Kilimanjaro Stars yadundwa 'Kiume' na Zanzibar heroes! Yapigwa 2 - 1

8c51d52df393af3892223e099fc82d07.jpg
 
Sio kweli hayo matokeo ni Expansion Joint tu


1. Hivi ni nani in-charge wa timu ya taifa?

2. Mwalimu wa timu za taifa taifa stars, kilimanjaro stars na zanzibar heroes wanachaguliwa kwa mchakato upi? Hivi Pluijm, Omog, Lwandamina yule was Azam n.k. wametafutwa kwa michakato na rasilimali za vilabu, timu zetu za taifa zinapataje makocha wake? mpaka tushindwe kupata kocha wa kiwango kinachofanana na hadhi ya taifa la Tanzania?

3. Tanzania tumewahi kuelewa faida ya kuwa na zanzibar heroes na kilimanjaro stars katika kutengeneza taifa stars? au kinyume chake, hasara ya kuwa na kilimanjaro stars na zanzibar heroes kutoka taifa stars moja?

4. Hivi wachezaji wa zanzibar heroes wana utambulisho gani unaowafanya wawe tofauti na bara wakati hati halisi ni passport ambazo ni sawa kwa wote? Hivi Aggrey Morris akisema yeye ni mtanzania bara atakataliwa kwa kigezo gani?

5. Leo Himidi Mao, Kilimanjaro Stars, Mudathir Yahaya, Zanzibar Heroes, nahisi hata wachezaji huwa wanajikuta wako nchi tofauti wakati wa mashindano haya bila kujua

6. Maelezo ya zanzibar heroes kuwa nzuri partly sababu wanacheza ligi ya bara, alafu wenye ligi yetu tunashindwa inashangaza

7. Hivi, tangu lini mchezaji anayecheza uarabuni amewahi kuja kucheza Tanzania akafanya vizuri bila kupigwa msasa kwanza? sina ubaguzi lakini nafikiri kuleta LYANGA, MAGURI na yule kutoka sijui Sony Sugar ya Kenya si sahihi. Ligi yetu ni kubwa na si mbovu sana na kwamba tuna uhakika na tunaowachagua kwa sababu tumewaona wakicheza hapa. Sasa Lyanga tangu atoke Simba sijui misimu mingapi hatujamsikia popote. Anayetoka nje na kustahili kucheza hapa awe na viwango vinavyofanana na Samatta, Banda na hata Msuva na si vinginevyo, othewise tunawakatisha tamaa vijana wanaojitahidi hapa.

8. Wa nje ambao tuna uhakika bado wako safi ni ABDI BANDA, Msuva kidogo lakini tumuangalie kwa karibu maana anavyoandikwa kwenye magazeti na tulivyomuona kwenye zile mechi mbili havifanani, hata Farid Mussa naye bado!

9. Kama vipi, tuanze kuwaandaa hawa akina Mlipili, Kihombo n.k. ndiyo watatufikisha mbali

10. Nje ya uwanja hawa wachezaji wa timu za taifa letu/yetu wakoje? wana ushirikiano na urafiki au ndiyo wana nuniana n.k. mtangazaji wa Azam TV alienda kambini wachezaji wanacheza computer games lakini walikuwa wanaonekana kama wako tense au u simba na u yanga wanaendeleza huko? naomba kusahihishwa.

11. Tunataka wachezaji wa timu ya taifa wanaoonyesha kuwa tayari na kuwa na ndoto kubwa

12. Tuombe Mungu washinde michezo yote iliyobaki la sivyo atafutwe consultant afanye utafiti wa chanzo na jibu la shida ya timu za taifa: Kilimanjaro Stars na Taifa Stars. Kwa sasa Zanzibar Heroes hawamo, wao wamefanya kazi yao vizuri.
 
Yule beki wa kulia alevaa no 3 sijui wa wapi? Anageuzwa geuzwa kama chapati.
 
Hayo ni matokeo ya kushinda goli tano kwa mlungura halafu makocha wanawaona wachezaji kama ma star!‰
 
Leo Kilimanjaro Stars imekubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa ndugu zao wa Zanzibar heroes ili kuunga mkono juhudi za JPM kudumisha muungano.
Tunawapongeza kwa uzalendo wao.
 
1. Hivi ni nani in-charge wa timu ya taifa?

2. Mwalimu wa timu za taifa taifa stars, kilimanjaro stars na zanzibar heroes wanachaguliwa kwa mchakato upi? Hivi Pluijm, Omog, Lwandamina yule was Azam n.k. wametafutwa kwa michakato na rasilimali za vilabu, timu zetu za taifa zinapataje makocha wake? mpaka tushindwe kupata kocha wa kiwango kinachofanana na hadhi ya taifa la Tanzania?

3. Tanzania tumewahi kuelewa faida ya kuwa na zanzibar heroes na kilimanjaro stars katika kutengeneza taifa stars? au kinyume chake, hasara ya kuwa na kilimanjaro stars na zanzibar heroes kutoka taifa stars moja?

4. Hivi wachezaji wa zanzibar heroes wana utambulisho gani unaowafanya wawe tofauti na bara wakati hati halisi ni passport ambazo ni sawa kwa wote? Hivi Aggrey Morris akisema yeye ni mtanzania bara atakataliwa kwa kigezo gani?

5. Leo Himidi Mao, Kilimanjaro Stars, Mudathir Yahaya, Zanzibar Heroes, nahisi hata wachezaji huwa wanajikuta wako nchi tofauti wakati wa mashindano haya bila kujua

6. Maelezo ya zanzibar heroes kuwa nzuri partly sababu wanacheza ligi ya bara, alafu wenye ligi yetu tunashindwa inashangaza

7. Hivi, tangu lini mchezaji anayecheza uarabuni amewahi kuja kucheza Tanzania akafanya vizuri bila kupigwa msasa kwanza? sina ubaguzi lakini nafikiri kuleta LYANGA, MAGURI na yule kutoka sijui Sony Sugar ya Kenya si sahihi. Ligi yetu ni kubwa na si mbovu sana na kwamba tuna uhakika na tunaowachagua kwa sababu tumewaona wakicheza hapa. Sasa Lyanga tangu atoke Simba sijui misimu mingapi hatujamsikia popote. Anayetoka nje na kustahili kucheza hapa awe na viwango vinavyofanana na Samatta, Banda na hata Msuva na si vinginevyo, othewise tunawakatisha tamaa vijana wanaojitahidi hapa.

8. Wa nje ambao tuna uhakika bado wako safi ni ABDI BANDA, Msuva kidogo lakini tumuangalie kwa karibu maana anavyoandikwa kwenye magazeti na tulivyomuona kwenye zile mechi mbili havifanani, hata Farid Mussa naye bado!

9. Kama vipi, tuanze kuwaandaa hawa akina Mlipili, Kihombo n.k. ndiyo watatufikisha mbali

10. Nje ya uwanja hawa wachezaji wa timu za taifa letu/yetu wakoje? wana ushirikiano na urafiki au ndiyo wana nuniana n.k. mtangazaji wa Azam TV alienda kambini wachezaji wanacheza computer games lakini walikuwa wanaonekana kama wako tense au u simba na u yanga wanaendeleza huko? naomba kusahihishwa.

11. Tunataka wachezaji wa timu ya taifa wanaoonyesha kuwa tayari na kuwa na ndoto kubwa

12. Tuombe Mungu washinde michezo yote iliyobaki la sivyo atafutwe consultant afanye utafiti wa chanzo na jibu la shida ya timu za taifa: Kilimanjaro Stars na Taifa Stars. Kwa sasa Zanzibar Heroes hawamo, wao wamefanya kazi yao vizuri.
Mhhh kushindwa kubaya,kaka kubali kushindwa...huu waraka hautasaidia chochote,nakumbuka Maximo aliwahi kusema Zanzibar iko juu katika viwanja vya kuchezea watoto(maeneo ya wazi)

Mtoto anatakiwa umuwahi tangu mdogo kama unataka afanikiwe kwa chochote kile,ikiwa kimziki,kimichezo,kimasomo nk,Ninachokiona Tanganyika hasa hapa Daresalam viwanja vya wazi vyote vimejengwa ofisi za CCM sasa watoto watapata wapi kujifundisha kucheza mpira au michezo mingine...,aibu kubwa sana kuona watoto hawana sehemu za kucheza lakini tunakimbilia "Flyingover"

Tuanze kufikiri kivingine tutafanikiwa....
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom