie makubaliano. Bei ya viwandani siitaki kwakuwa ni dhuluma kubwa sana kwa mkulima.