Kilimanjaro: Taarifa kwa Umma kuhusu kukamatwa kwa Waandishi wa habari 2 na Mmiliki wa Youtube Akaunti

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,796
11,959
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), unapenda kutoa taarifa ya hali ya ukamatwaji wa waandishi na watanzania wanaotumia mitandao ya kijamii katika kutoa taarifa kwa umma.

Mwaka 2018 Kanuni za Maudhui Mtandaoni zilitungwa na kuanza kutumika. THRDC kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu pamoja na Baraza la Habari Tanzania tulifungua kesi Mahakama Kuu kanda ya Mtwara kupinga kanuni hizo kutokana na ukweli pekee kwamba zinakiuka uhuru wa kujieleza pamoja na haki ya kutumia mitandao bila masharti na gharama yoyote. Kesi hiyo bado inaendelea mahakamni mpaka sasa.

Tangu kutungwa kwa Kanuni hizo, waandishi wengi wamekamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kuendesha au kumiliki akaunti mbalimbali mtandaoni bila ya kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Kukamatwa kwa waandishi hao jana ni muendelezo wa utekelezaji wa Kanuni hizi ambazo tangu kutungwa kwake tumezipigia kelele kuwa hazifai kwasababu zinaminya uhuru wa kujieleza kinyume na Katiba.

Waandishi hao na mmiliki huyo wa YouTube akaunti walikamatwa jana siku ya Jumapili tarehe 05 Aprili 2020 kwa tuhuma za kumiliki blog bila ya kuzisajili. Waandishi hao ni: Tumsifu Kombe na Johnson Jabir. Mmiliki wa YouTube akaunti bado jina lake halijafahamika.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Kilimanjaro Bw. Nakajumo James ni kwamba: Jana jumapili jioni waandishi hao walikamatwa na askari wa jeshi la polisi aliyejitambulisha kuwa anatokea Dar es Salaam. Waandishi hao walipelekwa kituo cha polisi kati mjini Moshi. Askari huyo alionyesha pia picha za waandishi wengine kadhaa ambao wapo kwenye orodha ya kukamatwa kutokana na tuhuma za kumiliki blog bila ya kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umemuagiza wakili wake Emmanuel Makiya kufuatilia haki za waandishi hao ili haki iweze kutendeka. Mtandao utaendelea kutoa taarifa zaidi kuhusu kushikiliwa kwa waandishi hao.

Wito wa Mtandao
1. Jeshi la Polisi linapaswa kuzingatia haki za watuhumiwa hao ikiwemo kuwaachia huru au kuwafikisha mahakamani ndani ya masaa 24 kwa mujibu wa kifungu cha 64 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai sura ya 20

2. Mtandao unatoa wito kwa wamiliki wa vyombo vya habari mtandaoni, watumiaji wa mtandaoni, watunga sheria na wadau wote wa haki nchini kuendelea kupinga Kanuni hizi ambazo kimsingi zipo kinyume na misingi ya haki ya uhuru wa watu kujieleza kwa kutumia njia yoyote ile ambayo wao wameichagua ikiwemo kutumia mitandao. Ikumbukwe kuwa mitandao ya kijamii ipo bure kwa kila mtu duniani kutumia na wenye mitandao hii hawajahi kudai wanaotumia walipie chochote.

Imetolewa
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)
Aprili 06, 2020
 
Sorry, kwa anayeelewa vizuri sheria na kanuni za matumizi ya mitandao. Inaposemwa kumiliki akaunti bila kujisajili TCRA maana yake ni nini? mipaka ya akaunti inaanzia wapi na kuishia wapi? kwa lugha nyingine, ni akaunti zipi zinapaswa kusajiliwa na ni zipi hazipaswi?

Kwa mfano, mtu mwenye User name hapa JF hiyo ni account au sio? na je inapaswa kusajiliwa au haipaswi na kwa nini? au watu walioko facebook, wanahesabiwa wana akaunti au? na wanatakiwa kusajili au hawatakiwi?

Na pia inapotajwa neon 'kuandika maudhui' huwa ni nini kinakuwa kinakusudiwa kisheria? kwa sababu unaweza ukakuta hizi ID zetu humu tunatakiwa tukazisajili TCRA halafu hatuna habari.

Mwenye uelewa atasaidia ufafanuzi.
 
Aisee lumumba mna kazi sana!! Unajua maana ya kumiliki account?
Unajua maana ya maudhui?

Yaani kundika maudhui mpaka uwe na kibali!!?
Kuandika maudhui bila kuwa na kibali nayo ni sifa ya kutetea?

Ni nchi gani ambayo unaweza kuchapisha taarifa bila utaratibu ukaachwa tu?

Chadema mtaacha lini kulialia na kutetea ujinga?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sorry, kwa anayeelewa vizuri sheria na kanuni za matumizi ya mitandao. Inaposemwa kumiliki akaunti bila kujisajili TCRA maana yake ni nini? mipaka ya akaunti inaanzia wapi na kuishia wapi? kwa lugha nyingine, ni akaunti zipi zinapaswa kusajiliwa na ni zipi hazipaswi?

Kwa mfano, mtu mwenye User name hapa JF hiyo ni account au sio? na je inapaswa kusajiliwa au haipaswi na kwa nini? au watu walioko facebook, wanahesabiwa wana akaunti au? na wanatakiwa kusajili au hawatakiwi?

Na pia inapotajwa neon 'kuandika maudhui' huwa ni nini kinakuwa kinakusudiwa kisheria? kwa sababu unaweza ukakuta hizi ID zetu humu tunatakiwa tukazisajili TCRA halafu hatuna habari.

Mwenye uelewa atasaidia ufafanuzi.
Maswali ya msingi kabisa haya. Account ya YouTube nayo ni sawa na Facebook, Twitter etc?

First, Facebook Notes allows you to blog directly on the most popular social media platform in the world where a huge audience and community for your message already exists. Blogging on Facebook is a win-win all around.
 
Sorry, kwa anayeelewa vizuri sheria na kanuni za matumizi ya mitandao. Inaposemwa kumiliki akaunti bila kujisajili TCRA maana yake ni nini? mipaka ya akaunti inaanzia wapi na kuishia wapi? kwa lugha nyingine, ni akaunti zipi zinapaswa kusajiliwa na ni zipi hazipaswi?

Kwa mfano, mtu mwenye User name hapa JF hiyo ni account au sio? na je inapaswa kusajiliwa au haipaswi na kwa nini? au watu walioko facebook, wanahesabiwa wana akaunti au? na wanatakiwa kusajili au hawatakiwi?
Nadhani mkuu hapa kinacho zungumzwa ni wamiliki wa chombo husika kukosa/kutokusajili vyombo vyao, mfano wa JF hiki ni chombo kilichosajiliwa.
Ukiwa na YouTube channel mfano ayo Tv n.k hao wamiliki ndio wanatakiwa kuwa na lessen na hata waandishi wake pia wawe nazo.

Ila hii taarifa pia nayo inaonekana kukaa kishabiki Sana hawa THRDC kwanini hawataki kutaja huyo mmiliki wa hiyo YouTube Channel na channel yenyewe ili tujue Kama kweli imesajiliwa au hapana, badala yake wamewataja waandishi tu sasa hapa wanataka tuwaamini wao moja kwa moja na mjadala uwe wa upande mmoja.
 
Kuandika maudhui bila kuwa na kibali nayo ni sifa ya kutetea?

Ni nchi gani ambayo unaweza kuchapisha taarifa bila utaratibu ukaachwa tu?

Chadema mtaacha lini kulialia na kutetea ujinga?

Sent using Jamii Forums mobile app
maudhui au content zinatofautiana kulingangana na mtoaji ina maana kuna baadhi ya maudhui ni ubunifu wa mtu tu na nyingine ni habari zinazopaswa kufuata kanuni zote za habari hata hivyo waliotunga hizi sheria wanapaswa kuangalia nje ya box pia mfano: kuna maudhui ya elimu ambayo mtu huweza toa bure kupitia youtube na kuna sheria za kulinda maudhui ya aina hii zilizowekwa na youtube yenyewe lakini kwa hapa tanzania unatakiwa ulipie kitu kama hiki ina maana kwenye janga kama hili la corona kuna walimu wangeweza kuwa na chaneli za bure kwa ajili ya wanafunzi lakini atatakiwa atoe fedha kuwa na ithibati ya kuwa na chaneli ambayo yeye anatoa elimu bure
 
Sheria itawasukuma watanzania kupublish content ikiwemo live TV kwenye mitandao kwa kutumia majina feki au washirika wao nnje ya nchi. Content hiyo itaonekana ,kusomwa, kusikizwa ,popote duniani. Intenet hakuna mipaka tuliyozoea au kufahamu.
 
Sheria itawasukuma watanzania kupublish content ikiwemo live TV kwenye mitandao kwa kutumia majina feki au washirika wao nnje ya nchi. Content hiyo itaonekana ,kusomwa, kusikizwa ,popote duniani. Intenet hakuna mipaka tuliyozoea au kufahamu.
Tatizo linakuja pale unapotaka kupokea malipo ya matangazo ya biashara kupitia hizo channel hasa matangazo ya biashara zilizo sajiriwa nchini na ukilenga kuwatangazia watu waliopo nchini.

Hapo utakwama tu, na utakutana na mkono wa dola.
 
Kama hawajajisajili wasaidiwe vipi?,utaratibu ni kujisajili,na kuna faida pia katika kujisajili,
Tuache blabla ,wamiliki wafuate taratibu zilizowekwa na mamlaka,hakuna atakaye wagusa
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), unapenda kutoa taarifa ya hali ya ukamatwaji wa waandishi na watanzania wanaotumia mitandao ya kijamii katika kutoa taarifa kwa umma.

Mwaka 2018 Kanuni za Maudhui Mtandaoni zilitungwa na kuanza kutumika. THRDC kwa kushirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu pamoja na Baraza la Habari Tanzania tulifungua kesi Mahakama Kuu kanda ya Mtwara kupinga kanuni hizo kutokana na ukweli pekee kwamba zinakiuka uhuru wa kujieleza pamoja na haki ya kutumia mitandao bila masharti na gharama yoyote. Kesi hiyo bado inaendelea mahakamni mpaka sasa.

Tangu kutungwa kwa Kanuni hizo, waandishi wengi wamekamatwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kuendesha au kumiliki akaunti mbalimbali mtandaoni bila ya kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Kukamatwa kwa waandishi hao jana ni muendelezo wa utekelezaji wa Kanuni hizi ambazo tangu kutungwa kwake tumezipigia kelele kuwa hazifai kwasababu zinaminya uhuru wa kujieleza kinyume na Katiba.

Waandishi hao na mmiliki huyo wa YouTube akaunti walikamatwa jana siku ya Jumapili tarehe 05 Aprili 2020 kwa tuhuma za kumiliki blog bila ya kuzisajili. Waandishi hao ni: Tumsifu Kombe na Johnson Jabir. Mmiliki wa YouTube akaunti bado jina lake halijafahamika.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Kilimanjaro Bw. Nakajumo James ni kwamba: Jana jumapili jioni waandishi hao walikamatwa na askari wa jeshi la polisi aliyejitambulisha kuwa anatokea Dar es Salaam. Waandishi hao walipelekwa kituo cha polisi kati mjini Moshi. Askari huyo alionyesha pia picha za waandishi wengine kadhaa ambao wapo kwenye orodha ya kukamatwa kutokana na tuhuma za kumiliki blog bila ya kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umemuagiza wakili wake Emmanuel Makiya kufuatilia haki za waandishi hao ili haki iweze kutendeka. Mtandao utaendelea kutoa taarifa zaidi kuhusu kushikiliwa kwa waandishi hao.

Wito wa Mtandao
1. Jeshi la Polisi linapaswa kuzingatia haki za watuhumiwa hao ikiwemo kuwaachia huru au kuwafikisha mahakamani ndani ya masaa 24 kwa mujibu wa kifungu cha 64 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai sura ya 20

2. Mtandao unatoa wito kwa wamiliki wa vyombo vya habari mtandaoni, watumiaji wa mtandaoni, watunga sheria na wadau wote wa haki nchini kuendelea kupinga Kanuni hizi ambazo kimsingi zipo kinyume na misingi ya haki ya uhuru wa watu kujieleza kwa kutumia njia yoyote ile ambayo wao wameichagua ikiwemo kutumia mitandao. Ikumbukwe kuwa mitandao ya kijamii ipo bure kwa kila mtu duniani kutumia na wenye mitandao hii hawajahi kudai wanaotumia walipie chochote.

Imetolewa
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)
Aprili 06, 2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
maudhui au content zinatofautiana kulingangana na mtoaji ina maana kuna baadhi ya maudhui ni ubunifu wa mtu tu na nyingine ni habari zinazopaswa kufuata kanuni zote za habari hata hivyo waliotunga hizi sheria wanapaswa kuangalia nje ya box pia mfano: kuna maudhui ya elimu ambayo mtu huweza toa bure kupitia youtube na kuna sheria za kulinda maudhui ya aina hii zilizowekwa na youtube yenyewe lakini kwa hapa tanzania unatakiwa ulipie kitu kama hiki ina maana kwenye janga kama hili la corona kuna walimu wangeweza kuwa na chaneli za bure kwa ajili ya wanafunzi lakini atatakiwa atoe fedha kuwa na ithibati ya kuwa na chaneli ambayo yeye anatoa elimu bure
Huna akili .

Kuandika maudhui kwamba kuna vifo vya corona zaidi ya 200 Tanzania ni ubunifu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makini sana ,umewang'amua lengo lao
Nadhani mkuu hapa kinacho zungumzwa ni wamiliki wa chombo husika kukosa/kutokusajili vyombo vyao, mfano wa JF hiki ni chombo kilichosajiliwa.
Ukiwa na YouTube channel mfano ayo Tv n.k hao wamiliki ndio wanatakiwa kuwa na lessen na hata waandishi wake pia wawe nazo.

Ila hii taarifa pia nayo inaonekana kukaa kishabiki Sana hawa THRDC kwanini hawataki kutaja huyo mmiliki wa hiyo YouTube Channel na channel yenyewe ili tujue Kama kweli imesajiliwa au hapana, badala yake wamewataja waandishi tu sasa hapa wanataka tuwaamini wao moja kwa moja na mjadala uwe wa upande mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huna akili .

Kuandika maudhui kwamba kuna vifo vya corona zaidi ya 200 Tanzania ni ubunifu?

Sent using Jamii Forums mobile app
inaonekana we ni mtu wa kukurupuka nimesema maudhui yapo ya aina mbali mbali kulingana na mtoa maudhui chaneli yake ina mlengo upi kama ni mambo ya ubunifu maana yake maudhui ya chaneli yake yatajikita hapo na si vinginevyo na kama ni ya habari basi yatafuata misingi yote ya habari, kama mtu katoa habari isiyokidhi vigezo vya habari basi amekiuka misingi na ndio maana unaposajiri gazeti unapeleka dummy yaani muundo wa jinsi gazeti lako litavyokuwa kurasa kwa kurasa kama ni michezo au habari mchanganyiko ama la vibonzo kama la habari mhariri wake ana vigezo vinavyohitajika? maudhui ni kile kitakuwamo ndani ya gazeti hilo nadhani neno maadhui ndio linachanganya kwani uaposoma kitabu unapokuta table of contents hua ina maanisha nini ?
 
Serikali iliyotangaza vita dhidi ya vijana wake huwa haina mwisho mzuri.

Sheria za hovyo kama hizi dawa yake ni kuzikaidi tu kwa ujumla wetu.
 
Back
Top Bottom