Kilimanjaro: Wananchi wabadili aina ya kilimo cha mseto kwa kuondoa zao la kahawa

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,847
15,252
Ukifika mkoani Kilimanjaro utaona ni jinsi gani kizazi hiki kinavyoenda kubadili kabisa aina ya kilimo cha kahawa kilichozoeleka tangu enzi ya mkoloni.

Vijiji vichache nilivyotembelea katika wilaya ya Hai na wilaya ya moshi vijijini nimejionea wanavijiji wengi wakiwa wameondosha kabisa zao la kahawa shambani na kuweka aina Moja tu ya mazao ambayo ni ndizi kama zao la biashara,
Na baadhi ya wanakijiji wachache wakiondoa zao la ndizi pamoja na kahawa na Kupanda matunda mbalimbali kama vile mapapai, machungwa, parachichi, embe nk. kwa ajili ya biashara.

Sababu mojawapo walizotaja kuwa ni kutokana mfumo wa Maisha ya sasa, maisha ya zamani ni tofauti na sasa, kwa kuwa kilogram moja ya kahawa haitoshi hata kununua nyama lakini akiuza ndizi mkungu mmoja ni afadhali kuliko kilo ya Kahawa.

Soko la ndizi ndani ya Nchi ni kubwa kwa sasa kutokana na kuwa magari ya mizigo kutoka Dar es Salaam na Mkoa kama Iringa hufika hadi huku vijijini ndani kabisa kutafuta ndizi hasa ndizi aina ya malindi ambazo zinapendwa na Wengi.

Unafuu wa gharama katika kutunza shamba la ndizi ni afadhali kuliko utunzaji wa kahawa ambao gharama zake ni kubwa ikiwa ni pamoja na kupiga dawa mara Kwa mara, na hata uvunaji wa kahawa ni msimu mmoja kwa mwaka kulinganisha na ndizi.

Baadhi ya wakulima waliopanda Matunda tofauti tofauti kwa kuondoa kahawa na ndizi wamedai kuwa achia mbali soko la ndani idadi kubwa ya wakenya hufuata mzigo wenyewe tena Ukiwa shambani kwa hiyo mkulima hasumbuki kutafuta masoko.

Elimu, kupata elimu kwa vijana kumesaidia sana mabadiliko haya ya Kilimo ambayo wengi wanaona ni kizuri zaidi kuliko aina. Ya. Kilimo kilicho kuwepo hapo kabla ambapo kahawa, ndizi matunda nk vyote vililimwa kwa pamoja katika shamba moja na hivyo kupelekea mavuno machache

Wakulima wengi wameanza kuchukua hatua katika aina hii mpya ya kilimo chenye tija kwa mkulima
DSC_1009.JPG

DSC_1008.JPG
 
Wakulima hawajapata soko la uhakika la kahawa. Wenzao wa Kagera wanavusha kwenda Uganda kwenye bei nzuri kuliko Kagera,wakikamatwa ni msala.

Wizara iwasaidie wakulima wa nchi hii upande wa masoko
 
Wakulima hawajapata soko la uhakika la kahawa. Wenzao wa Kagera wanavusha kwenda Uganda kwenye bei nzuri kuliko Kagera,wakikamatwa ni msala.

Wizara iwasaidie wakulima wa nchi hii upande wa masoko
Safi sana....

Acha hao bodi za kahawa wavaa suti mitumbo mikubwa walime wenyewe sasa

Ova
Mkulima siku zote amekuwa akihangaika mwenyewe shambani. Hizo bodi nk. zimekuwa pale kama picha tu.
Pindi mkulima atakapo uza mazao yake basi bodi humpangia wapi akauze na kwa bei gani.
 
Huko ndio kuinuka kiuchumi sasa sio mtu unalima kitu halafu unakuja kukikopesha chama cha ushirika wakulipe wanavyotaka wao. Nimesikia Tanga wananchi wanahimizwa wapande mkonge oohoo yani afadhali hata wenzao wa Mtwara na korosho unaweza ukamuuzia wa kangomba mkonge utamuuzia nani kama usipokubaliana na bei ya soko?
 
Wapo sahihi. Ulime kahawa sasahivi uiuze wapi kwa bei nzuri?

Kulima kahawa kwasasa ni stresses tu hapa Bongo.
Kuna makampuni makubwa ya wazungu yanalima kahawa hapa Kilimanjaro., baada ya kuvuna wanasafirisha kama malighafi kwao inatengezwa vizuri na kwenda kuuzwa duniani kote
 
Kahawa imeshuka bei sana nilifanya tafiti vyama vya ushirika kilimanjaro vinapumulia mashine hali ngumu kahawa hamna wakulima nao mavuno machache miti ya kahawa imezeeka ni fursa wajikite kwenye kilimo cha ndizi na matunda.
Nadhani issue sio bei ni hivyo vyama vilijiendea endea vikakosa uaminifu kwa wateja wao.
 
Ukifika mkoani Kilimanjaro utaona ni jinsi gani kizazi hiki kinavyoenda kubadili kabisa aina ya kilimo cha kahawa kilichozoeleka tangu enzi ya mkoloni.

Baada vijiji vichache nilivyotembelea katika wilaya ya Hai na wilaya ya moshi vijijini nimejionea wanavijiji wengi wakiwa wameondosha kabisa zao la kahawa shambani na kuweka aina Moja tu ya mazao ambayo ni ndizi kama zao la biashara,
Na baadhi ya wanakijiji wachache wakiondoa zao la ndizi pamoja na kahawa na Kupanda matunda mbalimbali kama vile mapapai, machungwa, parachichi, embe nk. kwa ajili ya biashara.

Sababu mojawapo walizotaja kuwa ni kutokana mfumo wa Maisha ya sasa, maisha ya zamani ni tofauti na sasa, kwa kuwa kilogram moja ya kahawa haitoshi hata kununua nyama lakini akiuza ndizi mkungu mmoja ni afadhali kuliko kilo ya Kahawa.

Soko la ndizi ndani ya Nchi ni kubwa kwa sasa kutokana na kuwa magari ya mizigo kutoka Dar es Salaam na Mkoa kama Iringa hufika hadi huku vijijini ndani kabisa kutafuta ndizi hasa ndizi aina ya malindi ambazo zinapendwa na Wengi.

Unafuu wa gharama katika kutunza shamba la ndizi ni afadhali kuliko utunzaji wa kahawa ambao gharama zake ni kubwa ikiwa ni pamoja na kupiga dawa mara Kwa mara, na hata uvunaji wa kahawa ni msimu mmoja kwa mwaka kulinganisha na ndizi.

Baadhi ya wakulima waliopanda Matunda tofauti tofauti kwa kuondoa kahawa na ndizi wamedai kuwa achia mbali soko la ndani idadi kuwa ya wakenya hufuata mzigo wenyewe tena Ukiwa shambani kwa hiyo mkulima hasumbuki kutafuta masoko.

Elimu, kupata elimu kwa vijana kumesaidia sana mabadiliko haya ya Kilimo ambayo wengi wanaona ni kizuri zaidi kuliko aina. Ya. Kilimo kilicho kuwepo hapo kabla ambapo kahawa, ndizi matunda nk vyote vililimwa kwa pamoja katika shamba moja na hivyo kupelekea mavuno machache

Wakulima wengi wameanza kuchukua hatua katika aina hii mpya ya kilimo chenye tija kwa mkulima
View attachment 2126635
View attachment 2126659
Siku hizi naona umekuwa JF reporter kutoka ukanda wa kaskazini.
 
Kahawa imeshuka bei sana nilifanya tafiti vyama vya ushirika kilimanjaro vinapumulia mashine hali ngumu kahawa hamna wakulima nao mavuno machache miti ya kahawa imezeeka ni fursa wajikite kwenye kilimo cha ndizi na matunda.
Ndicho wakulima wa sasa wameamua kubadili mfumo mzima wa aina ya kilimo,
Kilimo cha ndizi na matunda kinalipa kuliko kahawa.
 
Kwani kahawa ikichanganywa na migomba inaua, bei ya kahawa ni nzuri aisee,mwaka Jana kilo ilifika hadi tsh 7000 kwa kilo, Mimi nimenunua mashamba makete naingia kulima kahawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom